Kwa wajuvi wa Biblia, ni kweli Mfalme Daudi alipata UKIMWI kutokana na kupenda wanawake ovyo?

Kwa wajuvi wa Biblia, ni kweli Mfalme Daudi alipata UKIMWI kutokana na kupenda wanawake ovyo?

Teamanaconda

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2013
Posts
602
Reaction score
564
Hongereni na majukumu wanajukwaa.

Juzi jumapili nilikuwa nasikiliza mahubiri ya kuhani na muonaji Mwalimu MUSA RICHARD MWACHA, mahubiri yalikuwa yanahusu UKIMWI.

Sasa katika mahubiri yale nikamsikia akisema kuwa Mfalme DAUDI nae alipataga HIV (UKIMWI) kutokana na kupenda kwake wanawake hovyo

Kwa wajuvi wa Biblia, je kuna mstari wowote unaonyesha hii taarifa? Na kama ni kweli kumbe basi huu ugonjwa umeanza zamani sana. Naweka na sehemu ya mahubiri yake maana niliyarekodi japo sikurekodi mpaka mwisho.
 
WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA.

Tumesikia Yesu ana mke na sasa tunaambiwa mfalme Daudi alikufa kwa ngoma, kesho utasikia baadhi ya manabii walikuwa waganga

hatari sana hii kwa hiki kizazi chief
 
We amini unachoamini tu, ingawa kwa enzi hizo wanawake wengi wala haikuwa tatizo ndio ilikuwa ubabe (na hapa siongelei Biblia naongelea enzi zile wakati Biblia inatangazwa / promoted) ila tukija kwa wake Suleimani / Solomon nae vipi?

Pili ukifuata sana haya maandiko huenda na wewe unaweza ukafanya mbinu za kumuua rafiki yako ili uchukue mke wake au hata kumtoa mwanao sadaka / kutaka kumtoa sadaka eti sababu una Imani kali au umeambiwa ufanye hivyo.

Anyway... to each his/her own.
 
kinachotuponza watu wengi ni uvivu na hatuko tayari kutatua changamoto zetu wenyewe na katika hili tutazunguka sana kwa manabii na watumishi na hakuna tutakachofanikiwa.
  1. mapungufu ya watu wengi na hasa wanawake yamenisaidia kujifunza zaidi na mwisho wa siku nimeelewa kuwa ni uvivu na kupenda kuwa wajinga ndiko kunakosababisha udhaifu wao.
  2. natamani watu wajielewe wao wameubwaje na uhusiano wao ukoje na MWENYEZI MUNGU na uwezo wao wa kuwasiliana na MUNGU ukoje?
  3. wengi wameendelea kuburuzwa kwa kupenda ibada za mazingaombwe na hapa ndio chanzo cha manabii wengi kuona fursa kwao.
  4. MWENYEZI MUNGU awasaidie kwa kweli.
 
🤣🤣🤣🤣nimecheka hata kabla sijasoma uzi.

Kama ni wanawake basi awe mwanae King Solomon wake 700 concubines 300
 
kinachotuponza watu wengi ni uvivu na hatuko tayari kutatua changamoto zetu wenyewe na katika hili tutazunguka sana kwa manabii na watumishi na hakuna tutakachofanikiwa.
  1. mapungufu ya watu wengi na hasa wanawake yamenisaidia kujifunza zaidi na mwisho wa siku nimeelewa kuwa ni uvivu na kupenda kuwa wajinga ndiko kunakosababisha udhaifu wao.
  2. natamani watu wajielewe wao wameubwaje na uhusiano wao ukoje na MWENYEZI MUNGU na uwezo wao wa kuwasiliana na MUNGU ukoje?
  3. wengi wameendelea kuburuzwa kwa kupenda ibada za mazingaombwe na hapa ndio chanzo cha manabii wengi kuona fursa kwao.
  4. MWENYEZI MUNGU awasaidie kwa kweli.
Mkuu hebu tufundishena sisi mnavyopiga story na Mungu.
 
Ndivyo mchungaji alivyowafunga kamba hivyo?

Hujui b4 1980 hakukuwa na UKIMWI?
 
Tuthibitishie

1 Wafalme 2 :

10 Daudi alifariki, akazikwa katika mji wake.

11Alikuwa ametawala Israeli kwa muda wa miaka arubaini; miaka saba akiwa Hebroni, na miaka thelathini na mitatu akiwa Yerusalemu.

12Basi, Solomoni akaketi katika kiti cha enzi mahali pa Daudi, baba yake; na ufalme wake ukaimarika.
 
Back
Top Bottom