Kwa watumishi wa Mungu Joel na Munalove

Kwa watumishi wa Mungu Joel na Munalove

Pole sana kwa kuamini kuwa waimbaji wa nyimbo za gospel ni watu wachaMungu......refer to Rose,Mbasha F,Bahati Bukuku,Gozbat......hao ni vielelezo halisi vya kuni za motoni.
Hahahaaaaaa......kuni tena mkuu???!!
 
Mara nyingi huwa tunasikia watu wakubwa kabisa duniani wanaingia TZ kimya kimya na wanaondoka kimya kimya, hii inamaanisha Kama binaadamu kuna wakati wanahitaji faragha. Kila wakati kuzungukwa na makamera inachosha. Halafu kaja kwenye mazishi ya mtoto na sio kuuza sura! Tatizo tumezoea wasanii wetu ambao wengi ni wa hovyo hovyo huwa wanauza sura hadi kwenye misiba
Faragha hadi kwenye msiba. Acheni kutetea ujinga nyie,
Mtu kanywa bapa kalewa nyie mnamtetea eti ni maji! Maji yanalevya?
 
Kwani mtumishi wa Mungu hatakiwi kuwa na mahusiano ya kimapenzi? Ikiwa aliingia kwa kujifunika au kutokujifunika hayo ni maamuzi yake binafsi hayahusiani na utumishi wake! Kumsaidia Mona alipokuwa Kenya huo ni ubinaadamu tu ambao huenda umechagizwa na ukaribu wao. Kuhusu kumshauri au kutomshauri wewe na mimi hakuna tujualo huenda alimshauri ila Mona hakutaka kuupokea ushauri huo, huenda hakumshauri na huenda kila kilichofanywa na Mona kimefuata ushauri wa huyo mtumishi. Usiwe mtu wa kulaumu laumu tu kila wakati!!!!
iv cox kumbe upogo na huku
 
Faragha hadi kwenye msiba. Acheni kutetea ujinga nyie,
Mtu kanywa bapa kalewa nyie mnamtetea eti ni maji! Maji yanalevya?
Kwani faragha mipaka yake ni ipi? Kama hakutaka makamera Nadhani ni maamuzi binafsi na wala haihusiani na utumishi wake.
 
Wanajamvi katika sakata la kifo cha mtoto Patrick na mkanganyiko juu ya msiba uwe wapi na nani baba halisi wa mtoto kuna huyu mtumishi wa Mungu anaitwa Joel Lwaga. Joel Lwaga mimi namfahamu kama mtumishi wa Mungu aliyeushikilia wokovu na mwimbaji wa nyimbo za injili. Wimbo wake maarufu wa "Sitabaki kama nilivyo" ambao pia ruby aliufanyia cover hauishi kunibariki masikioni mwangu.

Katika hili swala la Muna Joel ametajwa kama bwana wa Muna wa sasa, ukiachilia mbali haijathibitishwa hizi tuhuma kwa Mtumishi wa Mungu siyo nzuri kwani zinalitukanisha jina la Bwana wa Majeshi tunayemuamini.

Pili, Joel alikuwa karibu na Muna mpaka Nairobi alikokuwa anamuuguza mtoto, hata tukichukulia kwamba ni urafiki tu wa watumishi kusaidiana (maana inasemekana Muna naye "eti" ameokoka), kwanini Joel Lwaga hakukaa na Muna kumshauri vyema kuhusu huu mkanganyiko wa baba wa mtoto na sakata zima la msiba?
Kuna maana gani kwa watumishi wa Mungu kuwa pamoja na kushirikiana huku hamshauriani katika maswala nyeti kama haya mpaka yanaleta taharuki kwenye jamii?

Tatu, Joel jana airport amepita kwa kujificha sana huku amejifunika usoni na poll over ni nini hiki? Anahofu ya nini? Ana hatia gani? Biblia inasema waovu ndiyo wenye hofu, hukimbia hata wasipokimbizwa.
Muna na Joel mliyoyafanya yamefanya watu wahoji ukristo wenu na utumishi wenu kwa Mungu. Mtumishi wa Mungu ukifikia hapo ni rahisi hata kulifanya jina la Mungu litukanwe na Roho Mtakatifu akufuriwe(God forbid).
Joel na Muna mjitafakari uhusiano wenu na Mungu na jinsi mnavyolitukanisha jina la Bwana wa Majeshi mnayemtumikia.View attachment 804179View attachment 804180
Hawa ni wasanii wa nyimbo za injili.
Usanii na wokovu ni vitu viwili tofauti. Unaweza ukawa msanii na kuimba nyimbo za injili na hujawahi kuzaliwa upya katika ufalme wa Mungu au kinyume chake. Wengi wa tunaowaita wasanii wa injili ni wafanya biashara ya injili tofauti ilivyofahamika kuwa kumwimbia Mungu ni huduma ya moyo kwa hiari (good faith)
 
Joel alienda Nairobi kwa show kazi Zake za uimbaji na sio kumsindika Muna kuuguza, Muna alivoona Joel anakazi Nairobi ndo akaamua kusafiri na mtoto Nairobi awe karibu na baby na inasemekana hyo mtoto natumika kutoa ushuhuda majukwaani Joel akiwa ana perform NB MBONA HAWASEMI MTOTO ALIKUA ANATIBIWA HOSPITAL GANI HUKO KENYA???
 
Mm nina mifano ya watu waliliojifanya wameokoka. Baadae wanatongoza waumini wao na kulala nao pasipo ndoa. Wengine wanashauri mtu aachane na mchumba wake ili yeye achukue mzigo utasikia huyo uliye nae sio chaguo la Mungu.tusidanganyane hakuna mkamilifu duniani.aliweza Yesu.binadamu asilimia kubwa tunatenda dhambi Na kujificha kujifanya watakatifu.
 
Mm nina mifano ya watu waliliojifanya wameokoka. Baadae wanatongoza waumini wao na kulala nao pasipo ndoa. Wengine wanashauri mtu aachane na mchumba wake ili yeye achukue mzigo utasikia huyo uliye nae sio chaguo la Mungu.tusidanganyane hakuna mkamilifu duniani.aliweza Yesu.binadamu asilimia kubwa tunatenda dhambi Na kujificha kujifanya watakatifu.
Unalolisema ni la kweli kabisa mkamilifu ni Mungu tu, hata Biblia inasema hakuna ambaye hafanyi dhambi.
 
Back
Top Bottom