Kwa wanandoa: nani ana jukumu la kufua nguo zenu za ndani?

Kwa wanandoa: nani ana jukumu la kufua nguo zenu za ndani?

Nimetebasamuu halafu nikataka kucheka ila kicheko kikapotea....

Haya mambo banaa, na usishangae kuna walioachana kisa kufua nguo za ndani....

Mke anasema mimi sifui boksa zako unavaa wiki nzima unarudia...
Mume anakasirika kwanini hunijali na mimi nispoona boksa safi navaa ya jana...!!!🤔🤔🤔 (ana mkomoa nani...! Mbupuuu au mkee..!!?). Ukurutu unaanzia hapa..

Kuoa au kuolewa ni zaidi ya kufanya harusi, shurti kwanza uwe umepevuka kiakili/maarifa na uwe na busara za kutosha.

Ukiwa na mihemko, hasira za mkizi na maamuzi yasiyo na kichwa wala miguu, umekwisha.....!!

Jiulize tuu, kutoa/kutolewa mahari ndo sababu ya kubadili mfumo wako wa maisha?

Kama wakati uko mseja ulikuwa unajimudu, kwanini baada ya kuoa/kuolewa uwe mlemavu mwenye viungo vyote? Hii ni hata kina dada, kama ulikuwa unajigharamia kwanini baada ya kuolewa ugharamikiwe...!!

Fanya huduma unayopewa na mwenza kama zawadi/nyongeza isipokuwepo isokuletee masononeko, maumivu au kuona hutendewi haki au kudhulumiwa.

Sikuzote penda maisha ya kujitegemea na si kutegemea flani kwa namna yeyote ile. Atayekupenda kwa dhati atakufata hapo ulipo ukiwa unajimudu na yeye asikufanyie jambo ili umuelekee, afanye bila kutarajia malipo.

Suluhiso la kuondoa hiyo kero tajwa, wekeni bajeti ya luku ya kutosha kwa mwezi, bajeti ya bili ya maji, nunueni mashine ya kufulia, chupi/boksa za kuvaa mwezi mzima bila kurudia.

Siku ya kufua iwe mara moja au 2 kwa wiki mnatumbukiza visinda vyenu humo, vesti, soksi, hendikachifu, brazia, gagulo, skin tite kisha mnaanika kama hamna mashine ya dryer.

Mkishindwa hapo tembeeni wizout. Yaani wewe usivae boksa, nayeye asivae kufuli wala brazia, nawewe usivae vesti wala soksi kukwepa nani afue na pia mtapunguza gharama ya kuzinunua.

NB: Dada wa kazi asifue nguo yeyote ya ndani. Mpeni suruali mashati magauni sketi blauzi basi. Hata hendikachifu asifue.

HYGENE: Usirudie kuvaa nguo ya ndani, vaa nguo ya ndani.mara moja kisha ifue.

Mwenye sikio asikie.

Bibi Kasinde.
Kumbe mwenye kuchekesha ye'huwa hacheki, huishia tu kutabasamu?

... 'Tembeeni wizout'..., hili limenivunja mbavu na nimecheka kwa sauti kifala🤣🤣🤣🤣.

Bonge la ushauri na kweli 'mwenye masikio na asikie'
 
Kila mtu anafua zake.Tuache ulemavu wa kuigiza kwenye ndoa.Mtataka mpigishwe mswaki na kulishwa kama vichanga.
Siyo kupigishwa mswaki tu na 'kushikiliziwa' mi nataka.

Ingewezekana hata kutafuniwa nitafuniwe na kumeza nimezewe, kazi yangu iwe ni kushiba tu.

Hata kuendewa haja niendewe, lakini dunia inagoma, eti lazima niende chooni mwenyewe na ku piz lazima nihusike moja kwa moja bila kusaidiwa na mtu!
 
Kwenye ukuaj wangu had Sasa hiyo ni kazi ya mke watu wasilete uzungu wa et kusaidiana ooh sijui 50/50 mim sitak hayo wewe nenda katafute mim na watoto tule mim nitakufulia hata kukufua na wewe nitafanya ivo

Hiyo boxer hainigharim chochote as long as nakula nashiba [emoji4]
.......mimi nitakufulia hata kukufua na wewe......😘 Nimeipenda sana hii.
Btw, umeolewa?
 
Siyo kupigishwa mswaki tu na kushikiliziwa mi nataka.

Ingewezeka hata kutafuniwa nitafuniwe na kumeza nimezewa, kazi yangu iwe ni kushiba tu.

Hata kuendewa haja niendewe, lakini dunia inagoma, eti lazima niende chooni mwenyewe na ku piz lazima nihusike moja kwa moja bila kusaidiwa na mtu!
Aise dunia ingekubali kuendewa chooni ingekuwa raha tupu.

Yaani mtu anaenda chooni kwa niaba yako
 
Nguo hufuliwa na mwanamke, ziwe nguo za ndani ama za kawaida, huo ndio upendo, Mwanaume atafua nguo hizo kama kuna changamoto ya namna fulani tu,kama mambo ya kiafya,mke mgonjwa, mke hayupo katika mazingira ya kalibu na ulipo nk.

Hakuna utaratibu wa kwamba kila mtu afue za kwake, eti za furani zinanuka,au zamu ya mme leo kesho ya mke nk. Mkianza mambo hayo hapo hakuna ndoa ila kuna washindanaji tu.

Mke mwema hufua nguo za mme wake, humuandalia mavazi mme wake na kuhakikisha usafi wote wa mme wake.

Kama mwanaume ukishaona umeanza kujifuria nguo mwenyewe , tambua kuna changamoto katika mahusiano yenu ya ndoa ambayo bado hayajiweka wazi , na utambue uzeeni utahangaika sana na huyo mwanamke. Mwenye masikio na asikie.
 
Kwenye ukuaj wangu had Sasa hiyo ni kazi ya mke watu wasilete uzungu wa et kusaidiana ooh sijui 50/50 mim sitak hayo wewe nenda katafute mim na watoto tule mim nitakufulia hata kukufua na wewe nitafanya ivo

Hiyo boxer hainigharim chochote as long as nakula nashiba [emoji4]
Kabisaaa, hata mke awe mtu wa ofisini , akirudi lazima afanye majukum yake ikiwemo na usafi wa wote wawili na watoto, mimi nawasha tv kabisa na kina junior tunanza kuangalia katuni zetu mama anafua boksa huko uani.

Hiyo ndio ndoa wakati wa amani, mkianza eti leo na wewe fua , boksa zako zinanuka , mara oooh mm leo nimechoka hiki kufanya , kwani wewe huna mikono, kwani zamani ulikuwa unafanyiwa na nani?. Kila kazi mm! Hapa na 50/50 hiiiiiiiiiii umekwisha mwanaume
HAPO NDOA HAKUNA ,ILA IPO NDOANO [emoji28][emoji28]
 
Wema Wangu uliniponza, nikasema KAMWE sitaingilia majukumu ya MTU, niliingia kuoga, nikajisahau kuvua boxer, basi baadae ya kuoga nikaamua niifue kabisa nikaiweka toilet. Duh hio kesi yake, imekuaje leo, kuna nini, blablablaaa. Nikajisemea eeghh Kumbe.....
 
Wema Wangu uliniponza, nikasema KAMWE sitaingilia majukumu ya MTU, niliingia kuoga, nikajisahau kuvua boxer, basi baadae ya kuoga nikaamua niifue kabisa nikaiweka toilet. Duh hio kesi yake, imekuaje leo, kuna nini, blablablaaa. Nikajisemea eeghh Kumbe.....
Hata mim ningekuhoji au Kuna jambo limetendeka lakukufanya wewe ufue hiyo nguo? Maana sio kazi yako kufua
 
Back
Top Bottom