Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Mi naamini bond hutengezwa utotoni lkn ukubwani hakuna, mimi najitahidi kwenye dini na kumuomba mungu anifanyie wepes labda naweza kujaribu kumfikiria lkn moyo unakataa kabisa, hata nikiandika msg ya kumjulia hali wakati mwingin naona niifute nisitume tena, kwa sasa wanae wengine wanampiga matukio ndo anajaribu kujirudi lkn kiukwel sina nae mazoea kabisa
Watoto wanaopendwa ndo huwa wanaharibika
 
Ubinafsi tu, mimi baba amelelewa na wazazi wawili na babu na bibi wanajali hasa , sasa kama umelelewa vizur roho ya kumtelekeza mtoto unatoa wapi kama si ubinafsi,
Mi nasema mtu ukikoroga ukazaa na mtu mkatibuana effect usihamishe kwa watoto,
Umejuaje kama baba kukutelekeza? Ukute mama ndo kakunyima nafasi ya kumjua
 
Mimi mpaka kufikia umri huu sijawahi kushuhudia wala kuona upendo wa dhati kutoka kwa mtu yeyote. Kwanza sijalelewa kabisa na mzazi yeyote yule. Nilibahatika kuishi na mlezi kidogo tu nae nikaona ananiongezea mapicha picha tu katika maisha yangu nikatemana nae.

Ninae mzazi mmoja, wenyewe mnamuita "Mama", ila kuhusu huyu Mama naomba niishie hapa hapa.
[emoji16][emoji16][emoji16] mkuu elezea kidogo
 
Niliwai kumkalisha chini nikamwambia ,baada ya kumwambia ukweli tangu siku hiyo mimi na yeye tumekuwa kama chui na paka anasema kwamba mimi nimemdharau, sijamuheshimu wakat nilikua namwambia ukwel tuu kwamba asifanye vitendo vya hovyo anaitia aibu familia
Analewa?
 
Ujue nilijua hili tatizo labda la kutokuelewana na mzee ni la kwangu pekee yangu.. form four nzima nimetumia uniform za washikaji,,, namaliza shule ,, matokeo hayakuwa poa sana mzazi anakwambia toka nyumbani kwangu kwani wewe sio mwanangu nenda kamuulize mama yako baba yako ni nani…..
Hivi kwanini wababa huwa wanawazingua watoto wa kiume[emoji16][emoji16]
 
Waafrika tumekua malimbukeni wa dini, mbona wazungu hawana maadili kabisa kwa issue za wazazi wao ila wanazidi kupaa ila sisi tunaojifanya tunajua sana maadili ndio umasikini wa kutisha!!

Biblia mbona imesema kuwa wazazi wasichokoze watoto Bali wawalee katika maadili meaning wakifeli Hilo jukumu obviously laana haiwezi kuwa reliable maana Kila kitu kina Haki na wajibu.

Mfano mzazi wangu alikua hafurahii mafanikio yangu yaani hata nikiwa chuo nikifaulu hawezi nipongeza. Nakumbuka nimepata ajira ya kwanza akanuna hata simu hapokei!! Nakumbuka hata siku naenda interview alininyima nauli na hakupokea simu sema ni vile tu bahati nasibu nikafanyiwa interview kwa simu!!. Na kabla sijapata kazi nlikua nmejiajiri Bado akawa ananikashifu kuwa siwezi fika kokote, nikaanza kuingiza pesa akaanza nifokea kuwa niache hiyo kazi hata kama inanipa Hela ila sio ya mtu mwenye degree!! Hahahah kazi Nako nikapata akanizimia simu!!

Kuna wakati huwa sielewi shida ni nini Hawa wazazi alafu Kuna mpuuzi anasema eti sijui utalaaniwa??

Hapo sijaongelea mama mzazi kabisa ambaye alikua hataki hata nilipiwe ada. Mimi sijawahi mwambia mtu Nina mama Wala kumpost sijui nani kama mama maana nikikumbuka niliyopitia huwa sihesabu kama nina mama. Tukiwa wadogo alikua yupo radhi tulale njaa Ila yeye ashibe!!

So kama Mungu ni mwenye haki kweli sidhani atapokea laana za watu wenye Roho za Giza kama hizo.
Mkuu kwani uliwakosea nini? Baba na mama wote wakuchukie?au ulikuwa mtukutu?
 
Be warned, This post is strictly for God's Believers. If you'll find it useless, you're strongly advised not to provoke or outrage targeted Audiences.

View attachment 2553687

Natumaini nyote mko salama, and so do I.

Tatizo la wa toto kutoku[patina na wazazi lipo sana, haijalishi ni mzazi wa kiume au wa kike wengi wetu humu inawezekani mzazi mojawapo kati ya baba na maama hatupatani nae. Achilia mbali mawasilianao kua hafifu bali unakuta mtoto Fulani na mzazi Fulani katika familia hawapatani kabisa, kutokana na nature ya maisha mara nyingi mzazi asiyekua na mahusiano mazuri na watoto au mtoto hua ni baba.

Lakini pia kwa watoto wa kike mara nyingi hua mzazi wao wa kike ndio hua hawapatani nae, lakini kwa sie wakiume ni aghalabu kusikia hatupatani na mama zetu. Ila rate ya baba kutopatana na watoto/mtoto wake ni kubwa Zaidi kuliko ya mama.

Kuna baadhi ya sababu zisizo rasmi zinazoweza kumfanya Baba asiwe na mahusiano mazuri na mwanae:- 1. Baba kutosimama kwenye misingi ya ubaba katika familia na kujikita katika uzinzi,uhuni, ugomvi,ubabe na ukorofi usio na msingi,kutekeleza familia nk. 2: baba kusahau kwamba wanawe wameshakua watu wazima hivyo wanaweza kujiamlia mambo yao katika maisha pia kuamua mustakabali wa familia yao, hivyo baba anakua anataka awachukulie kama watoto tu wasioweza kuamua chochote katika familia yake na hawana uwezo wa kumshauri,kumpinga,kumkosoa na kumuelekeza juu ya jambo Fulani katika famiia.

Baadhi ya sababu hizi zimewafanya wazazi wengi wa kiume kutokua na mawasiliano mazuri na watoto zao, unakuta mtoto anakaa miaka hana mawasiliano kabisa na baba. Kutokana na tabia au makossa anayoyafanya mzai yanaweza kumfanya mtoto asimpende wala kumuheshimu baba yake tena, pengine mtoto anaweza declare kabisa kwamba yeye hana Baba kwa ajili ya madhila anayofanya baba yake.

Inawezekana kutokana na tabia alizonazo baba yako amepoteza misingi ya ubaba hivyo Hupatani nae, labda amekua mlevi sana hadi anachukua vitu ndani ili akalewe akishalewa basi anajikojolea kabisa na kuongea matusi…tabia hiyo imekufanya umchukie,kumdharau na ukate mawasiliano nae. Nipende kukuambia kwamba unakosea sana..tena sana.

Katika Amari za Mungu kumi anasema kwamba Torati 5:16 “Waheshimu baba na mama yako kama BWANA Mungu wako alivyokuamuru,siku zako zipate kuzidi nawe upate kufanikiwa” katika amri zote alizotoa Mungu ukizivunja utakua na la kujibu siku ya hukumu lakini ukivunja amri ya kutowahehimu wazazi hukumu yake utaipata hapa hapa duniani. Kasema kwamba ukiwaheshimu wazazi basi utaishi miaka mingi yenye heri katika dunia lakini kama hutawaheshimu utapata taabu na karaha hapa duniani.

Inawezekana matokeo usiyaone sasa ila ukaja kuadhibiwa kupitia watoto wako, watoto wako wakaja kukusumbua na kukudharau hadi ukajutia kwanini uliwazaa kumbe ni kwakua ulishindwa kuwaheshima wazazi.

Haijalishi baba yako ana tabia gani na mabaya kiasi gani hata kama ni mlevi aliyepindukia hadi anajikojolea mbele yenu na kuwatukana au kumtukana mama yako matusi mbele yenu. Mafundisho yaanasema mkubwa amuheshimu mdogo na mdogo amuheshimu mkubwa , lakini pia yule mkubwa anaweza kumbariki yule aliye mdogo.

So kama mkubwa anaweza kumbariki mdogo hivyo hivyo pia si anaweza kumlaani?? haijalishi baba yako yupo katika hali gani, hata kama kashapoteza ile nafasi ya ubaba katika familia kwa ulevi wake, ukorofi, matusi, umalaya nk…tambua Kamba baba yako huyo bado kashikilia mlango wa Baraka mashani mwako hivyo anaweza kukufungulia Baraka au kukufungia maana yeye ni mzazi wako ulitoka maungoni mwake.

Inawezekana ni mtu mwema uliyeshika dini lakini labda siku moja baba yako kwakuambia kwamba inatakiwa mfanye tambiko la familia, au muende mkanywe au umpe pesa akanyw. Kwakua wewe ni mtu wa ibada hujihusishi na mambo hayo basi ulighafilika na kumjibu labda kwa tone ya hasira kuonyeshwa kutokupendezwa na jambo hilo, elewa hapo umetenda kosa kubwa.

Mungu anasema Zaburi 138:6 “Ingawa bwana yupo juu lakini humuona mnyenyekevu na kumjua mwenye kiburi kutokea mbaliMithali 3;34Hakika bwana huwadharau wennye kiburi bali huwapa wanyenyekevu neema” Kama tulivyoona hapo kwenye maandiko unyenyekevu ndio nguzo kuu kuna sehemu Mungu anasema kwamba yeye hakai nyumbani kwa mwenye kiburi bali kwa mtu mwenye unyenyekevu.

Hivyo basi wewe mtu wa Mungu baba yako anapokuambia maneno mbalimbali yasiyofaa mjbu kwa uyenyekevu kwamba baba haapana jambo hili haliwezekani kwa sababu Fulani lakini ukipandisha sauti kwa mzazi wako basi Mungu atajitenga nawe hata kama wewe ndio ulikua kwenye haki maana yeye kamwe hakai kwa mtu mwenye majivuno na kiburi.


View attachment 2553697
Baba yako kama kakukosea usimchukie na kumdharau kwani yeye ndio mzazi wako, unachotakiwa umuombnea neema ana Baraka aweze kurejea katika hali yake ya kawaida ili aweze kusimama katika ubaba. Ila pindi unapomuhukumu kwamba baba hafai, baba simtaki tena kutokan na tabia zake basi Mungu atajitnga nawe maana unakua umejivisha majivuni na kiburi japokua haki inakua yako ila pindi unapofanya hivyo basi utaoata laana kwani hukumu ni ya mungu sisi tunatakiwa tuombeane rehema na neema.

Nawausia ninyi na kuihusia nafsi yangu kwamba tujitahidi kurejesha mahusiano na mawasialiano mazuri kwa wazizi wetu japokua inawezekana wametenda mambo mabaya, lakini bado hao ni wazazi wetu wanauwezo wa kutulaani na kutubariki maana wao wameshikilia Baraka zetu. Najua ni ngumu sana kwa roho zetu hizi za kibinaadam basi tuombe rehema za kutuwezesha kufanya hivyo.

Kuna wakati kweli mzazi wako anakutenda kitu hadi unajutia kwanini ulizaliwa na baba wa namna hiyo, lakini ndio ishakua kwani hakuna mtu aliyepata privilege ya kuchagua azaliwe wapi na kwa nani. Wazazi pia acheni kufanya maisha ya watoto wenu hasa ya kiroho yawe magumu kutokana na matendo yenu. Mambo mengine hua mnafanya kwa makusudi kabisa ili kuwakomoa watoto wenu eti kwakua nyie ndio mmeshika mpini watoto wapo kwenye makali. Sio vyema kabisa, mnatuumiza na kutuweka katika wakatoi mgumu.

Inspired from true Events.
Da’Vinci

View attachment 2553684
OK mkuu
 
[emoji16][emoji16][emoji16] mkuu elezea kidogo
Mkuu kuna mambo hata nikikuambia unaweza ukapinga kabisa kwamba mzazi anaweza kufanya hivi kwa mwanae tena wa kumzaa. Ni mambo ya ajabu sana yani. Mimi naweza hata kumaliza mwaka bila kuwasiliana na Mzazi wala ndugu yeyote,kwanza hakuna anaejua mahala nilipo.
 
Ukitaka nichambue yote nnayotaka kusema ntamaliza kitabu cha page 800. Kwanza nimeongelea kitu ambacho nna experience nacho.

Sijawahi kulelewa na single mom so ukinitajia kajala na monalisa siwezi kuelezea changamoto zao.

Changamoto nlizoziona mimi zimetokana na mfumo dume. Narudia tena! Mfumo dumeeee!!!! Janaume linajiamulia tu kufanya vitu halitaki ushauri wala nini end of the day familia nzima Inakuja kuingia matatizoni na kulipa mateso ambayo mwanaume huyo ameyasababisha.

Majanga ni mengi na kila mtu ana ya kwake. Kwa waliopitia ya wazazi wa kike nao waseme.
Again hapo hauongelei mfumo dume. Kuwa muelewa. Mfumo dume ni mfumo unaomtambua kama baba kiongozi wa familia na mama msaidizi wake.

It means wote wanashirikiana. So kama mwanaume analeta ubabe hiyo sio structure ya mfumo dume bali hilo ni tatizo binafsi la muhusika.
 
Watz wengi wanamatatizo ya Afya ya Akili

Yaani Mimi Akili yangu bado hipo vizuri siwezi kumchukia Mtu awe au ndugu maana njaa na umasikini na Matatizo ya Afya Akili vikiungana lazima muwachukie watu. Eti Mtu anamchukia Mzazi au Mzazi anamchukia mtoto what a kid?
Kama umelelewa vizuri huwezi elewa vile watu wanapitia. Nimesoma visa vingi hapa nikamshukuru Mungu kwamba sikuwahi pitia waliyoyapitia. Familia yetu haina ugomvi hata chembe tunaishi peace sana.
Pole kwa wate wanaopitia changamoto na wazazi wao.
 
Mleta mada soma waefeso imeandika "ninyi kina baba msiwachokoze watoto wenu"... Mungu aliona upuuzi wa wazazi kujigeuza miungu kisa kwenye amri zake tumeamrishwa kuwatii wazazi. Mimi binafsi sina tatizo na wazazi wangu maana mapema sana nilishagundua kasoro nikaamua nisamehe kabisa kiroho safi na kwenda nao kijanja. Wakati natoka home kuja Dar kusaka LIFE sikua hata na nauli. Mzee mimi nilishamfuta kwenye ishu za kumwomba hela tangu niko Advance. Nakumbuka niliomba mama anikopeshe nauli nitamlipa baada ya wiki 1. Na kweli wiki ilivyopita akakumbusha deni ikabidi nilipe. Kimsingi nilikuwa na sababu nyingi sana za kuwapotezea wazazi ila nikawaza mambo mengi mno na kuamua kupotezea. Watu wote hawako sawa. Wazazi wengi sana wanalalamika kutelekezwa ila ukichunguza chanzo ni wao wenyewe.
 
Mleta mada soma waefeso imeandika "ninyi kina baba msiwachokoze watoto wenu"... Mungu aliona upuuzi wa wazazi kujigeuza miungu kisa kwenye amri zake tumeamrishwa kuwatii wazazi. Mimi binafsi sina tatizo na wazazi wangu maana mapema sana nilishagundua kasoro nikaamua nisamehe kabisa kiroho safi na kwenda nao kijanja. Wakati natoka home kuja Dar kusaka LIFE sikua hata na nauli. Mzee mimi nilishamfuta kwenye ishu za kumwomba hela tangu niko Advance. Nakumbuka niliomba mama anikopeshe nauli nitamlipa baada ya wiki 1. Na kweli wiki ilivyopita akakumbusha deni ikabidi nilipe. Kimsingi nilikuwa na sababu nyingi sana za kuwapotezea wazazi ila nikawaza mambo mengi mno na kuamua kupotezea. Watu wote hawako sawa. Wazazi wengi sana wanalalamika kutelekezwa ila ukichunguza chanzo ni wao wenyewe.
Baba Yako na baba yangu ni mapacha... mwambie baba Yako ana pacha wake Ambae ni baba angu...!
 
Baba Yako na baba yangu ni mapacha... mwambie baba Yako ana pacha wake Ambae ni baba angu...!
Tuwapotezee tu maana wanatia hasira. Mimi nimeamua tu kwenda naye kijanja maana bado kuna mambo ya kifamilia anahitajika. Na kama Mungu ashatubariki hakuna haja ya kupambana na mzazi ila muhimu tu ajue misimamo yako kuwa HUTAKI MAMBO YA KIFALA KWA SASA.
 
Tuwapotezee tu maana wanatia hasira. Mimi nimeamua tu kwenda naye kijanja maana bado kuna mambo ya kifamilia anahitajika. Na kama Mungu ashatubariki hakuna haja ya kupambana na mzazi ila muhimu tu ajue misimamo yako kuwa HUTAKI MAMBO YA KIFALA KWA SASA.
Ila naomba maelekezo unaishije nae kijanja...Mimi nashindwa kabisa kujizuia najikuta sitaki kabisa mawasiliano yoyote na yeye...ebu nifundishe unavyo ishi na mzazi wako
 
Back
Top Bottom