Kwa mtaji wa milioni 12, nifungue hardware, nafaka au phone and accessories?

Kwa mtaji wa milioni 12, nifungue hardware, nafaka au phone and accessories?

Fungua kampuni brella, nenda sido chukua mashine za kutengeneza mikate skonzi na maandaz , tafuta vibali , omba tenda kama kampuni kwnye mashule na taasisi uanze kusambaza vitafuno, kwa kuanzia kodi kirikuu uanze kazi.
Hii biashara kuna mjomba wangu anafanya sasa hv ana matawi mikoa 3 na kila tawi kanunua gari ya kusambaza bidhaa.
 
Sijajua wewe familia yako unaiendeshaje mkuu, nimezaliwa kwenye familia ya biashara mzee wangu ana duka kubwa la nguo anatoa biadhaa zake Kenya au Uganda, anaesimama dukani ni Mama mzee yeye anasafiri jumatatu anarudi alhamis/ijumaa, kwahiyo mtu ambae anashida kwenye biashara ni Mama, na wamefanikiwa kwa kiasi chao na kumiliki asset nyingi tu hapo Mwanza, lakini kwa kipindi chote hicho tulipokua wadogo Mama alikua hawezi kutoa hata shilling 100 bila kumtaarifu mzee, hata tulipokua tunahitaji matumizi ya shule tulikua tunampigia simu mzee sio Mama, kwahiyo Mama ni kama msimamizi/mhasibu tu, sio kwamba nampa biashara Mwanamke alafu Mimi naenda kustarehe, biashara ni ya kwangu Mimi yeye anakua msimamizi kwa muda mchache tu nikitoka.
Huyo ni mke wa ndoa au hawara?

Unaposema biashara ni yako unamaanisha nini?
 
Sio
Biashara ya hardware ina faida lakini inahitaji mtaji mkubwa angalau milioni 30 ili lionekane vizuri,biashara ya mazao ina faida lakini inahitaji muda mwingi sana wa kusafiri kwenda mashambani ndanindani huko ni ngumu uwe unaenda kazini kila siku halafu upate muda wa kuingia mashambani inahitaji ukisafiri kwenda huko angalau ukae wiki moja kuyasoma mazingira,kukagua mzigo na kuikusanya ili kuisogeza maeneo ya mjini,hata kama utawatuma watu au mawakala huwezi ukawaamini moja kwa moja uwepo wako bado ni muhimu sana.
Na ukija kwenye biashara ya vifaa vya simu inamfaa muajiriwa ni rahisi kila siku jioni au mchana kwenda kuikagua akimaliza kazi lakini faida zake ni ndogondogo na inachukua muda mrefu sana kuurudisha mtaji au labda kama lengo lake ni kupata hela ndogondogo tu za kula.
Ndio maana kuna wadau kama wawili kule mwanzoni walicomment kwamba biashara nzuri ni zile ambazo unabuni huduma fulani ya kipekee ambayo haifanywi na mtu mwingine yeyote katika eneo lako hapo ndipo utaona mafanikio ya haraka ila sio hizi za kuigana,mimi niliwaelewa sana pointi zao.
Sio kweli,vifaa vya simu vina faida kubwa tu,mfano kioo cha simu tunajumua elfu20 lakin kuuza kawaida tu ni elfu35 mpaka elfu30
 
Huwezi kubuni biashara tofauti na hizo acheni ku kariri hizo faida zinajulikana na kila mtu anaweza kuifungua........
Ndiyo maana amewasilisha wazo lake, maono yako, kama yanaona tofauti, weka hapa mawazo yako, afanye nini.
Hii itatusaidia hata sisi ambao hatauliza, ila ukinga wazo lake bila kumpa wazo lingine, ni uongo.
 
Sio

Sio kweli,vifaa vya simu vina faida kubwa tu,mfano kioo cha simu tunajumua elfu20 lakin kuuza kawaida tu ni elfu35 mpaka elfu30
Bila shaka hujanielewa faida niliyoongelea hapo,sijamaanisha faida hiyo unayoipigia hesabu wewe.
Kwa mfano hapo umesema kioo unanunua elfu 20 na kuuza elfu 35 sawa sikukatalii lakini uliwahi kupiga hesabu mtu akinunua hicho kioo inachukua miezi mingapi au miaka mingapi hadi kipasuke ili aje kununua tena?utafananisha na biashara ya chakula ambayo kila mtu ni lazima ale kila siku atake asitake,kamwe haviwezi kuwa sawa.
 
Simply,
1. Join 1xbet,then deposit 10mil
2. Do analysis at least 1.70 odds for four games
3. Stake your bank

Only do this four only 3-4 times for one month, then you'll thanks me one day
 
Fungua kampuni yaku kusafirisha miili ya marehemu kwy mazishi kw gar maalum na mashine zakushusha jeneza, kw mikoani pia wawez kufany utafit kw kina . . . ~Pesa nying ipo hapa
 
Mkuu mi nakushauri kwa mkoa wa Kigoma kwa jinsi navyoujua biashara ya electronicsz na vifaa vya simu itakufaa. Pia ujitahidi uweke na vifaa vya SOLAR utapiga pesa.

Hapo Kigoma wanaouza electronics ni wachache kama watatu tu, WAZIRI ELECTRONICS, STAN ELECTRONICS na ZAHIR kule mjini. Kwahiyo ushauri wangu ni huo

Hardware huwa inahitaji vitu vingi na kwa mtaji huo sioni kama utakuwa na mzigo wa kuweza kuleta ushindani kwa wenzako walio kutangulia
 
Bila shaka hujanielewa faida niliyoongelea hapo,sijamaanisha faida hiyo unayoipigia hesabu wewe.
Kwa mfano hapo umesema kioo unanunua elfu 20 na kuuza elfu 35 sawa sikukatalii lakini uliwahi kupiga hesabu mtu akinunua hicho kioo inachukua miezi mingapi au miaka mingapi hadi kipasuke ili aje kununua tena?utafananisha na biashara ya chakula ambayo kila mtu ni lazima ale kila siku atake asitake,kamwe haviwezi kuwa sawa.
Mkuu kwa siku vinauzwa vioo zaidi ya 50 sasa sijajua unazungumzia sehem gan,ila kama ni mjini ana uhakika wa kuuza vioo vingi tu
 
Mkuu mi nakushauri kwa mkoa wa Kigoma kwa jinsi navyoujua biashara ya electronicsz na vifaa vya simu itakufaa. Pia ujitahidi uweke na vifaa vya SOLAR utapiga pesa.

Hapo Kigoma wanaouza electronics ni wachache kama watatu tu, WAZIRI ELECTRONICS, STAN ELECTRONICS na ZAHIR kule mjini. Kwahiyo ushauri wangu ni huo

Hardware huwa inahitaji vitu vingi na kwa mtaji huo sioni kama utakuwa na mzigo wa kuweza kuleta ushindani kwa wenzako walio kutangulia
Ni kweli kabisa
 
Sijajua wewe familia yako unaiendeshaje mkuu, nimezaliwa kwenye familia ya biashara mzee wangu ana duka kubwa la nguo anatoa biadhaa zake Kenya au Uganda, anaesimama dukani ni Mama mzee yeye anasafiri jumatatu anarudi alhamis/ijumaa, kwahiyo mtu ambae anashida kwenye biashara ni Mama, na wamefanikiwa kwa kiasi chao na kumiliki asset nyingi tu hapo Mwanza, lakini kwa kipindi chote hicho tulipokua wadogo Mama alikua hawezi kutoa hata shilling 100 bila kumtaarifu mzee, hata tulipokua tunahitaji matumizi ya shule tulikua tunampigia simu mzee sio Mama, kwahiyo Mama ni kama msimamizi/mhasibu tu, sio kwamba nampa biashara Mwanamke alafu Mimi naenda kustarehe, biashara ni ya kwangu Mimi yeye anakua msimamizi kwa muda mchache tu nikitoka.
Hao ni wanawake wa zamani, wa sasa ni mchwa!
 
Kosa lako ni kutaka mafanikio kupitia biashara lakini kazi hutaki kuacha, nakuhakikishia Mimi kuwa utumishi wa umma na kipato kikubwa ni mbingu na ardhi na mchawi muda na usimamizi kwa sababu unataka ukabidhi watu walifanyie kazi itakula kwako na huwezi kuwa mtumishi wakati huohuo kuwa mfanyabiashara angalau ungekuwa DC, DED, RC etc lakini kazi ya ualimu halafu unataka kutusua you should not be serious na kitakacho kuumiza ni uoga vinginevyo hiyo hela itapotea na hutaelewa imepoteaje kama unataka kufanya biashara chukua maamuzi ya kufa umesimama otherwise endelea kuishi umepiga magoti
Mawazo mgando sana haya. Watumishi kede wana biashara zao na zina wapa faida sana mjn
 
Back
Top Bottom