Kwa nini kuupinga Mkataba wa Bandari inaitwa "udini" lakini kuunga mkono sio udini?

Kwa nini kuupinga Mkataba wa Bandari inaitwa "udini" lakini kuunga mkono sio udini?

Usipoteze nguvu na akili zako kumtetea mtu mweusi yule ni mtumwa na masikini watu weusi wote wanaopinga mkataba ni wanafiki kwani zikitangazwa nafasi za kazi dp world wataomba kazi sisi watu weusi nimesha gundua tunapenda utumwa na umasikini pamoja na kutawaliwa

Bandari ibinafsishwe kwa waarabu maisha yaendelee usimuonee huruma mtu mweusi acha ateseke
 
Hayawezi kuisha hadi mkataba wa bandari ufutwe au urekebishwe.

Kwenye waraka wa TEC kuna
kipengele kimezungumzia dini?
Wao tec ni watu wa dini tayari
Tanzania yetu haihitaji wadini wa aina yeyote kusukuma serikali kwa kuwa dini ya taifa ni katiba yetu ya jamhuri haiendeshwi kwa ukristo wala uislamu yeyote atakayepanda kwenye majukwaa ya siasa na afanye hivyo baada ya kustaafu uongozi wa dini la sivyo sheria na kanuni za jamhuri zisimamiwe ki sawa sawa dhidi ya wale wanaochezea tunu zetu suala la umoja na ustawi wa taifa sio la kucheka cheka na watu hata kidogo , leo wakianza tec kesho kutwa watakuja wale wa kujitoa mhanga tutajenga taifa gani sasa.
 
KWA NINI KUUPINGA MKATABA WA BANDARI INAITWA "UDINI" LAKINI KUUNGA MKONO SIO UDINI? MSIWE WAPUMBAVU.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Wanasiasa moja ya mambo yanayowashushia heshima ni kigeugeu na unafiki wao.
Wanasiasa wakisifiwa na viongozi wa dini hawasemi dini imeingizwa kwenye Siasa lakini wakikosolewe hapo utasikia Dini imeingizwa kwenye Siasa.

Wanasiasa wakitaka kuombewa na viongozi wa dini hiyo hawaiti dini imeingizwa kwenye Siasa. Wao wanataka tuu Sifa na utukufu Kutoka Kwa dini lakini wakikosolewa na kupondwa hapo wanaleta shida.

Tabia hiyo ya hovyo na kinafiki imekomaa Sana katika Nchi yetu. Na sasa tupo kwenye sakata la mkataba WA Bandari.

Viongozi wa dini waliosifia mkataba huu wao hawaambiwi kuwa ni UDINI. Lakini wanaoukosoa wanaambiwa ni udini. Hivi tutaacha lini huo upumbavu.

Kwa nini tusiangalie hoja ya msingi. Huo mkataba kama ni mbovu Kwa nini usibadilishwe? Kama kweli nia ni yakweli ya kutetea maslahi ya nchi. Kwa nini huo mkataba usiboreshwe vifungu vyenye utata?

Kujitetea kwa kujificha kwenye kichaka cha udini hakutabadili Jambo lolote.

Hekima na busara zitumike, kama kweli lengo ni kulinda maslahi ya Taifa letu na maslahi ya Watu wetu na rasilimali zetu.
Mtu akipinga Jambo kama anahoja ya msingi lazima asikilizwe.

kwanza hizo dini zenyewe tumeletewa.
pili, tupo watanzania wengi ambao hatuamini Kati hizo dini zenu za kigeni. Ingawaje tunawatambua na kuheshimu wanaoziamini.
Sasa msitake kuzifanya hizo dini zenu zinaumuhimu kuliko taifa letu.

Mnapojadiliana ishu za taifa msijifanye mnajificha kwenye udini. Oooh! Yule Mkristo ndio maana anakosoa. Lakini akisifia huwezi sikia Jambo Hilo.
Angalieni kinachokosolewa, je kina uhalali wa kukosolewa? Kama jibu ni ndio,basi fanyieni maboresho.

Uwe Mkristo au muislam, uwe wakabila gani, uwe Mtibeli kama Mimi au mpagani. Kwetu haina maana yoyote Ile. Tunachotaka ni kulinda maslahi ya nchi yetu na sio genge Fulani la Watu. Ni lazima tuangalie kizazi chetu kilichopo na kinachokuja.
Dini yako, au Cheo chako au mamlaka yako haina maana yoyote kwetu ikiwa unataka kuliingiza taifa katika hasara na ubinafsi wa hovyo.

Acheni upumbavu! Mtu akitoa hoja isikilizwe hoja yake na sio ni wadini gani.

Kama mkataba haufai, urekebishwe. Hiyo ndio hoja. Mambo ya sijui Amani, sijui mgawanyiko, hayo yote yataletwa na watu wabinafsi na wasiotaka kusikiliza wengine.
Mgawanyiko ni muhimu ikiwa tunatofautiana. Hiyo iwekwe wazi. Kama Watu hawataki wawe wamoja, kujaribu kuwaunganisha Watu wasiofanana ndio ukosefu wa Amani, mitafaruku, unyanyasaji na ukatili. Hatuwezi lazimisha umoja wa kinyonyaji, umoja wa wengine wanafaidi wengine wanasota, huo umoja haupogo labda kinafiki.

Nisikilizeni, umoja unaletwa Kwa kuangalia wengi wanasema nini, lakini pia Kwa kuzingatia maslahi ya taifa na kizazi kijacho.

Upendo, Haki, Ukweli na Akili hiyo ndio namna ya kuwaweka Watu pamoja. Utibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kuunga mkono ukandamizaji siyo udini

Kuwatetea wanaokandamizwa ndo udini wenyewe🤣
 
Wao tec ni watu wa dini tayari
Tanzania yetu haihitaji wadini wa aina yeyote kusukuma serikali kwa kuwa dini ya taifa ni katiba yetu ya jamhuri haiendeshwi kwa ukristo wala uislamu yeyote atakayepanda kwenye majukwaa ya siasa na afanye hivyo baada ya kustaafu uongozi wa dini la sivyo sheria na kanuni za jamhuri zisimamiwe ki sawa sawa dhidi ya wale wanaochezea tunu zetu suala la umoja na ustawi wa taifa sio la kucheka cheka na watu hata kidogo , leo wakianza tec kesho kutwa watakuja wale wa kujitoa mhanga tutajenga taifa gani sasa.
Katiba ambayo ndio dini yetu leo inavunjwa hadharani.
Tusimame kuitetea bila kuangalia dini wala kabila au jinsia
 
Katiba ambayo ndio dini yetu leo inavunjwa hadharani.
Tusimame kuitetea bila kuangalia dini wala kabila au jinsia
Ikivunjwa mahakama ndio sehemu sahihi ya kutafsiri hayo ila sio kwenye majukwaa ya taasisi za kidini.
 
Screenshot_20230820-222828_(1).png
 
Hebu tutafakari katika hii vuta ni kuvute:
[emoji117]Hawa jamaa na wenyewe ni majangili tu hebu tafakari tunachangiaga ujenzi wa hospitals, shule na vyuo vya kanisa ila gharama zao za ada zipo juu na sio rafiki kwa muumini wa hali ya chini kamwe huwezi tibiwa.

[emoji117]Na katika hili la bandari jamaa siwana ingizaga vitu nchini kupitia bandari na hawakatwagi kodi wala ushuru wowote na kuna baadhi viongozi wajanja wajanja wa kanisa wanatumia mwanya huu kupiga dili kibao kwa mgongo wa kanisa.
[emoji120]
Hawa waliingiza tende na halua!!??
JamiiForums-419861776.jpg
 
Kwa Rais Mstaafu @jmkikwete na mnaosema Baraza La Maaskofu wana chuki za kidini. Naombeni mnieleweshe:

[emoji3578]Baraza hili la maakofu (TEC) mwaka 2018 lilipotoa waraka wa Pasaka wa kupinga mauaji na utekaji wa watu uliofanywa na Serikali ya Jiwe walikua na vhuki ya Kidini na 'Mkatoliki' Mwenzao Magufuli?

[emoji3578]Mmesahau Askofu Severine Niwemuguzi alinyang’anywa Passport na kuambiwa sio raia kwa sababu ya kupinga uonevu wa
Jiwe, alikua na chuki na Mkatoliki mwenzake?

[emoji3578]Wakati wa COVID Baraza La Maaskofu lilipotoa waraka wa kumpinga Magufuli kuwa COVID haipo na kutaka serikali iruhusu watu wapewe chanjo, walikua na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Walivyo kemea madudu ya uchaguzi wa 2020 walikuwa na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Kama kila wakati kukiwa na mjadala wa kitaifa wanatoa Waraka, na hamkuwai kuona shida, kwanini mnataka sasa wasitoe?

[emoji3578]Kwahiyo wakitoa kwa Mkristo mwenzao sio chuki? Wakitoa sasa kwa Muislam ndio wana chuki?
Na hapo ndipo mnapojifichia, wajingawajinga wanatekwa hapo. Ni lini ziliingiliwa mbinu za kiuchumi za huyo jiwe wako na wengineo?!!! Wanazunguka huko na kujifanya kuililia demokrasia ili kuwafumba macho msione mamia ya mikataba ya kinyonyaji ya madini kwa wazungu. Mkapa ametawanya rasilimali kibaaao za nchi na hadi anamaliza hakupewa waraka. Jiwe hivyo hivyo. Kwanini mbinu za kiuchumi zinaonekana kuingiliwa pale tu kiongozi anayedhaniwa kuwa muislamu akiingia madarakani?!!!

Uchumi ndo kila kitu, wakifanikiwa kukudhibiti katika uchumi basi uongozi wako umekwisha.......ndo wanalolifanya hilo na ndipo hapo hisia za kidini zinapoibuka, hakuna pengine!!!
 
Ikivunjwa mahakama ndio sehemu sahihi ya kutafsiri hayo ila sio kwenye majukwaa ya taasisi za kidini.
Haya, wewe nenda mahakamani sisi tutaongelea popote cha msingi tunaitetea katiba ifuatwe.
Katiba hiyo hiyo ndio inayowaongoza hadi maaskofu na masheikh.
Na kuongelea katiba ni kuzungumzia sheria mama za nchi, sio siasa.

Ndio maana kila mTZ anapaswa aisome na kuielewa katiba ya nchi yake. Imependekezwa humu mara nyingi katiba ifundishwe kuanzia darasa la tatu.
Kuijadili katiba sio siasa bali ni uzalendo
 
This is really pathetic!

Sheikh Mussa Juma amesema Wapinzani na Maaskofu wanaomsaka Rais Samia Suluhu Hassan hawana shukrani wanaendekeza Udini na maslahi yao binafsi nakusahau hisani waliyowafanyia kipindi walipokuwa hawana kitu.

Akizungumza huko visiwani Zanzibar katika mawaidha Sheikh Mussa Juma amesema Rais Samia ni kiongozi wenye huruma na uadilifu ndani yake hivyo wanaomsakama wanafanya hivyo kwa maslahi yao binafsi.

"Hapa kwetu ndio kabisa madudu haya ya kisiasa sijui wakina Mbowe kina Lissu waliyoyaficha ndani ya mioyo yao yalikuwa ni makubwa zaidi kuliko wanayoyadhihirisha, angalia sasa hivi wanavyotapika maneno yale angalia ni udini tu ule, kama huyo Dkt. Slaa yeye ndio kamaliza mchezo mmemsikia mwenyewe Udini tu ule hakuna kitu kingine Udini tu..sasa yale ndio yaliyokuwa yamejificha hawana shukrani hata kidogo" alisema

Sheikh Mussa Juma amesema Rais Samia ni mtu mwenye imani wanaomuanda wanapaswa kumshukuru na kumheshimu kutokana nakuwafanyia hisani kwa kuwarejeshea vitu vyao walivyopoteza kipindi cha awamu ya Tano.

"Alikuwepo Magufuli kawanyongesha watu, kawaadhibu watu, kawatesa watu hawana hatia wamenyamaza kimya, Mwenyezi Mungu kafanya Rehema zake katuletea mtu ana imani watu wanaishi kwa raha , watu wanapendana, wanasaidiana, mnyonge anasaidiwa leo hawa wakina Mbowe, Lissu hawana Shukrani mtu kama huyo alowafanyia hisani kama huyu Lissu alipofanyiwa mambo mazito mtu wa kwanza kwenda kumtizama ni Rais Samia wale waliobakia wote maaskofu ambao sasa hivi ndio wanamtukana Samia kwa sababu ya uislamu hakuna kingine na maslahi yao waliyokuwa wanaipata kwenye ile bandari wanamsaka hawana shukrani wote hao maaskofu walikuwa wameufyata wanamuogopa Magufuli , lakini tazama alichomfanya Rais Samia kamlipa kila kitu chake kamrejeshea ambavyo alikuwa kanyang'anywa na huyo Mbowe hivyo hivyo kila kitu chake karejeshewa kalipwa pesa chungu mzima ambazo zingewasaidia wananchi , Rais Samia anaonyesha huruma kwa rai wake alafu hawa wanakuja juu wanamtukana na kumkashifu kwa maslahi yetu wenyewe sisi wananchi lakini kwa sababu wao kuna maslahi yao ya dini pale wanahisi atakuja kuondoka , pamoja na maslahi yao walikuwa wanapitisha vitu pale...." alisema Sheikh huyo

Pamoja na yote Sheikh Mussa dunia ilipofikia sasa mambo mema yanaonekana mabaya huku mabaya yakionekana mema hata hivyo amemuomba Rais Samia aendelee kuishi maisha marefu kutokana na uadilifu na huruma alionao katika uongozi wake.

"Mbona mambo sasa hivi yanaanza kuchimbuka yaliyokuwa yamejificha na sisi ndio tunayasubiri kwa hamu kwa sababu tulipokuwa tunasema nyinyi mlituona sisi wabaya lakini sasa hivi Mwenyezi Mungu anayachimbua, mmemsikia Slaa alivyosema nyie waislamu mmekaa tu mmemsikia na uislamu wenu mnasikia wanavyomfanyia muislamu mwenzenu wanavyomwandama, wanaranda kwenye mikoa kwa kutumia pesa hizi hizi wanazopewa zetu wenyewe kama rai wanamsakama Mhe. Rais Samia lakini Mwenyezi Mungu atamuhifadhi, atamlinda na shari zao ataendeleza uadilifu, ni Rais pekee aliyekuwa hana mfano na waliyokuwa wamepita mwenye huruma mpaka na vilema tunamuombea dua na tutazidi kumuombea sasa kama wewe unanuna nuna"_ Sheikh Mussa Juma akizungumza msikitini Zanzibar
20230821_110454.jpg
 
Kwa Rais Mstaafu @jmkikwete na mnaosema Baraza La Maaskofu wana chuki za kidini. Naombeni mnieleweshe:

[emoji3578]Baraza hili la maakofu (TEC) mwaka 2018 lilipotoa waraka wa Pasaka wa kupinga mauaji na utekaji wa watu uliofanywa na Serikali ya Jiwe walikua na vhuki ya Kidini na 'Mkatoliki' Mwenzao Magufuli?

[emoji3578]Mmesahau Askofu Severine Niwemuguzi alinyang’anywa Passport na kuambiwa sio raia kwa sababu ya kupinga uonevu wa
Jiwe, alikua na chuki na Mkatoliki mwenzake?

[emoji3578]Wakati wa COVID Baraza La Maaskofu lilipotoa waraka wa kumpinga Magufuli kuwa COVID haipo na kutaka serikali iruhusu watu wapewe chanjo, walikua na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Walivyo kemea madudu ya uchaguzi wa 2020 walikuwa na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Kama kila wakati kukiwa na mjadala wa kitaifa wanatoa Waraka, na hamkuwai kuona shida, kwanini mnataka sasa wasitoe?

[emoji3578]Kwahiyo wakitoa kwa Mkristo mwenzao sio chuki? Wakitoa sasa kwa Muislam ndio wana chuki?
Umeona tofauti apo
 
Hebu tutafakari katika hii vuta ni kuvute:
👉Hawa jamaa na wenyewe ni majangili tu hebu tafakari tunachangiaga ujenzi wa hospitals, shule na vyuo vya kanisa ila gharama zao za ada zipo juu na sio rafiki kwa muumini wa hali ya chini kamwe huwezi tibiwa.

👉Na katika hili la bandari jamaa siwana ingizaga vitu nchini kupitia bandari na hawakatwagi kodi wala ushuru wowote na kuna baadhi viongozi wajanja wajanja wa kanisa wanatumia mwanya huu kupiga dili kibao kwa mgongo wa kanisa.
🙏
Hapo mkuu hata kama utachukulia kanisa kuwa nyuma ya katika huo upingaji wao wa huo mkataba wa bandari ni kwa masilahi yao binafsi ila hiyo ni kwa sababu wameona upenyo, kwa maana waliyokosoa huo mkataba ni watu aina tofauti tofauti na makundi mbalimbali hivyo nao wamepitia humo humo na si kwamba Kanisa tu pekee ndio limeupinga huo mkataba. Hivyo muhimu kuangalia hoja tu na jambo kubwa ni watu kutaka baadhi ya vifungu virekebishwe ndio hoja yenye nguvu kuliko hao wasioutaka kabisa huo uwekezaji.

Hata hao masheikh wanaotetea huu uwekezaji na waarabu nao nyuma yao utakuta pengine kuna masilahi binafsi yasio ya kitaifa, ndio maana nasema muhimu kuangalia uzito wa hoja tu.
 
Tuwekee siasa aside,ila nchi yangu imezidi unafki ambao hata hawayani kama mbwa na mbuzi wanatushangaa.
Ni hivi karibuni nimeanza kusikia mfulilizo wa matangazo ya bandari redioni.
I can't recall tangu nazaliwa kama nlishawahi sikia matangazo ya bandari yetu hii isipokuwa siku mbili tatu hizi.Mara oooh bandari yetu fahari yetu mara lango la Africa mashariki.

Sijawahi ona ufanisi kama huu katika kuitangaza bandari yetu redion utadhani ni kampuni ya vodacoma (like we don't know the harbour exist.)

Wakuu hivi waarabu washaanza kazi?
 
Kukemea ufisadi wa CCM ni udini!!!!!!!! Ukisifia ufisadi wa CCM siyo udini!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Amkeni watanganyika!!! Amkeniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii,wezi haooooooooooooooooooooooooooooo, shetani amevaaaaaa bukta ameingia msambweni!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hebu tutafakari katika hii vuta ni kuvute:
👉Hawa jamaa na wenyewe ni majangili tu hebu tafakari tunachangiaga ujenzi wa hospitals, shule na vyuo vya kanisa ila gharama zao za ada zipo juu na sio rafiki kwa muumini wa hali ya chini kamwe huwezi tibiwa.

👉Na katika hili la bandari jamaa siwana ingizaga vitu nchini kupitia bandari na hawakatwagi kodi wala ushuru wowote na kuna baadhi viongozi wajanja wajanja wa kanisa wanatumia mwanya huu kupiga dili kibao kwa mgongo wa kanisa.
🙏
Misamaha ya kodi kwa Taasisi na watu mbalimbali umeainishwa katika sheria ya kodi sio hisani. Swala la dili lipo tu kila mahali inategemea na uadilifu wa wahusika.
 
Back
Top Bottom