Kwa tukio la kuuliwa Ali Kibao nawatetea polisi.Ni kundi lenye nia mbaya na nchi

Kwa tukio la kuuliwa Ali Kibao nawatetea polisi.Ni kundi lenye nia mbaya na nchi

Kuna wakati kukaa kimya ni jambo zuri sana kuliko kuongea, Unachojaribu kutaka kuongea sio tu kwamba ni ujinga bali ni jaribio lingine la unyama unaofanywa na kundi la wajinga kutetea ujinga amabo utakuja kuwagaharimu hata nyinyi wenyewe.
Kwanza mtu kama wewe unaamini uwepo wa vyama vingi ni dhambi, kwahiyo haya unayojaribu kutaka kuongea ni muendelezo wa imani yako ya kishetani dhidi ya dhulma inayoendelea.
Rais wako kajaribu kuongea lakin kwakuwa hata akili hamna hamjui hata kwenda na mwendo wa kiongzi wenu.
Ukijifanya una akili sana mwishowe unakuwa mjinga pia.
Usilazimishe kwamba sote tufikiri kama wewe.Hakutakuwa na faida ya kupewa akili.
 
ni akili za mtu aliyetimamu sana.Tumepita kati na kati.Kama waliotekeleza ni polisi basi ni wajumbe wa kundi ovu hakuna dalili ya kutumwa na jeshi lenyewe.Na hilo kundi ovu laweza kuwajumuisha mpaka wanachama wa vyama vya upinzani.
Sasa mtu anayetumiwa na watu waovu huku akijua, ni mtu wa kumtetea?
 
Acha dharau kwa jeshi la polisi ,unazidi kulidhalilisha kwamba hawana kitu ndiyo maana mtu anakuja kutekwa mchana kweupe bila wao kujua....Unawapaka matope vyombo vyote vya ulinzi na usalama...yaani wahuni wanakuja kuteka bus na kutokomea na mtu bila kukamatwa? Unataka kusema kama waliofanya hivyo sio wao wenyewe basi Mama Kizimkazi alifumue jeshi lote maana wananchi na nchi haiko salama.
Jeshi la polisi sio Mungu kwamba wanaona na kujua kila kitu.Wacha kututia kwenye ushirikina.
Kama wangekuwa wanajua kila kitu basi kusingekuwa na haja ya vituo vya polisi.
 
Kweli unabii unatumia. Tazama kila awazalo mwanadamu ni ovu na kamwe mwanadamu hatoifanya Dunia ikawa sehemu salama

Vyombo vya ulinzi vituletee hiko kikundi maana utekaji ulifanyika mchana kweupe

Mkuu wa nchi alisema ni Drama

Speaker wa bunge alisema hakuna utekaji nchini


Vyombo vya ulinzi vinaendelea na uchunguzi


Tanzania is bleeding Kwa maslahi ya watu wachache wanaohisi hili taifa ni lao
 
so, jeshi la polisi lisipokuja na majibu na kumbuka si mtu kwanza kutekwa kwa miezi hii ya karibuni na polisi bado hawajatoa majibu ya kueleweka siku zote ni kama vile wanapinga hili kuwa lipo. iwe alikuwa mgambo au mwanajeshi, tukio limetokea hadharani bila kuleta majibu itakuwa wanajua nani kafanya hiki kitendo. kitendo cha mtu kutekwa hadharani na watu wenye cruiser na mitutu inabidi iwe alarm kwao pia wachunguze kweli kweli maana inaonyesha kuwa kumbe kuna hatari ya kiusalama. kama likipita hivi hivi basi watakuwa wanajua nini kinaendelea.
wewe ndio umetumia akili zako ili watu wafaidike na uchambuzi wa tukio
 
Kazi ya Polisi ni kulinda Usalama wa raia na mali zao!
Wanastahili lawama zote.
 
Unataka kusemaje mkuu? Umeandika maelezo marefu lakini hayana kichwa wala mguu.
Unachokusudia kusema ni kwamba watu wote bila kuamini unachoamini wewe ni wajinga.Na kwamba wewe unajua zaidi kuliko sisi wakati hoja zako hazioneshi hivyo.
 
Ukijifanya una akili sana mwishowe unakuwa mjinga pia.
Usilazimishe kwamba sote tufikiri kama wewe.Hakutakuwa na faida ya kupewa akili.
Ndio kama ulivyothibitisha kiwango cha ujinga ulichonacho kichwani mwako, sio kila fikra kwa wakati fulani inaleta tija kisa tu umeruhusiwa kufikiri tofauti na wengine kwa uhuru, unawaza kijinga halafu unajitetea kwa kisingizio cha uhuru wa kufikiri.
Je kama mimi nitafikiria kuwa unatakiwa kubakwa mbele ya wazazi wako au mkeo kama unaye untasema nipo swa kwakuwa nimeamua kujipa uhuru wa kufikiri hivyo? Sasa tujaalie kuna kundi linataka kuwachafua unaowaita viongozi, JE Polisi wameshimdwa nini kwenye nchji yenye kila kitu kuwabaini hao watu wanmaouwa Watanzania wenzetu kila siku? Tumia akili hata kama akili huna na kukaa kimya pia sio ujinga ni njia bora ya kluja na hoja zenye nia njema hata kama wewe ni miongoni mwa hao waovu.
 
Sijafuatilia utekwaji na mauwaji ya huko nyuma.Lakini kwa hili na mauwaji ya Ali Mohamedi Kibao nina uhakika vyombo vya usalama havijahusika.
Waliohusika ni kundi lenye nia ya kuleta fujo nchini na ni wapinzani wa chama tawala.Waweza kuwa ni wakereketwa wa chama chochote kile cha upinzani na hata Chadema chenyewe.
Kwa maana hiyo hilo kundi halikutumwa na vyombo vya usalama na wala viongozi wa vyama vya upinzani isipokuwa wameona wakiongeza kasi ya matukio ya namna hiyo katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi basi kutatokea sintofahamu na kuitikisa nchi kwa maslahi yao.
Sababu kuu ya kuamini hivyo kwanza ni aina ya mtu waliyemlenga ambaye ana nafasi kubwa kwenye chama cha Chadema na namna walivyoamua kumuua.
Ingekuwa ni ugomvi na visasi vya kawaida basi wangemfuata nyumbani kwake na usiku au akiwa kwenye gari yake au ya ndugu zake ili isiwe rahisi kuleta hisia kwa wananchi.Badala yake wamekwenda kumkamata ndani ya basi na mchana kweupe.Kule walikomtupa ni maeneo yale yale maarufu wanakopatikana watu waliouliwa kiujambazi.
Kwanini wasimzike kwenye kaburi ambalo ingechukua muda kugundulika.Madhumuni yao ni kufanya matangazo kutokana na kifo chake ili kutokee fujo.
Kwa tukio hili sasa ndio uwezekano wa kupatikana waliokuwa wakitenda mauwaji watajulikana na kitendawili kuteguliwa pindi serikali itakapotia nia kulihitimisha.

Mh Rais ameagiza apelekewe ripoti ya kina nani waliyomteka na kumuua Mzee Meddy Kibao.....Kama Polisi wakishindwa basi tutakuwa hatuna jeshi kabisa ,kama issue ndogo kama hiyo wakishindwa vipi issue kubwa?

Kuwapata watekaji ni simple sana uki-envolve wataalam wa Cyber na watalam wa mitandao ya simu ,yaani ndani ya 3hrs tu unawapata watekaji wote maana walikuwa wanatumia simu means waliacha traces.

Hatua ya za kufanya:-

1. Kitengo cha Cyber Crime Central hapo na TCRA wakachukue real time triplets muda ambao bus likiwa linatoka Stand ,hapa manifesto waakikishe ilikuwa filled na yule mtekaji aliyekuwa ndani au abiria wahojiwe kujua yule mtekaji aliyekuwa ndani alipandia wapi,kama alipandia mwanzoni basi Watu wa Cyber/TCRA wachukue cells/sites dumps ambayo itakuwa na namba zote zilizokuwa covered maeneo ya magufuli stand.

2.Kisha wachukue tena Cells/Sites dump bus lilipotekwa hapo MJAPAN/TEGETA Complex ,hapa itacover sites zinazozunguka Tegeta/Bahari beach/Wazo/Boko/Ununio...Hapo inamaanisha hii dump ya pili itakuwa na numba zilizotoka mbezi+zilizopo maeneo hayo ya bus lilipotekwa.

3.Hatua ya tatu ni kufanya VLOOKUP -Hapo ni Microsoft Excel tu ,imatch numbers zilizokuwa Maguful stand na numbers zilizokuwa Tegeta wakati bus linatekwa ,hapa zitakazomatch ni zile ambazo zimetoka magufuli,hii inaamisha ndiyo watakuwa abiria wote waliotoka stand ya magufuli.

4.Baada ya watekaji kumchukua Meddy Kibao means bus likaendelea na safari na watekaji wakaondoka kuelekea Ununio then hapo wachunguzi wachukue cells/sites dump nyingine baada ya watekaji na bus kuondoka,then wafanye tena VLOOPUP ,hapa itamatch numbers zilizotoka magufuli/abiria ambao waliokuwa wanaenda tanga lakini baada ya bus kuondoka still zikasoma eneo hilo hilo la tegeta/boko/ununio/bahari beach ,hizo number zitakazomatch nidyo zitakuwa za hao watekaji maana ndiyo waliotoka magufuli na wakaishia tegeta/ununio/bahari beach.
 
Kuzuia hisia za mwenzako ni aina nyengine za upumbavu uliozidi kiwango.
Kama una taarifa zaidi kinyume na hizo basi tumia uhuru wako uziwasilishe hapa.
Pia kutetea hisia za mwenzako ambazo hazijabeba hoja za msingi na zisizokuwa na ushahidi wa kutosha nao pia ni upumbavu mwingine!
 
Pia kutetea hisia za mwenzako ambazo hazijabeba hoja za msingi na zisizokuwa na ushahidi wa kutosha nao pia ni upumbavu mwingine!
Mpaka sasa ni hisia tu.Ushahidi hatujaupata ili tuutetee au tuukatae.
Jee wewe una ushahidi wowote.
 
Unachokusudia kusema ni kwamba watu wote bila kuamini unachoamini wewe ni wajinga.Na kwamba wewe unajua zaidi kuliko sisi wakati hoja zako hazioneshi hivyo.
Mkuu usinifafanue mimi; fafanua hoja yako tuielewe.
 
Mh Rais ameagiza apelekewe ripoti ya kina nani waliyomteka na kumuua Mzee Meddy Kibao.....Kama Polisi wakishindwa basi tutakuwa hatuna jeshi kabisa ,kama issue ndogo kama hiyo wakishindwa vipi issue kubwa?

Kuwapata watekaji ni simple sana uki-envolve wataalam wa Cyber na watalam wa mitandao ya simu ,yaani ndani ya 3hrs tu unawapata watekaji wote maana walikuwa wanatumia simu means waliacha traces.

Hatua ya za kufanya:-

1. Kitengo cha Cyber Crime Central hapo na TCRA wakachukue real time triplets muda ambao bus likiwa linatoka Stand ,hapa manifesto waakikishe ilikuwa filled na yule mtekaji aliyekuwa ndani au abiria wahojiwe kujua yule mtekaji aliyekuwa ndani alipandia wapi,kama alipandia mwanzoni basi Watu wa Cyber/TCRA wachukue cells/sites dumps ambayo itakuwa na namba zote zilizokuwa covered maeneo ya magufuli stand.

2.Kisha wachukue tena Cells/Sites dump bus lilipotekwa hapo MJAPAN/TEGETA Complex ,hapa itacover sites zinazozunguka Tegeta/Bahari beach/Wazo/Boko/Ununio...Hapo inamaanisha hii dump ya pili itakuwa na numba zilizotoka mbezi+zilizopo maeneo hayo ya bus lilipotekwa.

3.Hatua ya tatu ni kufanya VLOOKUP -Hapo ni Microsoft Excel tu ,imatch numbers zilizokuwa Maguful stand na numbers zilizokuwa Tegeta wakati bus linatekwa ,hapa zitakazomatch ni zile ambazo zimetoka magufuli,hii inaamisha ndiyo watakuwa abiria wote waliotoka stand ya magufuli.

4.Baada ya watekaji kumchukua Meddy Kibao means bus likaendelea na safari na watekaji wakaondoka kuelekea Ununio then hapo wachunguzi wachukue cells/sites dump nyingine baada ya watekaji na bus kuondoka,then wafanye tena VLOOPUP ,hapa itamatch numbers zilizotoka magufuli/abiria ambao waliokuwa wanaenda tanga lakini baada ya bus kuondoka still zikasoma eneo hilo hilo la tegeta/boko/ununio/bahari beach ,hizo number zitakazomatch nidyo zitakuwa za hao watekaji maana ndiyo waliotoka magufuli na wakaishia tegeta/ununio/bahari beach.
Taarifa za mwanzo za kutekwa kwa huyo mzee zilisema ndani ya basi kulikuwa na askari wa traffic na namba zake zikatolewa.
Mlolongo ulioutoa ni wa kitaalamu na lazima vyombo kadhaa vya kiserikali vihusishwe.Kabla ya hapo ni kufuatiliwa huyo askari ili aeleze alichoshuhudia.
Na kwa maelezo tuliyosoma mpaka sasa ni kuwa watekaji waliteremka kutoka kwenye gari na mitutu ya bunduki.Kwa maana hiyo hawakutokea kituo cha Magufuli.
Jee eneo husika hakukuwa na kamera yoyote ile ya binafsi hata iwapo hakuna kamera za barabarani za mamlaka ya jiji.
 
Ndiyo mmeamka kuja kutetea, too late mtu wa ndani kishasema yote. Ile sinema yao waliyoicheza, ilikuwa hadharani. Traffic kwenye huo msafara wamemtambua, yeye ni muajiriwa wa Jeshi la polisi, hebu mtuache, tumuomboleze Mzee Ally kwa amani.

Huju jamaa anajiita Webabu ukimsoma vizuri nyuzi zake unaweza gundua kuna fuse imekatika kichwani.

1. Huyu jamaa alileta uzi hapa anamwamrisha mzee Bakhressa aache kufanya biashara kwasababu ya mrengo wa kidini.

2. Ukisoma leo bandiko lake unajiuliza mbona hakuna hoja ya maana anayoweka mbele ya hadhira? Je, huyu ni juha?
 
Sisi tunaopinga kuhusishwa serikali na matukio ya kihuni ndio tunaotetea nchi.
Aina ya viumbe kama wewe ndio mmejaa huko CCM. Uwezo wenu wa kujenga hoja hamana. Mpo kimasilahi na kujipendekeza kama mbwa.

Hapa ilitakiwa kuanzia sasa waziri mkuu, waziri wa mambo ya ndani, mkuu wa usalama na mkuu wa polisi wote wawe wamejiuzuru. Kwa haya matukio yanayoendelea nchini.

Maana yake sisi kama wananchi jukumu tulilowakabidhi wameshindwa. Wapishe waingie wengine.

mjinga kama wewe et unatetea unatetea upumbavu?. Uhai wa mtu ni wathamani kuliko vyeo na fedha.

Tht Y nasema bora ungekaa kimya tu. Kuliko kuandika upumbavu wako hapa.
 
Huju jamaa anajiita Webabu ukimsoma vizuri nyuzi zake unaweza gundua kuna fuse imekatika kichwani.

1. Huyu jamaa alileta uzi hapa anamwamrisha mzee Bakhressa aache kufanya biashara kwasababu ya mrengo wa kidini.

2. Ukisoma leo bandiko lake unajiuliza mbona hakuna hoja ya maana anayoweka mbele ya hadhira? Je, huyu ni juha?
Hana akili huyo dogo.
Ni aina ya watu hawajali thamani ya utu wao
 
Aina ya viumbe kama wewe ndio mmejaa huko CCM. Uwezo wenu wa kujenga hoja hamana. Mpo kimasilahi na kujipendekeza kama mbwa.

Hapa ilitakiwa kuanzia sasa waziri mkuu, waziri wa mambo ya ndani, mkuu wa usalama na mkuu wa polisi wote wawe wamejiuzuru. Kwa haya matukio yanayoendelea nchini.

Maana yake sisi kama wananchi jukumu tulilowakabidhi wameshindwa. Wapishe waingie wengine.

mjinga kama wewe et unatetea unatetea upumbavu?. Uhai wa mtu ni wathamani kuliko vyeo na fedha.

Tht Y nasema bora ungekaa kimya tu. Kuliko kuandika upumbavu wako hapa.
Asante!
 
Back
Top Bottom