Kwa sasa Yanga ndiyo timu inayocheza mpira mzuri barani Afrika

Kwa sasa Yanga ndiyo timu inayocheza mpira mzuri barani Afrika

Natafuta Ajira

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2020
Posts
9,016
Reaction score
24,650
Kwenye suala la kumiliki mpira na kucheza kandanda safi kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla, sioni timu ya kuwashinda wananchiwananchi. Tumaini pekee la wapinzani wanaokutana na Yanga ni kupaki basi na kucheza kaunta attack.

Mtihani wa benchi la ufundi kwa sasa ni kuja na mbinu za kuwafunua wapinzani, maana mara zote wanapaki, basi hii inapelekea kutengeneza nafasi chache sana za kufunga.

Watu wanawasema Al Hilal kwa mpira waliocheza, lakini siyo kwamba ule ndiyo mpira wao wa kila siku. Pale wanapokutana na timu wanazozimudu huwa wanamiliki mpira. Mfano mechi ya kirafiki dhidi ya Makolo na michezo yote miwili dhidi ya St. George, ila dhidi ya wananchi Ibenge hakuwa mjinga kupaki basi dakika zote 180, ni wazi alijua akiweka mpira chini hatoweza kushindana na Yanga.

Kitu pekee ambacho Pogba amemzidi Fei Toto ni uchawi tu. Kuna muda Dunia haina usawa, inasikitisha sana kuona Fred anakipiga Man UTD wakati aucho yupo Yanga. Mwangalie Aziz Ki anavyotembeza mpira, mtu unapata ile radha halisi ya soka. Nipe tofauti moja tu ya Sure Boy na Iniesta, nami nitakuonesha bucha la kitimoto kwenye kambi ya Al Qaeda!

Kuliko kupotezeana muda na nguvu hili kombe la CAF Confederation, ni bora wapewe tu wananchi.
 
1668028422354.jpg
 
Tuliiga jamani Hadi makolo wakatungaa mkono kwa umahiri mzuri bila kosa lolote lilo onekana
 
Halina ubishi kiwango chetu kilionekana dhahiri kule Hali hilal ndipo nimeona timu yangu ipo vzr mno bas tu Ni ajali tulipata
Kuna vitu vidogo vidogo sana vilipelekea kuwakosa wale wasudani.. kwanza papala za kusaka goli la pili na kujisahau kulinda ilo moja tulilopata pale taifa, kukosa utulivu wa akili baada ya jamaa kuchomoa goli tatu hatukuwa na mpango wa kutuliza kaunta attacks zao ila kwenye mechi mbili na hawa waarabu naona makosa yote yamefanyiwa kazi bado kuna kizingiti kimoja tu ili Yanga iwe timu tishio Afrika nacho ni kuzifunua safu za ulinzi za wapinzani wanaopaki basi
 
Sikuwa na comment yoyote Zaid ya ku like.

Asante sana makolo kwa kutuunga mkono na kuumia mioyo yenu kama mmeikabidhi kwa shetani.

Kwa kweli makolo wote mlaaniwe kwa wivu mliotuonesha na mbalikiwe muwe mnapata maumivu kama mliyopata Leo huku mmdindishiwa na singidani Kyle mmeonyeshwa kandanda LA kufa mtu.

Byeyiniii usiku goodluckndotoni
 
Wale wapuuzi waliokuwa wanamtukana Rrof Nabi tunawafungia miaka 3 kushabikia Yanga.
Hatutaki mashabiki maandazi ambao wanataka kocha afukuzwe kwa kutoshinda mechi chache tu.Huo upuuzi uishie kwa Makolo huko

Nabi ni kocha mwenye uchungu na timu yake, yani kuna saa unamuona akitokwa machozi ya furaha timu ikifunga.
 
Wale wapuuzi waliokuwa wanamtukana Rrof Nabi tunawafungia miaka 3 kushabikia Yanga.
Hatutaki mashabiki maandazi ambao wanataka kocha afukuzwe kwa kutoshinda mechi chache tu.Huo upuuzi uishie kwa Makolo huko

Nabi ni kocha mwenye uchungu na timu yake, yani kuna saa unamuona akitokwa machozi ya furaha timu ikifunga.
Walikua makolo wale wanachochea kuni tu ili moto uwake
 
Kwenye suala la kumiliki mpira na kucheza kandanda safi kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla, sioni timu ya kuwashinda wananchiwananchi. Tumaini pekee la wapinzani wanaokutana na Yanga ni kupaki basi na kucheza kaunta attack.

Mtihani wa benchi la ufundi kwa sasa ni kuja na mbinu za kuwafunua wapinzani, maana mara zote wanapaki, basi hii inapelekea kutengeneza nafasi chache sana za kufunga.

Watu wanawasema Al Hilal kwa mpira waliocheza, lakini siyo kwamba ule ndiyo mpira wao wa kila siku. Pale wanapokutana na timu wanazozimudu huwa wanamiliki mpira. Mfano mechi ya kirafiki dhidi ya Makolo na michezo yote miwili dhidi ya St. George, ila dhidi ya wananchi Ibenge hakuwa mjinga kupaki basi dakika zote 180, ni wazi alijua akiweka mpira chini hatoweza kushindana na Yanga.

Kitu pekee ambacho Pogba amemzidi Fei Toto ni uchawi tu. Kuna muda Dunia haina usawa, inasikitisha sana kuona Fred anakipiga Man UTD wakati aucho yupo Yanga. Mwangalie Aziz Ki anavyotembeza mpira, mtu unapata ile radha halisi ya soka. Nipe tofauti moja tu ya Sure Boy na Iniesta, nami nitakuonesha bucha la kitimoto kwenye kambi ya Al Qaeda!

Kuliko kupotezeana muda na nguvu hili kombe la CAF Confederation, ni bora wapewe tu wananchi.
Naagiza mtoa mada apewe ajira ya kuduma jeshi laa uokoaji
 
Back
Top Bottom