Kwa sera za namna hii, Tanzania inaweza badilisha hali yake ya kiuchumi na kuwa taifa imara ukanda wa Kusini mwa Afrika ama inahtaji mageuzi zaidi?

Kwa sera za namna hii, Tanzania inaweza badilisha hali yake ya kiuchumi na kuwa taifa imara ukanda wa Kusini mwa Afrika ama inahtaji mageuzi zaidi?

Rijali jandoni

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2018
Posts
1,936
Reaction score
1,972
Habari za jioni wana jamii leo nimekaa na kuwaza kuhusu nchi yetu ya Tanzania kwa kina na kwa upana sikuwa na budi bali kuandika haya mambo kwa sisi watanzania wote

Tanzania ni nchi ambayo imekaa vizuri kijiografia yaani tumezungukwa na nchi nane tunaweza sema tisa tukiweka na visiwa vya Comoros. Strategically Tanzania ni nchi nzuri kiuwekezaji na kiuchumi kwa namna ya kuzungukwa na nchi karibia tisa.

1725118111423.png

Tukija swala la pili Tanzania ni lango kuelekea kusini mwa afrika nchi kama maalawi,zambia na hata congo, hapa tunaweza jumuisha Burudi na hata Rwanda kwa namna fulani.

Tukiongezea kwenye idadi ya watu kwa ukanda huu wa kusini mwa afrika ni kati ya nchi yenye idadi kubwa ya watu pamoja na wanyama.

Tanzania ukiachana na idadi ya watu, ina eneo la mraba mkubwa sana zaidi ya nchi zilizo pakana nazo ukiachana na Congo upande wa magharibi.

Kwa namna hiyo kama taifa inawezekanaje bado tukawa na hali ya wasiwasi wa kichumi na ya kufikirisha na ukiongeza kwa rasilimali ni nchi naweza sema pekee duniani imezungukwa na maji katika kila pande kaskazini mashariki ,magharibi pamoja na kusini.

Kwa namna ya kawaida tunaweza sema ni nchi ya asali na maziwa ambayo kila binadamu pamoja na kiongozi huenda ana imezea mate japo sisi bado tuna wasiwasi wa namna tutakavyo amka kesho yake, hii ni kwa majority japo natambua wapo wasio na wasi wasi juu ya kesho yao, kwenye suala la kiuchumi.

1725118141251.png


Kama taifa, viongozi wake Ndugu Raisi, Makamu, Spika, Mawaziri, Wabunge, pamoja na viongozi wote kwanini tusiwe na sera za muda mrefu (miaka 10 - 20) au mfupi (miaka 2 mpaka 5) za kiuchumi kwa taifa kwenye mambo tofauti?. Juhudi za viongozi wote mlijitahidi kwenye kuitangaza nchi hasa kwenye utalii na mengine mengi lakini kuna mambo tunaweza yasahau madogo ama hata makubwa ambayo yanahitaji jicho makini na la tofauti ili kuendeleza taifa letu la Tanzania na kuweka ahuweni na imani kwa wana wa Tanzania hasa swala la uchumi :-

1. Itungwe sera ya kuwekeza kwenye miundo mbinu ya nchi kuanzia barabara, maji, umeme majengo ya shule na biashara.
Kama taifa na viongozi wake wanaweza kuweka sera ya miaka mitatu sababu tumesha jitangaza vya kutosha na kuwekeza hela kwenye utalii na mambo mengine. Je tunaweza jaribu haya:-

(i) Tujitahidi kuanza sera ya maji kwenye kila kijiji fedha zitakazo pangwa kwa ajili ya matangazo basi tuanze la maji na upatikanaji wake, kutokana na matumizi yake kuwa muhimu kwenye shughuli za kila siku. Hii tuipe hata sera ya miaka miwili itategemea na serikali itapanga bajeti kiasi gani kwa sababu kasi ya mradi nadhani huwa inategemea fungu lililowekwa pamoja na ufanisi wa watendaji wa huo mradi lakini muda utakuwa muhimu zaidi kwenye haya mambo.

(ii) Iwepo sera ya kusambaza umeme kila kijiji kila mtaa hii imeshafanyika huenda sehemu kubwa ya nchi inabidi tuupeleke kote ila hapa inatakiwa uwepo uangalifu na nyumba inayo fungiwa umeme ili kukwepa gharama za uharibifu pale ambapo majanga yatatokea hata madogo kama upepo na ukaharibu nyumba isio imara, kwasababu tunaelewa hali zetu watanzania vidole vyote havilingani na ndivyo hivyo kwenye swala la ujenzi pia kila nyumba itajengwa kwa ubora kutokana na kipato cha mtu. Hii sera ya umeme inaweza kuja baada ya maji kwa sababu uwekezaji wa bomba za maji huwa zina husisha uchimbaji wa mitaro mikubwa.

(iii) Kwenye sera ya tatu ni ujenzi wa barabara tujitahidi kila eneo ambalo linatumika kama chanzo kikubwa cha mapato basi barabara iweze kupita hapo ya kiwango bora cha lami, tujitahidi kupeleka hizi barabara mashambani, karibia na migodi, na hata mipakani mwa mbuga za wanyama bila kusahau vijijini kwa wakulima hii itasaidia usafirishaji wa hizi rasilimali zote pamoja na watu kufika kwenye maeneo hayo kwa usalama, uharaka na bila shida yoyote na hata mboga mboga pamoja nafaka zita safirishwa kwa muda mfupi kuliko sasa.

Kwa sababu kwenye uchumi wowote ili ukuwe tunatakiwa tujitahidi kupunguza muda wa usafirishaji wa rasilimali ama utengenezaji wa vitu kwa namna hiyo tutaifanya Tanzania kuwa nchi ambayo iko makini na haraka kwenye sekta na swala la uchukuzi.

(iv) Ya nne itashangaza lakini itasaidia tuwekeze kwenye ujenzi wa shule vyuo vikubwa hospitali za hadhi ya juu kwenye kutibu magonjwa na hata kuwekeza kwenye tafiti za kidunia sababu hakuna nchi ilio endelea kwa kushabikia mpira miziki na mengine kwa kiwango kinachozidi utafiti yaani researches, nchi zinazo endelea ni kutokana na sera nzuri za kwenye utafiti either science, uchumi na siasa tusome duniani nchi nyingine zina fanya nini na sisi tunaweza changia nini hii itaweza vutia wana zuoni wengi kuja Tanzania na kusoma mfano tunaona nchi ya afrika kusini ukiachana na miundombinu ila watu wengi wanatamani pia kwenda kusoma huko ukienda ulaya na Asia ndio usiseme, kila mwana wa Afrika anapatamani.

@ Kwenye sera ya ujenzi wa shule yaani vyuo vikubwa tujitahidi kila mkoa uwe na chuo chenye hadhi kama ya chuo kikuu dar es salaam ama zaidi hii itachangia pia uinuaji wa uchumi kwenye mikoa iliokuwa haionekani na pia itafanya wanafunzi wanaomaliza mikoa husika kusoma vyuo vikuu na vikubwa kwa kila mkoa ambao atakuwepo na wengine wanaweza pia kuomba nafasi ya kusoma kwenye hivyo vyuo lakini la muhimu hapa itaamsha shughuli za kiuchumi kwa kila mkoa wa Tanganyika na Zanzibar.

(b) Na kwenye hospitali kufanyike vivyo hivyo kwa sasa tunaweza anza na mikoa yenye idadi nyingi ya watu na ipo angalau vizuri kiuchumi kuendeleza hospitali zao mkoa ziwe kama muhimbili au kujenga hospitali kubwa za hadhi ya muhimbili au zaidi zenye vifaa na wataalamu wazuri ili kusaidia jamii za eneo husika kwenye nyanja tofauti. Hii itafanya nchi kuto endelea upande mmoja tuu tutajijuta kila mkoa wa Tanzania kuna fursa kutokana na upatikanaji wa vitu muhimu

(c) Kujijenga imara na kiteknolojia zaidi kwenye swala la ulinzi cha kwanza imani irudushwe kwa wananchi juu ya vyombo vyetu vya usalama, pili inawezekana kila mkoa kukawa na mfumo wa vinasa picha yaani kamera za matukio ambazo zita unganishwa na vituo vidofompaka vikubwa vya kila kata wilaya, mkoa na hata nchi kwa namna hii nawahakikishia kama suala la watu kwenda Serengeti, Zanzibar Udizungwa Kilimanjaro wata miminika mpaka tuweke sheria kali kama baadhi ya nchi kama China

Sababu tutakuwa tuko vizuri sehemu zote muhimu hili la ulinzi naimani wenye nafasi wanaweza liboresha zaidi na tuka aminika sababu hili ni kati ya changamoto kwa nchi zetu za afrika Tanzania tukitatua basi tutakuwa na ugeni usiokuwa na idadi kati ya 6Million hata 10Million kwa mwaka na itashangaza.

Kwa namna hii nadhani tunaweza peleka taifa letu mbele zaidi ila inahitaji watu wenye upendo wa kweli kwa nchi yetu. Tukumbuke tunaweza tukala kila kitu na kuiporoka Tanzania na hata kuona watu wake hawastahili mazuri ama wana stahili lakini sio kwa kiwango kikubwa, ila usije ukasahau hii ardhi ndio itakayo kupokea siku ikikuhitaji utajisikiaje umefanya mambo ambayo hukuweza kuondoka nayo wakati yalikuwa kwenye uwezo wako tuipende Tanzania tuipende afrika naelewa ni ngumu kwa sera zote kufanyika kutokana na vikwazo vingi vitakavyoweza kuinuka lakini tujitahidi hakuna Tanzania nyingine zaidi ya hii tunaweza kimbilia ulaya kula na kukaa ila kama ulitokea kwenye uso wa Tanzania basi kumbuka kuna siku utataka ukurudishe ardhini kwake utakumbukwa kwa lipi juubya taifa lako?
 
Habari za jioni wana jamii leo nimekaa na kuwaza kuhusu nchi yetu ya Tanzania kwa kina na kwa upana sikuwa na budi bali kuandika haya mambo kwa sisi watanzania wote

Tanzania ni nchi ambayo imekaa vizuri kijiografia yaani tumezungukwa na nchi nane tunaweza sema tisa tukiweka na visiwa vya Comoros. Strategically Tanzania ni nchi nzuri kiuwekezaji na kiuchumi kwa namna ya kuzungukwa na nchi karibia tisa.

View attachment 3083679

Tukija swala la pili Tanzania ni lango kuelekea kusini mwa afrika nchi kama maalawi,zambia na hata congo, hapa tunaweza jumuisha Burudi na hata Rwanda kwa namna fulani.

Tukiongezea kwenye idadi ya watu kwa ukanda huu wa kusini mwa afrika ni kati ya nchi yenye idadi kubwa ya watu pamoja na wanyama.

Tanzania ukiachana na idadi ya watu, ina eneo la mraba mkubwa sana zaidi ya nchi zilizo pakana nazo ukiachana na Congo upande wa magharibi.

Kwa namna hiyo kama taifa inawezekanaje bado tukawa na hali ya wasiwasi wa kichumi na ya kufikirisha na ukiongeza kwa rasilimali ni nchi naweza sema pekee duniani imezungukwa na maji katika kila pande kaskazini mashariki ,magharibi pamoja na kusini.

Kwa namna ya kawaida tunaweza sema ni nchi ya asali na maziwa ambayo kila binadamu pamoja na kiongozi huenda ana imezea mate japo sisi bado tuna wasiwasi wa namna tutakavyo amka kesho yake, hii ni kwa majority japo natambua wapo wasio na wasi wasi juu ya kesho yao, kwenye swala la kiuchumi.

View attachment 3083681

Kama taifa, viongozi wake Ndugu Raisi, Makamu, Spika, Mawaziri, Wabunge, pamoja na viongozi wote kwanini tusiwe na sera za muda mrefu (miaka 10 - 20) au mfupi (miaka 2 mpaka 5) za kiuchumi kwa taifa kwenye mambo tofauti?. Juhudi za viongozi wote mlijitahidi kwenye kuitangaza nchi hasa kwenye utalii na mengine mengi lakini kuna mambo tunaweza yasahau madogo ama hata makubwa ambayo yanahitaji jicho makini na la tofauti ili kuendeleza taifa letu la Tanzania na kuweka ahuweni na imani kwa wana wa Tanzania hasa swala la uchumi :-

1. Itungwe sera ya kuwekeza kwenye miundo mbinu ya nchi kuanzia barabara, maji, umeme majengo ya shule na biashara.
Kama taifa na viongozi wake wanaweza kuweka sera ya miaka mitatu sababu tumesha jitangaza vya kutosha na kuwekeza hela kwenye utalii na mambo mengine. Je tunaweza jaribu haya:-

(i) Tujitahidi kuanza sera ya maji kwenye kila kijiji fedha zitakazo pangwa kwa ajili ya matangazo basi tuanz la maji na upatikanaji wake, kutokana na matumizi yake kuwa muhimu kwenye shughuli za kila siku. Hii tuipe hata sera ya miaka miwili itategemea na serikali itapanga bajeti kiasi gani kwa sababu kasi ya mradi nadhani huwa inategemea fungu lililowekwa pamoja na ufanisi wa watendaji wa huo mradi lakini muda utakuwa muhimu zaidikwenye haya mambo.

(ii) Iwepo sera ya kusambaza umeme kila kijiji kila mtaa hii imeshafanyika huenda sehemu kubwa ya nchi inabidi tuupeleke kote ila hapa inatakiwa uwepo uangalifu na nyumba inayo fungiwa umeme ili kukwepa gharama za uharibu pale ambapo majanga yakitokea hata madogo kama upepo na ikaharibu nyumba isio imara, kwasababu tunaelewa hali zetu watanzania vidole vyote havilingani na ndivyo hivyo kwenye swala la ujenzi pia kila nyumba itajengwa kwa ubora kutokana na kipato cha mtu. Hii sera ya umeme inaweza kuja baada ya maji kwa sababu uwekezaji wa bomba za maji huwa zina usisha uchimbaji wa mitaro mikubwa.

(iii) Kwenye sera ya tatu ni ujenzi wa barabara tujitahidi kila eneo ambalo linatumika kama chanzo kikubwa cha mapato basi barabara iweze kupita hapo ya kiwango bora cha lami tujitahidi kupeleka hizi barabara mashambani karibia na migodi, na hata mipakani mwa mbuga za wanyama bila kusahau vijijini kwa wakulima hii itasaidia usafirishaji wa hizi rasilimali zote pamoja na watu kufika kwenye maeneo hayo kwa usalama, uharaka na bila shida yoyote na hata mboga mboga pamoja nafaka zita safirishwa kwa muda mfupi kuliko sasa.
Kwa sababu kwenye uchumi wowote ili ukuwe tunatakiwa tujitahidi kupunguza muda wa usafirishaji wa rasilimali ama utengenezaji wa vitu kwa namna hiyo tutaifanya Tanzania kuwa nchi ambayo iko makini na haraka kwenye sekta na swala la uchukuzi.

(iv) Ya nne itashangaza lakini itasaidia tuwekeze kwenye ujenzi wa shule vyuo vikubwa hospitali za hadhi ya juu kwenye kutibu magonjwa na hata kuwekeza kwenye tafiti za kidunia sababu hakuna nchi ilio endelea kwa kushabikia mpira miziki na mengine kwa kiwango kinachozidi utafiti yaani researches, nchi zinazo endelea ni kutokana na sera nzuri za kwenye utafiti either science, uchumi na siasa tusome duniani nchi nyingine zina fanya nini na sisi tunaweza changia nini hii itaweza vutia wana zuoni wengi kuja Tanzania na kusoma mfano tunaona nchi yavafrika kusini ukiachana na miundombinu ila watu wengi wanatamani pia kwenda kusoma huko ukienda ulaya na Asia ndio usisema kila mana wa Afrika anapatamani.

@ Kwenye sera ya ujenzi wa shule yaani vyuo vikubwa tujitahidi kila mkoa uwe na chuo chenye hadhi kama ya chuo kikuu dar es salaam ama zaidi hii itachangia pia uinuaji wa uchumi kwenye mikoa iliokuwa haionekani na pia itafanya wanafunzi wanaomaliza mikoa husika kusoma vyuo vikuu na vikubwa kwa kila mkoa ambao atakuwepo na wengine wanaweza pia kuomba nafasi ya kusoma kwenye hivyo vyuo lakini la muhimu hapa itaamsha shughuli za kiuchumi kwa kila mkoa wa Tanganyika na Zanzibar.

Kwa namna hii nadhani tunaweza peleka taifa letu mbele zaidi ila inahitaji watu wenye upendo wa kweli kwa nchi yetu. Tukumbuke tunaweza tukala kila kitu na kuiporoka Tanzania na hata kuona watu wake hawastahili mazuri ama wana stahili lakini sio kwa kiwango kikubwa ila usije ukasahau hii ardhi itakayo kupokea siku ikikuhitaji utajisikiaje umefanya mambo ambayo hukuweza kuondoka nayo wakati yalikuwa kwenye uwezo wako tuipende Tanzania tuipende afrika naelewa ni ngumu kwa sera zote kufanyika kutokana na vikwazo vingi vitakavyoweza kuinuka lakini tujitahidi hakuna Tanzania nyingine zaidi ya hii tunaweza kimbilia ulaya kula na kukaa ila kama ulitokea kwenye uso wa Tanzania basi kumbuka kuna siku utataka ukurudishe ardhi yake.

La muhimu ni tushikamane naimani hofu ya kesho kwa wengi wetu inaweza pungua na hata kuondoka, uliepewa dhamana ukishamaliza kufikiria ya familia basi fikiria ya kesho juu ya watanzania weka imani yao hata siku ukiondoka waseme kweli hapa alifanya kwa alipoweza japo huwezi fanya kwa asilimia sababu hata wana fizikia efficiency of machine isn't 100% yaani ufanisi wa mashine kwenye kazi zake hauwezi kuwa asilimja mia.

Ahsanteni nilikuwa na mengi juu ya hili swala nadhani tuiweke mada ya siku nyingine.
Inaendelea wana jamii


Kwenye swala la biashara, Tanzania ni lango la nchi za kusini mwa afrika tunaweza anzisha viwanda vya ndani vidogo hata vikubwa vya uzalishaji wa bidhaa zitumiwazo na wa afrika wengi na uhitaji wake ni mkubwa ili tuweze kuziuza na kusafirisha kwa nchi nyingine.

Nadhani kwenye hili tutaimarisha hela yetu zaidi kuliko kung'ang'ania masoko ya Ulaya, Ssia, na Amerika yenye vigezo na changamoto kubwa lakini tukikenga ukanda wetu basi hatutakuwa na wasiwasi hata wakianza kutokuangalia bidhaa zetu sababu tutakuwa la ndani na hilo ndio inaipa jeuri nchi kama china sababu ukiachana na ukweli kwamba ku export nchi kama za Amerika na Ulaya kuwa na faida lakini pia wazalishaji wa ndani wamejiwekea uhakika wa masoko ya nchi jirani za Asia na hata nyingine kama Urusi hili nalo tunaweza liangalia kwa ukanda wetu wa kusini mwa afrika

Na hili itabidi tuhusishe watu wote hata wahitimu wa vyuo nadhani nchi ikiwa na miundombinu mizuri na upatikanaji wa baadhi ya vitendea kazi na mashine inaweza changia kwa wahitimu, vijana wote, pamoja na watu wengine kuanza kidogo kwenye sekta ya biashara kupitia kilimo, na viwanda vidogo vya ndani vinavyo tambulika

Na kwenye suala la biashara inabidi uwepo uhalisia wa kufanya biashara zenye uhitaji na tija kwa watanzania na nchi zilizo zunguka Tanzania hii tunaweza wekeza sana kwenye viwanda vya mwanzo kwenye utengenezaji wa mashine za kilimonana vingine vingi tutakavyo ona vina umuhimu na hii itapelekea Tanzania kuwa mzalishaji mzuri na mkubwa wa vyakula na mbegu ambazo nchi kama Urusi na China hata Ukraine wanapata na walipata mapato makubwa kupitia huko.

Hili litahitaji pia upendo wa juu kwa taifa sababu hapa tunaweza lima mazao yanayo letwa kwetu kwa wingi na tuka badilisha muelekeo yakawa mazao ambayo tuna yalima na kuzalisha kwa wingi ama kiwango ambacho kina tosheleza na kuweza kuuza kwa wengie.

Kwa namna hii Tanzania tunahitaji malengo na sera thabiti kwa taifa letu ili tuweze kufuta ufukara kwenye nchi hii nawasilisha mwenye mawazo ruksa kuongeza natamani na wenye nafasi mtakao pitia basi sio mbaya mkaokota la kuokota na likafanyiwa kazi ahsanteni

La muhimu ni tushikamane naimani hofu ya kesho kwa wengi wetu inaweza pungua na hata kuondoka, uliepewa dhamana ukishamaliza kufikiria ya familia basi fikiria ya kesho juu ya watanzania weka imani yao hata siku ukiondoka waseme kweli hapa alifanya kwa alipoweza japo huwezi fanya kwa asilimia mia sababu hata wana fizikia wanasema efficiency of machine isn't 100% yaani ufanisi wa mashine kwenye kazi zake hauwezi kuwa asilimia mia.

Ahsanteni nilikuwa na mengi juu ya hili swala nadhani tuiweke mada ya siku nyingine
 
Hii ni quote ambayo sina uhakika na source yake lakini ina make sense sana ili kupata maendeleo ya kweli

"To ensure a thriving nation, it is essential to protect and guarantee genuine private enterprise, ownership rights, and democratic principles. When people have the freedom to engage in private business, secure their property, and participate in a true democracy, they are more likely to work hard, accumulate wealth, and contribute to the overall prosperity of the country."
 
Hii ni quote ambayo sina uhakika na source yake lakini ina make sense sana ili kupata maendeleo ya kweli

"To ensure a thriving nation, it is essential to protect and guarantee genuine private enterprise, ownership rights, and democratic principles. When people have the freedom to engage in private business, secure their property, and participate in a true democracy, they are more likely to work hard, accumulate wealth, and contribute to the overall prosperity of the country."
Hii ni kweli kwa Kila nchi na viongozi wake lazima iwe kama utii wa mgongo kwa wananchi wake yaani mifumo iwe imara kabla na baada ya mtu kunufaika kiuchumi itapelekea hata kuwa na moyo wa kuliendeleza na kulichangia taifa pasipo manung'uniko
 
Tz Ili isimame CCM inatakiwa itoke hapo madarakan ,ipishwe watu wenye weledi wa uongozi na c hawa wachumia tumbo wa ss
edon66 na je ni taasisi ipi au chama kipi kinafaa kuchukua hiyo nafasi na unadhani wanatakiwa na sera zipi ili tusonge mbele zaidi?
 
Sisiem ndio sababu kubwa ya umaskini. Ili maendeleo yawepo mabadiliko ya kisiasa ni muhimu na mabadiliko hayo ni kuiondoa ccm madarakani kwanza.
Lakini pasipo kuwa na sera nzuri na zenye tija kwa nchi unadhani bado wanaweza badili hali hii na kuipeleka nchi sehemu nzuri baada ya kupata kila kitu? sababu watu wanaweza dhani shida ni mtu ama taasisi fulani, lakini huenda kuna mengi
 
Hii ni kweli kwa Kila nchi na viongozi wake lazima iwe kama utii wa mgongo kwa wananchi wake yaani mifumo iwe imara kabla na baada ya mtu kunufaika kiuchumi itapelekea hata kuwa na moyo wa kuliendeleza na kulichangia taifa pasipo manung'uniko
CCM na majangiri mengi Africa wakikuchukia basi wanakimbilia kukusingizia uraia, madawa ya kulevya, kodi etc, then wanaishia kukufungia biashara na mzigo wa kodi na kutaifisha mali zako, na ukiwa una biashara una support wapinzani watakufanya mbaya tuu, kwa kweli hata tufanye kazi vipi lakini bila protections ya haya majanga ya kujitakia tutakuwa maskini na machawa mpaka mwisho wa dunia
 
Uko sahihi lakn kwa ninavojua akil za wabongo duuuh itachukua mda sana
Huenda ni kweli kwa asilimia kubwa ikachukua muda, lakini ni vema tuwe na dira pamoja na pakuanzia tunao waona wote duniani wamewekeza sio tuu kwenye hayo mambo lakini hata mengine mengi. Nadhani tukiamua inawezekana kikubwa ni kujitoa sio mengi yana fanyika Tanzania ila kuna mengine yakiguswa yata kuwa na impact kubwa zaidi
 
All the big revolutions, whether it’s the Industrial Revolution, the Arab Spring, those changes happened by economic and social shifts brought about by the people’s voices, and those things weren’t voted for. Most of our changes today are brought about through technology, not by voting.narudia TECHNOLOGY
 
CCM na majangiri mengi Africa wakikuchukia basi wanakimbilia kukusingizia uraia, madawa ya kulevya, kodi etc, then wanaishia kukufungia biashara na mzigo wa kodi na kutaifisha mali zako, na ukiwa una biashara una support wapinzani watakufanya mbaya tuu, kwa kweli hata tufanye kazi vipi lakini bila protections ya haya majanga ya kujitakia tutakuwa maskini na machawa mpaka mwisho wa dunia
Kabisa ni kweli ulilosema kwa nchi za afrika, lakini tunaweza kuondokana na siasa na mfumo wa namna hiyo kama tukiamua kuwa na mfumo imara utakao simamia maslahi ya nchi kuliko watu wala vikundi vingine nadhani tunaweza kulipa muda
 
All the big revolutions, whether it’s the Industrial Revolution, the Arab Spring, those changes happened by economic and social shifts brought about by the people’s voices, and those things weren’t voted for. Most of our changes today are brought about through technology, not by voting.narudia TECHNOLOGY
Ni kwelii kwa dunia ya sasa ili Tamzania iende mbele zaidi tunahitaji teknolojia nzuri na yenye kiwango kikubwa, Waliopo kwenye sehemu zao wana jitahidi pia japo kuongoza nchi na ikatulia hata kama sio kila kitu kinapatikana ni meema pia, kwa hili wazo linatakiiwa lichukuliwe tuwekeze sana kwenye tafiti za kisayanasi kama technolojia, kisiasa na Kiuchumi kwa kusoma na kuelewa dunia inapoenda naimani wapo watu namna hiyo wanashauri lakini ikisikika mbiu mbili tatu inawezekana likafanyika zaidi na tukaoma matokeo.

Kwa nchi zetu za afrika tuwekeze sana kwenye teknolojia na swala ya uchumi, pamoja na siasa imara isio na makundi wala weledi mdogo wa kiupambe zaidi kuliko ufanisi, kwa nchi zilizo endelea ni ngumu sana wao kwa wao kuzozana kisiasa kwa mtindo wa mind games siku 360 kama afrika yetu inatakiwa itoke huko na Tanzania tuoneshe mfano wa mabadiliko na mageuzi ya kiuchumi zaidi na wote wataamka kama lilivyokuwa miaka ya nyuma 1950's mpaka 1970's, tuna ushawishi na tuna huo uwezo.
 
Jeshi haliwezi hii kazi mkuu na vyama vikafutwa jeshi likaongozaa nchii maaana tunakoelekea c siko kbs..
Sidhani kama jeshi kuongoza inakuwa solution kwa nchi yetu imetulia na ina amani, nadhani zinaweza wekwa sera na zitungiwe sheria kali ili kiongozi ajue kabisa bila utekelezaji zitaweza muharibia hatua fulani ya maisha au maisha yake kwa ujumla.

Na kuhusu swala la jeshi nadhani hatutakiwi kuombea Tanzania kuwa kwenye machafuko na sidhani kama itatokea na kama ipo tuombe isiweze sababu amani yetu hapa inalisha watu zaidi hata nnje ya Tanzania huu ni mtazamo unaohitaji kutuliza kichwa.

Nchi kuwa na mageuzi kwa njia ya vita sio suluhisho au muafaka wa kupata maendeleo, kwa Tanzania kama lango kuu la kwenda kusini na hata kwenda kaskazini, kwa wanaotokea chini ni sehemu muhimu kubaki salama muda wote unadhani kukiwa hakueleweki kama majirani huu ukanda utakuaje na rasilimali hizi?

Huenda hata dunia kwa ujumla utaweza kupaogopa, kushoto pachafuke katikati pachafuke ni hatari.

La msingi ni sera ziwekwe zaidi na zilizopo zisimamiwe pasipo utayari wa kufaidisha watu wachache, lakini tujaribu hizi sera ngumu na nzito ndani ya miaka 20 tuone Tanzania itakuwa wapi wana jamii
 
kuna mambo tunaweza yasahau madogo ama hata makubwa ambayo yanahitaji jicho makini na la tofauti ili kuendeleza taifa letu la Tanzania na kuweka ahuweni na imani kwa wana wa Tanzania hasa swala la uchumi :-
Mkuu 'Rijali jandoni', nimekusoma toka huko juu, nikawa naona maneno mengi sana na mizunguko mingi, kama ilivyo kawaida yetu waswahili.
Hapana, sijasema kuwa uliyo eleza huko juu hayakuwa ya maana; lakini siyo yenye uzito na kuweka mwelekeo wa nchi kupata maendeleo stahiki.

Hayo maneno machache niliyo nyanyua hapo juu, natamani unge yawekea uzito zaidi, na kudadavua ulilenga nini hasa. Mimi nimeona hapo ndipo penye uzito sahihi; mahali pa kuanzia kukiwa na viongozi wenye maono juu ya nchi hii.

Kuepuka maneno mengi, nitoe mfano ulio niijia akilini nilipo soma maneno yako hayo.
Nchi ya Korea Kusini; ambayo miaka ile ile sisi tukipata uhuru (miaka ya 1960s), nchi hiyo ilikuwa ni nchi maskini sana, nchi iliyo sumbuliwa na janga la njaa; na mbaya zaidi ikawa imo vitani na wenzao wa Kaskazini.

Hicho ki-nchi cha Korea kusini, hakina sifa nyingi kama ulizo imiminia Tanzania yetu

Sasa nakuomba ukune kichwa: hawa watu wa Korea kusini, ambao sasa ndio tunao wakimbilia kwenda kupata missada, wao walifanya nini kwa muda mfupi vile hadi wakafikia walipo sasa?

Ndiyo: Najuwa tofauti zao na sisi kijadi. Wao jamii zao zilikuwa na historia ya muda mrefu sana kuliko sisi, ambao kama taifa, historia yetu inaanzia wakati wa ukoloni. Hii ni tofauti muhimu, lakini siyo inayofanya sisi tubaki nyuma sana kulingana na Korea Kusini.

Hebu tafadhali, ifanyie kazi 'assignment' hiyo; utueleze hawa Korea Kusini, ambao hawana mbuga za wanyama, hawana madini kama sisi, hawana ardhi ya kutosha kama sisi, n.k., n.k.; wao ni mambo gani hasa yaliwasukuma mbele haraka kiasi kile?

Huko chini ya mada yako hii muhimu sikufanikiwa kupasoma. Mada inapo kuwa ndefu bila ya sababu huchosha sana kusoma.
Sijui, lakini endapo niliyo kuomba uyatafute umeyaweka huko chini, basi nitakulaumu kwa uandishi usio kuwa na mpangilio mzuri; uandishi wa kumchosha msomaji huko mwanzo na mambo rasharasha, na yale ya muhimu zaidi anayaficha huko mwisho, wakati msomaji tayari akili iksha jichokea na mizunguko mingi.

Hii ni mada nzito sana, lakini ndio hivyo tena, sisi waswahili mambo ya aina hii hatuyapi uzito wowote stahiki.
Tukiletewa mada ya "mikeka" ya uteuzi au utumbuzi; hapo ndipo utakapoona akili zetu zilipo lalia.
Inasikitisha.
 
Mkuu 'Rijali jandoni', nimekusoma toka huko juu, nikawa naona maneno mengi sana na mizunguko mingi, kama ilivyo kawaida yetu waswahili.
Hapana, sijasema kuwa uliyo eleza huko juu hayakuwa ya maana; lakini siyo yenye uzito na kuweka mwelekeo wa nchi kupata maendeleo stahiki.

Hayo maneno machache niliyo nyanyua hapo juu, natamani unge yawekea uzito zaidi, na kudadavua ulilenga nini hasa. Mimi nimeona hapo ndipo penye uzito sahihi; mahali pa kuanzia kukiwa na viongozi wenye maono juu ya nchi hii.

Kuepuka maneno mengi, nitoe mfano ulio niijia akilini nilipo soma maneno yako hayo.
Nchi ya Korea Kusini; ambayo miaka ile ile sisi tukipata uhuru (miaka ya 1960s), nchi hiyo ilikuwa ni nchi maskini sana, nchi iliyo sumbuliwa na janga la njaa; na mbaya zaidi ikawa imo vitani na wenzao wa Kaskazini.

Hicho ki-nchi cha Korea kusini, hakina sifa nyingi kama ulizo imiminia Tanzania yetu

Sasa nakuomba ukune kichwa: hawa watu wa Korea kusini, ambao sasa ndio tunao wakimbilia kwenda kupata missada, wao walifanya nini kwa muda mfupi vile hadi wakafikia walipo sasa?

Ndiyo: Najuwa tofauti zao na sisi kijadi. Wao jamii zao zilikuwa na historia ya muda mrefu sana kuliko sisi, ambao kama taifa, historia yetu inaanzia wakati wa ukoloni. Hii ni tofauti muhimu, lakini siyo inayofanya sisi tubaki nyuma sana kulingana na Korea Kusini.

Hebu tafadhali, ifanyie kazi 'assignment' hiyo; utueleze hawa Korea Kusini, ambao hawana mbuga za wanyama, hawana madini kama sisi, hawana ardhi ya kutosha kama sisi, n.k., n.k.; wao ni mambo gani hasa yaliwasukuma mbele haraka kiasi kile?

Huko chini ya mada yako hii muhimu sikufanikiwa kupasoma. Mada inapo kuwa ndefu bila ya sababu huchosha sana kusoma.
Sijui, lakini endapo niliyo kuomba uyatafute umeyaweka huko chini, basi nitakulaumu kwa uandishi usio kuwa na mpangilio mzuri; uandishi wa kumchosha msomaji huko mwanzo na mambo rasharasha, na yale ya muhimu zaidi anayaficha huko mwisho, wakati msomaji tayari akili iksha jichokea na mizunguko mingi.

Hii ni mada nzito sana, lakini ndio hivyo tena, sisi waswahili mambo ya aina hii hatuyapi uzito wowote stahiki.
Tukiletewa mada ya "mikeka" ya uteuzi au utumbuzi; hapo ndipo utakapoona akili zetu zilipo lalia.
Inasikitisha.
Habari Kalamu, nilianza kwa kuelezea hayo yote hapo juu ili sote tupate uelewa ni namna gani Tanzania inaweza kujikwamua kutoka iliopo kutokana na upande na sehemu ilipo ninge anza na nini kifanyije nadhani watu wasingeweza kuelewa moja kwa moja nafasi gani (advantages) ambazo tunazo kama Tanzania

Kuhusu swala la korea kusini na nchi nyingine za Asia ziliweza changamkia kwa haraka mapinduzi ya viwanda ya pili japo hawakufanya kwa uharaka lakini walijitahidi kwa uwezo wao kwa kipindi hicho hiyo Era kwa sasa imeshapita kwa wenzetu lakini kwa Afrika ina enda kuanza japo tukianzisha hivyo viwanda na teknolojia ni nani atakuwa wateja wa hayo mataifa yaliyo jiwekeza huko kabla ya Afrika?

Kuna mmoja pia hapa alianfika teknolojia ni muhimu sana haya tunayo eleza yanaweza yafanyike ila bila kujitangaza na kurusha kwenye vyombo vya habari maana kufanya hivyo ni kujinasua kwenye mtego wa muda mrefu na wakati huohuo kujibebesha bomu mkononi

Kwahiyo kwa kuhitimisha Tanzania inahitaji mapinduzi ya hizo sekta ukiweka na viwanda vya awali na vya kati kama taifa ni mida wa kuzima siasa za kichama na makundi pamoja na uchawa uweledi uje kwenye nafasi yake nauhakika miaka 25 itakuwa mingi sana kwenye swala la kubafilisha uchumi na jamii yetu kuwa bora zaidi.
 
Back
Top Bottom