Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]kuna kampuni moja ha kukopesha.sasa hivi hawakopeshi wanasubiri walipwe Kwanza.
Na kila siku wanafungua ofisi ila hela ya kukopesha HAWANA ZOTE ZIPO KWA RAIA
Katika biashara kichaa ni ya kumkopesha mmbongo! Bora mkopeshane kwa dhamana ya mali ambayo ukiiuza unàrudisha chako mfano aweke bond simu 😁 hapo atalipa ila kwa maneno matupu tu eti tumekubaliana hivi!

Tena na kukuita msumbufu atakuita mbele za watu,,,utaskia "Eh bana huyu mxng msumbufu kweli yani ef 10 anapijapija simu kila saa 😂!" Lipa deni uone kama utasumbuliwa 😝
 
Katika biashara kichaa ni ya kumkopesha mmbongo! Bora mkopeshane kwa dhamana ya mali ambayo ukiiuza unàrudisha chako mfano aweke bond simu 😁 hapo atalipa ila kwa maneno matupu tu eti tumekubaliana hivi!

Tena na kukuita msumbufu atakuita mbele za watu,,,utaskia "Eh bana huyu mxng msumbufu kweli yani ef 10 anapijapija simu kila saa 😂!" Lipa deni uone kama utasumbuliwa 😝
Mimi kumkopesha mtu aweke Bondi tuu ili awe anakumbuka kua Kuna hela ya watu anayo na anatakiwa kuilipa sio mtu unamkopesha alafu anasahau kua anadaiwa
 
Mimi kumkopesha mtu aweke Bondi tuu ili awe anakumbuka kua Kuna hela ya watu anayo na anatakiwa kuilipa sio mtu unamkopesha alafu anasahau kua anadaiwa
Hahah tena ya kitu muhimu ambacho hawez kubali kukipoteza. Unampa na grace period kabisa akifeli unasebenza. Uone kama hatapambana aje kukomboa haraka 😂
 
Hahah tena ya kitu muhimu ambacho hawez kubali kukipoteza. Unampa na grace period kabisa akifeli unasebenza. Uone kama hatapambana aje kukomboa haraka 😂
lazima atairudisha ndani ya Muda husika kwasababu inamuuma,sio mtu unamtafuta wewe Kama wewe ndo mwenye shida bana
 
Mkuu ungekuwa karibu tungejoin tufanye collable mana zile 5000+ zimeota mbawa🤣🤣🤣
 
Habar wapenzi msaada tutani Nina mtaji

wa Million 1 , naomba idea za biashara

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Wakuu nipo kimara Dar es Salaam
Nahitaji kufanya biashara ili niweze kukuza mtaji, je nifanye biashara gani?
 
Dah, huwa tunatofautiana sana, huu ujasiri wa kuuliza idea ya biashara baada ya kupata mtaji huwa mnaupata wapi wakuu, wengine plan zipo za miaka 10 mbele na kila hatua na strategies zake kufikia lengo kuu na hakuna pesa itakayoingia ikose pa kwenda au ndio ianze kutafuta pa kwenda.

Idea za bishara za ndoto zangu huwa naandika hatakama sina hata mia na nimeshindia uji ila siachi kuandika idea za biashara.

Mkuu hapa utapata idea nyingi, uza nguo na viatu vya kike, fungua genge la matunda na mbogamboga, tafuta computer used ufungue biashara ya kuweka nyimbo na movie, tafuta eneo zuri choma mishkaki na mengine pia

Tatizo huwa linakuja.

1. Utayari wako (moyo wako utaridhia na hiyo biashara kiasi kwamba hata ukipata hasara hutojilaumu?)

2. Uelewa wa kutosha kuhusu biashara husika (lazima kuna muda wa kutenga kupata dondoo muhimu za biashara husika na hapa usipotilia maanani lazima utakula hasara).

3. Pesa yako kweli ni ya mtaji au umekusanya na ukaamua iwe mtaji kwakuwa unaona inaweza kupotea tu bila kufanyia chochote cha maana? Hiyo pesa unaweza itunza mwezi mzima ukifanya research ya biashara utakayoipenda au ndiyo ile pesa ya matumizi ndani ikiisha huwezi lala njaa huku una laki 7 ndani ?? Ukipata emergency yoyote utakuwa mwepesi kuitoa hiyo pesa ?.

Najaribu tu kuonyesha namna gani ilivyo muhimu kuwa na mpango mzima kabla hata hujapata pesa ya kutekeleza mpango huo ili pesa ikiingia tu basi hushajua wapi inaenda. Pesa haikai mkuu.

Vuta subira ila jitahidi ufanye utafiti wa kutosha kuhusu biashara utakayoamua kuifanya kabla ya kuanza ili ukiingia ukubaliane na matokeo yoyote kiroho safi kabisa.
 
Laki 8 ni nyingi sana kama unajicho pevu la tatu la kuziona fursa,binafsi nishaanzaga na mtaji wa Tsh40000(elfu arubain tu) right now nina ROI ya 7m kama faida every two weeks ni ngumu kuamini but thats it..anyway nisikuchoshe

Tafuta washing machine with dry cleaning system, used atleast ichukue kwa 400000 Huna haja ya kununu liquid soap you can make it by your own at your home.

Huna haja ya kukodi frem..tafuts eneo lavwazo hapo nyumbani kwako au chumba cha wazi
Tafuta hosteli na vyuo vyenye mkusanyiko wa watu wengi maeneo ya karibu yako..bandika ads kwamba unafua na kupasi nguo za wanafunzi na watu wengine kwa bei nafuu na ofa maalumu plus nguo za aina yoyote..lets say unafua na kupasi T-shirt na jeans kwa 2500 each@1250 plus ofa ya kufua boxer na vest/sidiria na chupi bure kwa mhusika mmoja..

400000 ivunje kama ifuatavyo: toa 50000 nunua baiskeli toa 100000 ingia mkataba wa miezi mitano kwanza na kijana mdogo kutoka uswekeni ambaye hana ajira wa kumlipa 20000 kila mwezi plus allowance ya 500 kwa kila complete order anayoileta(ya 2500)..mpe baiskel kwaajili ya kuchukua na kurudisha order za watu.huyu kijana usisahau kumpa motisha za malazi chakula na matibabu.
Imebaki 250000:Ivunje kama ifuatavyo

Toa 50000 nunua pasi na perfumes mbili moja ya kike na moja ya kiume(perfume ni mbwembwe tu kwa wateja wako)
Toa 30000 nunua enga za bei rahisi au tafuta muuza mitumba akuelekeze material ya kununua kwa ajili kutengeneza enga za gharama nafuu..hizi enga zitumike kutudukia na kudeliver nguo za watu..ila zisibaki kwa wateja.

Toa 30000 tengeneza kijikabti au sanduku nyuma ya ile baiskeli kwaajili ya kucollect na kudeliver order za watu.
Imebaki 140000 toa 50000 ingia mkataba na muuza maji wa karibu yako kuchukua dumu tatu kwa hesabu ya 750 kila siku za kazi kwa muda wa miez miwili..NB:Kama una'access na maji ya bure hii ni salama yako

Imebaki 90000 toa 40000 kwaajili ya kununua liquid soap materials pamoja na jiki material ya kutengeneza jiki nyumbani..
Imebaki 50000 toa 35000 iweke iwe pesa ya kulipia gharama za umeme kwa kipindi cha atleast mwezi mmoja na nusu..na 15000 kwaajili ya yale mabandiko ya printed white paper kama matangazo NB:inabidi wewe na yule kijana muwe nembo muhimu ya kuitangaza biashara yenu msitegemee mabandiko tu.

Kilichobaki ni kuanza kazi na kusubiri mvua ya wateja itakayo kuwa ikimiminika hapo ulipo..
Zingatia huduma nzuri kwa wateja wako.Na pia zingatia ulichowekeza na utakachokuwa ukikipata kama faida...pia zingatia ghatama nafuu kwakila huduma ya kuzisafisha nguo za wateja wao..lengo ni kuwa'outstand major dry cleaning franchises na kuprovide huduma kama yao ila kwa bei nafuu..Zaidi ya hapo SEE YOU AT THE TOP..WISHING YOU ALL THE BEST 😉
Mkuu PM namba yako ya WHAT'SAPP please [emoji120][emoji120], nna maswali mawili mafupi... thanks
 
Back
Top Bottom