Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Hii issue kheri upambane wewe na familia yako tu. Kama una uwezo wa chakula na vitu vingine fanya hivyo, protect your family tu.
Wengine washaelimishwa na bado wanasubiri masia atakaeiponya nchi baada ya siku tatu za maombi, then waache waamini hivyo.
Kwa nini tuna serikali na Rais akiwa mkuu wa nchi!!!? Acha dhana potofu.
 
Gazeti nzima lakini mapovu matupu au ni seme pumba tupu! Si ujifungie wewe mwenyewe au kama unaona Watz hawachukui hatua kwanini usihame nchi ili ukaishi milele. USA wako lockdown lakini mbona bado wanaambukizana zaidi ya mwezi sasa?

Hao wakenya walijaribu lockdown ikawashinda wakaamua kubadirisha kuwa curfew ya kuanzia saa moja jionj hadi SAA 11 asubuhi sasa wewe unaona hiyo ni lockdown? Kwani huna akili ya kujilinda wewe na familia yako mpaka usimamiwe na serikali.

Kwa taarifa yako USA sasa wametoka barabarani hawataki tena lockdown. Namalizia kwa kukueleza tuondolee umbumbumbu wako hapa!
Una hoja ya kipumbavu kama ile Polepole ya kupambana na korona kama mnavyopambana na wapinzani!!! Yaani mnatumia ghiliba hata kwenye korona!!!?
 
Kwa nini tuna serikali na Rais akiwa mkuu wa nchi!!!? Acha dhana potofu.

Rais ni kiongozi wa nchi ila hawezi kuwa kila kitu na ndio maana anawekewa wasaidizi hadi wajumbe wa nyumba kumi kwa kila mtaa. Kila mtu ana muhimu kutokana na level yake mkui

Kama kwako Rais ni mtu anaetakiwa kuangalia hadi maslahi ya familia yako bhasi utakuwa useless father/mother..
 
Rais ni kiongozi wa nchi ila hawezi kuwa kila kitu na ndio maana anawekewa wasaidizi hadi wajumbe wa nyumba kumi kwa kila mtaa. Kila mtu ana muhimu kutokana na level yake mkui

Kama kwako Rais ni mtu anaetakiwa kuangalia hadi maslahi ya familia yako bhasi utakuwa useless father/mother..
Ndugu, labda una akili ndogo hivyo inakuwiya vigumu kuelewa kinachozungumziwa. Tuko katika Vita vya kupambana na korona, amiri Jeshi mkuu Ni lazima aonyeshe njia ya mapambano. Mimi nitaiongoza familia yangu, lakini hiyo haiondoi uongozi wa kitaifa kuchukua hatua madhubuti
 
Duh! Mkuu labda wewe tu hujanielewa, mara nyingi watu wamekuwa wakitaja Marekani Italy na Spain kuwa zilifanya uzembe na kututaka sie tujifunze kupitia makosa waliyofanya hizo nchi ili kudhibiti huo ugonjwa. Lakini wakati sie tunataja hizo nchi kuwa zilifanya uzembe kiuhalisia huko ulaya ni nchi nyingi tu zilizoathirika na corona na ndiyo hoja yangu kwamba tatizo sio uzembe na kudharau bali hili ni janga la wote na ndiyo maana hata wale wasiosemwa kufanya uzembe nao hawako salama wanakufa kama wenzao. Urusi alichukua hatua mapema kufunga mipaka ila mpaka sasa ana idadi kubwa ya vifo kuliko sisi huku. Sasa kung'ang'ania kwamba sijui tulisema mapema hivyo ni uzembe sioni cha maana katika hizo lawama.

Mkuu nilikutonya mapema mchawi kama lazima tumtafute baadaye baada ya kuudhibiti huu ugonjwa. Huuoni umuhimu huo?

Lakini kwa hakika, haya hapa chini yalijulikana mapema na kabla sana na ugonjwa usingeingia kama yangezingatiwa:

1. Funga mipaka.
2. Zuia ndege na wasafiri toka nchi zilizo athirika.
3. Weka quarantine wageni wote wanaotaka kuingia nchini toka nje kwa siku 14.
4. Nk nk

Majibu toka serikalini nani hayakumbuki? Nani hajui nani alisema nini? Au unataka tukukumbushe Prof Kabudi alisema nini?

Mkuu kuiandika upya historia ya kilichotokea siyo rahisi sana.

Ni kwa sababu hizo hizo mh. rais angejitathmini sana hasa hapa tulipo. Kwa maana anajielekeza kuliko na lawama kubwa zaidi. Kwa hakika historia itakuwapo hai mno kumhukumu.
 
Mkuu nilikutonya mapema mchawi kama lazima tumtafute baadaye baada ya kuudhibiti huu ugonjwa. Huuoni umuhimu huo?

Lakini kwa hakika, haya hapa chini yalijulikana mapema na kabla sana na ugonjwa usingeingia kama yangezingatiwa:

1. Funga mipaka.
2. Zuia ndege na wasafiri toka nchi zilizo athirika.
3. Weka quarantine wageni wote wanaotaka kuingia nchini toka nje kwa siku 14.
4. Nk nk

Majibu toka serikalini nani hayakumbuki? Nani hajui nani alisema nini? Au unataka tukukumbushe Prof Kabudi alisema nini?

Mkuu kuiandika upya historia ya kilichotokea siyo rahisi sana.

Ni kwa sababu hizo hizo mh. rais angejitathmini sana hasa hapa tulipo. Kwa maana anajielekeza kuliko na lawama kubwa zaidi. Kwa hakika historia itakuwapo hai mno kumhukumu.
Mkuu umejikita kwenye lawama nani alikosea wakati mie nakueleza jinsi uhalisia wa hali ilivyo kuhusu huu ugonjwa, kwani huko kote ulaya palipo athirika na corona hakukuwa na washauri kama wewe au ndiyo walishauriwa ila hawakufuata ushauri ndio maana corona ikaingia? Hao warusi walifunga mipaka kama mlivyoshauri kwa Tanzania ila bado hali mbaya sasa huko.
 
lockdown haiepukiki, inaweza kuwa sasa au baadae lakini ili ugonjwa uishe hapa nchini itabidi tujifungie ndani tu ndio njia inayotumika kama kweli tunataka tuumalize huu ugonjwa. Labda kama kuna mtu anayejua njia nyingine yakumaliza gonjwa hili aje atuambie
 
Wew ungekuwa Raisi ungefanya nn?

Raisi naye ni mwanadamu tofauti ni kuwa yupo katika nafasi yenye mamlaka.Okey Ulitaka afanyaje?

Kiongozi yoyote anapofanya jambo,huangalia maslahi mapana ya watu wake,hata kama litawaathiri wachache kikubwa litawafaidisha wengi.

Wew nakuona kibwabwaza kwa kuona mtu anaemtegemea Mungu anakosea[emoji57][emoji57][emoji57]

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna haja kweli ya kuhamasisha mikusanyiko kipindi hiki misikitini, makanisani na hata huko kunakoitwa makazini ??!!.

Kuna shindikana nini Dar na Zanzibari kuwekewa vizuizi ili ugonjwa usienee nchi nzima ??!!

Kweli tunazidiwa kiasi hicho na nchi kama Rwanda na Uganda ?! Mbona wameweza wao na maambukizi yao hayana madhara . Pia wanahudumia watu wao . Sisi inashindikana nini ?!

Odhis *
 
Mnasoma mkaelewa au yaleyale ya kudandia treni kwa mbele?

Marekani kama ilivyokuwa Spain, Italy, Germany, china nk ugonjwa wamesha udhibiti. Wanaopona in a given time ni wengi kuliko wanaoambukizwa. Kwa maana nyingine idadi ya wagonjwa mahospitalini inapungua.

Ikifikia hapo kwa uangalifu na logically hatua kali zinaanza kupunguzwa kurudi kwenye normal life. Kumbe wewe unadhani imewashinda?

Mnakwenda shule kuhitimu umburula? Kwa nini hawawapokonyi hizo PhD. Usomi wenu mbona ni aibu kwa jamii?

Hata videbe unavyosema huenda ninavyo, sina Ila hata kwa uji tu najua siwezi kufa njaa katika siku 21.

Mbona jela na rumande mnawalisha watu mlo mmoja bado hawafi?

Msitake kuwaweka watu wote hatarini kwa tamaa tamaa zenu za kula kula kilafi. Kula ni muhimu lakini si kuwa ndicho pekee ambacho inabidi kuwa akilini na hata kama unahakikishiwa kuwa hakuna atakaye kufa njaa.

Halafu rejea hizi za kuangalia marekani na ulaya ni kwa ajili ya kulikuza mno suala hili ili kuonekana kuwa haiwezekani?

Hapo Kenya, Uganda au Rwanda hohehahe kama sisi hakufai kupigiwa mfano wala kuwepo katika rejea zenu?

Ama kweli mburula ni mburula tu hata liende shule vipi na hata likazamia kabisa ni mburula tu na litabakia pale pale.
Acha ugoro. Huwezi kumuweka lock up mtu asiye na hatia. Lock down ni sawa na lockup.
Kwanza kwa uchumi upi tulionao? Kibaya zaidi hujui tatizo litaisha lini, ni uchizi! Je tatizo likikaa mwaka mzima?
Usikariri njia moja ya kusolve tatizo,
UpUnaakiri timamu sio hadi ushikiwe bakora, jitahidi kuepuka maambukizi either kwakuji- lockdown, kunawa kwa usahihi mara kwa mara au kuvaa barakoa. Itapendeza kama utafanya vyote kwapamoja.
 
Uganda wamefanyaje kwani au hao siyo binadamu?Afya ni muhimu pamoja na hilo la kufuata riziki huko mjini kwa wale ambao hawana ajira
Mleta uzi unapodai lockdowns vile vile dai na mikakati ya kiuchumi kuwasaidia hao mnaotaka wafungiwe ndani!!
Msipokuwa makini njaa, sonona n.k vitaua watu wengi zaidi ya #Covid-19

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapoamua kuchukua hatua zako usianze kujilinganisha na watu wengine, ikiwa china na ulaya wana ubora katika kila kitu iweje vifo viwe vingi kwao kuliko Africa ambako huduma ni duni. Ulishajiuliza kwa nini maskini anaweza asikanyage hospitali kwa miaka kumi, lakini tajiri kila wiki yupo kwa daktari...
Point yako ni nini



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usifanye lockdowns kwa sababu wengine wanafanya... Kuna mahali nimesoma jinsi Rwanda na Uganda walivyokaribu na familia na ndugu waliopo kwenye lockdowns kwa misaada na auweni/nafuu ya hapa na pale kwenye maisha yao ya kila siku!!
Please mnaposhauri njia/hatua mshauri na tahadhari ya hizo njia/hatua...
Mimi sipingi... Lakini pia sikubaliani na lockdowns za matamko matamko bila kujali hali halisi za watu...!!
Tutakatisha maisha ya wengi!!

Kuna mahali niliandika...
Sisi tutavaa barakoa na kunawa mikono...
Hatutashika midomo, pua na macho... Lakini serikali ifanye makubwa zaidi!!
Tunatakiwa kufanya Lockdown sio kwa sababu wengine wanafanya bali kwa sababu ndio njia kuu inayoshauriwa na wataalam wa afya katika kupunguza maambukizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom