Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Fanya Biashara ya kununua na kuuza nguo za ndani za, na hasa zile za bei za kawaida za kike na kiume wakubwa na watoto kutoka Dar kariakoo.
Dukani kwetu Tunauza bidhaa hizo kwa Jumla Kwa kuanzia Nusu Dozen.
Na tuna saidia kutuma mzigo wako Popote tanzania.
Wasiliana nasi kwa ushauri zaidi kwa whatsapp/simu #0743207176
JPEG_20210328_091710_1191237941.jpg
 
Ndugu zangu JF nikiwa na mtaji wa shilingi laki 3, ni biashara gani naweza kuifanya kwa hapa Dar es salaam?
 
Ndugu zangu JF nikiwa na mtaji wa shilingi laki 3, ni biashara gani naweza kuifanya kwa hapa Dar es salaam?
Wewe unadhani ni biashara gani unaweza kufanya? Je una mipango gani na ni eneo gani unatarajia kuanzia biashara? Nani walengwa wa biashara hiyo? Je unao uzoefu wowote? Je umefanya utafiti wowote? Nini malengo yako ya muda mfupi na muda mrefu mwanangu? Hebu tuanzie hapa.
 
Wewe unadhani ni biashara gani unaweza kufanya? Je una mipango gani na ni eneo gani unatarajia kuanzia biashara? Nani walengwa wa biashara hiyo? Je unao uzoefu wowote? Je umefanya utafiti wowote? Nini malengo yako ya muda mfupi na muda mrefu mwanangu? Hebu tuanzie hapa.
Shkrani mno, una nafasi yako peponi, naamini nikipata majibu ya maswali hayo, nitakuwa nipo biasharani tayri[emoji120]
 
Dah, huwa tunatofautiana sana, huu ujasiri wa kuuliza idea ya biashara baada ya kupata mtaji huwa mnaupata wapi wakuu, wengine plan zipo za miaka 10 mbele na kila hatua na strategies zake kufikia lengo kuu na hakuna pesa itakayoingia ikose pa kwenda au ndio ianze kutafuta pa kwenda.

Idea za bishara za ndoto zangu huwa naandika hatakama sina hata mia na nimeshindia uji ila siachi kuandika idea za biashara.

Mkuu hapa utapata idea nyingi, uza nguo na viatu vya kike, fungua genge la matunda na mbogamboga, tafuta computer used ufungue biashara ya kuweka nyimbo na movie, tafuta eneo zuri choma mishkaki na mengine pia

Tatizo huwa linakuja.

1. Utayari wako (moyo wako utaridhia na hiyo biashara kiasi kwamba hata ukipata hasara hutojilaumu?)

2. Uelewa wa kutosha kuhusu biashara husika (lazima kuna muda wa kutenga kupata dondoo muhimu za biashara husika na hapa usipotilia maanani lazima utakula hasara).

3. Pesa yako kweli ni ya mtaji au umekusanya na ukaamua iwe mtaji kwakuwa unaona inaweza kupotea tu bila kufanyia chochote cha maana? Hiyo pesa unaweza itunza mwezi mzima ukifanya research ya biashara utakayoipenda au ndiyo ile pesa ya matumizi ndani ikiisha huwezi lala njaa huku una laki 7 ndani ?? Ukipata emergency yoyote utakuwa mwepesi kuitoa hiyo pesa ?.

Najaribu tu kuonyesha namna gani ilivyo muhimu kuwa na mpango mzima kabla hata hujapata pesa ya kutekeleza mpango huo ili pesa ikiingia tu basi hushajua wapi inaenda. Pesa haikai mkuu.

Vuta subira ila jitahidi ufanye utafiti wa kutosha kuhusu biashara utakayoamua kuifanya kabla ya kuanza ili ukiingia ukubaliane na matokeo yoyote kiroho safi kabisa.
[emoji110] safii kijana
 
Mwana,chukua beli moja la mtumba jeans za kiume. Chambua nzuri weka pembeni.zinazobaki piga mnada hata kwa buku buku hata jero.matambala yanayobaki yakatekate wauzie wenye gereji kwa mafungu.

Zile nzuri ulizopata kwa kua upo arusha zipeleke migodini kwa wana aporo uza moja moja.piga ka miezi 2 halafu urudi hapa useme imekuaje.

kwa hapa dar beli zuri unaweza pata kwa tsh160000/-.mia
Zinapatikana maeneo gani kiongozi???
 
Kopesha watu hapo hapo ulipo weka na riba ya elf mbili kila baada ya siku saba.
10,000×10+2000×10=120,000 kwa siku saba. ila jipange mkuu.
Nimefanya hii biashara ya kukopesha. Inahitaji ukopeshe watu waaminifu hasa tena hakikisha wana miji yao.

hakikisha unakopesha 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐰𝐚𝐤𝐞, hawa wengi wao wana hofu na mikopo

toka nianze kukopesha sijawahi pigwa

kwa kila elfu kumi, unarudisha 13,000 baada ya wiki 2.
 
Habarini ndugu zangu, nilikuwa naomba nisaidiwe msaada wa kimawazo ya biashara kutoka kwenu ndugu zangu.

Hapa nilipo nina kiasi cha shilingi laki moja na nusu, so nilikuwa naomba msaada wa Wazo la biashara ambalo litaweza kufit kutokana na hiki kiasi cha pesa nilichonacho.
 
Wazo lolote utakalo lipata linaweza kukulipa lakini kwa kiasi cha mtaji ambacho umejaliwa kwa sasa nadhani unahitaji sana subra kupita wazo la kibiashara.

Najua wazo la kibiashara unalo tayari labda unaweza ukawa uamini kama ni wazo sahihi.Kikubwa ili wadau waweze kuwa wa msaada kwako jaribu kuwaeleza kwa uzuri hiyo biashara yako unataka iwe maeneo yapi? if possible eleza social profile yako(sio lazima) nasema hivi kwa sababu mtu anaweza akakwambia anza kuuza karanga kumbe mwenzetu unavitabu vyako vingi kichwani kwahiyo ukawa unapata ugumu uanze vipi hiyo kazi.

Kuhusu eneo ni muhimu sana kueleza kwa sababu jambo ambalo mtu atakwambia linalipa Dodoma linaweza lisikupe faida ukiwa Morogoro
 
Habarini ndugu zangu, nilikuwa naomba nisaidiwe msaada wa kimawazo ya biashara kutoka kwenu ndugu zangu
Hapa nilipo nina kiasi cha shilingi laki moja na nusu, so nilikuwa naomba msaada wa Wazo la biashara ambalo litaweza kufit kutokana na hiki kiasi cha pesa nilichonacho
Hapo unapoishi angalia Kama wauza mkaa wapo wangap Kama wachache unga teller au chukua mihogo na miguu shingo filigisi kaanga uza Kama una Brenda kipind Cha joto hichi tengeneza na juice uza
 
Nina mtaji wa laki 9 nataka kuanzisha biashara. kwa mchanganuo naombeni ushauri wenu ni biashara gani ambayo naweza fanya kwa mtaji huo? Nipo Dar na sijapanga
Tafuta bucha Anza kuuza utumbo nunua kabat refu la kioo mizan ndogo nenda machinjion nunua utumbo njoo omba eneo mbele ya bucha uza kg ya utumbo elf 4 had 5 Kaz kwako
 
Back
Top Bottom