uttoh2002
JF-Expert Member
- Feb 3, 2012
- 17,060
- 32,400
Kuna idadi kubwa sana ya Waafrika nchini China, Waghana na Wanajeria wana mpaka food joints zinazopika vyakula vyao, hii yote ni kuhudumia idadi kubwa ya watu wao waliokwenda kutafuta maisha huko.
Canada wanatoa offer za scholarships kwa undergraduates kusoma degree katika vyuo. Lengo kuu ni kupata skilled workers nchini mwao. Kutokana na idadi ya watu kupungua.
Ureno walitoa nafasi za dada/kaka wa kulea watoto, kuuza supermarkets, kusafisha mahospitali. Kutokana na Covid 19 ajira za usafi ma hospitalini zimeongezeka sana Ulaya.
Tangu nchi za Afrika zipate Uhuru kutoka kwa Wakoloni, uhaba wa ajira kwa vijana umeongezeka. Nchi huru zimeshindwa kuzalisha ajira mpya baada ya wawekezaji wengi kuondoka.
Vijana wa Afrika wanasafiri safari za hatari kuvuka bahari kutafuta ajira Ulaya. Idadi ya Waafrika katika kazi zisizo na ujuzi inazidi kuongezeka na pia Waafrika wanaoishi Ulaya ni wengi na wakiwa na familia tayari.
Tumekua wazalishaji wa nguvu kazi Ulaya, nguvu ambazo zingetumuika kuendeleza bara letu kufikia maendeleo wakiyofikia Ulaya.
Wacha tu hili bara liishe hata lipotee, maana hawapendi wana nchi wao!
Nimepita Karume Jana ile picha mpaka Leo ipo kichwani; acha tu nguvu Kazi iende!
Maisha magumu Sana Kwa Vijana wengi, Hali imekuwa ngumu kuzidi maelezo.