Kwa ulimwengu huu wa sasa Fani ya Procurement bado inafundishwa vyuoni kwa sababu gani?

Kwa ulimwengu huu wa sasa Fani ya Procurement bado inafundishwa vyuoni kwa sababu gani?

Soma mada na kuelewa, usikariri ndugu. Mleta mada amekuja kuzungumzia kozi moja mahususi ya Procurement and Supply. Zipo kozi nyingi za ovyo na zisizo na kichwa wala mkia hapa Tz kwa sasa, Procurement and Supply ni mojawapo katika hizo, tena huenda ni kinara.
Wewe unafanya Nini ambacho ni useful kumshinda mtu wa procurement, kwa taarifa tu yeye hasubiri mshahara wa mwisho wa mwezi[emoji16]
 
Pahali napofanya kazi kampuni ya watu zaidi ya 100 mtu mwenye taaluma ya manunuzi na ugavi ni mmoja tu tena kwenye ofisi moja wapo kati ya zilizopo.

Ofisi zilizosalia wanaofanya iyo kazi wanataaluma ya mambo mengine kabisa na wanaifanya vyema tu iyo kazi
 
Wale tulio Soma nao ss wengi wao Ni maafsa mikopo wa hz taasis za mitaani na unamkuta mtu Ana mpk hyo board yao lkn wapi mzingo umegomaa mazima kwa nch za kiafrica hyo coz Ni big noo
Unaongea kana kwamba umekatwa kichwa ndugu, haya niambie watu wangapi wamesoma Sheria na hawapati nafasi hata kwenye hizo taasisi za mitaani
 
inshu niliyo iona hqpa ni kuwa kuna tatizo flani mtu kuiamini taaluma yake ni bora zaidi ya taaluma zingine, serious unakuja bilq hoja unasema procurement ifutwe? kisa et self employment? haya nikakuambia kuwa unaweza kufungua warehouse near port au railwy station, hoja ikawa kuwq ni ngumu kwa flesh graduate, okay iv dokta kujiajiri kwake ni maduka ya dawa na hospital binafsi, vipi kuhush flesh graduate ataweza?
 
Punguzenj chuki na watu wa procurement, ili kukufanya uendelee kuwa na machungu zaidi nj kwamba watu wa procurement wamezungukwa tu na pesa ,

Kuhusu kujiajiri msiwapeleke shule watoto ili muwafundishe kujiajiri huko majumbani
Laiti kama ungejua huenda mimi ni muhanga wa kusomea hiyo kozi huenda usingesema hayo.
 
Laiti kama ungejua huenda mimi ni muhanga wa kusomea hiyo kozi huenda usingesema hayo.
Kwanza nikupe pole, cha pili ukimwambia mtu aliepo kwenye ajira tayari ya Procurement hatokuelewa, cha tatu unaonyesha uko selfish Sana kisa wewe umeisoma ukakosa nafasi basi ndo imekua haina maana!
 
Wale tulio Soma nao ss wengi wao Ni maafsa mikopo wa hz taasis za mitaani na unamkuta mtu Ana mpk hyo board yao lkn wapi mzingo umegomaa mazima kwa nch za kiafrica hyo coz Ni big noo
Kweli kabisa classmate. Watu wanazo mpaka CPA ila wapo mtaani tu. Hali ni mbaya sana.
 
Wewe unafanya Nini ambacho ni useful kumshinda mtu wa procurement, kwa taarifa tu yeye hasubiri mshahara wa mwisho wa mwezi[emoji16]
Wale wajamaa wa procurement (ugavi) wanapiga sana asee 🤣🤣🤣

Niliwahi kufanya nao kazi fulani ya zabuni daaah! Kweli hawasubiri mshahara mwisho wa mwezi

Wanajilipa kwenye tenda wanazosimamia
 
Mkuu mbona Kuna mkunga ambaye hajui kusoma Wala kuandika na anazalisha vizuri je taaluma ya ukunga ifutwe?
Hajui kusona wala kuandika? Bado ni mkunga? KWA dunia ya leo huyo kakariri tu, situation ikibadilika anaweza kweli kufuata maelekezo ya Dr?
 
Sasa kwa Nini accounting ndo isifutwe?
Accounting ni noble course sawa na engineering ama Doctor wa binadamu ama sheria. Hizo ni taaluma zimekuwepo miaka yote kabla ya Kristo.

Procurement ni fani changa sana haina hata miaka 15 Tanzania, ni course ambayo ukiangalia Duniani nasikia haipo maana hii ni kwa ajili ya manunuzi ya umma tu. Sasa usipoajiriwa na serikali utafanya nini?

Hatuwezi kua na fani ambayo inalenga kuajiriwa serikalini tu, haiwezekani.
 
Tukizungumzia uhalisia wa mambo hasa sekta ya taaluma, bado tunachanga moto kubwa mnoo. Course nyingi zinaanzishwa kwetu lakini hazitumiki ipasavyo.
Ukisoma vitabu vya accounting vya wenzetu wa magharibi, utaona katika idara ya fedha kuna finance director, chini wapo accountant and tax personnel. Hizo course zote tumeletewa kwetu, applicability yake ndo kizungumkuti, makampuni mengi hayana tax department, majukum ya kikodi hufanywa na mhasibu. Hawa maelfu wanaosoma kodi wanaishia kufanya related task au kujikuta nje ya mfumo. Japo ni nje ya mada, ina-reflect na mada tunayojadili hasa kwa kada hiyo.
Mkuu, haujakosea hata kidogo. Taaluma ya taxation na procurement ndio hizo hizo za baba na mama moja. Graduate wa taxation asipoajiriwa TRA ndio baaaaas tena kwa maana elimu yetu ipo theoretically saaaana. Elimu haifundishi kazi, wao wanafundisha masuala yaliyo katika muktadha wa Ulaya na Marekani.
 
Kuna kabifu kati ya accountancy na procurement
Hilo bifu litakua la watu wasio na akili. Accountancy ipo zaidi ya miaka 5000, Procurement imeanza Tanzania haina hata miaka 15 uje kua na bifu na noble profession kweli, utakua na akili kweli?
 
Baadhi ya vyuo Duniani vimekuwa vikifanya mabadiliko ya mitaala na kufuta ama kuachana na fani ambazo haziendani na wakati.

Bado najiuliza, kwa Dunia ya sasa fani ya Procurement inafundishwa vyuoni kwa sababu gani? Ni fani ambayo haina umuhimu wowote kwa karne hii ya 21.

Mtoto akisoma Procurement basi umuhimu wake ni aajiriwe Serikalini zaidi ya hapo fani haina umuhimu wowote,na haina msaada wowote kwa mhitimu. kwanini iendelee kufunishwa vyuoni?

Hii fani ilipaswa kuwa sehemu ya course za watu wanaosoma finance/accounts lakini sio kuwa independent course.

Wakati tunafanya mabadiliko ya mitaala ya elimu, tusisahau ya vyuo vikuu. Vyuo wao wanachotaka ni hela tu kwa kuanzisha fani sizizo na maana yoyote ambazo hazina msaada kwa wahitimu.

Fani ya Procurement inapaswa kufutwa. Mzee Kishimba aliwahi kuuliza, mtu anasoma fani ya manunuzi ananunua nini?
Be careful guy!! Huko duniani hawajafuta bali imeboreshwa na kuitwa majina mengine. Kuna wengi e wanaita Supply Chain, wengine Logistics.

I can tell you as well pamoja na kudhani kuwa Serikali ndiyo wanaajiri zaidi, lakini NGO, International Organization kama FAO, UNDP, UN, WHO hiyo ni moja kati ya core professions.
 
Be careful guy!! Huko duniani hawajafuta bali imeboreshwa na kuitwa majina mengine. Kuna wengi e wanaita Supply Chain, wengine Logistics.

I can tell you as well pamoja na kudhani kuwa Serikali ndiyo wanaajiri zaidi, lakini NGO, International Organization kama FAO, UNDP, UN, WHO hiyo ni moja kati ya core professions.
Ndugu yangu, katika muktadha wa kujiajiri kwa kijana ambaye ni fresh graduate, taaluma ya procurement ina msaada gani?
 
Accounting ni noble course sawa na engineering ama Doctor wa binadamu ama sheria. Hizo ni taaluma zimekuwepo miaka yote kabla ya Kristo.

Procurement ni fani changa sana haina hata miaka 15 Tanzania, ni course ambayo ukiangalia Duniani nasikia haipo maana hii ni kwa ajili ya manunuzi ya umma tu. Sasa usipoajiriwa na serikali utafanya nini?

Hatuwezi kua na fani ambayo inalenga kuajiriwa serikalini tu, haiwezekani.
Ok mtu wa accountancy anajiajiri vipi, hii ndo ilikuwa hoja yako
 
Ndugu yangu, katika muktadha wa kujiajiri kwa kijana ambaye ni fresh graduate, taaluma ya procurement ina msaada gani?
Infantry nyie mnachotafuta hapa ni kui undermine kozi ya procurement, mbona kozi ambazo huwezi kujiajiri ni nyingi tuu,. Nyie mmeona tu watu wa procurement aisee[emoji16]

Sawa mtoto aliesoma bachelor of business administration anajiajiri vipi?
 
Mbona wanauhitaji sana mkuu. Mtu wa store anayecheza na stock ya store ni muhimu sana eneo lolote ambapo kuna store kama hotelini, mgahawa, gereji, hospital, popote pale ambapo kuna store.
Acha uongo mbona mtaani hatuoni matangazo ya kazi km wanahitajika?
 
Back
Top Bottom