Kwa hili la mzigo huu, wacha tu bandari ibinafsishwe

Kwa hili la mzigo huu, wacha tu bandari ibinafsishwe

Unacheza na maneno, unafikiri container likifika unaenda kuchukua kama unavyotumiwa kifurushi cha mzigo Kimbinyiko?
Oya acha kuonesha ujinga wako basi, kama unakufaa sana kaa nao mwenyewe.
 
Nina konteina kutoka china, leo ni wiki ya pili tangu meli imefika dar port ila mzigo haujashushwa, sasa hapa kuna nini? Zaidi ni tubinafsishe tu hii bandari ili tulete maendeleo hakuna njia wala namna

Wanaopinga vaeni viatu vya mfanyabiashara kwanza halafu ndio uje na point, tena ziwe fupi fupi
Acha propaganda za kitoto,usifikiri upo mwenyewe unaye import bidhaa tuko wengi tena wengi sana.

Mzigo unaweza kuchelewa kupata kwasababu nyingi.Kubwa kuliko zote ni TRA au mamlaka nyingine eg TBS.

Hichi ulichoandika ni namna ya kuhalalisha ujinga uliofanywa na serikali ambayo haipo kwaajili ya maslahi ya Tanganyika.
 
Unachanganya sana contena haliwezi kukaa kwenye meli wiki,hiyo haipo najua hiyo shuhuri vizuri,sema tatizo lingine,kama umetumwa mwambie aliyekutuma kuwa huku nje watu wako vizuri kuliko unavyo zani
 
Inatia hasira sana ,kitu unakijua vizuri harafu anatokea mtu anasema uongo kwa faida zake na si za nchi,inauma inauma inauma
 
Hayo mapungufu yote hatuwezi kurekebishana wenyewe mpaka aje mtu kutoka nje? Yaani nchi imekua ngumu hivi kuisimamia mpaka tupate usaidizi kutoka nje?

Hao wanaofanya hizo vitu hawana maboss wao wa kuwawajibisha?
Bandarini pagumu pasikie tuu! Kwa mfumo ulivyo pale (mfumo usio rasmi, lakini), hata wewe ukiajiriwa pale, hata kama ni mwadilifu wa kupindukia, utachagua moja:
(a) Kufuata mfumo huo usio rasmi (unaokulazimu lazima uwe "mpigaji"). (b) Ukubali kufukuzwa kazi kutiwa gerezani, n.k. kwa "mizengwe".
(c) Kuawa (kwa "juju", vijana wa kazi, n.k.).
Bandarini Dar ni pagumu sana. Ni bonge la "shamba la bibi", usipime.
 
Bandarini pagumu pasikie tuu! Kwa mfumo ulivyo pale (mfumo usio rasmi, lakini), hata wewe ukiajiriwa pale, hata kama ni mwadilifu wa kupindukia, utachagua moja:
(a) Kufuata mfumo huo usio rasmi (unaokulazimu lazima uwe "mpigaji"). (b) Ukubali kufukuzwa kazi kutiwa gerezani, n.k. kwa "mizengwe".
(c) Kuawa (kwa "juju", vijana wa kazi, n.k.).
Bandarini Dar ni pagumu sana. Ni bonge la "shamba la bibi", usipime.
Umewai fanya kazi hapo?
 
Nina konteina kutoka china, leo ni wiki ya pili tangu meli imefika dar port ila mzigo haujashushwa, sasa hapa kuna nini? Zaidi ni tubinafsishe tu hii bandari ili tulete maendeleo hakuna njia wala namna

Wanaopinga vaeni viatu vya mfanyabiashara kwanza halafu ndio uje na point, tena ziwe fupi fupi
kichaa mwingine kajitokeza!!
 
Wanaopinga wana hoja wasikilizwe! Wanaosapoti mmeshindwa kujibu hoja za wanaopinga!! NB; Haiwezekan et mkeo analiwa na jiran halafu solution yako ni kuhama mtaa 🤣🤣🤣🤣
😆😆. Kama analiwa na hakusikii huku bado unamhusudu, wewe hauwezi hama kuikimbia fedheha na kwenda kuificha sura yako mbali? Majaribu hayo mkuu ujue!

Tuje kwenye mada:
Kumekuwa na ujinga na upumbaf pamoja na ushabiki kwenye hii hoja muhimu ya kiTaifa.

Wote wanaopinga hawapingi kijinga, wanapinga kwa fact zilizo wazi na zenye mshiko!

Wanaoshadadia kuunga mkono, wanaunga mkono kipmbaf bila kujali haiba ya mtu wala cheo chake.

Ninadhani wote hao wana maslahi binafsi ya moja kwa moja kuingiza matumboni mwao ama ni wanufaika kwa indirect!

Maswali machache sana ya kisheria na kikatiba yameulizwa, lakini kuanzia mwanasheria mkuu, waziri mkuu ama Waziri mhusika, hawajatoka hadharani kujenga hoja na kuja na majibu ya kina kuridhisha umma.

Raia wa Tz tumekuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji, kuna ombwe kubwa sana la uongozi hivi sasa nchini mwetu.

Nafikiri kuna nia ya agenda za siri ama za makusudi kuchafua na kuivuruga nchi.

Ninakuunga mkono sana kwa mawazo yako yakinifu.
 
Nina konteina kutoka china, leo ni wiki ya pili tangu meli imefika dar port ila mzigo haujashushwa, sasa hapa kuna nini? Zaidi ni tubinafsishe tu hii bandari ili tulete maendeleo hakuna njia wala namna

Wanaopinga vaeni viatu vya mfanyabiashara kwanza halafu ndio uje na point, tena ziwe fupi fupi
Unachokiongelea wewe si agenda ya kiTaifa kwa sasa!

Kinachoongelewa ni mikataba mibovu ya kinyonyaji na ya hovyo iliyoingiwa kisheria kati ya DP na Serikali period

Ufanisi na utendaji wa Bandari si agenda kwa sasa na hakuna hata mmoja aliyekataa wala kupinga uwekezaji wenye tija.

Unapotoka hadharani kuunga mkono jambo lenye utata katika jamii, ni sawa na kukoleza moto kwa petroli.
Kama hautaki kusikiliza hoja enye mashiko zinazotolewa na wanasheria wasomi, zinazofafanua uozo uliomo katika mkataba huo, basi ni heri ukajikalia kimya na kukaa kimya siyo ujinga.
 
Wanaopinga wana hoja wasikilizwe! Wanaosapoti mmeshindwa kujibu hoja za wanaopinga!! NB; Haiwezekan et mkeo analiwa na jiran halafu solution yako ni kuhama mtaa 🤣🤣🤣🤣
Kwamba akihama ndo haliwi tena..!! 😄 😄 😄
 
Nina konteina kutoka china, leo ni wiki ya pili tangu meli imefika dar port ila mzigo haujashushwa, sasa hapa kuna nini? Zaidi ni tubinafsishe tu hii bandari ili tulete maendeleo hakuna njia wala namna

Wanaopinga vaeni viatu vya mfanyabiashara kwanza halafu ndio uje na point, tena ziwe fupi fupi
Hivi unakijua kinachopingwa..!!??
Nani kakuambia kuwa kinachopingwa ni muarabu kupewa bandari!??
Hivi umeusoma mkataba upoje ukajua nini kimeandikwa!??
 
Majitu mengi ya

Majitu mengi yanayopinga hayana hoja yanapinga kwa ushabiki tu na chuki za uzanzibari v/s ubara
Hapana, usiende huko. Mkataba ule, binafsi uko vizuri ILA unatakiwa kupitiwa upya kwa makini na kisha kufanyiwa marekebisho (kama hakuna "hila" yoyote). Kimsingi (kisheria), Mkataba (Makubaliano) lazima uwe wazi wenye kueleweka unaojieleza kwa kujitegemea wenyewe. Hautakiwi kuwa na makando-kando. Ujitosheleze kwa maelezo na takwimu ili anayeyasoma auelewe pasi kumwacha na mashaka. Uwe wenye manufaa kwa pande zote mbili zilizoingia Makubaliano husika.
Hili la DPW na TPA (i.e. Tanzania na Dubai) halijakaa vizuri kivile; lina "matundu", mfano; Kifungu cha 23 inatakiwa kipitiwupya na kifanyiwe marekebisho ya msingi.
Lakini tunapaswa kujua, suala hili halipaswi kuchukuliwa kisiasa, kidini, n.k. bali, lichukuliwe kisheria kwa maslahi mapana ya ustawi na maendeleo ya nchi yetu. Hata hivyo, tunatakiwa kuwa waangalifu extra na wanasiasa, kwani hutumia masuala serious kama haya kuwa fursa kwao na vikundi vyao. Hakuna dini kwenye hili. Hakuna.
 
Unachokiongelea wewe si agenda ya kiTaifa kwa sasa!

Kinachoongelewa ni mikataba mibovu ya kinyonyaji na ya hovyo iliyoingiwa kisheria kati ya DP na Serikali period

Ufanisi na utendaji wa Bandari si agenda kwa sasa na hakuna hata mmoja aliyekataa wala kupinga uwekezaji wenye tija.

Unapotoka hadharani kuunga mkono jambo lenye utata katika jamii, ni sawa na kukoleza moto kwa petroli.
Kama hautaki kusikiliza hoja enye mashiko zinazotolewa na wanasheria wasomi, zinazofafanua uozo uliomo katika mkataba huo, basi ni heri ukajikalia kimya na kukaa kimya siyo ujinga.
Kwahiyo nyie mpinge na sie tuwaunge kindezi ndezi tu,

unavyoona wewe sivyo ninavyoona mimi
Si lazima ukubali maoni yangu na usinilazimishe kukubali yako

Hao unaowaona wasomi kwangu ni wajinga na watu wa maslahi tu, na wengu wamenunuliwa na kenya kwa faida ya kenya, maadui wa tz ni wengi sana
 
Kwahiyo nyie mpinge na sie tuwaunge kindezi ndezi tu,

unavyoona wewe sivyo ninavyoona mimi
Si lazima ukubali maoni yangu na usinilazimishe kukubali yako

Hao unaowaona wasomi kwangu ni wajinga na watu wa maslahi tu, na wengu wamenunuliwa na kenya kwa faida ya kenya, maadui wa tz ni wengi sana
Hapa ndugu umepiga siasa nikwambie.

Umetumia maneno ambayo yameonesha namna gani ulivyojengeka kiakili.

Na haujatoa hoja yoyote kwa points unazoungia mkono!

Angalia majority wanazungumziaje kuhusu issue hii na utafakari.

Unavyosema haunilazimishi kukuunga mkono kwa maoni yako ambayo umeyaweka katika mjadala ni makosa kwa sababu mjadala haujafungwa, ni mjadala wa wazi.

Tukianza kujibishana namna hiyo, mada hii haitafika mwisho.

Kwa hiyo sasa na mimi niseme kwa kuwa hauungi mkono mawazo yangu na mimi sikuungi mkono mawazo yako na tuishie hivyo bila kuweka points zozote?

Mi nadhani ungetandaza fact zako za kisayansi kuunga mkono mikataba ili baadaye tufikie hitimisho la kisomi pamoja.

Hili la kusema nchi ina maadui wengi kwa watu wanaotoa hoja jadidifu ni uongo mtupu na wala Kenya hahusiki kwa vyovyote katika sakata hili.

Sisi hao wanaoukosoa mkataba huu kwa hoja ndiyo tunawaona kama wazalendo wa kweli wa nchi hii.
 
Ilikuwa ni kuwakaribisha rasmi waje tuongee sasa kuhusu mkataba

Propaganda za kijinga hizo. Halafu kuna siku mjukuu wako ntakuuliza kwann mwafrica maskini ijapo bara lao lina kila kitu, kumbe babu yake umepewa peremende uwasaliti wajukuu zako.

Ngozi nyeupe wanatafuta mali kwa ajili ya wajukuu wa wajukuu zao, ila ngozi ya laana nyeusi inatapanya kilichoachwa na babu zao ili wajukuu wakija wasikute kitu.
 
Back
Top Bottom