Kwa nini kuupinga Mkataba wa Bandari inaitwa "udini" lakini kuunga mkono sio udini?

Kwa nini kuupinga Mkataba wa Bandari inaitwa "udini" lakini kuunga mkono sio udini?

Kwa Rais Mstaafu @jmkikwete na mnaosema Baraza La Maaskofu wana chuki za kidini. Naombeni mnieleweshe:

[emoji3578]Baraza hili la maakofu (TEC) mwaka 2018 lilipotoa waraka wa Pasaka wa kupinga mauaji na utekaji wa watu uliofanywa na Serikali ya Jiwe walikua na vhuki ya Kidini na 'Mkatoliki' Mwenzao Magufuli?

[emoji3578]Mmesahau Askofu Severine Niwemuguzi alinyang’anywa Passport na kuambiwa sio raia kwa sababu ya kupinga uonevu wa
Jiwe, alikua na chuki na Mkatoliki mwenzake?

[emoji3578]Wakati wa COVID Baraza La Maaskofu lilipotoa waraka wa kumpinga Magufuli kuwa COVID haipo na kutaka serikali iruhusu watu wapewe chanjo, walikua na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Walivyo kemea madudu ya uchaguzi wa 2020 walikuwa na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Kama kila wakati kukiwa na mjadala wa kitaifa wanatoa Waraka, na hamkuwai kuona shida, kwanini mnataka sasa wasitoe?

[emoji3578]Kwahiyo wakitoa kwa Mkristo mwenzao sio chuki? Wakitoa sasa kwa Muislam ndio wana chuki?
Tatizo elimu ndogo na inferiority complex
 
Udini tu unawasumbua hii nchi haina dini hili taifa letu wote ni kitu kimoja kama wanasiasa wameridhiana wamereconcile basi tusubirie uchaguzi ujao watapata tume huru kwa kuwa Tanzania ni yetu sote haijalishi uwe mpinzani au nani na pia hekima ya kushauri ni kukubali pia ushauri wako ukikataliwa kwa kuwa unayemshauri anahiari ya kukubali au kukataa au atachagua mwenyewe lini atekeleze ila sio kumuwekea presha za kisiasa na kidini hapo ndio ukosefu wa hekima unaingia mwisho kabisa ndugu yangu rafiki yangu hii nchi imetoka kuwa tegemezi kwa asilimia kubwa sana toka huko kwenye bajeti ya kutegemea donor kwa kiwango kikubwa hadi sasa ambapo bajeti inautegemezi wa chini ya 30% hii yote ni kutokana na kazi nzuri ya uwekezaji na ubinfasishaji uliochangia pato la taifa kuongezeka kuanzia kwa Mwinyi, Mkapa ,JK , Magufuli na sasa Samia tena huyu ataweka historia ya kufuta utegemezi kabisa,sasa kwa nini mradi kama huu wa bandari uwekezaji huu utatutoa kabisa ktk utegemezi na kuwa na bajeti ambayo tutajisupport wenyewe 100% why not , hapo ndio emotions tupa kule maslahi ya uhuru wa kiuchumi kwanza, waswahili wanasema baniani mbaya kiatu chake dawa.
Wewe unasema tutapata wakati mkataba unasema hatupati, tutapataje na kutoka wapi. Umeusoma au unakariri yanayosemwa kwenye majukwaa?
 
Kwa Rais Mstaafu @jmkikwete na mnaosema Baraza La Maaskofu wana chuki za kidini. Naombeni mnieleweshe:

[emoji3578]Baraza hili la maakofu (TEC) mwaka 2018 lilipotoa waraka wa Pasaka wa kupinga mauaji na utekaji wa watu uliofanywa na Serikali ya Jiwe walikua na vhuki ya Kidini na 'Mkatoliki' Mwenzao Magufuli?

[emoji3578]Mmesahau Askofu Severine Niwemuguzi alinyang’anywa Passport na kuambiwa sio raia kwa sababu ya kupinga uonevu wa
Jiwe, alikua na chuki na Mkatoliki mwenzake?

[emoji3578]Wakati wa COVID Baraza La Maaskofu lilipotoa waraka wa kumpinga Magufuli kuwa COVID haipo na kutaka serikali iruhusu watu wapewe chanjo, walikua na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Walivyo kemea madudu ya uchaguzi wa 2020 walikuwa na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Kama kila wakati kukiwa na mjadala wa kitaifa wanatoa Waraka, na hamkuwai kuona shida, kwanini mnataka sasa wasitoe?

[emoji3578]Kwahiyo wakitoa kwa Mkristo mwenzao sio chuki? Wakitoa sasa kwa Muislam ndio wana chuki?
Walio wengi husahau ya jana., na walio wengi niwavivu wa kusoma., watu hawa ni rahis sana kuwapotosha. Maana huamini kutoka kwa mtu aliyesoma nakuwasimlia wasiopenda kusoma, nao huyachukua kama yalivyo nakuanza kutembea nayo., daima akili yakuambiwa CHANGANYA NAZAKWAKO.
 
KWA NINI KUUPINGA MKATABA WA BANDARI INAITWA "UDINI" LAKINI KUUNGA MKONO SIO UDINI? MSIWE WAPUMBAVU.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Wanasiasa moja ya mambo yanayowashushia heshima ni kigeugeu na unafiki wao. Wanasiasa wakisifiwa na viongozi wa dini hawasemi dini imeingizwa kwenye Siasa lakini wakikosolewe hapo utasikia Dini imeingizwa kwenye Siasa.

Wanasiasa wakitaka kuombewa na viongozi wa dini hiyo hawaiti dini imeingizwa kwenye Siasa. Wao wanataka tuu Sifa na utukufu Kutoka Kwa dini lakini wakikosolewa na kupondwa hapo wanaleta shida.

Tabia hiyo ya hovyo na kinafiki imekomaa Sana katika Nchi yetu. Na sasa tupo kwenye sakata la mkataba WA Bandari.

Viongozi wa dini waliosifia mkataba huu wao hawaambiwi kuwa ni UDINI. Lakini wanaoukosoa wanaambiwa ni udini. Hivi tutaacha lini huo upumbavu.

Kwa nini tusiangalie hoja ya msingi. Huo mkataba kama ni mbovu Kwa nini usibadilishwe? Kama kweli nia ni yakweli ya kutetea maslahi ya nchi. Kwa nini huo mkataba usiboreshwe vifungu vyenye utata?

Kujitetea kwa kujificha kwenye kichaka cha udini hakutabadili Jambo lolote.

Hekima na busara zitumike, kama kweli lengo ni kulinda maslahi ya Taifa letu na maslahi ya Watu wetu na rasilimali zetu. Mtu akipinga Jambo kama anahoja ya msingi lazima asikilizwe.

Kwanza hizo dini zenyewe tumeletewa. Pili, tupo watanzania wengi ambao hatuamini Kati hizo dini zenu za kigeni. Ingawaje tunawatambua na kuheshimu wanaoziamini. Sasa msitake kuzifanya hizo dini zenu zinaumuhimu kuliko taifa letu.

Mnapojadiliana ishu za taifa msijifanye mnajificha kwenye udini. Oooh! Yule Mkristo ndio maana anakosoa. Lakini akisifia huwezi sikia Jambo Hilo. Angalieni kinachokosolewa, je kina uhalali wa kukosolewa? Kama jibu ni ndio,basi fanyieni maboresho.

Uwe Mkristo au muislam, uwe wakabila gani, uwe Mtibeli kama Mimi au mpagani. Kwetu haina maana yoyote Ile. Tunachotaka ni kulinda maslahi ya nchi yetu na sio genge Fulani la Watu. Ni lazima tuangalie kizazi chetu kilichopo na kinachokuja.

Dini yako, au Cheo chako au mamlaka yako haina maana yoyote kwetu ikiwa unataka kuliingiza taifa katika hasara na ubinafsi wa hovyo.

Acheni upumbavu! Mtu akitoa hoja isikilizwe hoja yake na sio ni wadini gani. Kama mkataba haufai, urekebishwe. Hiyo ndio hoja. Mambo ya sijui Amani, sijui mgawanyiko, hayo yote yataletwa na watu wabinafsi na wasiotaka kusikiliza wengine.

Mgawanyiko ni muhimu ikiwa tunatofautiana. Hiyo iwekwe wazi. Kama Watu hawataki wawe wamoja, kujaribu kuwaunganisha Watu wasiofanana ndio ukosefu wa Amani, mitafaruku, unyanyasaji na ukatili. Hatuwezi lazimisha umoja wa kinyonyaji, umoja wa wengine wanafaidi wengine wanasota, huo umoja haupogo labda kinafiki.

Nisikilizeni, umoja unaletwa Kwa kuangalia wengi wanasema nini, lakini pia Kwa kuzingatia maslahi ya taifa na kizazi kijacho.

Upendo, Haki, Ukweli na Akili hiyo ndio namna ya kuwaweka Watu pamoja. Utibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
ccm ndio wapumbafu wanaangalia jana na sio kesho
 
Wewe unasema tutapata wakati mkataba unasema hatupati, tutapataje na kutoka wapi. Umeusoma au unakariri yanayosemwa kwenye majukwaa?
Kwa hio wewe ndio una akili nyingi kuwazidi watu wote wale yaani wao hawana uchungu kabisa hembu tuwape watu utulivu wafanyie kazi maoni yenu kadiri watakavyoona inafaa na kulifanyia kazi njema taifa letu na pia feedback si mtaiona kazi zikianza na wao pia ni watanzania na wanandugu watoto jamaa ,wajukuu pia na kizazi kitakachoendelea kuishi ktk taifa hili.
 
Hebu tutafakari katika hii vuta ni kuvute:
[emoji117]Hawa jamaa na wenyewe ni majangili tu hebu tafakari tunachangiaga ujenzi wa hospitals, shule na vyuo vya kanisa ila gharama zao za ada zipo juu na sio rafiki kwa muumini wa hali ya chini kamwe huwezi tibiwa.

[emoji117]Na katika hili la bandari jamaa siwana ingizaga vitu nchini kupitia bandari na hawakatwagi kodi wala ushuru wowote na kuna baadhi viongozi wajanja wajanja wa kanisa wanatumia mwanya huu kupiga dili kibao kwa mgongo wa kanisa.
[emoji120]
Hujalazimishwa kuchangia, michango ya kanisa sio kama kodi za serikali.
 
S
Kwa hio wewe ndio una akili nyingi kuwazidi watu wote wale yaani wao hawana uchungu kabisa hembu tuwape watu utulivu wafanyie kazi maoni yenu kadiri watakavyoona inafaa na kulifanyia kazi njema taifa letu na pia feedback si mtaiona kazi zikianza na wao pia ni watanzania na wanandugu watoto jamaa ,wajukuu pia na kizazi kitakachoendelea kuishi ktk taifa hili.
Sawa lakini si kwa masharti haya.
 
KWA NINI KUUPINGA MKATABA WA BANDARI INAITWA "UDINI" LAKINI KUUNGA MKONO SIO UDINI? MSIWE WAPUMBAVU.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Wanasiasa moja ya mambo yanayowashushia heshima ni kigeugeu na unafiki wao. Wanasiasa wakisifiwa na viongozi wa dini hawasemi dini imeingizwa kwenye Siasa lakini wakikosolewe hapo utasikia Dini imeingizwa kwenye Siasa.

Wanasiasa wakitaka kuombewa na viongozi wa dini hiyo hawaiti dini imeingizwa kwenye Siasa. Wao wanataka tuu Sifa na utukufu Kutoka Kwa dini lakini wakikosolewa na kupondwa hapo wanaleta shida.

Tabia hiyo ya hovyo na kinafiki imekomaa Sana katika Nchi yetu. Na sasa tupo kwenye sakata la mkataba WA Bandari.

Viongozi wa dini waliosifia mkataba huu wao hawaambiwi kuwa ni UDINI. Lakini wanaoukosoa wanaambiwa ni udini. Hivi tutaacha lini huo upumbavu.

Kwa nini tusiangalie hoja ya msingi. Huo mkataba kama ni mbovu Kwa nini usibadilishwe? Kama kweli nia ni yakweli ya kutetea maslahi ya nchi. Kwa nini huo mkataba usiboreshwe vifungu vyenye utata?

Kujitetea kwa kujificha kwenye kichaka cha udini hakutabadili Jambo lolote.

Hekima na busara zitumike, kama kweli lengo ni kulinda maslahi ya Taifa letu na maslahi ya Watu wetu na rasilimali zetu. Mtu akipinga Jambo kama anahoja ya msingi lazima asikilizwe.

Kwanza hizo dini zenyewe tumeletewa. Pili, tupo watanzania wengi ambao hatuamini Kati hizo dini zenu za kigeni. Ingawaje tunawatambua na kuheshimu wanaoziamini. Sasa msitake kuzifanya hizo dini zenu zinaumuhimu kuliko taifa letu.

Mnapojadiliana ishu za taifa msijifanye mnajificha kwenye udini. Oooh! Yule Mkristo ndio maana anakosoa. Lakini akisifia huwezi sikia Jambo Hilo. Angalieni kinachokosolewa, je kina uhalali wa kukosolewa? Kama jibu ni ndio,basi fanyieni maboresho.

Uwe Mkristo au muislam, uwe wakabila gani, uwe Mtibeli kama Mimi au mpagani. Kwetu haina maana yoyote Ile. Tunachotaka ni kulinda maslahi ya nchi yetu na sio genge Fulani la Watu. Ni lazima tuangalie kizazi chetu kilichopo na kinachokuja.

Dini yako, au Cheo chako au mamlaka yako haina maana yoyote kwetu ikiwa unataka kuliingiza taifa katika hasara na ubinafsi wa hovyo.

Acheni upumbavu! Mtu akitoa hoja isikilizwe hoja yake na sio ni wadini gani. Kama mkataba haufai, urekebishwe. Hiyo ndio hoja. Mambo ya sijui Amani, sijui mgawanyiko, hayo yote yataletwa na watu wabinafsi na wasiotaka kusikiliza wengine.

Mgawanyiko ni muhimu ikiwa tunatofautiana. Hiyo iwekwe wazi. Kama Watu hawataki wawe wamoja, kujaribu kuwaunganisha Watu wasiofanana ndio ukosefu wa Amani, mitafaruku, unyanyasaji na ukatili. Hatuwezi lazimisha umoja wa kinyonyaji, umoja wa wengine wanafaidi wengine wanasota, huo umoja haupogo labda kinafiki.

Nisikilizeni, umoja unaletwa Kwa kuangalia wengi wanasema nini, lakini pia Kwa kuzingatia maslahi ya taifa na kizazi kijacho.

Upendo, Haki, Ukweli na Akili hiyo ndio namna ya kuwaweka Watu pamoja. Utibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Usisahau kwamba imeanza kuitwa ni kosa la uhaini, kisha uchochezi na sasa udini, itaenda ukabila, ukanda na itikadi
 
S

Sawa lakini si kwa masharti haya.
Yasitutishe hakuna kisichozungumzika ktk ulimwengu huu tuwape nafasi bila kufanya hivyo tunapoteza muda wa kusonga mbele mwishowe tunakosa vyote sasa inakuwa hakuna hata lengo la kupiga makelele , maana hata mbwa unampigia kelele yenye malengo mfano kamata yule anakamata ila sasa ikiwa zogo huku na kule anashindwa ashike wapi, basi yanakuwa makelele tu yasiyokuwa na maana mwishowe kutupeleka kubaya .
 
KWA NINI KUUPINGA MKATABA WA BANDARI INAITWA "UDINI" LAKINI KUUNGA MKONO SIO UDINI? MSIWE WAPUMBAVU.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Wanasiasa moja ya mambo yanayowashushia heshima ni kigeugeu na unafiki wao. Wanasiasa wakisifiwa na viongozi wa dini hawasemi dini imeingizwa kwenye Siasa lakini wakikosolewe hapo utasikia Dini imeingizwa kwenye Siasa.

Wanasiasa wakitaka kuombewa na viongozi wa dini hiyo hawaiti dini imeingizwa kwenye Siasa. Wao wanataka tuu Sifa na utukufu Kutoka Kwa dini lakini wakikosolewa na kupondwa hapo wanaleta shida.

Tabia hiyo ya hovyo na kinafiki imekomaa Sana katika Nchi yetu. Na sasa tupo kwenye sakata la mkataba WA Bandari.

Viongozi wa dini waliosifia mkataba huu wao hawaambiwi kuwa ni UDINI. Lakini wanaoukosoa wanaambiwa ni udini. Hivi tutaacha lini huo upumbavu.

Kwa nini tusiangalie hoja ya msingi. Huo mkataba kama ni mbovu Kwa nini usibadilishwe? Kama kweli nia ni yakweli ya kutetea maslahi ya nchi. Kwa nini huo mkataba usiboreshwe vifungu vyenye utata?

Kujitetea kwa kujificha kwenye kichaka cha udini hakutabadili Jambo lolote.

Hekima na busara zitumike, kama kweli lengo ni kulinda maslahi ya Taifa letu na maslahi ya Watu wetu na rasilimali zetu. Mtu akipinga Jambo kama anahoja ya msingi lazima asikilizwe.

Kwanza hizo dini zenyewe tumeletewa. Pili, tupo watanzania wengi ambao hatuamini Kati hizo dini zenu za kigeni. Ingawaje tunawatambua na kuheshimu wanaoziamini. Sasa msitake kuzifanya hizo dini zenu zinaumuhimu kuliko taifa letu.

Mnapojadiliana ishu za taifa msijifanye mnajificha kwenye udini. Oooh! Yule Mkristo ndio maana anakosoa. Lakini akisifia huwezi sikia Jambo Hilo. Angalieni kinachokosolewa, je kina uhalali wa kukosolewa? Kama jibu ni ndio,basi fanyieni maboresho.

Uwe Mkristo au muislam, uwe wakabila gani, uwe Mtibeli kama Mimi au mpagani. Kwetu haina maana yoyote Ile. Tunachotaka ni kulinda maslahi ya nchi yetu na sio genge Fulani la Watu. Ni lazima tuangalie kizazi chetu kilichopo na kinachokuja.

Dini yako, au Cheo chako au mamlaka yako haina maana yoyote kwetu ikiwa unataka kuliingiza taifa katika hasara na ubinafsi wa hovyo.

Acheni upumbavu! Mtu akitoa hoja isikilizwe hoja yake na sio ni wadini gani. Kama mkataba haufai, urekebishwe. Hiyo ndio hoja. Mambo ya sijui Amani, sijui mgawanyiko, hayo yote yataletwa na watu wabinafsi na wasiotaka kusikiliza wengine.

Mgawanyiko ni muhimu ikiwa tunatofautiana. Hiyo iwekwe wazi. Kama Watu hawataki wawe wamoja, kujaribu kuwaunganisha Watu wasiofanana ndio ukosefu wa Amani, mitafaruku, unyanyasaji na ukatili. Hatuwezi lazimisha umoja wa kinyonyaji, umoja wa wengine wanafaidi wengine wanasota, huo umoja haupogo labda kinafiki.

Nisikilizeni, umoja unaletwa Kwa kuangalia wengi wanasema nini, lakini pia Kwa kuzingatia maslahi ya taifa na kizazi kijacho.

Upendo, Haki, Ukweli na Akili hiyo ndio namna ya kuwaweka Watu pamoja. Utibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kikwete aliitwa na Cardinal Pengo "Chaguo la Mungu", akachekelea Wala hakumwambia Pengo anachanganya dini na siasa, lakini Waraka wa TEC umemtoa Mheshimiwa pangoni na kuwaambia TEC wanachanganya dini na siasa, hata hivyo, dini na siasa unazitenga vipi?
 
Kwa Rais Mstaafu @jmkikwete na mnaosema Baraza La Maaskofu wana chuki za kidini. Naombeni mnieleweshe:

[emoji3578]Baraza hili la maakofu (TEC) mwaka 2018 lilipotoa waraka wa Pasaka wa kupinga mauaji na utekaji wa watu uliofanywa na Serikali ya Jiwe walikua na vhuki ya Kidini na 'Mkatoliki' Mwenzao Magufuli?

[emoji3578]Mmesahau Askofu Severine Niwemuguzi alinyang’anywa Passport na kuambiwa sio raia kwa sababu ya kupinga uonevu wa
Jiwe, alikua na chuki na Mkatoliki mwenzake?

[emoji3578]Wakati wa COVID Baraza La Maaskofu lilipotoa waraka wa kumpinga Magufuli kuwa COVID haipo na kutaka serikali iruhusu watu wapewe chanjo, walikua na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Walivyo kemea madudu ya uchaguzi wa 2020 walikuwa na chuki za kidini na Magufuli Mkristo mwenzao?

[emoji3578]Kama kila wakati kukiwa na mjadala wa kitaifa wanatoa Waraka, na hamkuwai kuona shida, kwanini mnataka sasa wasitoe?

[emoji3578]Kwahiyo wakitoa kwa Mkristo mwenzao sio chuki? Wakitoa sasa kwa Muislam ndio wana chuki?
Umeongea point sana, Baraza la Maaskofu miaka yote hukemea maovu bila kujali anayeongoza ni nani, kazi ya viongozi wa dini ni kukemea maovu. Kwa Wakristo, Yohana mbatizaji alimkemea mtawala Herode kwa uovu wa kumuoa mke wa ndugu yake akakatwa kichwa, Yesu alikemea maovu hadharani mpaka akasulubiwa. Kwa Waislamu, Mtume Muhammad alipigana vita vingi vya Badr, Uhud, Khandak na Hunayn, je alichanganya dini na siasa? Viongozi wa dini wakemee uovu hadharani bila kujali nani anaongoza.
 
Ndio haya mambo yaishe sasa viongozi wa dini wabakie kwenye field zao ni hatari wao kuingia kwenye siasa na nyakati zinaonyesha hivyo kwa sasa tunahitaji serikali imara leo kesho na keshokutwa sisi na viongozi wa dini na waumini na waamini yetu ni kwenye sanduku la kura na kutoa maoni yetu tu ila sio kuiendesha serikali kwa rimoti na kupush agenda zenye maslahi na taasisi zetu.
Dini unazitenga vipi na siasa? Dini inahudumia watu, siasa inahudumia watu.
 
Kitu cya ajabu ni kwamba, waliolichukua jambo hili kulitoa kwenye majukwaa ya siasa na kulipeleka madhabahuni na kulifanya kuwa ni sehemu ya ibada yao na kulifanya kuwa ni kampeni ktk dini yao hadi kwenye ngazi ya familia, hao hao wenyewe ambao kutwa nzkma kwenye dini yao walifanya kuwa ndio gumzo wenyewe ndio wapo mbele kila siku kusema tusilifanye hili jambo kidini wakati huo wanazidi kuchapisha nakala kwa waumini wao na kuendelea na kampeni yao. Waliokaa kimnya, ndik sasa wamekuwa wabaya na wanasemwa kuwa wao ndio wadini.
 
Tunasema ni udini kwa sababu wapingaji wakubwa ni Wakristo, tena unajadiliwa Makanisani.
Na hata waliofungua kesi wote ni wagalatia, sio bahati mbaya. Hata Padri Slaa kaibuka sasa hv ni kwa sababu tu maslahinya kanisa lake yameguswa.

Tusidanganyanye zama hz, hapo issue ni UDINI TU
Wale waliopigiana simu na kumwita Magufuli mshamba ile haikuwa udini?Watu hao hao unakuja kuwapa tena vyeo
 
Kikwete aliitwa na Cardinal Pengo "Chaguo la Mungu", akachekelea Wala hakumwambia Pengo anachanganya dini na siasa, lakini Waraka wa TEC umemtoa Mheshimiwa pangoni na kuwaambia TEC wanachanganya dini na siasa, hata hivyo, dini na siasa unazitenga vipi?

Sifa ni tamu Mkuu
 
KWA NINI KUUPINGA MKATABA WA BANDARI INAITWA "UDINI" LAKINI KUUNGA MKONO SIO UDINI? MSIWE WAPUMBAVU.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Wanasiasa moja ya mambo yanayowashushia heshima ni kigeugeu na unafiki wao. Wanasiasa wakisifiwa na viongozi wa dini hawasemi dini imeingizwa kwenye Siasa lakini wakikosolewe hapo utasikia Dini imeingizwa kwenye Siasa.

Wanasiasa wakitaka kuombewa na viongozi wa dini hiyo hawaiti dini imeingizwa kwenye Siasa. Wao wanataka tuu Sifa na utukufu Kutoka Kwa dini lakini wakikosolewa na kupondwa hapo wanaleta shida.

Tabia hiyo ya hovyo na kinafiki imekomaa Sana katika Nchi yetu. Na sasa tupo kwenye sakata la mkataba WA Bandari.

Viongozi wa dini waliosifia mkataba huu wao hawaambiwi kuwa ni UDINI. Lakini wanaoukosoa wanaambiwa ni udini. Hivi tutaacha lini huo upumbavu.

Kwa nini tusiangalie hoja ya msingi. Huo mkataba kama ni mbovu Kwa nini usibadilishwe? Kama kweli nia ni yakweli ya kutetea maslahi ya nchi. Kwa nini huo mkataba usiboreshwe vifungu vyenye utata?

Kujitetea kwa kujificha kwenye kichaka cha udini hakutabadili Jambo lolote.

Hekima na busara zitumike, kama kweli lengo ni kulinda maslahi ya Taifa letu na maslahi ya Watu wetu na rasilimali zetu. Mtu akipinga Jambo kama anahoja ya msingi lazima asikilizwe.

Kwanza hizo dini zenyewe tumeletewa. Pili, tupo watanzania wengi ambao hatuamini Kati hizo dini zenu za kigeni. Ingawaje tunawatambua na kuheshimu wanaoziamini. Sasa msitake kuzifanya hizo dini zenu zinaumuhimu kuliko taifa letu.

Mnapojadiliana ishu za taifa msijifanye mnajificha kwenye udini. Oooh! Yule Mkristo ndio maana anakosoa. Lakini akisifia huwezi sikia Jambo Hilo. Angalieni kinachokosolewa, je kina uhalali wa kukosolewa? Kama jibu ni ndio,basi fanyieni maboresho.

Uwe Mkristo au muislam, uwe wakabila gani, uwe Mtibeli kama Mimi au mpagani. Kwetu haina maana yoyote Ile. Tunachotaka ni kulinda maslahi ya nchi yetu na sio genge Fulani la Watu. Ni lazima tuangalie kizazi chetu kilichopo na kinachokuja.

Dini yako, au Cheo chako au mamlaka yako haina maana yoyote kwetu ikiwa unataka kuliingiza taifa katika hasara na ubinafsi wa hovyo.

Acheni upumbavu! Mtu akitoa hoja isikilizwe hoja yake na sio ni wadini gani. Kama mkataba haufai, urekebishwe. Hiyo ndio hoja. Mambo ya sijui Amani, sijui mgawanyiko, hayo yote yataletwa na watu wabinafsi na wasiotaka kusikiliza wengine.

Mgawanyiko ni muhimu ikiwa tunatofautiana. Hiyo iwekwe wazi. Kama Watu hawataki wawe wamoja, kujaribu kuwaunganisha Watu wasiofanana ndio ukosefu wa Amani, mitafaruku, unyanyasaji na ukatili. Hatuwezi lazimisha umoja wa kinyonyaji, umoja wa wengine wanafaidi wengine wanasota, huo umoja haupogo labda kinafiki.

Nisikilizeni, umoja unaletwa Kwa kuangalia wengi wanasema nini, lakini pia Kwa kuzingatia maslahi ya taifa na kizazi kijacho.

Upendo, Haki, Ukweli na Akili hiyo ndio namna ya kuwaweka Watu pamoja. Utibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Jibu rahisi sana sio udini sababu unaunga mkono jambo la serikali, serikali ambayo Haina dini.

Kingine watu hawakatazwi kukosoa tatizo unakosoa kwa misingi gani ? Kwanini hufati utaratibu ? Kama kweli viongozi walipeleka mashauri yao kwa raisi, hao Wakatoliki (Vilaza) walitakiwa wasubiri na hivi ndio dini inataka. Kiherehere Chao Cha kusoma Waraka lengo lao ni nini ? Kuleta taharuki na wao kama nani kwenye nchi hii ?

Kingine kwanini walichanganya dini na siasa ? Yaani kwao wao wametumia dini kufanya siasa na harakati, hawana tofauti na Wanasiasa na Wanaharakati wengine.
 
Kikwete aliitwa na Cardinal Pengo "Chaguo la Mungu", akachekelea Wala hakumwambia Pengo anachanganya dini na siasa, lakini Waraka wa TEC umemtoa Mheshimiwa pangoni na kuwaambia TEC wanachanganya dini na siasa, hata hivyo, dini na siasa unazitenga vipi?
Hata wewe ni chagua la Mungu kwa kulifanya uishi.

Pili, kuitwa na kuambiwa jambo kwa siri kama kiongozi hii ndio namna nzuri na dini ndio inavyo taka. Ila kujitokeza na kutumia vifingu vya katika katika kivuli Cha siasa huku ni kuchanganya dini na siasa.

Kingine, kuandika uongo na kuwasemea wengine kwamba wanapinga mkataba, huu ni uzandiki na kuleta udini.
 
Hata wewe ni chagua la Mungu kwa kulifanya uishi.

Pili, kuitwa na kuambiwa jambo kwa siri kama kiongozi hii ndio namna nzuri na dini ndio inavyo taka. Ila kujitokeza na kutumia vifingu vya katika katika kivuli Cha siasa huku ni kuchanganya dini na siasa.

Kingine, kuandika uongo na kuwasemea wengine kwamba wanapinga mkataba, huu ni uzandiki na kuleta udini.
Lkn pia mwanzishi wa hiyo dhana ya udini na uzanzibar anafahamika, tuanzie hapo.
 
Back
Top Bottom