Uchaguzi 2020 Kwa vituko vya Seif na CHADEMA, hakika upinzani bado sana Tanzania

Uchaguzi 2020 Kwa vituko vya Seif na CHADEMA, hakika upinzani bado sana Tanzania

giphy.gif
 
Na wewe angalau tumia akili Kwani mdhamini hana haki ya kuondoa udhamini au unawaona watanzania wajinga sana mara ngapi wanafunzi pale UDSM wameonfolewa kwa kufutiwa udhamini.

Sasa cha ajabu kitu gani hivyo vyama kuamuwa kubadilisha uamuzi wao. Imekuuma sana kwavile lengo lao ni moja tu kuiondoa CCM kuna ubaya gani kuunganisha nguvu katika hilo.

Hata sisi tusio na vyama tunaona ni wazo zuri kuunganisha nguvu ili mradi hawakiuki sheria ya uchaguzi maana wanaunga mkono mgombea siyo coalition
 
hawa ndio wanamlaumu Magufuli kwa udikteta lakini kna tofauti kubwa Magufuli anafanya hivyo kupitia vikao halali lakini wao hata vikao halali hawavieshimu bali wanatoa matamko jukwaani.
Ni kama walivyofanya maamuzi ya kumteua Lowassa waliogopa wakiweka ushindani asingepitishwa, kwa siasa za namna hii ccm wataendelea kubaki madarakani muda mrefu.

Hivi wakati anapitisha wale wagombea walinunuliwa kutoka upinzani kugombea tena kuna vikao vilikuwa vinafanyika
 
Huyu mlemavu akipata kura mil 3 itabidi akatambike.

Sasa mbona mgombea wenu hadi anapiga magoti mara ataongeza mshahara ngoja sindano iwaingie mnadhania kuwavalisha tshirt za chama hao wanafunzi kuongeza vichwa ndo watawapigia kura subirini muziki tarehe 28 October.
 
Kama wana ubavu waiambie NEC na ZEC kuondoa kwenye ballot paper majina ya Mgombea wa ACT Bara na Mgombea Chadema visiwani. wakishindwa kufanya hivyo maana yake bado ni wagombea na nihalali kwa wafuasi wao kuwapigia kura. Rekodi itasema vyama hivyo vimepata kura ngapi za wagombea wao katika uchaguzi.

Record zikisema wamepata zero wakati wagombea walioungwa mkono kuna shida gani, unadhani wanachama wanapiga kura kama robot wapigie kura jina ambalo wameambiwa wasilipigie kura
 
Watamkumbuka sana Edo, ruzuku hawatafikisha hata milioni moja!

Wakati Edo hatukuona mgombea anapiga magoti na kutuma msg kwa watu sasa hivi upepo umebadilika hata ukimuangalia usoni amepoteza kabisa matumaini hata kampeni anauliza kama kujenga flyover ndo makosa yake amegundua kuwa amekimbiwa na wananchi kazi mwaka huu anayo. Ndo Rais wa kwanza kutawala miaka 5 tu katika historia sababu ya ubabe
 
Walimshobokea Membe? Walijua ni snitch na ili wamkamate vizuri walionesha kumkubali ili waweze kumkaba vizuri. Chatu ndivyo anavyokula mbwa. Maccm mkajua agent wenu anaingia ndani ili awape mikakati inavyoenda.

Amekawekwa kitako. Ndio maana mmepoteana na kuweweseka kama mmekunywa dawa za kichawi. Mpigieni kampeni hii wiki iliyobaki. Mwisho wenu inzi wa kijani umefika.
 
Wao walishadhamiria hivyo. Ni mbinu na mkakati waliokuwa wameupangilia toka manzo. We kaa ukidhani wamedandia hewani,28 nina langu jambo mzee.
 
Lissu kaifuta CCM huko Umasaini Wenyekiti wa Vijiji warudisha Bendera za CCM
 
Upinzani hawajipanga kabisa yaani. Hivi Membe so alipitishwa kwenye vikao rasmi vya chama? Sasa inakuwaje analazimishwa kumsapoti mgombea urais wa chama kingine? Mambo ya ajabu kabisa haya.

Wapinzani tangu mwanzo walikuwa na wazo la mgombea mmoja wasiwasi ulikuwa kwa NEC wakipeleka mmoja tu asije akakatwa ndo maana wakaenda na wote wawili na walikubaliana kuwa hata kwenye majimbo kama ikionekana mhombea anakubalika zaidi badala ya kugawa kula waungane ili kuondoa CCM ndicho kinachofanyika sasa.
 
Upinzani bado sana, labda tuamke wenyewe sisi wananchi na kuleta mabadiliko bila kujali vyama vya hawa wasaka vyeo na wababaishaji
Umegonga nyundo utosini
hawa ndio wanamlaumu Magufuli kwa udikteta lakini kna tofauti kubwa Magufuli anafanya hivyo kupitia vikao halali lakini wao hata vikao halali hawavieshimu bali wanatoa matamko jukwaani.
Ni kama walivyofanya maamuzi ya kumteua Lowassa waliogopa wakiweka ushindani asingepitishwa, kwa siasa za namna hii ccm wataendelea kubaki madarakani muda mrefu.
Naona mmewekewa bando kuja kumwaga utopolo wenu humu Lissu anawachoma kama mkuki na baado atawakimbiza mchakamchaka
 
Back
Top Bottom