Kwa Rais huyu, CCM wana hali mbaya sana!

Kwa Rais huyu, CCM wana hali mbaya sana!

HATOGOMBEA!!!
Sasa mapicha mitaani ni ya nini?
Na hawa "waandishi maalum", na "MACHAWA" ni wa kazi gani?

Ujue wote hawa ni makupe na chawa hasa hasa, ni lazima yanyonye damu kwa gharama kubwa.

Mama anahaha, anahangaika kutafuta pesa ya kumrudisha madarakani kwa kila njia iwezekanayo.

Njia pekee ya kumzuia, ni huko huko CCM, paibuke kundi la vichaa wasiopenda ujuha wa chama chao kinaoufanya kila mwaka wa uchaguzi.
Hilo pekee ndilo linaloweza kuwa kikwazo kwa Samia kutogombea., au hata akilazimisha kugombea anasindwa uchaguzi na hawezi kuiba kura kama ilivyozoeleka.
 
Samia hafai kabisa, hayupo yeyote anayejielewa anamuamini tena, ameshapoteza uaminifu kwa wale anaowaongoza, sasa anajiendea tu ilimradi..

Naamini ni JK na kundi lao ndio wanaonuona anafaa kuendelea kukalia kile kiti, lakini nje ya pale, hakuna mwingine yeyote mwenye imani nae.
 
Acha uongo wako hapa na upotoshaji wako hapa wa kijinga.

Rais samia anakubalika ,kupendwa na kuungwa mkono na watanzania wa makundi yote kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.

Katika kugusa maisha ya wananchi wa kipato cha chini ambao wengi wao ni wakulima ,Rais samia aliamua kuchukua hatua za makusudi na za kijasiri kwa kuhakikisha kuwa anawapatia mbolea za Ruzuku zinazogharimu Takribani Billion mia moja hamsini ,hali iliyopelekea mbolea kushuka bei sokoni,,mfano mbolea ya DAP iliyokuwa ikiuzwa laki na 40 ikaanza kupatikana kwa Elfu 70 tu,.sasa ni mkulima yupi au mwananchi yupi atakaye shindwa kumshukuru Rais samia hasa kwa kuzingatia asilimia kubwa ni wakulima? Alifanya hivi kwa kutambua ukweli kuwa uchumi mzuri ni ule unaowagusa watu wengi ,na hapa Tanzania ili uwaguse watu wengi nisharti uwekeze katika shughuli za kilimo kama alivyofanya rais samia ,ikiwepo kuongeza bajeti kufikia billion 970.

Ukija kwa vijana nako ni kicheko furaha na Tabasamu ,hasa baada ya kumwaga maelfu ya ajira mitaani katika ndani ya muda mfupi,lakini pia miradi mbalimbali ambayo imekuwa ikijengwa hapa nchini imechochea ajira nyingi sana kupatikana kwa vijana,lakini pia kwa vijana wanaomaliza kidato cha sita wanapewa mikopo bila shida ,na wawapo vyuoni ni raha tupu na Tabasamu hasa baada ya kuongeza fedha ya kujikimu kufikia elfu kumi kwa siku.

Ukienda kwa wafanyabishara nako ni matumaini kibao ,ambapo kwa sasa kila mfanyabiashara anajisikia fahari kufanyia biashara hapa nchini,kutokana na kuboreshwa kwa mazingira ya biashara hapa nchini,sasa wafanyabishara wanakadiriwa mapato kwa haki na palipo na dosari milango ipo wazi kwa mazungumzo,hali hii ndio imepelekea mapato kwa mwezi kupanda kufikia Trioni 2. Wafanyabishara kwa sasa wanajiona huru kuweka fedha zao benki bila wasiwasi wa kuchotewa fedha zao bila utaratibu wa kisheria au kibenki.

Ukija kwa watumishi wa umma unakuta nako ni shangwe ,nderemo na vifijo hasa baada ya mama wa shoka kuwapandishia mishahara kwa 23% hasa wa kima cha chini,kuwapandisha madaraja,kuwapa nyongeza ya mishahara ya kila mwaka,kuwalipa malimbikizo ya madeni yao na maboresho mengine mengi tu.

Sasa ukitaka kufungua hata biashara katika mwaka wako wa kwanza husumbuliwi na ulipaji wa mapato,kwa kuwa serikali imetoa nafasi ya kukuwa kimtaji na kupata uzoefu wa biashara na kusimama kibiashara.

Ukienda katika huduma za kijamii unakuta Rais samia amegusa kila eneo na kila mahali,iwe ni katika miradi ya maji au umeme au miundombinu una ona namna alivyowekeza vya kutosha ,ndio maana imefika hatua bwawa la nyerere linaanza mapema mwakani kuzalisha umeme.

Ni kundi lipi ambalo halijaguswa na utendaji wa Rais samia? Lipi ambalo halijafikiwa? Lipi ambalo halijatazamwa?

Masuala ya Tozo, je nchi gani ya ulaya au Marekani au zilizoendelea zilizopata maendeleo yake kwa kushushwa kutoka angani? Ni wapi ambako watu wake hawakujibana bana kulipa Tozo ili wajenge nchi zao? Ni wapi huko ambako mataifa yao na wananchi wao walikaa na kubweteka kusubiri wenzao kutoka mataifa mengine walipe Tozo na kodi ili wao wapewe maendeleo.

Watanzania hawajawahi kupinga Tozo na wakati wote wameunga mpango huo wa serikali,ndio maana walikuwa Tayari kuijenga nchi yetu kwa mikono yao ,maana waliona ni aibu kusubiri misaada kwa ajili ya kujengea matundu ya vyoo vya wanafunzi wetu mashuleni. Matokeo chanya ya Tozo hizo ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya Elfu ishirini nchini kwote yaliyopelekea wanafunzi wote wanaofaulu kuanza masomo kwa wakati mmoja, utolewaji wa Elimu bure hadi kidato cha sita,Ujenzi wa vituo vya Afya kila kona ya nchi ikiwepo 234 miezi michache iliyopita ,utolewaji wa Ruzuku ya billion mia moja kila mwezi katika mafuta wakati wa mfumuko wa bei ya mafuta Duniani uliokuwa umesababishwa na vita vya ukrein, n.k.

Mambo aliyoyafanya Rais samia huwezi kumaliza kuandika hapa maana ni mengi sana ,hapo sijazungumzia namna alivyokuza uchumi wetu na kupelekea mzunguko mzuri wa fedha mitaani,kukuza na kuimarisha Demokrasia n.k
Mi sikutaka hata kujibu hizo takataka zao. Wamekusanyana wenyewe na kujibizana wenyewe kimada chao hiki eti wanawavisha watanzania! Miongo na minafiki hii dadadeki!!! ahsante kwa kuwasaidia.

Ukweli ni kuwa majuha haya a.k.a nyumbu hizi a.k.a haters hawa wamekwama na wanamuogopa Mama Samia, The Mother of Modern Tanzania, kuliko maelezo......si kwa sababu ni mkali bali kwa mipango ya kimapinduzi ya kimaendeleo mikubwa kabisa inayoenda kutokea nchi hii tangu ipate uhuru. Wanahofu na hawapendi kwelikweli kwa sababu zao za kiubaguzi, kikanda, wivu tu, kijinsi na pengine kidini. Kadiri mambo yanavyosonga mbele kwa kasi ndivyo wanavyozidi kuchanganyikiwa. Katika kujidariji na kuchanganyikiwa huko ndo 'wamebuni' huu mtindo wa kuja na vithread vyao vya kijingajinga kila dakika.

Ukwdli ni kuwa WATANZANIA HALISI HUKU MITAANI TUPO PAMOJA MNO NA MAMA YETU....TENA SAANA. Hivi vijitu 15-20 vya humu jf vinavyojivika kofia ya watanzania wote ni vya kuvipuuza tu.
 
Rais Samia kwa sasa hakubaliki nchini lakini kibaya zaidi hakubaliki ndani ya kundi kubwa la watu wenye maisha ya chini ambao ni wengi nchini na hutumiwa kama “kete” ya CCM katika chaguzi.
Huku kitaa watu wakijani wenye matumbo makubwa tena wengine ni wateule wake wanamnanga vibaya
 
Wewe endelea na “uchawa” wa kijinga!

Uliza wakongwe wa Jamiiforums watakuambia mimi ni nani!

Mimi nimekuwa ndani ya CCM na serikali kabla hujazaliwa achilia mbali kuijua Jamiiforums mwaka 2022.
Kama ni hivyo basi ni bora walivyokutema, kwa hoja hii uliyoleta hapa ni dhahiri kuwa si kwamba hutoshi tu lakini pia hujielewi.....samahani lkn maana umesema we ni mkongwe.
Halafu, wakongwe wenyewe wa kuwauliza humu si ndo hao hao walio'like' na kussuport mada yako; yaani kina erythrocyte & co? Ndo tuwaulize hao na unataka utuambie kuwa uko serious?!!!!🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Acha uongo wako hapa na upotoshaji wako hapa wa kijinga.

Rais samia anakubalika ,kupendwa na kuungwa mkono na watanzania wa makundi yote kutokana na kazi kubwa aliyoifanya ndani ya muda mfupi wa uongozi wake.

Katika kugusa maisha ya wananchi wa kipato cha chini ambao wengi wao ni wakulima ,Rais samia aliamua kuchukua hatua za makusudi na za kijasiri kwa kuhakikisha kuwa anawapatia mbolea za Ruzuku zinazogharimu Takribani Billion mia moja hamsini ,hali iliyopelekea mbolea kushuka bei sokoni,,mfano mbolea ya DAP iliyokuwa ikiuzwa laki na 40 ikaanza kupatikana kwa Elfu 70 tu,.sasa ni mkulima yupi au mwananchi yupi atakaye shindwa kumshukuru Rais samia hasa kwa kuzingatia asilimia kubwa ni wakulima? Alifanya hivi kwa kutambua ukweli kuwa uchumi mzuri ni ule unaowagusa watu wengi ,na hapa Tanzania ili uwaguse watu wengi nisharti uwekeze katika shughuli za kilimo kama alivyofanya rais samia ,ikiwepo kuongeza bajeti kufikia billion 970.

Ukija kwa vijana nako ni kicheko furaha na Tabasamu ,hasa baada ya kumwaga maelfu ya ajira mitaani katika ndani ya muda mfupi,lakini pia miradi mbalimbali ambayo imekuwa ikijengwa hapa nchini imechochea ajira nyingi sana kupatikana kwa vijana,lakini pia kwa vijana wanaomaliza kidato cha sita wanapewa mikopo bila shida ,na wawapo vyuoni ni raha tupu na Tabasamu hasa baada ya kuongeza fedha ya kujikimu kufikia elfu kumi kwa siku.

Ukienda kwa wafanyabishara nako ni matumaini kibao ,ambapo kwa sasa kila mfanyabiashara anajisikia fahari kufanyia biashara hapa nchini,kutokana na kuboreshwa kwa mazingira ya biashara hapa nchini,sasa wafanyabishara wanakadiriwa mapato kwa haki na palipo na dosari milango ipo wazi kwa mazungumzo,hali hii ndio imepelekea mapato kwa mwezi kupanda kufikia Trioni 2. Wafanyabishara kwa sasa wanajiona huru kuweka fedha zao benki bila wasiwasi wa kuchotewa fedha zao bila utaratibu wa kisheria au kibenki.

Ukija kwa watumishi wa umma unakuta nako ni shangwe ,nderemo na vifijo hasa baada ya mama wa shoka kuwapandishia mishahara kwa 23% hasa wa kima cha chini,kuwapandisha madaraja,kuwapa nyongeza ya mishahara ya kila mwaka,kuwalipa malimbikizo ya madeni yao na maboresho mengine mengi tu.

Sasa ukitaka kufungua hata biashara katika mwaka wako wa kwanza husumbuliwi na ulipaji wa mapato,kwa kuwa serikali imetoa nafasi ya kukuwa kimtaji na kupata uzoefu wa biashara na kusimama kibiashara.

Ukienda katika huduma za kijamii unakuta Rais samia amegusa kila eneo na kila mahali,iwe ni katika miradi ya maji au umeme au miundombinu una ona namna alivyowekeza vya kutosha ,ndio maana imefika hatua bwawa la nyerere linaanza mapema mwakani kuzalisha umeme.

Ni kundi lipi ambalo halijaguswa na utendaji wa Rais samia? Lipi ambalo halijafikiwa? Lipi ambalo halijatazamwa?

Masuala ya Tozo, je nchi gani ya ulaya au Marekani au zilizoendelea zilizopata maendeleo yake kwa kushushwa kutoka angani? Ni wapi ambako watu wake hawakujibana bana kulipa Tozo ili wajenge nchi zao? Ni wapi huko ambako mataifa yao na wananchi wao walikaa na kubweteka kusubiri wenzao kutoka mataifa mengine walipe Tozo na kodi ili wao wapewe maendeleo.

Watanzania hawajawahi kupinga Tozo na wakati wote wameunga mpango huo wa serikali,ndio maana walikuwa Tayari kuijenga nchi yetu kwa mikono yao ,maana waliona ni aibu kusubiri misaada kwa ajili ya kujengea matundu ya vyoo vya wanafunzi wetu mashuleni. Matokeo chanya ya Tozo hizo ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya Elfu ishirini nchini kwote yaliyopelekea wanafunzi wote wanaofaulu kuanza masomo kwa wakati mmoja, utolewaji wa Elimu bure hadi kidato cha sita,Ujenzi wa vituo vya Afya kila kona ya nchi ikiwepo 234 miezi michache iliyopita ,utolewaji wa Ruzuku ya billion mia moja kila mwezi katika mafuta wakati wa mfumuko wa bei ya mafuta Duniani uliokuwa umesababishwa na vita vya ukrein, n.k.

Mambo aliyoyafanya Rais samia huwezi kumaliza kuandika hapa maana ni mengi sana ,hapo sijazungumzia namna alivyokuza uchumi wetu na kupelekea mzunguko mzuri wa fedha mitaani,kukuza na kuimarisha Demokrasia n.k
Wewe ni zwazwa!
 
Siku Ya Kufa Nyani, Miti Yote Huteleza
Kwasasa Wameanza Kujitafakari Mmoja Mmoja Wameshapata Yupi Atolewe Bangusiro (Kondoo Wa Kafara)
 
Labda hamumkubali wewe na mumeo.
Bibi FaizaFoxy Kwa maadili ya dini yetu hii inaruhusiwa ?😂😂😂
images (13).jpeg
 
Umesema ukweli kabisa.Mimi nimetembea sehemu nyingi Tanzania nzima,vijiji na vijiji kote huko kila mmoja hawamkubali kabisa huyu mother.
 
Samia hafai kuwa Rais. Katiba iboreshwe isije kutokea tena upuuzi wa namna hii
Hata uje Katiba kutoka wapi au Tume huru kutoka sayari ipo bado mamilioni ya watanzania tutamchagua Rais Samia.Ndio maana tumeamua kuwa naye mpaka 2030,hutaki hama nchi na familia yako maana sisi watanzania chaguo letu ni Rais samia
 
Atakuwa anazuga ili mumchague muhula wa pili auze kila kitu. Hata apige magoti aombe msamaha hachaguliwi kabisa. Labda aibe na afanikiwe kuwashawishi majeshi wamweke kwa lazima.
Sauti za mamilioni ya watanzania zimeshapaza sauti kuhitaji utumishi wa mama samia kutuongoza muhula wa pili,kwa hiyo utake usitake,upende usipende watanzania tumeshaamua kwenda na kumchagua Tena Rais samia,jua liwake au mvua inyeshe tutakwenda na Rais samia na ndiye Rais ajaye kwa mara nyingine Tena.kama hutaki tafuta nchi yako uende na watoto wako
 
Back
Top Bottom