Kwa utendaji kazi uliotukuka wa Rais Samia naanza kuziona dalili za upinzani kutafuta visingizio vya kumkimbia na kumkwepa katika Uchaguzi Mkuu ujao

Kwa utendaji kazi uliotukuka wa Rais Samia naanza kuziona dalili za upinzani kutafuta visingizio vya kumkimbia na kumkwepa katika Uchaguzi Mkuu ujao

Kazi uliyotumwa unaifanya vizuri manake huangalii hoja zaidi ya kukomaa na ulichotumwa, inasound good
Nawasilisha Yale yanayoonekana na kuzungumza na watanzania walioonyesha upendo mkubwa na uungwaji mkono kwa mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani
 
Ccm siyo kanu ,CCM Ina misingi yake ambayo hakuna awezaye kuitikisa hapa nchini, hayupo na hatakuwepo
Chenye mwanzo kina mwisho acha kukufuru!!!!

CCM Ina mwanzo, ilizaliwa na itakufa sku moja.

Dunia hii na ukubwa wote tunaambiwa itakamatwa na kukunjwa kama karatasi na Kutupwa JEHANUM.

CCM ilijengwa ktk misingi imara ya HAKI na USAWA, imehama kwenye misingi hiyo ya uanzishwaji wake.

Imekumbatia Wala RUSHWA, wabunge wengi ni matajiri, WAKWEPA Kodi wanaotumia pesa haramu kununua Sanduku la kura.

Nakuambia CCM italala USINGIZI wa mauti verry soon.

Tusubiri.
 
Mama yangu, "Mlezi" wa taifa, atapata surprise ambayo hajawahi kudhania itakuja kutokea kamwe!

watu wanao mposti kwenye social media "kumsifia" na wengine "kumuabudu" ndani ya chama chake, wanalao kuelekea uchaguzi mkuu, awe makini sana!
 
CCM Ni chama kilichobeba matumaini ya watanzania, Ni chama kiongozi, Ni chama chenye Sera na ajenda zinazogusa maisha ya watanzania, ndio maana mtu akifika ofisi ya CCM anakuwa na Imani ya kupata suluhisho la kero yake
Tozo inakugusa wewe???Uporaji kura unakugusa wewe???Matumizi mabaya ya madaraka yanakusa wewe??? Ni matumaini gani ambayo ccm imekupa???Mimi naamini katika Mungu,haki na wajibu wa kila mwanadamu aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu na si katika chama au uongozi,hayo ni matokeo ya muda ambayo yanaweza kuwa chanya kama ilivyokuwa katika utawala wa Nyerere na Mkapa au yanaweza kuwa hasi kama yalivyokuwa katika utawala wa Magufuri na yaliyopo leo katika utawala wa Mama Samiah Suluhu.
 
Nawasilisha Yale yanayoonekana na kuzungumza na watanzania walioonyesha upendo mkubwa na uungwaji mkono kwa mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani
Hakuna anaemchukia Rais Samia ila nyie mnaosifu kila wakati nahisi ndio mnamchukia sio bure, kama binadamu mengi anapatia machache anakosea hivyo tuu na watu wanaona so watapima tuu wenyewe sio lazima kulazimisha mtu aelewe
 
Huo mharo wako hata ukimweleza chizi mwenzio lazima akupige.sasa kama vyama vya sisa vimezuiwaiwa kufanya mikutano unaetegemea usiache kuongea huo ujinga wako wambie waache wafanye mikutano ya hadhala uone watavyochafua hali ya hewa wananchi watatamani kuiponda mawe hio nanii yako unayoiaminia.
 
Mleta mada elewa kuwa; hakuna kipindi laini cha kupindua meza kama hiki elewa hilo!
Nchi inapita ktk kipindi kigumu mno mno na sijui upinzani upo wapi kwa ajili ya kupata "credits'
Tatizo unaandika kwa ushabiki badala ya ukweli uliopo
 
Ndugu zangu hivyo ndivyo hali halisi ilivyo, kwasasa upinzani umefika hatua hauelewi ushike lipi na uache lipi, uongee nini na usimame na lipi, ubebe lipi na uache lipi, utembee na lipi na usimame na lipi.

Imefika hatua hata kuaminiana wao kwa wao wameacha, maana kila mtu anahisi mwenzie anadalili za kusaliti chama na kwenda kumuunga mkono Mh. Rais wetu mpendwa, hapa unaweza kurejea habari za Mch. Peter Msigwa namna alivyo tukanwa na vitoto vidogo kiumri kisa tu kusimamia mtizamo wake katika kuiunga mkono serikali juu ya suala la Loliondo.

Ndugu zangu kwa sasa hata wenyewe hawaoni wakuweza kushindana na Mh. Rais Samia maana kila waliyemuona awali kuwa ndio kamanda wa kuongoza mapambano, wanakuta amerudi mstari wa nyuma akiunga juhudi za Mh. Rais na hata kama ni kukosoa anakosoa kwa kushauri baadhi ya maeneo kwa heshima na staha, jambo linalozidi kuwa changanya na kuwalaza na viatu vijana wa upinzani.

Hii yote ni kwa kuwa Mh. Rais kafanikiwa kugusa kila eneo kiutendaji, watanzania wana matumaini makubwa sana na Mh. Rais kwa kuwa wanaona juhudi zake katika kujenga nchi yetu, wanaona namna kila mtu, kila kundi na kila eneo linavyoguswa kiutendaji. Hakuna anayeachwa nyuma wala kutengwa au kubaguliwa, wote wanapata huduma sawa.

Kila mtu anapata huduma sawa,kila mtu anasikilizwa, kila mtu anathaminiwa,kila mtu anaona anayo nafasi ya kuchangia ujenzi wa Taifa hili na kila mtu anaona anaweza kutimiza Ndoto na malengo yake katika nchi hii kwa kuwa fursa zipo wazi kwa kila mtu mwenye kuzitaka.

Sasa hapa ndioo mtihani mkubwa walionao upinzani kwa sasa katika kuweza kusimamisha mgombea kiti cha Urais maana hawaelewi watamsimamisha nani? Kwa sera na ajenda zipi, hawaelewi watawashawishi kipi watanzania, maana Mh. Rais amefanya kazi zilizogusa maisha ya watanzania hasa wanyonge wasio na sauti.

Wameona namna Mh. Rais alivyo shapu kuchukua hatua katika kumsaidia mwananchi pale panapojitokeza tatizo la kidhalula kama alivyo fanya kutoa Ruzuku katika kilimo na nishati ya mafuta, kiukweli kasi hii ya Mh. Rais imewaweka pabaya sana kisiasa.

Ushauri wangu kwao ,kwa kuwa wameonyesha kukubali utendaji kazi wa mh Rais Basi hawana budi Kuendelea kumuunga mkono Mh. Rais wetu, waendelee kutoa ushauri watakapoona panafaa kwa lugha ya heshima na staha.

Maana mama ni msikivu na mnyenyekevu anayemjali na kumsikiliza kila mtu, kwa sasa mama amekaa katika mioyo ya watanzania. Watanzania walitaka maendeleo na mtumishi mnyenyekevu atakayewasikiliza, sasa amepatikana Mh. Rais Samia anatekeleza kwa vitendo ndoto za watanzania.

Kazi iendeleee.

Umekumbuka kuweka katiba mpya, tume huru na mahakama huru kuwa ndiyo visingizio vikuu?
 
Mleta mada elewa kuwa; hakuna kipindi laini cha kupindua meza kama hiki elewa hilo!
Nchi inapita ktk kipindi kigumu mno mno na sijui upinzani upo wapi kwa ajili ya kupata "credits'
Tatizo unaandika kwa ushabiki badala ya ukweli uliopo
Hakuna upinzani kwa Sasa hapa nchini ndugu yangu, ili uchaguliwe lazima uwe na Sera na ajenda za kuwashawishi watu, Sera na ajenda hizo ni sharti ziwe zinagusa maisha ya watu, kitu ambacho kwa Sasa upinzani hauna vitu hivyo vyote, hauna kitu au Jambo linalogusa maisha ya watu ndio maana unaona umekosa uungwaji mkono toka kwa wananchi Wala habari zao huzisikii popote kwa kuwa hazina uzito Wala ushawishi kwa watu,

Lakini ukija kwa upande wa CCm chini ya uenyekiti wa mama Samia unakuta amebeba Sera na ajenda zinazogusa maisha ya watanzania, Ndio maana unaona uungwaji mkono mkubwa Sana kwake kutoka kwa mamilioni ya watanzania
 
Huo mharo wako hata ukimweleza chizi mwenzio lazima akupige.sasa kama vyama vya sisa vimezuiwaiwa kufanya mikutano unaetegemea usiache kuongea huo ujinga wako wambie waache wafanye mikutano ya hadhala uone watavyochafua hali ya hewa wananchi watatamani kuiponda mawe hio nanii yako unayoiaminia.
Mikutano wafanye kuwaeleza Nini watanzania kwa Sasa? Huu Ni muda wa CCm kutekeleza ilani na mkataba wake wa kuwatumikia watanzania, subirini uchaguzi ujao Kama hamtakimbia uwanjani, kajifunze au angalia marekani Nini kinafuaata baada ya uchaguzi, ulishaona wanazulula mitaani Kama nyinyi wapinzani na matisheti yenu?
 
Hakuna upinzani kwa Sasa hapa nchini ndugu yangu, ili uchaguliwe lazima uwe na Sera na ajenda za kuwashawishi watu, Sera na ajenda hizo ni sharti ziwe zinagusa maisha ya watu, kitu ambacho kwa Sasa upinzani hauna vitu hivyo vyote, hauna kitu au Jambo linalogusa maisha ya watu ndio maana unaona umekosa uungwaji mkono toka kwa wananchi Wala habari zao huzisikii popote kwa kuwa hazina uzito Wala ushawishi kwa watu,

Lakini ukija kwa upande wa CCm chini ya uenyekiti wa mama Samia unakuta amebeba Sera na ajenda zinazogusa maisha ya watanzania, Ndio maana unaona uungwaji mkono mkubwa Sana kwake kutoka kwa mamilioni ya watanzania
Sera za kupiga watu risasi,sera za kuengua wagombea,sera za kupora uchaguzi,sera za kufunga wapinzani,sera za kukashifiana,sera za kutoa watu magerezani na kwenda kuwaapisha ubunge,sera zisizo na dira ila tu maslahi.
 
Mikutano wafanye kuwaeleza Nini watanzania kwa Sasa? Huu Ni muda wa CCm kutekeleza ilani na mkataba wake wa kuwatumikia watanzania, subirini uchaguzi ujao Kama hamtakimbia uwanjani, kajifunze au angalia marekani Nini kinafuaata baada ya uchaguzi, ulishaona wanazulula mitaani Kama nyinyi wapinzani na matisheti yenu?
Mikutano ya vyama lengo lake ni kusahihisha na kukosoa pale ambapo mambo hayatekelezwi vema,mbona kipindi cha Mkapa na Kikwete watu walifanya mikutano na nchi ilisonga vizuri?? Acheni woga.
 
Mama Samia Ahukumiwe na kulaumiwa kwa matokeo ya matendo kauli na hatua zake akiwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, usianze kumhukumu na kumbebesha mashitaka yasiyo kuwa yake, Nchi kwa Sasa ipo katika mikono salama ya mama Samia, katika mikono hiyo hakuna kitakachopotea Wala kuharibika Wala kuumia Wala kuteswa Wala kunyanyaswa, Tumuunge mkono mh Rais wetu
Sera za kupiga watu risasi,sera za kuengua wagombea,sera za kupora uchaguzi,sera za kufunga wapinzani,sera za kukashifiana,sera za kutoa watu magerezani na kwenda kuwaapisha ubunge,sera zisizo na dira ila tu maslahi.
 
Mama Samia Ahukumiwe na kulaumiwa kwa matokeo ya matendo kauli na hatua zake akiwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, usianze kumhukumu na kumbebesha mashitaka yasiyo kuwa yake, Nchi kwa Sasa ipo katika mikono salama ya mama Samia, katika mikono hiyo hakuna kitakachopotea Wala kuharibika Wala kuumia Wala kuteswa Wala kunyanyaswa, Tumuunge mkono mh Rais wetu
Haipo salama kwa sababu anatekeleza ilani aliyoianzisha mwendakuzimu.
 
Kwa upinzani upi wa kuogopwa? Upinzani hauna hata Sera na ajenda za kueleweka ndio maana unaona wanakwenda na upepo, kwa Sasa mama kawazima kwa utumishi wake uliotukuka ndio maana unaona namna walivyofifia
Mikutano ya vyama lengo lake ni kusahihisha na kukosoa pale ambapo mambo hayatekelezwi vema,mbona kipindi cha Mkapa na Kikwete watu walifanya mikutano na nchi ilisonga vizuri?? Acheni woga.
 
Ule Ni ukaguzi wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi, Hata marekani uchaguzi ukipita kinachofuata Ni kazi tu kwa waliopewa dhamana

Acha uongo, mbona siasa marekani inaendelea. Umesahahu impeachment ya Trump?. Tusitumie mifano kwa nia ovu. Mbona juzi imepigwa kampeni mpaka gavana was New York akatoka na uchaguzi kufanyiwa.
 
Kwa upinzani upi wa kuogopwa? Upinzani hauna hata Sera na ajenda za kueleweka ndio maana unaona wanakwenda na upepo, kwa Sasa mama kawazima kwa utumishi wake uliotukuka ndio maana unaona namna walivyofifia
Kama upinzani wa Tanzania hauna sera kwa nin mwendakuzimu wakati wote wa utawala wake alikuwa anapambania sera za upinzani,na wapinzani wakiunga juhudi mara moja wanapewa promosheni ya nguvu,mpaka sasa wale wamama 19 wapo kule kwa sababu wametoka kwenye sera nzuri na ccm inawalinda bila utaratibu.
 
Back
Top Bottom