Kwa Rais huyu, CCM wana hali mbaya sana!

Kwa Rais huyu, CCM wana hali mbaya sana!

Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha malefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.

Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.
atika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.
Hata kikwete na magufuli mliwasema hivyo hivyo kwa hiyo hata akija mwingine mtamsema hivyohivyo
 
CCM wana wakati mno walisahahu kwamba vizazi cha leo ni tofauti na wale wa 1977. Chadema nao mmmh.
Swala si kizazi ni mtu kuingia mkataba mbovu. Nashangaa watu kila mara wanadai kizazi. Lakini kiukweli kizazi kilichopita ndo kulikuwa na misimamo haswa. Kumbuka Bunge lilivyokuwa moto enzi hata za chama kimoja.
Wabunge bila kuogopa walisimama na kudai Tanganyika. Leo watathubutu?

Wakati Loliondo inauzwa Waandishi wa habari kama akina Katabaro, Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema, alisimamia swala na kuandika ukweli hadi akauwawa kwa mazingira ya ajabu pale ofisini kwake mitaa ya mnazi mmoja.
Leo waandishi waandishi wanaotumia digital ndo kwanza wanausifia mkataba. Waandishi wa habari wamekuwa wa kujikomba hasa wa kizazi hiki.

Kuna watu walikuwa hawamuogopi Rais, ndani ya CCM akina Munasa Sabbi Munasa, huyu alikuwa akisema nami nachukua fomu ya kugombea Urais. Hakumwogopa Nyerere.

Zamani hakukuwa na uchawa. Vijana sikuhizi wamekuwa machawa. Hata kama jambo ni la kipumbavu wanashadadia. Hiyo miaka unayoisema upumbavu huu haukuwepo.

Zamani hakukuwa na muheshimiwa, watu walitumia neno ndugu, ati siku hizi uheshimiwa ndo umewekwa mbele watu wanalambwa miguu. Upuuzi huu haukuwepo.

Hivyo acheni kupondea kizazi cha zamani ukadhani watu walikuwa wajinga. Zamani watu tulifundishwa uzalendo. Tunakimbia mchakamchaka, nyimbo za uzalendo. Kwanza zamani tuliifaidi serikali sana.
Matibabu yalikuwa bure, kusoma bure hadi vitabu na madaftari wapewa skuli. Watu wa sekondari na chuo walisafirishwa na serikali wakati wa likizo kwenda na kurudi.

Ebu acheni kuwa mnataka kudharirisha miaka ya zamani mkadhani tulikuwa wajinga. Miaka hiyo kulikuwa na park, au garden karibu kila mkoa. Siku hizi mmejenga kila sehemu, mnauza tu maeneo Dar haina hata sehemu ya kupumlia.

Ebu acheni kuona watu wa zamani kama ndo walikuwa wajinga. Nambia hiyo zamani unayoiponda ulisikia kuna mikataba ya kipumbavu kama hii inayoingiwa leo? Ha ha ha, acheni kusema miaka ya zamani ukadhani watu walikuwa wajinga. Wanaopinga hiyo mikataba leo wote ndio hao wa zamani wanao waelimisha ninyi vijana wa miaka ya 90 na 2000.
 
Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha malefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.

Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, hujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kupiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa”.

Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.

Rais Samia amebandika mabango ya kujitangaza nchi nzima lakini kinyume chake watu wakiyaona wanaanza kuyatukana!

Sakata la kuwapa DP-World bandari zetu limekuwa ndio msumari wa mwisho katika kaburi lake la kisiasa baada ya tozo mbalimbali.

Ndani ya CCM wameanza kukubali kuwa hali ni mbaya sana mpaka wameamua kuanza ziara za “kuwatongoza” wananchi hasa wa kupato cha chini huku wakisema eti Rais hawezi “kuiuza” nchini.

Katika hali ya kutapatapa wameanza kutumia mbinu ya udini ili kugusa hisia za imani ya dini angalau kundi la watu lenye mlengo wa dini yake lianze kumuunga mkono hasa kundi la watu wa kipato cha chini ambalo halitaki hata kumsikia.

Kinachowashitua zaidi ndani ya CCM ni kuona kuwa juhudi zote za kuwaleta ndani ya utawala wake wapinzani hasa CHADEMA katika “dhana ya kujenga umoja” haijazaa matunda endelevu na badala yake wananchi wa kipato cha chini hawataki hata kumsikiliza achilia mbali kumuona.

Ukiwauliza wananchi wengi kama wanakumbukumbu ya jambo lolote ambalo Rais Samia amelifanya na hawawezi kumsahau watakuambia ni tozo na kugawa bure raslimali zetu za Taifa.

Hotuba zake husahaulika pindi anapomaliza kutoa hotuba. Nadhani hata mawaziri wake ukiwauliza baada ya baada ya hotuba yake wawawezi kukumbuka alichokisema! Garbage in, garbage out.

Historia nchini huonyesha kuwa Rais huanza kuchokwa na kuchukiwa katika kipindi cha pili cha utawala wake lakini Rais Samia imemchukua miaka miwili tu kuchukiwa na wananchi wengi.

Kwa jinsi hali ilivyo mbaya kuna uwezekano mkubwa Rais Samia akawa ni Rais wa kipindi kimoja katika historia ya Tanzania kwa sababu katika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.
Amka!!!

Nchi inazo Fursa nyingi sana za KIBIASHARA kaleta huyu Rais!

Hata Wafugaji wanauza Ng'ombe Nje ya Nchi siku hizi we unaleta masikhara wewe!

NFRA wananunua Mahindi kwa 850/= kwa kilo-Unataka Rais wa kukuogesha?

Kura zikipigwa kesho asubuhi Rais Samia ana 80%

Hapo bado Uchumi haujafunguka...mpk ifike 2025 hakutakuwa na haja ya Kampeni.

Tatizo moja watu ni Wavivu sana!!!

Pale KIA ndege zinapishana kutoka Ulaya...Royal Tour-Acha kabisa!!

Halafu siku hizi watalii ni Celebrities...

Andika kitu kama hiki mwakani mwezi kama huu!!

Utabadili mtizamo wako!


Tufanye kazi!!!
 
Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha malefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.

Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, hujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kupiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa”.

Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.

Rais Samia amebandika mabango ya kujitangaza nchi nzima lakini kinyume chake watu wakiyaona wanaanza kuyatukana!

Sakata la kuwapa DP-World bandari zetu limekuwa ndio msumari wa mwisho katika kaburi lake la kisiasa baada ya tozo mbalimbali.

Ndani ya CCM wameanza kukubali kuwa hali ni mbaya sana mpaka wameamua kuanza ziara za “kuwatongoza” wananchi hasa wa kupato cha chini huku wakisema eti Rais hawezi “kuiuza” nchini.

Katika hali ya kutapatapa wameanza kutumia mbinu ya udini ili kugusa hisia za imani ya dini angalau kundi la watu lenye mlengo wa dini yake lianze kumuunga mkono hasa kundi la watu wa kipato cha chini ambalo halitaki hata kumsikia.

Kinachowashitua zaidi ndani ya CCM ni kuona kuwa juhudi zote za kuwaleta ndani ya utawala wake wapinzani hasa CHADEMA katika “dhana ya kujenga umoja” haijazaa matunda endelevu na badala yake wananchi wa kipato cha chini hawataki hata kumsikiliza achilia mbali kumuona.

Ukiwauliza wananchi wengi kama wanakumbukumbu ya jambo lolote ambalo Rais Samia amelifanya na hawawezi kumsahau watakuambia ni tozo na kugawa bure raslimali zetu za Taifa.

Hotuba zake husahaulika pindi anapomaliza kutoa hotuba. Nadhani hata mawaziri wake ukiwauliza baada ya baada ya hotuba yake wawawezi kukumbuka alichokisema! Garbage in, garbage out.

Historia nchini huonyesha kuwa Rais huanza kuchokwa na kuchukiwa katika kipindi cha pili cha utawala wake lakini Rais Samia imemchukua miaka miwili tu kuchukiwa na wananchi wengi.

Kwa jinsi hali ilivyo mbaya kuna uwezekano mkubwa Rais Samia akawa ni Rais wa kipindi kimoja katika historia ya Tanzania kwa sababu katika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.
Hayo mabango ni akina nape na akina mwigulu waliyaweka ili kuweza kumfunika mtangulizi wake. .lakin ndo kwwnza amekuwa kituko
 
Amka!!!

Nchi inazo Fursa nyingi sana za KIBIASHARA kaleta huyu Rais!

Hata Wafugaji wanauza Ng'ombe Nje ya Nchi siku hizi we unaleta masikhara wewe!

NFRA wananunua Mahindi kwa 850/= kwa kilo-Unataka Rais wa kukuogesha?

Kura zikipigwa kesho asubuhi Rais Samia ana 80%

Hapo bado Uchumi haujafunguka...mpk ifike 2025 hakutakuwa na haja ya Kampeni.

Tatizo moja watu ni Wavivu sana!!!

Pale KIA ndege zinapishana kutoka Ulaya...Royal Tour-Acha kabisa!!

Halafu siku hizi watalii ni Celebrities...

Andika kitu kama hiki mwakani mwezi kama huu!!

Utabadili mtizamo wako!


Tufanye kazi!!!
Hiyo asilimia 80 tutaziona kwenye uchaguz wa serikali za mitaa
 
Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha malefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.

Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, hujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kupiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa”.

Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.

Rais Samia amebandika mabango ya kujitangaza nchi nzima lakini kinyume chake watu wakiyaona wanaanza kuyatukana!

Sakata la kuwapa DP-World bandari zetu limekuwa ndio msumari wa mwisho katika kaburi lake la kisiasa baada ya tozo mbalimbali.

Ndani ya CCM wameanza kukubali kuwa hali ni mbaya sana mpaka wameamua kuanza ziara za “kuwatongoza” wananchi hasa wa kupato cha chini huku wakisema eti Rais hawezi “kuiuza” nchini.

Katika hali ya kutapatapa wameanza kutumia mbinu ya udini ili kugusa hisia za imani ya dini angalau kundi la watu lenye mlengo wa dini yake lianze kumuunga mkono hasa kundi la watu wa kipato cha chini ambalo halitaki hata kumsikia.

Kinachowashitua zaidi ndani ya CCM ni kuona kuwa juhudi zote za kuwaleta ndani ya utawala wake wapinzani hasa CHADEMA katika “dhana ya kujenga umoja” haijazaa matunda endelevu na badala yake wananchi wa kipato cha chini hawataki hata kumsikiliza achilia mbali kumuona.

Ukiwauliza wananchi wengi kama wanakumbukumbu ya jambo lolote ambalo Rais Samia amelifanya na hawawezi kumsahau watakuambia ni tozo na kugawa bure raslimali zetu za Taifa.

Hotuba zake husahaulika pindi anapomaliza kutoa hotuba. Nadhani hata mawaziri wake ukiwauliza baada ya baada ya hotuba yake wawawezi kukumbuka alichokisema! Garbage in, garbage out.

Historia nchini huonyesha kuwa Rais huanza kuchokwa na kuchukiwa katika kipindi cha pili cha utawala wake lakini Rais Samia imemchukua miaka miwili tu kuchukiwa na wananchi wengi.

Kwa jinsi hali ilivyo mbaya kuna uwezekano mkubwa Rais Samia akawa ni Rais wa kipindi kimoja katika historia ya Tanzania kwa sababu katika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.
...You have solemnly swore to tell the truth, the whole truth, and nothing but the truth, and you will keep secret all of the proceedings of the grand jury conducted in your presence? So help you God.
 
Swala si kizazi ni mtu kuingia mkataba mbovu. Nashangaa watu kila mara wanadai kizazi. Lakini kiukweli kizazi kilichopita ndo kulikuwa na misimamo haswa. Kumbuka Bunge lilivyokuwa moto enzi hata za chama kimoja.
Wabunge bila kuogopa walisimama na kudai Tanganyika. Leo watathubutu?

Wakati Loliondo inauzwa Waandishi wa habari kama akina Katabaro, Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema, alisimamia swala na kuandika ukweli hadi akauwawa kwa mazingira ya ajabu pale ofisini kwake mitaa ya mnazi mmoja.
Leo waandishi waandishi wanaotumia digital ndo kwanza wanausifia mkataba. Waandishi wa habari wamekuwa wa kujikomba hasa wa kizazi hiki.

Kuna watu walikuwa hawamuogopi Rais, ndani ya CCM akina Munasa Sabbi Munasa, huyu alikuwa akisema nami nachukua fomu ya kugombea Urais. Hakumwogopa Nyerere.

Zamani hakukuwa na uchawa. Vijana sikuhizi wamekuwa machawa. Hata kama jambo ni la kipumbavu wanashadadia. Hiyo miaka unayoisema upumbavu huu haukuwepo.

Zamani hakukuwa na muheshimiwa, watu walitumia neno ndugu, ati siku hizi uheshimiwa ndo umewekwa mbele watu wanalambwa miguu. Upuuzi huu haukuwepo.

Hivyo acheni kupondea kizazi cha zamani ukadhani watu walikuwa wajinga. Zamani watu tulifundishwa uzalendo. Tunakimbia mchakamchaka, nyimbo za uzalendo. Kwanza zamani tuliifaidi serikali sana.
Matibabu yalikuwa bure, kusoma bure hadi vitabu na madaftari wapewa skuli. Watu wa sekondari na chuo walisafirishwa na serikali wakati wa likizo kwenda na kurudi.

Ebu acheni kuwa mnataka kudharirisha miaka ya zamani mkadhani tulikuwa wajinga. Miaka hiyo kulikuwa na park, au garden karibu kila mkoa. Siku hizi mmejenga kila sehemu, mnauza tu maeneo Dar haina hata sehemu ya kupumlia.

Ebu acheni kuona watu wa zamani kama ndo walikuwa wajinga. Nambia hiyo zamani unayoiponda ulisikia kuna mikataba ya kipumbavu kama hii inayoingiwa leo? Ha ha ha, acheni kusema miaka ya zamani ukadhani watu walikuwa wajinga. Wanaopinga hiyo mikataba leo wote ndio hao wa zamani wanao waelimisha ninyi vijana wa miaka ya 90 na 2000.
Shukrani kwa kutoa hoja yenye kina kirefu.

Nadhami uzalendo nchini umeanza kupungua baada ya kuingia kwenye siasa za mfumo wa vyama vingi na uchumi wa soko huria. Kwa sasa pesa zinatangulia katika uongozi
 
Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha malefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.

Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, hujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kupiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa”.

Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.

Rais Samia amebandika mabango ya kujitangaza nchi nzima lakini kinyume chake watu wakiyaona wanaanza kuyatukana!

Sakata la kuwapa DP-World bandari zetu limekuwa ndio msumari wa mwisho katika kaburi lake la kisiasa baada ya tozo mbalimbali.

Ndani ya CCM wameanza kukubali kuwa hali ni mbaya sana mpaka wameamua kuanza ziara za “kuwatongoza” wananchi hasa wa kupato cha chini huku wakisema eti Rais hawezi “kuiuza” nchini.

Katika hali ya kutapatapa wameanza kutumia mbinu ya udini ili kugusa hisia za imani ya dini angalau kundi la watu lenye mlengo wa dini yake lianze kumuunga mkono hasa kundi la watu wa kipato cha chini ambalo halitaki hata kumsikia.

Kinachowashitua zaidi ndani ya CCM ni kuona kuwa juhudi zote za kuwaleta ndani ya utawala wake wapinzani hasa CHADEMA katika “dhana ya kujenga umoja” haijazaa matunda endelevu na badala yake wananchi wa kipato cha chini hawataki hata kumsikiliza achilia mbali kumuona.

Ukiwauliza wananchi wengi kama wanakumbukumbu ya jambo lolote ambalo Rais Samia amelifanya na hawawezi kumsahau watakuambia ni tozo na kugawa bure raslimali zetu za Taifa.

Hotuba zake husahaulika pindi anapomaliza kutoa hotuba. Nadhani hata mawaziri wake ukiwauliza baada ya baada ya hotuba yake wawawezi kukumbuka alichokisema! Garbage in, garbage out.

Historia nchini huonyesha kuwa Rais huanza kuchokwa na kuchukiwa katika kipindi cha pili cha utawala wake lakini Rais Samia imemchukua miaka miwili tu kuchukiwa na wananchi wengi.

Kwa jinsi hali ilivyo mbaya kuna uwezekano mkubwa Rais Samia akawa ni Rais wa kipindi kimoja katika historia ya Tanzania kwa sababu katika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.
Tuna jamii mfu ambayo haiwezi kuhoji kwa sauti inayosikia yaani bora liende ama fuata mkumbo
 
Amka!!!

Nchi inazo Fursa nyingi sana za KIBIASHARA kaleta huyu Rais!

Hata Wafugaji wanauza Ng'ombe Nje ya Nchi siku hizi we unaleta masikhara wewe!

NFRA wananunua Mahindi kwa 850/= kwa kilo-Unataka Rais wa kukuogesha?

Kura zikipigwa kesho asubuhi Rais Samia ana 80%

Hapo bado Uchumi haujafunguka...mpk ifike 2025 hakutakuwa na haja ya Kampeni.

Tatizo moja watu ni Wavivu sana!!!

Pale KIA ndege zinapishana kutoka Ulaya...Royal Tour-Acha kabisa!!

Halafu siku hizi watalii ni Celebrities...

Andika kitu kama hiki mwakani mwezi kama huu!!

Utabadili mtizamo wako!


Tufanye kazi!!!
Mkuu, maelezo marefu halafu unahitimisha kwa kuwashutumu wananchi kuwa ni wavivu kama vile huwa unawalisha!

Hoja zako zimebeba fikra za tabaka aali katika jamii (elitist mentality). Ninyi ndio mnaowaona machinga ni wavivu na wachafu na kwa mantiki hiyo hawapaswi kuonekana katika miji na majiji.

Fursa ulidhorodhesha unadhani ni mpya wakati hata kabla ya uhuru zilikuwepo. kwani NFRA imeanzishwa na Rais Samia? Kwani lini mifugo ilikuwa haiuzwi nchi za nje?

Acha kuandika vichekesho!
 
Mkuu msemaji ukweli upo? Habari ya siku nyingi?

Samia sifa ya kua kiongozi hata wa nyumba 10 hana, lakini ajabu ndie rais wa Tanzania. Inawezekana kabisa huko sayari nyingine za Aliens wakitaka vituko ama vichekesho hua wanaangalia Tanzania.

Samia hana authoritative speech, hana commanding speach, hana convincing speech, hana chochote, hana.

Juzi akiwa kwao Zanzibar anasema mungu kampa mtihani mgumu sana hata hajui afanyeje, halafu anataka tena agombee 2025, unajiuliza kwani kalazimishwa, si aache ama ajiuzuru.

Rais Samia speech zake zimejaa maneno kama mkalitizame na hili, mkaliangalie na hili, hili pia litizamwe, hili liangaliwe, hili likafanyiwe kazi, hili lifikirieni. Unajiuliza anawaambia kina nani?

Nchi ina safari ndefu sana.
 
Kwa mara ya kwanza Tangu nikufahamu umeandika jambo la kweli , Hongera sana .
Nilisha msahau huyu kuwa aliwahi kuwepo hapa na zile makala zake za ajabu ajabu!

Sijui alipotelea wapi, na leo kaibuka na sura mpya kabisa!
 
Ilinichukua miezi mitano kufahamu kuwa Rais Samia hana maisha marefu ya kisiasa kwa sababu hana karama, kipaji na ujuzi wa uongozi.

Unaweza kuukataa ukweli lakini hata kama ukiukataa hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.

Mwl. Nyerere aliwahi kusema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana, haujali mkubwa wala mdogo, hujali adui wala rafiki. Kwake watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kupiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwapuuzwa”.

Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.

Rais Samia amebandika mabango ya kujitangaza nchi nzima lakini kinyume chake watu wakiyaona wanaanza kuyatukana!

Sakata la kuwapa DP-World bandari zetu limekuwa ndio msumari wa mwisho katika kaburi lake la kisiasa baada ya kuwabambikia wananchi tozo mbalimbali.

Ndani ya CCM wameanza kukubali kuwa hali ni mbaya sana mpaka wameamua kuanza ziara za “kuwatongoza” wananchi hasa wa kupato cha chini huku wakisema eti Rais hawezi “kuiuza” nchi.

Katika hali ya kutapatapa wameanza kutumia mbinu ya udini ili kugusa hisia za imani ya dini angalau kundi la watu lenye mlengo wa dini yake lianze kumuunga mkono hasa kundi la watu wa kipato cha chini ambalo halitaki hata kumsikia.

Kinachowashitua zaidi ndani ya CCM ni kuona kuwa juhudi zote za kuwaleta ndani ya utawala wake wapinzani hasa CHADEMA katika “dhana ya kujenga umoja” haijazaa matunda endelevu na badala yake wananchi wa kipato cha chini hawataki hata kumsikiliza achilia mbali kumuona.

Ukiwauliza wananchi wengi kama wanakumbukumbu ya jambo lolote ambalo Rais Samia amelifanya na hawawezi kumsahau watakuambia ni tozo na kugawa bure raslimali zetu za Taifa.

Hotuba zake husahaulika pindi anapomaliza kutoa hotuba. Nadhani hata mawaziri wake ukiwauliza baada ya hotuba yake wawawezi kukumbuka alichokisema! Garbage in, garbage out.

Mikutano yake ya barabarani kwa sasa inakuwa na magari mengi zaidi ya wananchi ukiondoa wale wanaovalishwa nguo za CCM!

Historia nchini huonyesha kuwa Rais huanza kuchokwa na kuchukiwa katika kipindi cha pili cha utawala wake lakini Rais Samia imemchukua miaka miwili tu kuchukiwa na wananchi wengi.

Kwa jinsi hali ilivyo mbaya kuna uwezekano mkubwa Rais Samia akawa ni Rais wa kipindi kimoja katika historia ya Tanzania kwa sababu katika nchi yoyote wanaoleta mabadiliko ni watu wa kipato cha chini ambao kwa sasa hawataki hata kumsikia.

Hata kama rais huyu achokwe vipi, bado hakuna namna ya kumtoa madarakani kwa njia ya kura, labda machafuko au mapinduzi. Tuna katiba inayokibeba chama tawala, na inampa nguvu rais aliyeko madarakani kuamua kiwango cha ushindi akitakacho. Hili lilidhibita wazi wazi chini ya utawala wa Magufuli.

Kwa hiyo rais huyu yupo madarakani hadi amalize vipindi vyake bila kujali matokeo ya kura. Magufuli ameotesha mbegu mbaya sana ya kutoheshimu chaguzi zetu, na hakuna kiongozi yoyote wa CCM atakayeacha kutumia mbinu zile chafu. Sana sana wapiga kura hawatajitokeza kwa wingi kupiga kura, na kuna uwezekano wa chama tawala kuamua idadi ya kura za kupika.
 
Acha uongo wako hapa na upotoshaji wako hapa wa kijinga.

Rais samia anakubalika ,kupendwa na kuungwa mkono na watanzania wa makundi yote kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.

Katika kugusa maisha ya wananchi wa kipato cha chini ambao wengi wao ni wakulima ,Rais samia aliamua kuchukua hatua za makusudi na za kijasiri kwa kuhakikisha kuwa anawapatia mbolea za Ruzuku zinazogharimu Takribani Billion mia moja hamsini ,hali iliyopelekea mbolea kushuka bei sokoni,,mfano mbolea ya DAP iliyokuwa ikiuzwa laki na 40 ikaanza kupatikana kwa Elfu 70 tu,.sasa ni mkulima yupi au mwananchi yupi atakaye shindwa kumshukuru Rais samia hasa kwa kuzingatia asilimia kubwa ni wakulima? Alifanya hivi kwa kutambua ukweli kuwa uchumi mzuri ni ule unaowagusa watu wengi ,na hapa Tanzania ili uwaguse watu wengi nisharti uwekeze katika shughuli za kilimo kama alivyofanya rais samia ,ikiwepo kuongeza bajeti kufikia billion 970.

Ukija kwa vijana nako ni kicheko furaha na Tabasamu ,hasa baada ya kumwaga maelfu ya ajira mitaani katika ndani ya muda mfupi,lakini pia miradi mbalimbali ambayo imekuwa ikijengwa hapa nchini imechochea ajira nyingi sana kupatikana kwa vijana,lakini pia kwa vijana wanaomaliza kidato cha sita wanapewa mikopo bila shida ,na wawapo vyuoni ni raha tupu na Tabasamu hasa baada ya kuongeza fedha ya kujikimu kufikia elfu kumi kwa siku.

Ukienda kwa wafanyabishara nako ni matumaini kibao ,ambapo kwa sasa kila mfanyabiashara anajisikia fahari kufanyia biashara hapa nchini,kutokana na kuboreshwa kwa mazingira ya biashara hapa nchini,sasa wafanyabishara wanakadiriwa mapato kwa haki na palipo na dosari milango ipo wazi kwa mazungumzo,hali hii ndio imepelekea mapato kwa mwezi kupanda kufikia Trioni 2. Wafanyabishara kwa sasa wanajiona huru kuweka fedha zao benki bila wasiwasi wa kuchotewa fedha zao bila utaratibu wa kisheria au kibenki.

Ukija kwa watumishi wa umma unakuta nako ni shangwe ,nderemo na vifijo hasa baada ya mama wa shoka kuwapandishia mishahara kwa 23% hasa wa kima cha chini,kuwapandisha madaraja,kuwapa nyongeza ya mishahara ya kila mwaka,kuwalipa malimbikizo ya madeni yao na maboresho mengine mengi tu.

Sasa ukitaka kufungua hata biashara katika mwaka wako wa kwanza husumbuliwi na ulipaji wa mapato,kwa kuwa serikali imetoa nafasi ya kukuwa kimtaji na kupata uzoefu wa biashara na kusimama kibiashara.

Ukienda katika huduma za kijamii unakuta Rais samia amegusa kila eneo na kila mahali,iwe ni katika miradi ya maji au umeme au miundombinu una ona namna alivyowekeza vya kutosha ,ndio maana imefika hatua bwawa la nyerere linaanza mapema mwakani kuzalisha umeme.

Ni kundi lipi ambalo halijaguswa na utendaji wa Rais samia? Lipi ambalo halijafikiwa? Lipi ambalo halijatazamwa?

Masuala ya Tozo, je nchi gani ya ulaya au Marekani au zilizoendelea zilizopata maendeleo yake kwa kushushwa kutoka angani? Ni wapi ambako watu wake hawakujibana bana kulipa Tozo ili wajenge nchi zao? Ni wapi huko ambako mataifa yao na wananchi wao walikaa na kubweteka kusubiri wenzao kutoka mataifa mengine walipe Tozo na kodi ili wao wapewe maendeleo.

Watanzania hawajawahi kupinga Tozo na wakati wote wameunga mpango huo wa serikali,ndio maana walikuwa Tayari kuijenga nchi yetu kwa mikono yao ,maana waliona ni aibu kusubiri misaada kwa ajili ya kujengea matundu ya vyoo vya wanafunzi wetu mashuleni. Matokeo chanya ya Tozo hizo ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya Elfu ishirini nchini kwote yaliyopelekea wanafunzi wote wanaofaulu kuanza masomo kwa wakati mmoja, utolewaji wa Elimu bure hadi kidato cha sita,Ujenzi wa vituo vya Afya kila kona ya nchi ikiwepo 234 miezi michache iliyopita ,utolewaji wa Ruzuku ya billion mia moja kila mwezi katika mafuta wakati wa mfumuko wa bei ya mafuta Duniani uliokuwa umesababishwa na vita vya ukrein, n.k.

Mambo aliyoyafanya Rais samia huwezi kumaliza kuandika hapa maana ni mengi sana ,hapo sijazungumzia namna alivyokuza uchumi wetu na kupelekea mzunguko mzuri wa fedha mitaani,kukuza na kuimarisha Demokrasia n.k
Karibu mtetezi wa mafisadi na uporaji wa bandari zote za Tanganyika
 
Mimi ni CCM lakini siwezi kumpa Mama kura yangu! HATOSHI!
Hahitaji kura yako, wala hategemei kura ya mtu yoyote kukaa madarakani. Vyombo vya dola na tume isiyo huru ya uchaguzi zinatosha kufanya kazi hiyo ya kumpatia kura. Huu ni ukweli mchungu boss wangu.
 
Back
Top Bottom