Kwa kizazi hiki na tabia za sasa kuna umuhimu gani wa kupoteza fedha nyingi kutoa mahari?

Nilijua tu utakuja na hoja nyepesi ambazo hazina uzito wowote wa kimantiki.

Eti familia ya KE inapotoa Binti yao aolewe ni kama wanapoteza rasilimali... Kwa dunia hii ya leo? Hii hoja yako ingeweza kuwa na mashiko kama tungekuwa Bado tuko miaka ya 1970s huko lakini sio leo hii, yes, zamani Binti akiolewa alikuwa anaenda kuwa chini ya umiliki wa mume wake kwa maisha yake yote yaliyobaki na mume wake huyo atamtumia kwenye shughuli za uzalishaji Mali kadri anavyotaka na Binti huyo akuruhusiwa kurudi nyumbani kwao haijalishi ni changamoto gani atazopitia kwenye ndoa yake.

Hebu Sasa tuangalie suala hili kwa dunia ya leo hii kama Bado mantiki yake ni ile ile... Je, Sasa hivi wanawake Bado mkiolewa mnaenda kuwa chini ya total ownership ya mumeo kana kwamba chochote unachokuwa unakifanya kinakuwa ni kwa ajili ya maslahi ya mume wako kama ilivyokuwa kwa mabibi zetu?? Jibu ni HAPANA.

Siku hizi wanawake mnaolewa mkiwa tayari mna career zenu ambazo wazazi wako wamekujengea kwa kukusomesha, licha ya wewe kuolewa ila wanakuwa wanategemea kupata misaada kutoka kwako kupitia hiyo career yako. Kwa hiyo Sasa unakuta wewe umeolewa lakini Bado una uhusiano wa karibu sana na familia yako kwa maana ya kuwapa misaada na hivyo wanakuwa hawajapoteza nguvu kazi yoyote ile.... Na kama hiyo haitoshi unakuta Kuna muda unamshirikisha mume wako kutatua shida za nyumbani kwenu na anafanya hivyo kama uwezo Yuko nao....Sasa hapa Bado unasema wewe Binti ukiolewa familia yako inapoteza nguvu kazi??

" Mwanaume anapoteza nini? au wazazi wake wanapoteza nini?"

Wewe dada hivi kabla ya kuuliza hayo maswali ya kitoto ukifanya tafakari kwa kuangalia na uhalisia wa maisha ya leo? Au umeuliza tu kulingana na ulivyokariri maandiko?

KWa hii Karne tuliopo kwenye suala la ndoa mwanaume na familia yake wanapoteza vingi sana, wakati huo mwanamke na familia yake Wana gain vingi sana...

Mwanaume akioa kama yeye alikuwa ndio nguzo huko kwenye familia yake, itabidi apunguze majukumu na kuanza kuingalia familia yake mpya ambayo ni wewe... Yaani kama alikuwa anasomesha wadogo zake itabidi aache, kama alikuwa anatunza wazazi wake itabidi aache au apunguze, yaani kwa maana nyingine familia yake Inakuwa imepoteza nguvu kazi au rasilimali muhimu kwa ajili yako.

nimewahi kuona mwanaume aliyeacha kusomesha wadogo zake na kisha kuanza kumuendeleza kielimu mke wake mara tu alivyomuoa, halafu huyo mke baada ya kumaliza masomo yake na kupata kazi nzuri akaanza kuwasomesha wadogo zake(yaani shemeji zake na mumewe)... Sasa hapo ni familia ya nani ilipoteza?

Wanaume Karne hii wanaoa wanawake ambao wanalingana nao vipato au muda mwingine wanawake wao wanawazidi vipato, lakini pesa inayotumika kwenye ujenzi wa familia kama kununua assets, kujenga n.k kwa kiasi kikubwa unakuta ni ya mume, ila siku ndoa ikivunjika wanagawana Mali hizo 50-50, halafu bado unuliza mwanaume anapoteza nini akioa?

Hilo suala la mtoto kuitwa ubini wa baba ni hoja isiyokuwa na kichwa Wala miguu... Mtoto anaweza akabeba jina langu lakini asiwe na connection yoyote na Mimi yenye faida, angalia hata bwana Nasibu amebeba jina la Abdul.

Bado hujaleta hoja ya maana ni kwanini tuendelee kuwatolea mahari???
 
Mahari haina umuhimu wowote ni jambo la kitamaduni. Ngumu kubadilisha tamaduni na hata mabadiliko yake huja taratibu , na hata hivyo tuna chance ya kuleta utamaduni mpya , kama tulivyopokea tamaduni zote za kigeni na mpya (zilizoanzishwa)

Ili tupate tamaduni mpya, tunahitaji wa kuianzisha, hivyo ukitaka kuoa; iambie familia unapoenda kuoa wakutolee mahari, walete mahari kwenu.

Wahindi wanafanya hivi.
 
sababu za ugumu wa kubadilika kwa hii tamaduni ziko wazi sana dada, kwa mabadiliko ya kijamii yanayoendelea kwa Kasi Hilo suala mahari lingekuwa liko kinyume na lilivyo sasa lingekuwa limeshabadilika mbona, yaani kama ingekuwa mwanaume ndio anatolewa mahari tangu enzi na enzi, Sasa tunavyoandika hapa lingekuwa limegeuka kama sio kufutwa kabisa kama ambavyo tamaduni zingine zilizoonekana kumnyima manufaa mwanamke zilivyofutwa... Ila kwa vile Hili la mahari linaonekana kunufaisha zaidi familia ya mwanamke ndio maana Bado lipo na hata wanaolipinga hawalipingi kwa uzito.

Yes, tunajua mabadiliko ya kitamaduni ni matokeo ya radical feminism.
 
Mahari ni shukrani tu kwa wazazi
Toa hili neno "shukrani" halihusiki hapo.

Mahari ni biashara kama wewe unavyoenda kununua mbuzi,kondoo ama punda mnandani.

Kwa sababu mnakaa pande zote mbili mnaanza makubaliano. Makubaliano hayo huechukua si chini ya masaa5 au zaidi. Hivyo Kuna kushindwana Kwa upande wa muoaji kutokufikia bei na kushindwa kuoana(kuoa)


Kama mahari ingetolewa na muoaji bila ya makubaliano yoyote kutoka pande mbili ni sahihi kuita shukrani. Tofauti na hapo ni biashara kama biashara zingine tu
 
Mimi huwa nawaambia wanaume humu kuchukua actions, mnatakiwa kuadvocate mambo yanayomkandamiza mwanaume na kuyafanyia kazi . Kulalamika hakusaidii sana.

Wanawake tulipochoka tulikutana Beijing😂😭
 
Mimi huwa nawaambia wanaume humu kuchukua actions, mnatakiwa kuadvocate mambo yanayomkandamiza mwanaume na kuyafanyia kazi . Kulalamika hakusaidii sana.

Wanawake tulipochoka
Changamoto ya sisi wanaume hatuwezi kuwa wamoja kwenye yale yanayotumiza au kuona kuwa unyanyasaji. Mtu akiongelea unyanyasaji katika mindset ya mwanaume anaona wanaonyanyasika ni wanawake tu. @Natufuta Ajira kila siku analeta hoja hapa za kumwelimisha na kumkomboa mwanaume akini wanaompinga kwa nguvu zote ni wanaume. Mwanaume akishafanya maamuzi kwa kutumia kichwa cha chini mara nyingi anaona mwanaume mwenzie ni kama adui wake. Leo wanaume tunazungumza kwenye mitandao huku tukiwa na fake ID maana tukisema public tunaona kama tunashusha thamani yetu ya uanaume lakini tunajikaanga kwa mafuta yetu wenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…