Kwa mtaji wa milioni 12, nifungue hardware, nafaka au phone and accessories?

Kwa mtaji wa milioni 12, nifungue hardware, nafaka au phone and accessories?

Wakuu, nipo hapa napambania kujikwamua kwenye umaskini, nipo nachakata mawazo kwa ajili ya kufanya harakati, wengi walianzia chini sana na wakafanikiwa kupata pesa nyingi.

Mawazo yangu niliyonayo ni Nafaka, vifaa vya simu pamoja na umeme, mwisho ni hardware,

Nafaka nilitaka nideal na maharage, mchele pamoja na nafaka nyingine means nazitoa porini nakuja kuziuza mjini, changamoto Mimi ni Mwalimu kwahiyo muda wa kuzunguka porini nakua nimekosa, makazi Kwa Sasa nipo kigoma.

Vifaa vya simu, kigoma huku naona vitu ni bei kubwa sana mfano USB ni 7000, earphone 5000 na vitu vingine, nikatamani niingie kwenye hii biashara kwa sababu machimbo kariakoo ya bei rahisi nayafahamu.

Vifaa vya ujenzi, hii ni hobby yangu, naipenda sana na watu wamepata pesa kweli, kigoma mfuko wa cement ni 26,000/= pamoja na vifaa vingine changamoto mji ni mdogo na competition ni kubwa, hapa kwenye hardware nilitaka nijichanganye kwwnye kununua machine ya uchomeleaji pamoja na aluminum.

Wakuu, lengo langu nipate faida ya laki 5 tu kwa mwezi.

Asanteni
mkuu hebu chomoa kwanza hata 5m ukatumie... maendo ya starehe ndipo utakapopata idea nzuri za biashara gani ufanye
 
Watu wakigoma wanasifika kwa ujanja ujanja wa Elimu Dunia,wakija mjini huku tunaona sifa zao, hustle,hela zao za moto,wewe umeenda kwao l,haitakua rahisi,but inawezekana,..

Usifikiri mtu wa dar au Mwanza atakupa idea itakayo work out kigoma,,wewe mwenyewe jipe muda tembea mji wote,usome kwa jicho la MTAFUTAJI,andika fursa tano tu ambazo umeziona Kigoma,andika mchanganuo, pick the best one,,

Mimi Kigoma nimefika,mji huo mgumu,jaribu kuuza HUDUMA,sio Merchandise
Yeah wewe unapajua kigoma, mji mgumu sana na ushirikina ni wakutisha, kati ya 100%, 99% wanaupractise uchawi nimeona kabisa mwenyewe, na wakati natafuta information mtu mmoja alinambia inabidi nijiweke vizuri pia kwenye hayo mambo, ndio wazo la nafaka likaingiaa maana nafaka ni need, kila mtu anataka ukiwa na nafaka nzuri plus ubora bei chini nauza tu.
 
Yeah wewe unapajua kigoma, mji mgumu sana na ushirikina ni wakutisha, kati ya 100%, 99% wanaupractise uchawi nimeona kabisa mwenyewe, na wakati natafuta information mtu mmoja alinambia inabidi nijiweke vizuri pia kwenye hayo mambo, ndio wazo la nafaka likaingiaa maana nafaka ni need, kila mtu anataka ukiwa na nafaka nzuri plus ubora bei chini nauza tu.
Nafaka haiwezi kukuangusha ila Faida ndogo sana,Wanasema biashara ambayo inatoka sana,Haina Faida kubwa...kwa vile huko tumeona watu wagumu sana,hujawahi kupata wazo la Kutoa huko Vitu kuleta Dar??Ushapata ABC za Tangawizi??
 
Nafaka haiwezi kukuangusha ila Faida ndogo sana,Wanasema biashara ambayo inatoka sana,Haina Faida kubwa...kwa vile huko tumeona watu wagumu sana,hujawahi kupata wazo la Kutoa huko Vitu kuleta Dar??Ushapata ABC za Tangawizi??
Tangawizi wanalima wilaya Moja inaitwa buhigwe, sijawahi kukaa kuwaza kuhusu tangawizi, maana ni biashara itakayonifanya nitafute mzigo na gari na kusafirisha kuja huko dar, mwanza n.k...
Ulivyosema ni ukweli, Mchele au nafaka kwa jumla inatoka sana lakini faida kidogo lakini hizo biashara zingine ukiupata mzunguko unatoa faster sema changamoto kama ulivyosema huku Watu wanaamini katika ushirikina sana.
 
Tangawizi wanalima wilaya Moja inaitwa buhigwe, sijawahi kukaa kuwaza kuhusu tangawizi, maana ni biashara itakayonifanya nitafute mzigo na gari na kusafirisha kuja huko dar, mwanza n.k...
Ulivyosema ni ukweli, Mchele au nafaka kwa jumla inatoka sana lakini faida kidogo lakini hizo biashara zingine ukiupata mzunguko unatoa faster sema changamoto kama ulivyosema huku Watu wanaamini katika ushirikina sana.
Tugusie nilichokwambia kwanza,kuhusu kuuza HUDUMA,wewe SI mwalimu,fikiria kitu kama Shule ya chekechea,kitu gani umeona kwenye miji mikubwa kipo but kwa Kigoma Bado hakijafika au watu Bado hawajaanza kuona kama kitu Cha maana?? Nail shop??duka la ice cream??
 
Nakazia hapa biashara yoyote au jambo au kitu au shughuli ya kuingiza kipato inahitaji usimamizi wa karibu Sana wa muhusika

Dunia ya sasahivi imekosa uaminifu kabisa na biashara au shughuli yoyote inahitaji uaminifu kwa mara ya Kwanza inapoanza

Risk taker ndo huwa wanafanikiwa Kwaiyo akitaka kufanikiwa ni lazima achukue maamuzi magumu otherwise atakua wa kawaida Sana
Kosa lako ni kutaka mafanikio kupitia biashara lakini kazi hutaki kuacha, nakuhakikishia Mimi kuwa utumishi wa umma na kipato kikubwa ni mbingu na ardhi na mchawi muda na usimamizi kwa sababu unataka ukabidhi watu walifanyie kazi itakula kwako na huwezi kuwa mtumishi wakati huohuo kuwa mfanyabiashara angalau ungekuwa DC, DED, RC etc lakini kazi ya halafu unataka kutusua you should not be serious na kitakacho kuumiza ni uoga vinginevyo hiyo hela itapotea na hutaelewa imepoteaje kama unataka kufanya biashara chukua maamuzi ya kufa umesimama otherwise endelea kuishi umepiga magoti
 
Biashara ya vifaa vya simu inataka usimamizi especially kama akiongeza na uwakala, alafu kwa hio capital bado ni ndogo kufanya uwakala akapata hela inayoeleweka. Hapa nazungumzia experience kabisa. Nafaka zina hela mzee, hio hela anai double chap sana. Maana gunia zinakuja na vipimo kama ni mahindi ni gunia za kg 128 na inajulikana bei zake.
Biashara ya hardware ina faida lakini inahitaji mtaji mkubwa angalau milioni 30 ili lionekane vizuri,biashara ya mazao ina faida lakini inahitaji muda mwingi sana wa kusafiri kwenda mashambani ndanindani huko ni ngumu uwe unaenda kazini kila siku halafu upate muda wa kuingia mashambani inahitaji ukisafiri kwenda huko angalau ukae wiki moja kuyasoma mazingira,kukagua mzigo na kuikusanya ili kuisogeza maeneo ya mjini,hata kama utawatuma watu au mawakala huwezi ukawaamini moja kwa moja uwepo wako bado ni muhimu sana.
Na ukija kwenye biashara ya vifaa vya simu inamfaa muajiriwa ni rahisi kila siku jioni au mchana kwenda kuikagua akimaliza kazi lakini faida zake ni ndogondogo na inachukua muda mrefu sana kuurudisha mtaji au labda kama lengo lake ni kupata hela ndogondogo tu za kula.
Ndio maana kuna wadau kama wawili kule mwanzoni walicomment kwamba biashara nzuri ni zile ambazo unabuni huduma fulani ya kipekee ambayo haifanywi na mtu mwingine yeyote katika eneo lako hapo ndipo utaona mafanikio ya haraka ila sio hizi za kuigana,mimi niliwaelewa sana pointi zao.
 
Tugusie nilichokwambia kwanza,kuhusu kuuza HUDUMA,wewe SI mwalimu,fikiria kitu kama Shule ya chekechea,kitu gani umeona kwenye miji mikubwa kipo but kwa Kigoma Bado hakijafika au watu Bado hawajaanza kuona kama kitu Cha maana?? Nail shop??duka la ice cream??
Yeah, nilipokua dsm niliona watu wakiwa na Banda special kwa ajili ya kuuzia juice (kama juice shop flani),maziwa n.k huku kigoma hakuna.
 
Biashara ya hardware ina faida lakini inahitaji mtaji mkubwa angalau milioni 30 ili lionekane vizuri,biashara ya mazao ina faida lakini inahitaji muda mwingi sana wa kusafiri kwenda mashambani ndanindani huko ni ngumu uwe unaenda kazini kila siku halafu upate muda wa kuingia mashambani inahitaji ukisafiri kwenda huko angalau ukae wiki moja kuyasoma mazingira,kukagua mzigo na kuikusanya ili kuisogeza maeneo ya mjini,hata kama utawatuma watu au mawakala huwezi ukawaamini moja kwa moja uwepo wako bado ni muhimu sana.
Na ukija kwenye biashara ya vifaa vya simu inamfaa muajiriwa ni rahisi kila siku jioni au mchana kwenda kuikagua akimaliza kazi lakini faida zake ni ndogondogo na inachukua muda mrefu sana kuurudisha mtaji au labda kama lengo lake ni kupata hela ndogondogo tu za kula.
Ndio maana kuna wadau kama wawili kule mwanzoni walicomment kwamba biashara nzuri ni zile ambazo unabuni huduma fulani ya kipekee ambayo haifanywi na mtu mwingine yeyote katika eneo lako hapo ndipo utaona mafanikio ya haraka ila sio hizi za kuigana,mimi niliwaelewa sana pointi zao.
Yeah ni kweli mzee, hata Forest Hill amegusia hapo, lakini sidhani kama Kuna biashara mpya, biashara nyingi zipo tayari Mimi nadhani kikubwa ni kujua unataka uifanyaje
 
Nafaka haiwezi kukuangusha ila Faida ndogo sana,Wanasema biashara ambayo inatoka sana,Haina Faida kubwa...kwa vile huko tumeona watu wagumu sana,hujawahi kupata wazo la Kutoa huko Vitu kuleta Dar??Ushapata ABC za Tangawizi??

Nafaka Faida ndogo, pia kuna swala moja watu wenye mitaji mikubwa huwezi kushinda nao.
 
Back
Top Bottom