Kwa mara ya kwanza nimeona mwanaume analia kwa sababu isiyohusisha msiba wala mapenzi

Kijana mwenye uwezo wa kujitegemea unaendeleaje kukaa kwa baba yako, huku ukiwa huna shughuli ya kufanya! Tena na mtoto wako mdogo uliyezaa na binamu yako!

Mimi nadhani anastahili kabisa kutukanwa na huyo baba yake.
 
Kama ili ujue rafiki yako alilala na binamu wakapata mtoto inabidi uende kwao ushuhudie akisemwa huyo siyo rafiki yako.

Ndiyo sababu umeweza kuja kumuanika humu.

Wanaume ambao tuna urafiki ishu kama hizo hua tunaambiana hata kwenye simu, kama mzee ni tatizo tunasema. Tunajua pia mshkaji sasa hivi anatembelea chaki.

Umeenda pale imekua kama vile kila kitu unakiona hapo, siyo rafiki yako
 
au ni yeye mwenyewe
 
Nanukuu: " Ni kijana wa miaka 28,.......Hata hivyo, kwa sababu ambazo sikuwahi kujiuliza, hakufanikiwa kumaliza chuo kikuu, .... alinitambulisha kwa mtoto wake mdogo, ambaye pia anaishi naye hapo nyumbani. ...mtoto wake ni matokeo ya uhusiano wake ...na binamu yake, jambo ambalo linamletea changamoto nyingi. Pia alikiri kuwa alikuwa na tatizo la pombe ...... na maisha yake kwa sasa yamejikita nyumbani kwa wazazi wake."
Sasa vijana hebu jiulizeni: Je, mzazi hakuwahi kumuonya dhidi ya tabia na mwenendo wake tangu akiwa anakua, anaenda shuleni na kujiepusha na mambo ya wakubwa kabla ya wakati????
Wahenga alisemaga "Majuto ni mjukuu huja kinyume". Hapo kijana /rafiki yako anavuna alichopanda. Kijana ameharibika. Ni ngumu sana kumrekebisha kwani ilitakiwa Samaki mkunje akingali mbichi. Huyo ni mtu mzima ameshakomaa sana.
Mzazi/Mlezi labda alichelea au hakuzingatia "Spare the rod; spoil the child"
naye kwa wakati wake anavuna alichopanda kwa kijana wake huyo. Hakumsimamia kidete, hakuona umuhimu wa kutembeza kichapo kwa huyo kijana wake pale alipokuwa ana anza kuzembea au anapotoka au kutotii na ujeuri dhidi ya maelekezo kutoka kwake kama mzazi au mlezi (hilo ni kasoro iliyopo kwa wazazi wengi wa kisasa). Halafu hatujasikia lalamiko au kero kutoka kwa mama yake huyo kijana rafiki yako au mama hayupo?? na mambo yamekaaje -pengine mama ana mchango mkubwa sana kwenye hali iliyopo.
Hayo niliyobold ni kuonesha udhaifu uliokuwepo kwa kijana- rafiki yako.
 
Hiyo kijana anatakiwa apigwe na makonzi mbele ya wageni mpuuzi sana hiyo,amekaa nyumbani kwa babaye na mtoto wake halafu anatetewa na watu humu,halafu kazaa na binamu yake ambaye ni dada yake hiyo analeta laana kwenye familia
 
Nilimshauri ahame apange somewhere maana akiweza kumudu majukumu ya kodi basi hata mengine yataenda vizuri
 
Nilimshauri ahame apange somewhere maana akiweza kumudu majukumu ya kodi basi hata mengine yataenda vizuri
Kuhama ni sawa lakini nadhani angeenda kwa hatua kama ifuatavyo:
1. Amwombe sana msamaha mzazi/mlezi wake; ikibidi atafute hata mtu mzima wa kumsaidia. zingatia alifanya kosa kubwa sana kuzaa na binamu i.e. dada wa baba yake. It is a shame - unamwonesha baba yako kwamba ww bingwa unajua kuliwasha rungu??
2. Amwombe baba yake Mzazi mkopo ili akaanzie maisha mahali pengine - kupanga.
3. Asichague kazi. Kazi yoyote halali itakayomjia mbele yake yy afanye.
 
Haya ndiyo mashauri ya kumshauri mtu,siyo kumlaumu mzazi kwa ujinga wa mtoto,kongole sana ndugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…