Kwa usalama wa nchi yetu, huyu afande anafaa kuwa IGP ajaye

Kwa usalama wa nchi yetu, huyu afande anafaa kuwa IGP ajaye

Mkuu ki2c Siro hana mnyororo wowote wa kuweza kum save pale anapokumbana na rungu la boss wake. Kumbuka jeshi la polisi ni kubwa, na lina makamanda wengine ambao huenda wanakubalika ndan ya jeshi hilo zaidi ya vile anavyokubalika Siro. Raisi ni mkuu wa nchi, ni amiri jeshi mkuu na boss wa vyombo vyote vya ulinzi na usalama. Kwa maana hiyo ana mkono wake katika kila idara ya usalama nchini (watu wake wa kumpa taarifa nyeti kimya kimya). Kwahiyo Siro anaweza kuona amezungukwa na makamanda ambao yeye anahisi ndio backup wake wa kumpambania pale anapofikwa na tatizo, kumbe nyuma ya pazia hao hao makamanda anaowategemea ndio wanaopeleka taarifa zake kwa boss wao (raisi) Kinachomsaidia Siro ni aina ya raisi. Amekuta raisi Samia sio mtu wa kukimbilia kukurupuka kisa tu kasikia mtu anamuongelea mafumbo katika radio, tv au chombo chochote cha habari. Laiti kama raisi Samia angekuwa mtu wa kuchukua hatua kwa kila sauti anayoisikia inamsema yeye, au kumhukumu kila anaelalamika kama ilivyo kwa Siro, basi angekuwa ashafunga na kufukuza wengi ndan ya serikali, chama na uraiani. Maana wenye kulalamika ni wengi na sauti za kejeli dhidi yake anazisikia na kuzipuuza. Kuna makamanda wa polisi walikuwa wazito na wenyeji ndani ya jeshi hilo kama vile kina Mahita, Mwema nk. Lkn leo hawapo na maisha yanaendelea kama kawa. Hata mkuu mungine wa polisi Ernest Mangu juzikati alitumbuliwa na hakuna alie mkwamisha mtumbuaji. Kwahiyo jamaa amepata bahati ya kuongea mambo yake chini ya uongozi wa raisi mvumilivu na mstahamilivu. Lkn angekuwa ni yule wa kutumia nguvu zake moja kwa moja basi Siro angeisha na angeshangaa wanaompa mpa support wangemkimbia. Maana hakuna ambae angekubali kuupoteza ugali wake kwa ajili ya muungine.
Mmmmh....! labda na overrate nguvu ya IGP bila kujua zaidi.
 
incompetent people don't get fired to earn credit. they are ignored, as it is
Is it possible to ignore someone who is said to be incompetent (by not firing him) while you are capable to do what is expected by many?
It is a matter of fact that the General is some how feared due to the power and influence he has...
 
Habari za asubuhi wana JF wenzangu.

Ndugu zang baada ya kufuatilia kwa makini utendaji wa kazi unaofanywa na jeshi la polisi, pamoja na mbinu mbalimbali zinazotumiwa na makanda wa jeshi hilo katika jitihada za kupambana na uhalifu nchini, hasa kwa mkoa wenye uhalifu mwingi kama Dar es Salaam.

Kwa kweli nilikuwa nashauri kwamba ikitokea IGP Simon Sirro amemaliza muda wake wa utumishi katika jeshi hilo kwa mujibu wa sheria, basi ikimpendeza Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mama Samia Suluhu Hassan amteuwe kamanda Jummane Muliro kuwa IGP mpya wa jeshi hilo, ili kushika nafasi itakayoachwa na Sirro.

Huyu kamanda amekuwa akipambana na uhalifu kwa njia zote za kijeshi, na mapambano yake huwa yanaleta ahueni kwa wananchi. Kamanda Muliro ni mwiba mkali kwa wahalifu wa aina zote nchini, na kamwe hajawahi kushindwa na wahalifu.

Nawasilisha mawazo huru.
Wewe Chawa usitupangie
 
Nani kakudanganya kuwa Samia ana full power?
Samia ni Rais kivuli tu.

Na uwezo wa kumtoa sirro Hana huo ni ukweli mchungu.
Waliopo behind wanaelewa nachomaaisha.
acha hizo wewe aliwatoa Top security officials Kaji na mbungo ashindwe kumtoa Sirro ??? nadhani anamsubiri tu astaafu 2023.....
 
Wewe Chawa usitupangie
Nimewapangia kwa sababu serikali ni ya kwetu. Subiri na nyie mkishika dola 😀😀😀 (japo ni ndoto) mje mtupangie. Najua ww ni chawa wa siro unapenda aendelee pale, hata baada ya muda wake kuisha.
 
acha hizo wewe aliwatoa Top security officials Kaji na mbungo ashindwe kumtoa Sirro ??? nadhani anamsubiri tu astaafu 2023.....
Mkuu Obama wa Bongo nashukur kwa kunisaidia kuwaelewesha hawa baadhi ya vijana wasiojua sheria na katiba ya nchi yetu inasemaje kuhusu mamlaka ya raisi. Wengi wa hawa vijana nimewapa somo katika post namb #16.. namb #20 na.. namb #80. So baada ya somo hilo wengi wamenielewa japo kuna wachache bado hawajelewa kitu kutokana na eidha kuamua tu kujifanya hawajaelewa huku moyoni wakiwa wameelewa vizuri, au hawajaelewa kutokana na kutokutaka wao wenyewe tu kuelewa.
 
Nani kakudanganya kuwa Samia ana full power?
Samia ni Rais kivuli tu.

Na uwezo wa kumtoa sirro Hana huo ni ukweli mchungu.
Waliopo behind wanaelewa nachomaaisha.
Anatolewa vizuri tu tena kwa barua yenye paragraph moja.
 
Mkuu mkorinto naheshimu sana mawazo yako, ila yule jamaa hana back up yoyote ya kumnyima mama usingizi. Kuanzia ndani ya jeshi lake mpaka nje ya jeshi lake. Kwa hatua ambayo mama kafikia sasa hivi, hakuna mtu yoyote anaeweza kumfanya chochote as longer as cdf wa sasa yeye ndo kamteuwa na kumuapisha. Ukishakuwa na backup ya mameja na majeneral wa jeshi nyuma yako basi inatosha. Hawa wengine unaweza tumbua wakati wowote na siku yoyote na wasikufanye chochote. Nafikiri unakumbuka kilichotokea kwa igp Ernest Mangu. Pamoj na wapinzani kudai jeshi la polisi lilihusika kwa kiwango kikubwa kuiba kura za wapinzani mwaka 2015, lkn hiyo haikuwa kinga kwake kutumbuliwa. Mangu alilala usiku akiwa igp na akaamka asubuhi akiwa raia wa kawaida, je alifamfanya nini raisi na hao wenzao au wenzake unaodai wanafanyaga mgomo baridi, mbona hawakuufanya na je pamoj na mkui wao kutumbuliwa mbona mwaka 2020 katika uchaguzi mambo yalikuwa ni yale yale na ccm ikashinda. Ndio maana mi nasema katiba yetu imempa madaraka makubwa mno raisi na akiamua kuyatuma kuna wengi wataumia. So inategemea na uungwana wa raisi alie madarakani. Siro ni mwepesi sana mbele ya mkuu wa nchi na amiri jeshi mkuu wa nchi hii. Anaweza kutoka kazini igp ile kufika nyumban kufungua tv au radio akasikia kuwa raisi kamteuwa fulan kuwa igp wa tanzania shughuli ya kuapishwa itafanywa kesho asubuh na aliekuwa igp wa jeshi hilo atapangiwa kazi nyingine ya kufanya. Na hapo ndo itakuwa imetoka hiyoo, anaweza kupangiwa kazi nyingine au asipangiwe, na pengine ikaamuliwa asirudi kuonekana hata karibu na gate la ikulu maana ashavuliwa vyeo vyote, so amekuwa raia wa kawaida. Kuna watu waliokuwa wamekita mizizi ndani ya chama na serikali kama vile bashiru, polepole nk. Hao ni watu waliokuwa wanajua hasa ccm ilishindaje uchaguzi mwaka 2020 maana wao ndio walikuwa wanamikakati ya ushindi wa ccm, leo hii wako wapi? Si wametumbuliwa mchana kweupe na watu wanaona. Walifanya nini zaidi ya mmoja pole pole kulalamikia pembeni. Na malalamiko yake wala hayakuweza kumfanya mama ashindwe na badala yake mama akawavua na vile vyeo vyote vya chamani kuanzia katibu mkuu na mwenezi wake.
haina afya kumchonganisha rais na wateule wake.

ishu ya mangu ni tofauti sana nailiwahusisha anaowasimamia,ndio maana akajikuta kasimama mwenyewe.

magu alipigiwa kelele kwa kudhalilisha maofisa wake na viongozi wake wasaidizi hadharani,lakini ukiona hivyo ujue anayesemwa ni mzigo kweli kweli.lakini huyu mtu yeye siku alipojibiwa alikuwa analalamikia hatua,wakati huo huo anaulizia matokeo chanya(UNAFIKI).kaalikwa kwenye sherehe ya maafari ya maafisa badala ya kuwapongeza anawananga!!!

huyo saimoni akitolewa wala sio habari maana amekaa hapo muda sana,ila unamtoa kwa mamlaka uliyo nayo au sababu kakujibu vibaya!
 
Mkuu kwa katiba yetu na madaraka makubwa aliyonayo raisi, ni rahisi sana kumchomoa huyo jamaa. Ni kitendo cha raisi kumuagiza katibu mkuu kiongozi atangaze kwamba raisi amemteuwa fulani kuwa IGP, na IGP wa sasa amepangiwa kazi nyingine ya kufanya. Basi hapo kazi inakuwa imekwisha na kwa madaraka makubwa aliyokuwa nayo raisi, jamaa atakuwa hana lolote la kumfanya zaidi ya kunung"unukia pembeni tu. Si unakumbuka ilikuaje kwa IGP Ernest Mangu? Sema kama nilivyokwambia kuwa kama kweli kuna kutoelewana, basi ni jamaa ndo mwenye tatizo ila sio mama.
Mtu unakosanaje na bosi wako? Yakikushinda acha kazi
 
Muliro ni mkubwa kwa sirro.
Sirro Bado young na tupo naye sana tu.

Sirro aliwahi kuukwaa u IGP
Na hapa anatafrani na mama yenu na huyo mama yenu hawezi na Hana ubavu wa kumtengu sirro.[emoji41]
Tukishashiba magimbi huwa tunawaza fitna tuu.
 
Mkuu kwa katiba yetu na madaraka makubwa aliyonayo raisi, ni rahisi sana kumchomoa huyo jamaa. Ni kitendo cha raisi kumuagiza katibu mkuu kiongozi atangaze kwamba raisi amemteuwa fulani kuwa IGP, na IGP wa sasa amepangiwa kazi nyingine ya kufanya. Basi hapo kazi inakuwa imekwisha na kwa madaraka makubwa aliyokuwa nayo raisi, jamaa atakuwa hana lolote la kumfanya zaidi ya kunung"unukia pembeni tu. Si unakumbuka ilikuaje kwa IGP Ernest Mangu? Sema kama nilivyokwambia kuwa kama kweli kuna kutoelewana, basi ni jamaa ndo mwenye tatizo ila sio mama.
Bora umenfafanulia. Kama mhimili mwingine uling'olewa kirahisi tu huyo IGP ni kufumba na kufumbua anakuwa kapoteza cheo. Nguvu za rais wa TZ hazielezeki.
 
haina afya kumchonganisha rais na wateule wake.

ishu ya mangu ni tofauti sana nailiwahusisha anaowasimamia,ndio maana akajikuta kasimama mwenyewe.

magu alipigiwa kelele kwa kudhalilisha maofisa wake na viongozi wake wasaidizi hadharani,lakini ukiona hivyo ujue anayesemwa ni mzigo kweli kweli.lakini huyu mtu yeye siku alipojibiwa alikuwa analalamikia hatua,wakati huo huo anaulizia matokeo chanya(UNAFIKI).kaalikwa kwenye sherehe ya maafari ya maafisa badala ya kuwapongeza anawananga!!!

huyo saimoni akitolewa wala sio habari maana amekaa hapo muda sana,ila unamtoa kwa mamlaka uliyo nayo au sababu kakujibu vibaya!
Mkuu Mkorintho kama nilivyosema hapo mwanzo kuwa naheshimu sana mawazo yako na ya wana JF wengine kwa uchangiaji wenye hekima. Ila sasa nafikiri ww umeanza kunisoma kati kati ya comment, na wala haukuanzia juu kwenye thread yenyewe. Laiti ungeanzia kwenye thread yenyew na kuielewa basi nina imani usingefikiri kuwa mimi nipo wrong katika hili. Thread yang haikuwa imemtaja Siro katika swala la kutumbuliwa, bali ilikuwa inazungumzia pale atapomaliza muda wake wa utumishi wa jeshi la polisi kwa mujibu wa sheria, basi ikimpendeza mh raisi amteuwe kamanda J4 Muliro kuwa igp mpya, maana jamaa ameonesha uthubutu na uwezo wa hali ya juu wa kupambana na wahalifu nchini. Wakati watu wakichangia kuhusu uwezo, uchapaji kazi na umri wa huyo Muliro, ndo akatokea mkuu mmoja katika post namb #8 (unaweza kuitafuta ukaisoma) akasema eti raisi hawezi na hana uwezo wa kumfuta kazi Siro. Kauli hiyo imetushangaza wengi. Kwamba mkuu wa nchi na amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama asiwe na uwezo wa kumfuta kazi askari polisi, kwa kinga na uwezo upi alionao huyo polisi hadi ashindikane kutolewa hapo na boss wake. Kwahiyo hapo ndo mjadala ulipoanzia na nimeelezea vizuri hasa katika post namb #80. Nina imani ukiisoma pia utaelewa. Ila lengo la kuandika mada hii haikuwa hiyo unayofikiria mkuu.
 
Mtu unakosanaje na bosi wako? Yakikushinda acha kazi
Sizani hata kama hawa watu wana ugomvi, ila kuna baadhi ya watu ndo wanajaribu kutuaminisha kuwa wakuu hawa wawili wenye vyeo na mamlaka tofauti wamegombana. Hawajui na hawafahamu kwamba kwa sheria zetu ni lazima igp aripoti kwa raisi na amir jeshi mkuu kila siku asubuhi akiingia kazini, na jioni akitoka kazini.
 
Bora umenfafanulia. Kama mhimili mwingine uling'olewa kirahisi tu huyo IGP ni kufumba na kufumbua anakuwa kapoteza cheo. Nguvu za rais wa TZ hazielezeki.
Mkuu MamaSamia2025 . wengi waliosoma post zang namb #77 na #80 wameelewa. Maana nimefafanua sasa vizur kule.
 
Habari za asubuhi wana JF wenzangu.

Ndugu zang baada ya kufuatilia kwa makini utendaji wa kazi unaofanywa na jeshi la polisi, pamoja na mbinu mbalimbali zinazotumiwa na makanda wa jeshi hilo katika jitihada za kupambana na uhalifu nchini, hasa kwa mkoa wenye uhalifu mwingi kama Dar es Salaam.

Kwa kweli nilikuwa nashauri kwamba ikitokea IGP Simon Sirro amemaliza muda wake wa utumishi katika jeshi hilo kwa mujibu wa sheria, basi ikimpendeza Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mama Samia Suluhu Hassan amteuwe kamanda Jummane Muliro kuwa IGP mpya wa jeshi hilo, ili kushika nafasi itakayoachwa na Sirro.

Huyu kamanda amekuwa akipambana na uhalifu kwa njia zote za kijeshi, na mapambano yake huwa yanaleta ahueni kwa wananchi. Kamanda Muliro ni mwiba mkali kwa wahalifu wa aina zote nchini, na kamwe hajawahi kushindwa na wahalifu.

Nawasilisha mawazo huru.

View attachment 2279028
IGP atoke JWTZ ili alinyooshe Jeshi la Polisi vinginevyo hakuna mabadiliko yoyote ya maana yatakayofanyika mfano mzuri umeonekana Magereza mwenye macho haambiwi tazama
 
Back
Top Bottom