Kwa kauli hii ya rais Samia ni dhahiri awamu ya tano ilikuwa 'One Man Show'

Kwa kauli hii ya rais Samia ni dhahiri awamu ya tano ilikuwa 'One Man Show'

Kama kuna kitu alikosea raisi SSH ni kurith viongozi wa magufuli.
Yaani hujuma lazima itokee
Wale waliopiga pesa wizara ya fedha si wateule wake?,na Hawa waliopiga pesa ndefu bandarini si wateule wake?
Ni rahisi kutambua sukumagang lakini kumtumbua mtoto wa Dada ni ngumu.
 
Sabaya aliyekuwa kiongozi awamu ya nne ndiye jambazi kuu. Laiti kama ingetokea akawa kiongozi chini ya magufuli kwa jinsi alivyokuwa anaogopwa yaliyogunduliwa na mahakama kamwe yasingetokea. Mama safisha nyumba, wezi wengi ni wale waliobakia baada ya baba yao kuondolewa na Mungu kwa makusudi kabisa.
Yaani sympathizers wa mafisadi ni wajinga sana. Yaani wana akili finyu sana. Yaani badala ya kujua kuwa Dkt Magufuli aliogopwa na watandaji kiasi kwamba waliogopa kufanya ufisadi na baada ya kufa walishangilia wakijua mkali kaondoka ili waibe wanadhani mama hana akili za kulijua hilo.
 
Hajasema awamu ya tano, aisee, wabongo wazushi kinoma.
 
Rais amesema " upigaji ulifanyika awamu ya tano lkn jumba bovu inaanushiwa awamu ya sita. Sitakubali".

Kama angekuwa mshiriki mkuuktk uendeshaji wa serikali ya awamu ya tano rais SSH asingekubali hata awamu ya tano idhalilike.

Lkn anaona ni sawa kwakuwa hakuhusika kwa chochote. Alikuwepo kama picha tu. Mambo yote yalikuwa yakiamuliwa na kuendeshwa na JPM pekee. ....one man show.
iAcha uongo wako, wewe ni sehemu ya wezi ndio maana unamtetea. Bodi ya bandari alishaibadili yeye mwenyewe muda mfupi tu baada ya kuapishwa na ikaundwa upya anacholaumu kitu gani?

Hakuna kitu kinachoitwa 'one man show' kila kitu kinakubaliwa ndani ya baraza la mawaziri yeye alikuwa sehemu yake halafu mtendaji mkuu ni rais hapo unamwondoa kwa sababu zipi?

Serkali imemshinda na hafiki popote Mungu hataniwi kamwe eti unatupiwa lawama chumba ulichokuwa ukiingia kwa kazi maalumu halafu unajisafisha

Ufisadi umetamalaki maradufu mno sasa hivi na gharama za ziara zake zote alizozifanya tayari wapigaji wamemwingiza chaka utakuja kuzisikia wakati wa ukaguzi wa CGA sijui atamtupia nani tena lawama hapo.

Kiota cha majani kilicho katikati ya msitu unaoungua moto
 
Basi atakuwa mmoja ya viongozi wa hovyo kuwahi kutokea kama unayosema ni kweli. Yaani awe makamu wa rais halafu anyimwe nguvu alizopewa kikatiba halafu abaki kusifu na kutukuza tu kila kilichokuwa kinatokea? Kwa nini hakujiondoa?
😄😄😄 Tupe mfano wa makamu wa rais mmojawapo wa Tz aliyewahi kujiondoa,?
 
Mama tumekupa ikulu na majeshi yote, wewe ndio kamanda mkuu aka amir jeshi mkuu wa majeshi yooote....wizara zote ziko chini yako, wewe ndio bosi mtoa amri.....MAMA TUMIA HIVYO VYOMBO KUCHUKUA MAAMUZI NCHI IENDE MBELE....chukua maamuzi makali dhidi ya wapumbavu wote kama kweli una nia ya dhati nchi iende mbele..
 
Rais amesema " upigaji ulifanyika awamu ya tano lkn jumba bovu inaanushiwa awamu ya sita. Sitakubali".

Kama angekuwa mshiriki mkuuktk uendeshaji wa serikali ya awamu ya tano rais SSH asingekubali hata awamu ya tano idhalilike.

Lkn anaona ni sawa kwakuwa hakuhusika kwa chochote. Alikuwepo kama picha tu. Mambo yote yalikuwa yakiamuliwa na kuendeshwa na JPM pekee. ....one man show.
Wasukuma wanatakiwa wajifunze kukaa kimya,na wasijione kua wajuaji au wasiwaone watu hawajui ya awamu ya 5


Ni ushamba kutaka kuendelea kuwaaminisha watu kua wao na awamu yao ya 5 ndio bora na wasafi kuliko awamu zilizopita
 
Bwana wee, hizi lectures tumeshazisikia sana nilikua namjibu huyo niliyemnukuu aliyesema Mama alitakiwa asiwachukue waliokua kwenye awamu iliyopita.

Sasa kama yeye mwenyewe alikua sehem ya hiyo awamu iliyopita na mtoa hoja point yake ni kwamba wote waliokua awamu iliyopita, una muenguaje Mama?

Hapo hoja ilitakiwa iwe Mama aweke wazi nini anataka na apate watu anaona watamsaidia kutimiza anachotaka.
Mama kasema sana,anataka HAKI kitu ambacho watu wa awamu ya tano hawawezi
 
Back
Top Bottom