Kwa kauli hii ya IGP Wambura, Lissu na wengine nawashauri futa wazo la kurudi nchini

Kwa kauli hii ya IGP Wambura, Lissu na wengine nawashauri futa wazo la kurudi nchini

Nadhani alipaswa kuwa na muda kujiandaa maneno ya kusema, ukimfuatilia unaona kama alikuwa anatafuta maneno ya kuongea kutokana na hicho cheo kipya ila kwa sababu ni ijp ndo imetoka hiyo no retreat to correct it 🤓.

IMG_20220721_160748.jpg

Huyo wa pembeni hapo ndiye alipaswa kuwa IJP kwa mkunjo huo wa mdomo aaah!.
 
Siasa ni mapambano lazima ukubali kwa lolote litakalo kutokea Jambo la muhimu ni ile dhamira yako uliyonayo ni kutoiacha labda kifo kikutenganishe na dhamira yako .hata harakati za kudai Uhuru duniani kote hazikuwahi kuwa nyepesi Kuna wengine walikufa katika safari ya mapambano walio hai wanaendeleza mapambano mpaka dhamira yao ya kudai Uhuru ikatimia . Kwa hiyo wao wasihofie chochote Jambo la muhimu Kama wamekubali kuipigania Tanzania kweli kutoka mioyoni mwao basi wasikate tamaa ya kurudi nchi na kuendeleza mapambano yao Ila Kama hawana dhimira yoyote mioyoni mwao basi watakata tamaa na wakuwa na hofu itakayo pelekea wao kuto kurudi nchi . Shujaa haogopi kufia kwenye uwanja wa Vita/mapambano. Na uwanja wa mapambano ni Tanzania na wala sio huko ughaibuni walipo jihifadhi . Ni mara mia moja kufa katika ardhi ya mapambano [ Tanzania ] na kuhesabika Kama shujaa kuliko kufia ng'ambo na kuhesabika Kama mkimbizi wa Kisiasa maana halisi ya mapambano yao haitaonekana wala kuthaminika.

- Hata Mandela alikimbia kwetu na Mwalimu akahaidi kumpa hifadhi lakini kadiri muda ulivyokuwa una zidi kwenda Mandela alirudi nyumbani kwenye uwanja wa mapambano [ S.A ] na kuendelea mapambano licha ya kufungwa miaka 27 Ila dhamira take ya ukombozi nchini wake ilitimilika .

- Hivyo hivyo kwa Kenneth Kaunda , Samora Machel, Robert Mugabe na wengine wengi tuliwapa hifadhi na mafunzo ila mwisho wa siku Hawa kuendelea kuwa wakimbizi wa Kisiasa nchi mwetu walirudi mwao kwenye viwanja vya mapambano na kupambania zile dhamira zilizomo mioyoni mwao mpaka ukombozi ukakamilika

# SHUJAA WA KWELI HAKIMBII UWANJA WA MAPAMBANO BALI ANAFIA UWANJA WA MAPAMBANO.


# MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI TANZANIA FUNGUA FIKRA ZA WATANZANIA WAJIPAMBANIE WENYEWE KUTOKA MIKONONI MWA WANYANG'ANYI.

* ISHI MILELE TANZANIA MAPAMBANO WACHA YAENDELEE✊🇹🇿
Sio kazi ngumu sana kutambua mtu mwenye dhamira ya moyo wake katika jambo analoliamini.

Nikiangalia katika viongozi wote walioko CCM kwa sasa hivi, simwoni hata mmoja kati yao mwenye dhamira ya moyo wake kwa nchi yetu hii na wananchi wake. Ninaowaona huko sasa hivi ni wenye dhamira ya kujinufaisha wao kwanza kwa kila fursa wanayoweza kuipata kutokqna na nafasi walizonazo kwenye uongozi.

Kwenye watu walio nje, namwona Lissu kuwa ni mtu mwenye dhamira isiyotetereka katika anayoyaamini. Sioni kamwe, kwamba kutorejea kwake nchini ni kwa sababu ya kukosa dhamira hiyo, au kwa kuogopa matokeo ya yatakayomkuta.

Sina shaka, kwa kutorudi kwake nchini kutakuwa na sababu maalum. Hata unapokuwa na dhamira na jambo, huwezi kuacha kutumia akili ili mipango yako ya kutimiza unayodhamiria yapate ufanisi.

Nimalize kwa kusema kuwa, nchi hii inao wengi tu wenye dhamira juu ya maslahi ya waTanzania kuwa mbele zaidi ya mengine yote.
 
Sio kazi ngumu sana kutambua mtu mwenye dhamira ya moyo wake katika jambo analoliamini.

Nikiangalia katika viongozi wote walioko CCM kwa sasa hivi, simwoni hata mmoja kati yao mwenye dhamira ya moyo wake kwa nchi yetu hii na wananchi wake. Ninaowaona huko sasa hivi ni wenye dhamira ya kujinufaisha wao kwanza kwa kila fursa wanayoweza kuipata kutokqna na nafasi walizonazo kwenye uongozi.

Kwenye watu walio nje, namwona Lissu kuwa ni mtu mwenye dhamira isiyotetereka katika anayoyaamini. Sioni kamwe, kwamba kutorejea kwake nchini ni kwa sababu ya kukosa dhamira hiyo, au kwa kuogopa matokeo ya yatakayomkuta.

Sina shaka, kwa kutorudi kwake nchini kutakuwa na sababu maalum. Hata unapokuwa na dhamira na jambo, huwezi kuacha kutumia akili ili mipango yako ya kutimiza unayodhamiria yapate ufanisi.

Nimalize kwa kusema kuwa, nchi hii inao wengi tu wenye dhamira juu ya maslahi ya waTanzania kuwa mbele zaidi ya mengine yote.
Hakika mkuu ulichosema Ila nimependa zaidi ulichosema hapo mwisho na hicho ndicho kimebeba zaidi ujumbe wangu wote kwa WATANZANIA na ujumbe wako wote kwa WATANZANIA . na nukuu “ Nchi hii inao wengi tu wenye dhamira juu ya maslahi ya WATANZANIA kuwa mbele zaidi ya mengine yote”.

- Hakika Tanzania Ina dhamira ya kupiganiwa na WATANZANIA walio wengi waliobeba dhamira sahii na hai mioyoni mwao na sio kuwaachia jukumu la kuipigania watu walio wachache waliobeba dhamira.
 
Hakika mkuu ulichosema Ila ningependa zaidi ulichosema hapo mwisho na hicho ndicho kimebeba zaidi ujumbe wangu wote kwa WATANZANIA na ujumbe wako wote kwa WATANZANIA . na nukuu “ Nchi hii inao wengi tu wenye dhamira juu ya maslahi ya WATANZANIA kuwa mbele zaidi ya mengine yote”.

- Hakika Tanzania Ina dhamira ya kupiganiwa na WATANZANIA walio wengi waliobeba dhamira sahii na hai mioyoni mwao na sio kuwaachia jukumu la kuipigania watu walio wachache waliobeba dhamira.
Binafsi naamini haya yanayotokea sasa ni maandalizi yatakayoleta mabadiliko chanya kwa nchi yetu.
 
Binafsi naamini haya yanayotokea sasa ni maandalizi yatakayoleta mabadiliko chanya kwa nchi yetu.
Sahihi kabisa mkuu ni Kama watawala wanalitengeneza bomu wao wenyewe litakalo kuja kuwalipukia.
 
Nadhani alipaswa kuwa na muda kujiandaa maneno ya kusema, ukimfuatilia unaona kama alikuwa anatafuta maneno ya kuongea kutokana na hicho cheo kipya ila kwa sababu ni ijp ndo imetoka hiyo no retreat to correct it [emoji851].

View attachment 2298777

Huyo wa pembeni hapo ndiye alipaswa kuwa IJP kwa mkunjo huo wa mdomo aaah!.
Jamaa ni kilaza kuliko siro
 
Hili liliua wachina kwa mamilioni!
Ndio hivyo mkuu revulution yoyote ile ya kiuongozi/kiutawala Ina positive impact na Ina negative impact jambo la muhimu na la faida ni kuwa political revolution siku zote huleta positive change within the country . Licha ya kuwa China , France, America, Iran, Russia etc political revulution zao ziligharimu maisha ya watu Ila leo hii . hii America, France, Russia, China, Iran tunazoziona Ni kutokana na watu kujitoa kafara kwa ajili ya wajukuu zao wafurahie mema ya nchi zao.
 
The author is suffering from the effects of the cannabis sativa and that's why he has posted this rubbish.

He gives an impression that this country only belongs to ccm and its puppets like him. We shall never be in the same school of thought as his.
 
The author is suffering from the effects of the cannabis sativa and that's why he has posted this rubbish.

He gives an impression that this country only belongs to ccm and its puppets like him. We shall never be in the same school of thought as his.
sijakuelewa context ya jibu lako....
 
Kama walishahakikishiwa usalama wao nao wakawa tayari kurudi wakikamilisha mambo yao, sioni sababu kwao ya kuogopa kurudi nchini.

This life is too short, waje kuungana na ndugu, jamaa, na marafiki zao na waendeleze harakati zao. Kuogopa kurudi nyumbani ni sawa na kuogopa kufanya siasa.
Jamaa wanarudi
 
Back
Top Bottom