Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Mbona Corona imeshaenea nchi nzima tayari
MODs tafadhalini msiufute huu uzi kama mlivyofuta ule wa siku tatu za sala ambao pia ulikuwa wa nia njema mno. Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na bado hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gazeti nzima lakini mapovu matupu au ni seme pumba tupu! Si ujifungie wewe mwenyewe au kama unaona Watz hawachukui hatua kwanini usihame nchi ili ukaishi milele. USA wako lockdown lakini mbona bado wanaambukizana zaidi ya mwezi sasa?

Hao wakenya walijaribu lockdown ikawashinda wakaamua kubadirisha kuwa curfew ya kuanzia saa moja jionj hadi SAA 11 asubuhi sasa wewe unaona hiyo ni lockdown? Kwani huna akili ya kujilinda wewe na familia yako mpaka usimamiwe na serikali.

Kwa taarifa yako USA sasa wametoka barabarani hawataki tena lockdown. Namalizia kwa kukueleza tuondolee umbumbumbu wako hapa!

Kiongozi imara utamjua wakati wa matatizo ya watu wake. Hapa ndio kiongozi imara hujitenga na kiongozi katili.
 
Kakimbilia chato uko yupo kimya hata kanisani leo ajaenda, chezea covid-19 wewe,

Yeye anajua mtafufa nyie yeye ataendelea kuwa rais kwaiyo pambaneni na hali zenu na hapa anatamani serikali isigharamie chochote ukiupata kama kufa wewe kufa inchi inataka maendeleo

Siye tunawaza corona utakuta yeye uko anamuwaza membe na genge lake na uchaguzi 2020

Swali la kujiuliza hayo maendeleo anayoyataka ajiri ya nyani na tembo mbina ajari uhai wa raia

Tulifamya makosa sana 2015
 
Haya mambo watu wameshaongea sana, mimi nafikiri ni suala la kila uongozi wa taasis fulani kuzuia watu wake wasiende mpaka pale hali itakapokuwa sawa kama alivyofanya yule wa kagera.
Yaani itakuwa ni automatic lockdown. Tusiongee sana maana majanga tu
 
Kakimbilia chato uko yupo kimya hata kanisani Leo ajaenda, chezea covid-19 were,

Yeye anajua mtafufa nyie yeye ataendelea kuwa raising kwaiyo pambaneni na hali zenu na hapa anatamani serikali isigharamie chochote ukiupata kama kufa we we kufa inchi inataka maendeleo

Swali LA kujiuliza hayo maendeleo yakipatikana wakufaidi nani wakati watu hawapo

Tulifamya makosa sana 2015

Mkuu ni kweli hata kanisani hajaenda? Inakuwaje kwa hawa wanaojazana kwenye nyumba za ibada kusali ili kuomba corona iishe?
 
"Eti gharama ya kuwalisha watu wakiwa majumbani mwao ni ndogo mno".
Hivi wewe unajua gharama za kuwalisha watu milioni 60.
Asubuhi, mchana na usiku?
Unajua lockdown down itakaa siku ngapi?.
JE corona isipo isha Ina maana watu watakaa ndani mwaka mzima.
Utaweza kuwalisha?

"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"
 
Usifanye lockdowns kwa sababu wengine wanafanya... Kuna mahali nimesoma jinsi Rwanda na Uganda walivyokaribu na familia na ndugu waliopo kwenye lockdowns kwa misaada na auweni/nafuu ya hapa na pale kwenye maisha yao ya kila siku!!
Please mnaposhauri njia/hatua mshauri na tahadhari ya hizo njia/hatua...
Mimi sipingi... Lakini pia sikubaliani na lockdowns za matamko matamko bila kujali hali halisi za watu...!!
Tutakatisha maisha ya wengi!!

Kuna mahali niliandika...
Sisi tutavaa barakoa na kunawa mikono...
Hatutashika midomo, pua na macho... Lakini serikali ifanye makubwa zaidi!!

Mkuu haya yameelezwa sana katika nyuzi nyingi tu. Kuna kupata uzoefu kwa wenzetu hiyo ni faida kwetu. Kwa wenzetu hali tofauti za kiuchumi zimezingatiwa asife mtu njaa:

IMG_20200416_125352_093.jpg


Zaidi kabisa yamo humu:

Hoja za wanaoona lockdown haifai ni zipi? Tuelimishane - JamiiForums
 
Gazeti nzima lakini mapovu matupu au ni seme pumba tupu! Si ujifungie wewe mwenyewe au kama unaona Watz hawachukui hatua kwanini usihame nchi ili ukaishi milele. USA wako lockdown lakini mbona bado wanaambukizana zaidi ya mwezi sasa?

Hao wakenya walijaribu lockdown ikawashinda wakaamua kubadirisha kuwa curfew ya kuanzia saa moja jionj hadi SAA 11 asubuhi sasa wewe unaona hiyo ni lockdown? Kwani huna akili ya kujilinda wewe na familia yako mpaka usimamiwe na serikali.

Kwa taarifa yako USA sasa wametoka barabarani hawataki tena lockdown. Namalizia kwa kukueleza tuondolee umbumbumbu wako hapa!
Eleza njia mbadala nini kifanyike. Maana hata mkirushiana rundo la matusi haitasaidia kutatua tatizo.
 
MODs tafadhalini msiufute huu uzi kama mlivyofuta ule wa siku tatu za sala ambao pia ulikuwa wa nia njema mno. Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na bado hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!
Hili swala la CORONA kama lingekuwa ni kihatarishi cha CCM kuendelea kukaa Madarakani, lingechukuliwa kwa uzito wa kipekee kabisa tena haraka sana lakini kwa vile ni jambo linalowahusu Wananchi wote ndiyo maana wamezembea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu ni kweli hata kanisani hajaenda? Inakuwaje kwa hawa wanaojazana kwenye nyumba za ibada kusali ili kuomba corona iishe?
Ajaenda uyo angekuwa kaenda ungeona vyombo vya habari vinahabarisha yani katwambia katoa siku tatu za kuliombea taifa uyo kaingia chimbo, usikute mda huu yupo chini ya handaki anakula kiyoyozi tu mziki kwa mbali hana muda

Kwaiyo dawa iliyopo sasa in wewe na Mimi kujiongeza hakuna kwenda kanisani, msikitini, bar sehemu yoyote ile nikujipa lockdown wewe ukisubilia hii watangaze unakufa ndugu yangu
 
MODs tafadhalini msiufute huu uzi kama mlivyofuta ule wa siku tatu za sala ambao pia ulikuwa wa nia njema mno. Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na bado hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!
Mr. Wakati unayazungumza hayo uneangalia na upande wako ambao unaweza kukaa ndani miezi kadhaa ukitumia kile ulichonacho ndani.Wakati unayazungumza haya,kuna watu wanaomba hii lock down isitokee ili watu wasave familia zao kwa kurudi na chochote kitu.

Mhe.Raisi atasikiliza nani aache nani?.hata kenya watu walilazimika kutoka kwasababu kuliko kufia ndani akiwa na nguvu anaona bora atoke kutafuta chochote.Msipende kulaumu tu bila kufikiri.unadhani yeye haoni hali ilivyo?shida ni kuwa anaangalia pia ni familia ngapi zitakuwa hatarini kwa kukosa chakula kwasababu ya lockdown.

Acheni hizo lawama za kijinga jaribuni kufikiria familia ambazo pia zipo hatarini kwa kupato.Kuanzia bodaboda na wale wote waliojiajiri ambao wanategemea kipato kinachotokana na nguvu zao za siku.Hiyo NO yako iambie familia yako wajifungia hujalazimishwa kutoka.

Mkijifungia familia nzima ndani mtakuwa salama hivyo deal na familia yako ijifungie.Si ajabu unazungumza NO zako kumbe kwenu mna fensi mlishaamua kujitenga na majirani hata kabla ugonjwa haujaingia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Km unataka lockdown kaa Ndani Wewe na familia

Hivi vitumishi vyenye uhakika wa mwisho wa mwezi kero kweli

Kumbuka kuna watu lazima watoke Ndio wale

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna watu wajinga kweli. Uso mkavu anakwambia gharama za kuwalisha watanzania ni ndogo. Hivyo vyakula vitatoka wapi ikiwa vyakula vingi tunavyokula ukiacha nafaka uzalishaji wake ni wa kila siku na hatuna uwezo wa kuvihifadhi?

Watanzania wangapi wanayo majokufu ya kuhifadhi mbogamboga angalau za wiki moja? Mfano, mimi shughuli zangu ni bustani na ufugaji (mayai). Ukisema watu tukae nyumbani hata soko likiwa wazi sitapeleka hizo bidhaa zangu.

Pia bustani siyo green house hivyo ukishinda siku moja tu inaanza kufa. Watanzania wengi shughuli zao ni za namna hii. Sasa hawa ndugu zetu wengi wao hawana kazi za kufanya au maisha yao ni uhakika hivyo ukiwaambia haya wanakuona taahira tu.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tutakapofikia hatua ya lockdown usisahau kuja na bandiko jingine kusifia... na ndiko tunakoelekea maana hakuna namna hata hao Uganda na Rwanda hawakupenda ila ilibidi...
Siasa na corona ni vitu visivyofananishwa...
Mkuu corona imeanza muda mrefu hadi sasa tulitakiwa tuone watu wakipukutika zaidi ya marekani au italy, ila hali iko tofauti maana kama ni uzembe nasi tuliufanya na bado tunaendelea na shughuli zetu tunakusanyana kama kawaida.
 
Mpaka kafikisha malalamiko kwa Mungu ujue yeye yamemshinda.tumepata kiongozi kibwambwaza kabisa.
Wew ungekuwa Raisi ungefanya nn?

Raisi naye ni mwanadamu tofauti ni kuwa yupo katika nafasi yenye mamlaka.Okey Ulitaka afanyaje?

Kiongozi yoyote anapofanya jambo,huangalia maslahi mapana ya watu wake,hata kama litawaathiri wachache kikubwa litawafaidisha wengi.

Wew nakuona kibwabwaza kwa kuona mtu anaemtegemea Mungu anakosea[emoji57][emoji57][emoji57]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii issue kheri upambane wewe na familia yako tu. Kama una uwezo wa chakula na vitu vingine fanya hivyo, protect your family tu.
Wengine washaelimishwa na bado wanasubiri masia atakaeiponya nchi baada ya siku tatu za maombi, then waache waamini hivyo.
Mkuu mwisho watakuambukiza tu maana hutaishi na familia yako kisiwani,hata yeye mwache ajifiche chato Ila atafikiwa tu unless Kama Mungu ni Athuman
 
Back
Top Bottom