Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Huyu Rais linapokuja suala la majanga anakuwa wa hovyo kwelikweli. Sijui huo upendo anaohubiri ni upi zaidi ya kupambana na majanga kwa watu wake. Ila sishangai maana kwenye utawala wake yamefanyika mambo mengi sana ya kikatili dhidi ya binadamu.

Rais anapokea fedha za kuyakabili majanga yeye anaenda kuzihifadhi BoT ili zi boost uchumi! Sijawahi kuona aisee!
Huyu amekosa weledi wa kuwa Mkuu wa nchi, uwezo wake unaishia kwenye ujenzi wa barabara tu.
 
Kiukweli mh. Amewaangusha sana watanzania namna ya kupambana Na ugonjwa huu, alishauriwa mipaka ifungwe ili usiingie nchini, lakini akapuuza.Kwa sasa dar ndo inatumika kusambaza mikoani huu ugonjwa, serikali imeshauriwa itenge dar Na mikoani mingine lakini bado viburi vimetawala.Nikiangalia bunge letu pale Dodoma halina msaada kabisa namna ya kusaidia umma kupambana Na ugonjwa huu, yaani hata kujadili tu kama taifa barakoa Na sanitizer zinawafikiaje wananchi kwa bei ya chini hakuna.
 
Mleta uzi unapodai lockdowns vile vile dai na mikakati ya kiuchumi kuwasaidia hao mnaotaka wafungiwe ndani!!
Msipokuwa makini njaa, sonona n.k vitaua watu wengi zaidi ya #Covid-19
Lockdown sio lazima kuwafungia ndani ndugu, twaweza Fanya kama mataifa mengine.mfano dar Na mikoani mingine watu wazuiwe kutoka Na kuingia.
 
Kiukweli mh. Amewaangusha sana watanzania namna ya kupambana Na ugonjwa huu, alishauriwa mipaka ifungwe ili usiingie nchini, lakini akapuuza.Kwa sasa dar ndo inatumika kusambaza mikoani huu ugonjwa, serikali imeshauriwa itenge dar Na mikoani mingine lakini bado viburi vimetawala.Nikiangalia bunge letu pale Dodoma halina msaada kabisa namna ya kusaidia umma kupambana Na ugonjwa huu, yaani hata kujadili tu kama taifa barakoa Na sanitizer zinawafikiaje wananchi kwa bei ya chini hakuna.
Hawana maarifa hayo Mkuu, wao wanachoweza ni kuteka na kupoteza raia wema tu. Serikali ya hovyo mno hii.
 
Mkuu ingekuwa TB au ukimwi self protection ingewezekana. Lakini huu, kwa kasi ya maambukizi yake, ugeni wake (nani ajuaye 100%?), kasi yake ya kuuwa, kwamba siyo airborne per se, nk nk.

Mkuu mbona self protection is actually queueing silently waiting for ones' turn?

View attachment 1423746

Lets do the necessary mkuu. Ugonjwa ni mpya hivyo hakuna mwenye uhakika fully kama ilivyp kwa mengine ya muda mrefu kama HIV. Ila tayari tushaelekezwa ni ni cha kufanya mwanzoni ila kama zikitokea findings zinginezo hautodhuru
 
MODs tafadhalini msiufute huu uzi kama mlivyofuta ule wa siku tatu za sala ambao pia ulikuwa wa nia njema mno. Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi, hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na bado hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!
Hii ni petition
Ungeiandika na kuattach majina na sahihi zako pia ukatuomba na sisi kuongeza sahihi kesho ifowadiwe kwa Rais kupitia account yake ya twiter na email ya ikulu
 
Mpaka sasa ventilators zimepungua mloganzila na amana.
Soon zinachukuliwa za muhimbili wakati za Mkapa zimefuatwa.
Tutakufa haswaaaaa
 
MODs tafadhalini msiufute huu uzi kama mlivyofuta ule wa siku tatu za sala ambao pia ulikuwa wa nia njema mno. Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi, hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na bado hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!
Wenzio marekani wanaandamana hawataki lock down. Wewe unaleta ngonjera zilizowashinda wenye uwezo kiuchumi. Iko hivi, maisha yako yanathamani kwako. jifungie ndani wewe na familia yako na serikali itakuunga mkono. Hivyo videbe vyako vya mahindi ulivyoweka stock visikutie kiburi ukaona umeyapatia maisha.
 
Nimekwambia huko ulaya nchi nyingi watu wanapukutika haijarishi aliyefanya uzembe au asiyefanya ila wewe bado unashikilia habari za uzembe na huko Russia watu 300 washapukutika na wakati wao walifunga mapema tu mipaka yake.

Mkuu unajielewa lakini?

Hiki hapa nilichokuandikia:

"Kwamba ulaya au marekani ugonjwa uliingia hakuhalalishi kutokuwepo uzembe uliopelekea ugonjwa huu kuingia kwetu."

Unaionaje statement hiyo pamoja na maelekezo iliyoambatana nayo?

Palikuwa na nyuzi nyingi tu kabla ya ugonjwa kuingia na kabla sana ya ugonjwa kusambaa:

Corona ni uzembe wetu isingetufikia, na itatumaliza tusipoamka sasa - ukweli mchungu - JamiiForums

Mkuu au ndiyo kuwasili tokea sayari nyingine?
 
Wenzio marekani wanaandamana hawataki lock down. Wewe unaleta ngonjera zilizowashinda wenye uwezo kiuchumi. Iko hivi, maisha yako yanathamani kwako. jifungie ndani wewe na familia yako na serikali itakuunga mkono. Hivyo videbe vyako vya mahindi ulivyoweka stock visikutie kiburi ukaona umeyapatia maisha.
Sasa tufanyeje? Dereva wa fuso kazuiliwa mtukura ana corona unadhani tajiri yake atamlipa? Huoni keshafukuzwa kazi tayari? Tajiri atapeleka dereva mwingine huyo atajijua, semeni chakula hamna ndio kwanza mmeanza kununua mahindi sumbawanga
 
Hii ni petition
Ungeiandika na kuattach majina na sahihi zako pia ukatuomba na sisi kuongeza sahihi kesho ifowadiwe kwa Rais kupitia account yake ya twiter na email ya ikulu

Mkuu maboresho ruksa lakini hiyo ndiyo habari yenyewe. Hakuna woga wala nini. Baba askofu kaonyesha njia.

Beleshi kwa jina lake. Huu ni mwanzo tu. Mabadiliko ya sera na mtizamo kwa ugonjwa huu ni sasa.

Ulokole na ucha Mungu ni suala zuri tu. Lakini hilo ni suala binafsi haliwezi kuwa agenda ya nchi.
 
Wenzio marekani wanaandamana hawataki lock down. Wewe unaleta ngonjera zilizowashinda wenye uwezo kiuchumi. Iko hivi, maisha yako yanathamani kwako. jifungie ndani wewe na familia yako na serikali itakuunga mkono. Hivyo videbe vyako vya mahindi ulivyoweka stock visikutie kiburi ukaona umeyapatia maisha.

Mnasoma mkaelewa au yaleyale ya kudandia treni kwa mbele?

Marekani kama ilivyokuwa Spain, Italy, Germany, china nk ugonjwa wamesha udhibiti. Wanaopona in a given time ni wengi kuliko wanaoambukizwa. Kwa maana nyingine idadi ya wagonjwa mahospitalini inapungua.

Ikifikia hapo kwa uangalifu na logically hatua kali zinaanza kupunguzwa kurudi kwenye normal life. Kumbe wewe unadhani imewashinda?

Mnakwenda shule kuhitimu umburula? Kwa nini hawawapokonyi hizo PhD. Usomi wenu mbona ni aibu kwa jamii?

Hata videbe unavyosema huenda ninavyo, sina Ila hata kwa uji tu najua siwezi kufa njaa katika siku 21.

Mbona jela na rumande mnawalisha watu mlo mmoja bado hawafi?

Msitake kuwaweka watu wote hatarini kwa tamaa tamaa zenu za kula kula kilafi. Kula ni muhimu lakini si kuwa ndicho pekee ambacho inabidi kuwa akilini na hata kama unahakikishiwa kuwa hakuna atakaye kufa njaa.

Halafu rejea hizi za kuangalia marekani na ulaya ni kwa ajili ya kulikuza mno suala hili ili kuonekana kuwa haiwezekani?

Hapo Kenya, Uganda au Rwanda hohehahe kama sisi hakufai kupigiwa mfano wala kuwepo katika rejea zenu?

Ama kweli mburula ni mburula tu hata liende shule vipi na hata likazamia kabisa ni mburula tu na litabakia pale pale.
 
Usifanye lockdowns kwa sababu wengine wanafanya... Kuna mahali nimesoma jinsi Rwanda na Uganda walivyokaribu na familia na ndugu waliopo kwenye lockdowns kwa misaada na auweni/nafuu ya hapa na pale kwenye maisha yao ya kila siku!!
Please mnaposhauri njia/hatua mshauri na tahadhari ya hizo njia/hatua...
Mimi sipingi... Lakini pia sikubaliani na lockdowns za matamko matamko bila kujali hali halisi za watu...!!
Tutakatisha maisha ya wengi!!

Kuna mahali niliandika...
Sisi tutavaa barakoa na kunawa mikono...
Hatutashika midomo, pua na macho... Lakini serikali ifanye makubwa zaidi!!
Naona unataka kucopy Rwanda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona unataka kucopy Rwanda

Sent using Jamii Forums mobile app

Sidhani kama ni hivyo. Tufanye kivyetu lakini tuna nafasi ya kujifunza kwa wengine. Tukijiridhisha hata ikibidi kucopy na ku paste ni sawa tu. Muda unayoyoma sana.

Hivi hawa mabalozi wetu huko nje wanafanya nini? Kada hii nyingine nayo ni ya kuangaziwa. Inafanya nini? Hata kutushauri tu, kuweza kupenya hapa salama hakuna?

Au yaleyale woga kwa kwenda mbele? Si mjiuzuru basi tujue kuwa angalau hamkukubaliana?
 
Mkuu unajielewa lakini?

Hiki hapa nilichokuandikia:

"Kwamba ulaya au marekani ugonjwa uliingia hakuhalalishi kutokuwepo uzembe uliopelekea ugonjwa huu kuingia kwetu."

Unaionaje statement hiyo pamoja na maelekezo iliyoambatana nayo?

Palikuwa na nyuzi nyingi tu kabla ya ugonjwa kuingia na kabla sana ya ugonjwa kusambaa:

Corona ni uzembe wetu isingetufikia, na itatumaliza tusipoamka sasa - ukweli mchungu - JamiiForums

Mkuu au ndiyo kuwasili tokea sayari nyingine?
Duh! Mkuu labda wewe tu hujanielewa, mara nyingi watu wamekuwa wakitaja Marekani Italy na Spain kuwa zilifanya uzembe na kututaka sie tujifunze kupitia makosa waliyofanya hizo nchi ili kudhibiti huo ugonjwa. Lakini wakati sie tunataja hizo nchi kuwa zilifanya uzembe kiuhalisia huko ulaya ni nchi nyingi tu zilizoathirika na corona na ndiyo hoja yangu kwamba tatizo sio uzembe na kudharau bali hili ni janga la wote na ndiyo maana hata wale wasiosemwa kufanya uzembe nao hawako salama wanakufa kama wenzao. Urusi alichukua hatua mapema kufunga mipaka ila mpaka sasa ana idadi kubwa ya vifo kuliko sisi huku. Sasa kung'ang'ania kwamba sijui tulisema mapema hivyo ni uzembe sioni cha maana katika hizo lawama.
 
Back
Top Bottom