Kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma Makao Makuu, wote imekuwa ni njia moja Dar

Kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma Makao Makuu, wote imekuwa ni njia moja Dar

Kama uko makini kwenye siasa za kimataifa unaweza fahamu nani mwenye nguvu kati ya katiba ya nchi na rais alieko madarakan..naomba urejelee utendaji kaz wa trump aliekuwa rais wa marekani..pamoja na kwamba wamarekani wengi wako vzur kichwani haswa kwenye masuala la nchi yao na katiba..lakin kichaa trump aliwatingisha kweli kweli had wakanyoosha mikono..sembuse haka ka nchi kalichojaa mazwazwaa kila kona..nakuhakikishia hata hiyo katiba iwejee rais kama hana heshima na ustaarabu kwenye ubongo wake ataikanyaga mchana kweupe na hatafanywa kitu

..Nakubaliana na wewe kwa 50%.

..Ni kweli Wamarekani walitingishwa na kiongozi mhuni Donald Trump.

..Lakini ni kweli pia katiba yao ndio iliyowaokoa wasisambaratishwe moja kwa moja.

..kama katiba ya Marekani isingekuwa imesukwa kwa namna ambayo Raisi wao hawezi kuingilia uchaguzi na kupanga matokeo leo hii Trump angekuwa bado ni Raisi.

..kwa hiyo bado tunahitaji katiba bora pamoja na kwamba upo uwezekano wa wananchi kuchagua viongozi wa hovyo.

..katiba bora ndiyo itakayowapa nguvu na ulinzi WAADILIFU kumfunga breki kiongozi wa hovyo-hovyo.
 
Kama uko makini kwenye siasa za kimataifa unaweza fahamu nani mwenye nguvu kati ya katiba ya nchi na rais alieko madarakan..naomba urejelee utendaji kaz wa trump aliekuwa rais wa marekani..pamoja na kwamba wamarekani wengi wako vzur kichwani haswa kwenye masuala la nchi yao na katiba..lakin kichaa trump aliwatingisha kweli kweli had wakanyoosha mikono..sembuse haka ka nchi kalichojaa mazwazwaa kila kona..nakuhakikishia hata hiyo katiba iwejee rais kama hana heshima na ustaarabu kwenye ubongo wake ataikanyaga mchana kweupe na hatafanywa kitu
Uonaji wa mambo wako una hitilafu.
Unatoa mfano huo wa Katiba ya marekani, unasahau ilivyo imara na jinsi inavyofanya kazi?

Huo mfano wa 'Trump' unaoutumia, wewe huoni kama ingekuwa ni katiba kama hii hapa ya kwetu Trump hadi sasa angekuwa anawaendesha wananchi wake?
Unajuwa ni mambo mamngapi, pamoja na ukichaa wake, Trump hakuweza kuyafanya kwa kushindwa kuitingisha katiba imara?
Hukumbuki lolote kuhusu 'impeachment' aliyofanyiwa?

Kwa katiba yetu hapa ni nani angethubutu kum'peach' Magufuli?
 
LOooo, wewe unasubiri 'mindset' zibadilike, na hata hujisumbui kueleza 'mindset' za nani na zitabadilishwa na nani?
Kama mawazo kama haya siyo maajabu sijui tuyaite ni kitu gani hicho!

Yaani hoja nzima ni ya ajabu kabisa: katiba isibadilishwe, isubiri 'mindset' zibadilishwe!

Kwa nini usiangalie angalao uwezekano wa hiyo katiba mpya ndiyo iwe chachu ya kubadilisha 'mindset' za watu kuithamini hiyo katiba, na kujitahidi kuilinda isikanyagwe hovyo hovyo na watawala?
Hili kwako hulioni kuwa na maana yoyote; umejikita tu kwenye 'mindset'!
Hapo sasa ndipo tunaingia kwenye mjadala wa kati ya kuku na yai kipi kinamtangulia mwenzake
Ni hivi nikisema mindset naamina utambuzi wa mtu binafsi kuelewa nini mana ya kuwa na katiba na jinsi ya kuiheshimh na kuilinda hiyo katiba.kama watu hawafika kwenye hiyo level ya kutambua umuhimu wa kuiheshimu na kuilinda katiba baas ujue hata hiyo mpyaa itasiginwaa mchana na usiku..
Jambo la pili nani wakuibadilisha hiyo kindset.? Jibu ni moja tu mindset haibadilishwi na mtu mwingine yyte yule isipokuwa na muhusika mwenyewe..leo ww ukiwa na mindset inayoheshimu uhuru wa mtu basi huyo mtu uliemuheshimu leo kesho na yeye ataheshimu wengine and it keeps on evolving..
Mfano hivi unazani leo hii chadema wakikamata nchi wataheshimu uhuru wa wapinzani wao? Hakuna kwa sabab wao hawakuheshimiwaaa...hivyo to change a mindset, begins with an individual him/herself.
 
LOooo, wewe unasubiri 'mindset' zibadilike, na hata hujisumbui kueleza 'mindset' za nani na zitabadilishwa na nani?
Kama mawazo kama haya siyo maajabu sijui tuyaite ni kitu gani hicho!

Yaani hoja nzima ni ya ajabu kabisa: katiba isibadilishwe, isubiri 'mindset' zibadilishwe!

Kwa nini usiangalie angalao uwezekano wa hiyo katiba mpya ndiyo iwe chachu ya kubadilisha 'mindset' za watu kuithamini hiyo katiba, na kujitahidi kuilinda isikanyagwe hovyo hovyo na watawala?
Hili kwako hulioni kuwa na maana yoyote; umejikita tu kwenye 'mindset'!
Mwisho kabisaaa..kipi kianze kati ya mindset au katiba..
Jibu ni rahisi..ili uwe na katiba bora, lazima wanaoiandaa hiyo katiba wawe na mindset nzuri ambazo hazitakuwa na bias zozote au kufanya muhiml mmoja kuwa na nguvu zid ya mwingine..hivyo katiba bora huundwa na watu wenye mindset bora na sio katiba bora ilete watu wenye mindset bora..
 
Yaani kwa sasa ni nadra sana kuwakuta hawa viongozi wapo Dodoma makao makuu - wote imekuwa ni njia moko Dar - Magari yenye bendera za Mawaziri na Watendaji wengine wa Serikali wamerudi Dar kwa kasi kubwa mno. Yaani haipiti saa tatu ukiwa Morogoro kila siku unaona gari la kiongizo liko spidi kutoka au kwenda Dar na Dodoma. Matrafiki siku hizi hawana hata mpango wa kuyasimamisha tena. Wamechoka wanaangalia tu.

Gharama hizo za magari kukimbia njia ya Dar Dom ninaona ni kuwa mno kiasi kwamba angekuwepo Mwendazake isingekuwa hivi - wengine hadi juzi wamediriki kuamua kurudisha Ofisi zao Dar - Waziri yule kaitoa Ofisi Moro kuipeleka Dar badala ya Dodoma. Ninamkumbuka sana Mwendazake jamani!

Hivi leo hii tukiitisha roll call ya Viongozi Dodoma ni Mawaziri na Wanaibu Waziri na Makatibu Wakuu wangapi watakuwepo Dodoma leo?
Kumbuka juzi tu karibu wote walikuwa Dar kwa Sabasaba - leo Ijumaa tayari wanne wamepanga ndege na kuna magari zaidi ya 6 yanaelekea Dar now bila hata sababu yeyote. Pumzika kwa Amani Mwendazake! Tumekumiss sana sana!
Utasemwa unaanza chokochoko ,wakati wasema ukweli, jamani viongozi Dodoma haiepukiki, hatuwezi kua twafanya Jambo twarudi nyuma, mh rais stop that
 
..Nakubaliana na wewe kwa 50%.

..Ni kweli Wamarekani walitingishwa na kiongozi mhuni Donald Trump.

..Lakini ni kweli pia katiba yao ndio iliyowaokoa wasisambaratishwe moja kwa moja.

..kama katiba ya Marekani isingekuwa imesukwa kwa namna ambayo Raisi wao hawezi kuingilia na kupanga matokeo leo hii Trump angekuwa bado ni Raisi.

..kwa hiyo bado tunahitaji katiba bora pamoja na kwamba upo uwezekano wa wananchi kuchagua viongozi wa hovyo.

..katiba bora ndiyo itakayowapa nguvu na ulinzi WAADILIFU kumfunga breki kiongozi wa hovyo-hovyo.
Katiba ,katiba, katiba
 
Endelea kushangaa
Huwa nawashangaa sana watu wanaodai katiba mpyaa...mnashindwa kujua shida iko wap..hata ukiwa na katiba bora kama nn..bila kuwa na watu wanaoiheshimu ni kaz bure..katiba haijindeshi yenyewwwe..wapo watu wanaisimamia hiyo katiba..kama hao watu ni hovyoo baas wataikanyagaa tu hiyo katibaaa...hivyoo kinatakiwa ni mind set za hao watu zibadilike hapo ndipo katiba itasaidia..la sivyo ni kutwanga maji kwenye kinu..
Hii iliyopo tu inasiginwaa mchana kutwaa..
 
Nigeria, Malawi wamejenga na kuhamia makao makuu mapya, kama kutaja mifano kunasaidia kuwekea uzito hoja.

Uamzi wa kufanya Dodoma kuwa makao makuu ya serikali haukuwa na hauna ubaya wowote. Dar es Salaam itaendelea kuwa kituo kikuu cha biashara, sioni tatizo liko wapi.

Hawa viongozi inatakiwa watulizane tu wafanye kazi za wananchi hapo hapo Dodoma.

Moja ya historia mbaya inayoweza kumwandama Samia ni huku kuhangaika na safari za kila siku kwenda Dar es Salaam, na atakaporuhusu na mawaziri wake waige tabia hiyo, atajiwekea alama mbaya katika uongozi wake.

..mifano uliyoitoa ni ya kweli.

..mimi hoja yangu ni kwamba uamuzi wetu haukuwa na tija, wala ulazima.

..kwanini tujengee mawaziri maofisi mapya wakati tayari walikuwa na ofisi hizo Dsm?

..Ni uamuzi umeshafanyika. Kama ni fedha zimeshakwenda hivyo nakubaliana na wewe kuwa viongozi waishi na uamuzi wao.
 
Watakwambia wapo kwenye safari za kikazi Dar, kwa nini tusiwaone na mikoa mingine.......jambo la muhimu kama hao maafisa wana mishe zao binafsi Dar watumie magari yao binafsi siyo ya umma......
 
Huwa nawashangaa sana watu wanaodai katiba mpyaa...mnashindwa kujua shida iko wap..hata ukiwa na katiba bora kama nn..bila kuwa na watu wanaoiheshimu ni kaz bure..katiba haijindeshi yenyewwwe..wapo watu wanaisimamia hiyo katiba..kama hao watu ni hovyoo baas wataikanyagaa tu hiyo katibaaa...hivyoo kinatakiwa ni mind set za hao watu zibadilike hapo ndipo katiba itasaidia..la sivyo ni kutwanga maji kwenye kinu..
Hii iliyopo tu inasiginwaa mchana kutwaa..
Kwahiyo unataka tuondoe kwanza viongozi waliopo tulete wapya watakaoiheshimu katiba ?
 
Kama uko makini kwenye siasa za kimataifa unaweza fahamu nani mwenye nguvu kati ya katiba ya nchi na rais alieko madarakan..naomba urejelee utendaji kaz wa trump aliekuwa rais wa marekani..pamoja na kwamba wamarekani wengi wako vzur kichwani haswa kwenye masuala la nchi yao na katiba..lakin kichaa trump aliwatingisha kweli kweli had wakanyoosha mikono..sembuse haka ka nchi kalichojaa mazwazwaa kila kona..nakuhakikishia hata hiyo katiba iwejee rais kama hana heshima na ustaarabu kwenye ubongo wake ataikanyaga mchana kweupe na hatafanywa kitu
Trump aliwatingisha wamarekani au alijitingisha mwenyewe na kudondoka ??
 
Kama uko makini kwenye siasa za kimataifa unaweza fahamu nani mwenye nguvu kati ya katiba ya nchi na rais alieko madarakan..naomba urejelee utendaji kaz wa trump aliekuwa rais wa marekani..pamoja na kwamba wamarekani wengi wako vzur kichwani haswa kwenye masuala la nchi yao na katiba..lakin kichaa trump aliwatingisha kweli kweli had wakanyoosha mikono..sembuse haka ka nchi kalichojaa mazwazwaa kila kona..nakuhakikishia hata hiyo katiba iwejee rais kama hana heshima na ustaarabu kwenye ubongo wake ataikanyaga mchana kweupe na hatafanywa kitu
Hapana brother,hiyo katiba tunayoiongelea hapa sio hii,raisi akiikanyaga anajua kabisa atafunguliwa mashtaka so watawala hawa wame-relax kwa sababu wanajua katiba hii haina meno na mihimili mingine wameitia mfukoni.tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa utawala wa bwana yule,na mtu yeyote mwenye akili timamu hatopenda mtawala kama yule atokee tena kwenye nchi yetu.
 
Ni wazi walikuwa wanamheshimu mwenda zake kinafiki,hawakupenda kuhamia Dodoma,hii sasa ni sawa na kumpeleka punda mtoni kunywa maji wakati hana kiu hatokunywa,na sidhani kama Bi mkubwa anaweza kuwadhibiti.
 
Hivi hata PM naye hayaoni haya. Yeye ndiye msimamizi mkuu wa shughuli za serikali kule bungeni na kiranja wa hao mawaziri.

Kwa nini hamsaidii mama?

Mpango naye naona sasa ameelewa nafasi yake ya umakamu,maana mwanzoni alijiona kama rais wa nchi.

Tuwahimize wajue ofisi ni dodoma, sijui zile taasisi zilizokuwa na mipango ya Dom kama bado wanamawazo hayo pia.

Mwendazake ameenda na mengi sana.
 
Huwa nawashangaa sana watu wanaodai katiba mpyaa...mnashindwa kujua shida iko wap..hata ukiwa na katiba bora kama nn..bila kuwa na watu wanaoiheshimu ni kaz bure..katiba haijindeshi yenyewwwe..wapo watu wanaisimamia hiyo katiba..kama hao watu ni hovyoo baas wataikanyagaa tu hiyo katibaaa...hivyoo kinatakiwa ni mind set za hao watu zibadilike hapo ndipo katiba itasaidia..la sivyo ni kutwanga maji kwenye kinu..
Hii iliyopo tu inasiginwaa mchana kutwaa..
Yote kwa yote katiba mpya iwepo kwanza wasiotaka kuishemu katiba wembe ni ule ule uliotumika kumnyolea Jacob Zuma ndio huohuo utakaotumika kuwanyolea wasiotaka kuiheshimu katiba
 
Hayo ni matunda ya utawala wa kiimla ya dikteta Magufuli. Watendaji walijaa unafiki mtupu. Watu waliacha kufanya kazi kufuata miongozo na wakawa busy kumridhisha Magufuli huku wakitesa watanzania.
Si mlikuwa mnamtukana Magufuli?

Si mlisema mama anaupiga mwingi na sasa ufipa mnapumua?

Season ya nyumbu migration imeanza rasmi
 
Back
Top Bottom