Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Dawa ya moto moto.
Ujinga na upumbavu wa kukumbatia nge vimewaua wengi sana.
Mzazi mshenzi kaa naye mbali.
Mimi father simpendi.
Kati ya watoto wake 3 ambao tulimaliza la saba siku moja Mimi pekee aliniombea nifeli na cha ajabu ni Mimi pekee nikatoboa tena shule ya vipaji maalumu.
 
Mkuu kwani kutokuelewana na heshima mbona ni vitu viwili tofauti... Kutokuelewana ni hali ya ninyi wawili kutokwenda njia moja ila heshima ni tabia.

Unaweza usielewane na kiongozi wako ila kutokana na nafasi yake ukatii maelekezo (ukamuheshimu)

Kuelewana na kutokuelewana ni suala la kawaida kwenye maisha, Hata wewe mwenyewe unaweza ukakosa kuelewana na Mungu wako kutokana na kutokuelewa njia zake ila Heshima ikabaki palepale kutokana na ukuu wake.

Kuelewana na Kutokuelewana kunajengwa na hoja na utaratibu wa kuendana kinamna fulani wakati Heshima ni kutokana na tabia na mazingira ya makuzi fulani.
 
Haya Mambo Kama mtu hayajawahi
Kumkuta anaweza akaona watu wanaolalamika basi wanachekesha au wamechanganyikiwa,aisee hakuna kitu inaumiza au kumfanya mtu aone maisha machungu Kama kukosa upendo autakaye mtoto kutoka kwa mzazi wake
 
Ni Mimi mkuu. Siku hizi nimejitenga, Ni mwaka mmoja Sasa hawajui nilipo na Mimi sijui wapo hai au wamekufa and I don't care kwa sababu hakuna atakayeishi milele

Ila kwenye familia kuna mambo yanakera sana ,unatamani hata uzaliwe kwingine kumbe kila sehemu kuna shida,nadhan ni utu na upendo hawana
Toka uache kumshirikisha mambo yamenyooka?
 
Kuna makosa mengine mtu hawezi kumsamehe mzazi mfano mzuri ni rafiki ndugu yangu mmoja ambaye baba yake ni mganga wa Jadi huko Shinyanga, huyu mzee alikuwa na wivu wa wazi kwa mtoto wake na mara zote alipinga jamaa kwenda shuleni na hata tupo advance level mzee wake alikuwa hampi sapport yoyote mpaka tuna maliza tunaingia chuoni mzee hana mawasiliano na jamaa wala hatumi pesa.
Sisi ndiyo tunamsaidia hapa na pale jamaa alipomaliza chuo na kupata kazi mzee akaanza maneno kuwa jamaa hasaidii familia kwanza kamtelekeza baba yake kisa amesoma anadharau. Mimi nikamshauri omba msamaha kwani mzazi hakosei ( hizi ni fikra zangu wakati huo saivi nimebadilika).

Kikawekwa kikao jamaa akaomba msamaha mambo mengine yanaendelea. Alivyotaka kuoa ikawa shida mzee hamtaki mwanamke wa jamaa ila tuli force tukamaliza vizuri.

Baada ya ndoa mzee akaleta maneno kuwa mwali akae pale nyumbani ili wachunguze kumbe yule mzee ana nia mbaya na mke wa jamaa. Kwa kutumia dawa zake za kiganga alifarakanisha uhusiano kati ya jamaa (mtoto wake) na mkewe.

Baadaye ikaja kugundulika huyu mzee anamahusiano na mke wa mtoto wake baada ya mke kushika mimba jamaa akaikataa. Sasa wewe hapo unaweza kusamehe uchawi wa hivo? Mimi sio mnafki hapa nilimshauri mwamba akate mawasiliano.

Mfano Mimi sijawahi kuungwa mkono kitu na baba yangu wala mama yangu. Ila waliwapenda sana mpaka sasa wanawapenda dada na kaka yangu na wadogo zangu ila mimi nikawa kama black sheep sihirikishwi kwa chochote lakini sasa hivi nishajua ile familia ni karmic relationship. Hakuna picha hata moja nimepiga nipo na wazazi wangu au nimepiga na baba au mama hakuna wala hawajawahi kuniweka status. Ila sina ubaya nao japo siongei nao kila mtu na maisha yake na sasa nina familia nimeoa lakini sikuwa shirikisha kitu wala sikutaka mchango wao. Na wala hawana taarifa za life yangu kuwa nina watoto lakini hawajawahi kuwaona. Huu ni mwaka wa saba sijawahi kukanyaga nyumbani kwetu lakini sio kama kwa ubaya cz nina amani kila mtu sijamkosea kitu. Kama shida walianza wao na uhusiano ni kama daraja kama hukunipenda na kuweka uhusiano mzuri na mimi utotoni usidhani ukubwani nita kupa time wala nafasi Never.
Hili ni tatizo kwa sisi wazazi wa kiume, hata mm nimepitia hili Kuna kipindi nilikosa viatu na shati la shule kuchanika halafu mzee akawa anapiga misele tu Hana time na mm.
 
Hili ni tatizo kwa sisi wazazi wa kiume, hata mm nimepitia hili Kuna kipindi nilikosa viatu na shati la shule kuchanika halafu mzee akawa anapiga misele tu Hana time na mm.
Yani hyo kitu iko hata kwa wanyama wengine, madume hatunaga fikra za kusaidia au kusupport familia zetu.

Sent from my TECNO KG7h using JamiiForums mobile app
 
Me Mzee wangu kavurugwa na mama wa kàmbo ili anione Mimi kinyesi, inafika muda Mzee unampigia Simu hapokei kwa kuhofia nitamlilia shida haya Mzee wangu uliikuta missed call basi nitafute uniulize kunani kijana wangu mbona ulinipigia Simu mida Fulani.

Hana kabisa time kisingizio ubuzy wa kazi kweli Mzee wangu, au akipokea hata haniulizi mwanangu unaendeleaje na majukumu. Mzee anafahamu fika kuwa maisha yangu yameharibiwa na walimwengu hivyo msaada wake nauhitaji lakini Hana time na Mimi.

Anyway namuacha apande mazao yake kikamilifu kwani atakachokuja kuvuna Mungu ndiye anajua.
So sad

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Me Mzee wangu kavurugwa na mama wa kàmbo ili anione Mimi kinyesi, inafika muda Mzee unampigia Simu hapokei kwa kuhofia nitamlilia shida haya Mzee wangu uliikuta missed call basi nitafute uniulize kunani kijana wangu mbona ulinipigia Simu mida Fulani.

Hana kabisa time kisingizio ubuzy wa kazi kweli Mzee wangu, au akipokea hata haniulizi mwanangu unaendeleaje na majukumu. Mzee anafahamu fika kuwa maisha yangu yameharibiwa na walimwengu hivyo msaada wake nauhitaji lakini Hana time na Mimi.

Anyway namuacha apande mazao yake kikamilifu kwani atakachokuja kuvuna Mungu ndiye anajua.

Pole sana man,i can feel your pain bro
 
Kupitia uzi huu nimejifunza mambo mengi Sana nilidhan mm pekee ndyo napitia magumu ya familia yangu kumbe tupo wengi Sana

Kikubwa tuchukulie changamoto hizo tulizopitia kurekebisha familia zetu (watotowetu) tiwatendee mema tuwasikilize na tuwashaur vyema


Binafsi mzaz wangu wa kiume alinipa kila kitu kadir ya uwezo wake lakn kitu kimoja pekee udikteta Tena kwangu tuu kutonisikiliza Wala kinishirikisha kwa Jambo lolote badala yake wanasikilizwa watoto wengne na wanakaa nakupanga mambo ya familia mm naambiwa tu

Jambo hili lilinipa msongo wa mawazo Sana ukizingatia mm nilikuwa mtoto mkubwa kat ya wote lakn n mtoto wa nje ya ndoa na nilijipeleka tu kwa baba yangu baada ya shida kuwa nyingi huko nilokokuwa nakaa (kwa Bibi) ujio wangu pale unaonekana uliharibu kanuni na taratibu zao lakn nifanye nn n mm shida zilinikimbiza wakat mzaz wangu anakila kitu alikuwa engineer wa tanroads mkoa X

Hali ya kutengwa kimaamuzi iliendelea had nilipofika chuo pesa za matumizi had nimpigie mdogo wangu ndyo itumwe ukimpigia mzee hapokei simu na akipiga atanilaumu kwanini nilimpigia mda wa kazi ukipiga jion atakuambia yupo na marafk zake nisimsumbue

Amekuja kustaafu mm nipo chuo mwaka wa 4 namalizia akawagawia wanae wote Kia's Cha pesa Kama 5M kwa kila mtu mm sikupata hata shilingi na hii nilikuja kuambiwa na mdogo wangu alikuja kufunga mzgo wa biashara akaniambia wewe pesa yako utafanyia Nini ? Ndipo nikajua kumbe wamepewa pesa

Lakn MUNGU n mwema maisha Sasa yanasonga Nina familia yangu najitahid kuilea kwa upendo ili nisije kosea Kama mm nilivyoona nakosewa

Kwa Sasa mzazi wangu anailaumu simshirikishi katika maamuz ya mambo yangu najitenga Sana na familia sipigi simu mara kwa Mara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya Mambo Kama mtu hayajawahi
Kumkuta anaweza akaona watu wanaolalamika basi wanachekesha au wamechanganyikiwa,aisee hakuna kitu inaumiza au kumfanya mtu aone maisha machungu Kama kukosa upendo autakaye mtoto kutoka kwa mzazi wake
Ukiacha yote aliyowahi kunifanyia ikiwa ni pamoja na haki ya kumjua baba lkn hii kauli ( NATAKA KUAGIZA GARI LINGINE KWA SASA HVYO SIWEZI KUKUTUMIA MATUMIZI HUKO CHUONI )ndio ilinfanya nione ilikua bahati mbaya sana yeye kunizaa ingawaje hata upendo wa kinafki nimeushindwa.

Yan una mzazi si fukara lkn unaishi maisha ya kuomba omba yeye yupo busy kuhangaika kulinda ndoa yake and worse yeye ni mama, boalra angekua baba huenda ningempa excuse kalishwa limbwa na mke wake sasa mama nae kapewa limbwata na mume wake aisee wazazi ni mtihan mkubwa

ITS SEVEN YEARS NOW NAONA VEMA KUKAA MBALI NAYE, YANI MZAZI ANAKUCHUKIA MPAKA HUELEWI ULIKOSEA NINi
 
Kwa nini wengi wanaamini siku zote mzenguaji ni mzazi? Kuna watoto wao ndiyo wanakuwa chanzo cha kukosekana maelewano na wazazi wao. Aidha, naamini imani kwamba mzazi hatimaye ataishia kumtegemea mtoto ina walakini. Mzazi akiona hakuna maelewano na mtoto anawez kabisa kujiandaa kwa maisha ya uzeeni bila kumtegemea huyo mtoto na kubaki kumtegemea Mungu wake amvukishe safari yake salama.
Nimeipenda hii! Huu ndiyo ukweli, kwanini umtegemee mtoto atakayekurudi? Lazima mtoto atakuwa na kiyongo kwa vile ulimrudi akiwa mtoto ili kumrekebisha
 
Ukiacha yote aliyowahi kunifanyia ikiwa ni pamoja na haki ya kumjua baba lkn hii kauli ( NATAKA KUAGIZA GARI LINGINE KWA SASA HVYO SIWEZI KUKUTUMIA MATUMIZI HUKO CHUONI )ndio ilinfanya nione ilikua bahati mbaya sana yeye kunizaa ingawaje hata upendo wa kinafki nimeushindwa. Yan una mzazi si fukara lkn unaishi maisha ya kuomba omba yeye yupo busy kuhangaika kulinda ndoa yake and worse yeye ni mama, boalra angekua baba huenda ningempa excuse kalishwa limbwa na mke wake sasa mama nae kapewa limbwata na mume wake aisee wazazi ni mtihan mkubwa
ITS SEVEN YEARS NOW NAONA VEMA KUKAA MBALI NAYE
YANI MZAZI ANAKUCHUKIA MPAKA HUELEWI ULIKOSEA NINi
Hii ni kawaida kwa mabinti kuchukiwa na mama zao. Wala usijali sana. Ukitaka nikupe mifano 5 kutoka wanachama wa JF ambao mama zao wa kuwazaa wanawachukia bila sababu, nitakupa
 
Ukiacha yote aliyowahi kunifanyia ikiwa ni pamoja na haki ya kumjua baba lkn hii kauli ( NATAKA KUAGIZA GARI LINGINE KWA SASA HVYO SIWEZI KUKUTUMIA MATUMIZI HUKO CHUONI )ndio ilinfanya nione ilikua bahati mbaya sana yeye kunizaa ingawaje hata upendo wa kinafki nimeushindwa. Yan una mzazi si fukara lkn unaishi maisha ya kuomba omba yeye yupo busy kuhangaika kulinda ndoa yake and worse yeye ni mama, boalra angekua baba huenda ningempa excuse kalishwa limbwa na mke wake sasa mama nae kapewa limbwata na mume wake aisee wazazi ni mtihan mkubwa
ITS SEVEN YEARS NOW NAONA VEMA KUKAA MBALI NAYE
YANI MZAZI ANAKUCHUKIA MPAKA HUELEWI ULIKOSEA NINi
Aisee.....
 
Back
Top Bottom