Uchaguzi 2020 Kwani Maandamano yana tatizo gani watu kudai haki na ni halali askari kuyazuia?

Uchaguzi 2020 Kwani Maandamano yana tatizo gani watu kudai haki na ni halali askari kuyazuia?

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Wasalaam wajumbe!

Mimi ninashangaa sana wanaodai kuwa ooh sijui maandamano yatavuruga amani ya nchi, kwani maandamano si yapo kikatiba na yameruhusiwa kabisa pale mtu anapohisi kua haki yake imepokwa?

Kama waandamanaji wanadai kua maandamano ni ya amani na wao hawatashika silaha au kitu chochote chenye kuumiza watembea mikono mitupu pengine na watakua na majani ya miti tu kuashiria amani, utaitaje kua maandamano ni ya haramu?

Ni askari yupi au chombo kipi cha dola chenye mamlaka ya kufyatua Risasi kupiga raia ambao hawana hatia yeyote anatembea kwa amani? Anaweza kufyatua risasi hiyo kwa mamlaka ya nani na anaruhusiwa kufanya hivyo kwa kifungu kipi kisheria au kwenye katiba ya nchi?

Kama watu wamekamata kura zilizopigwa tayari na ushahidi upo wazi, matokeo yanabadilishwa vituoni watu wanaona, mawakala wanatekwa na wengine wanatolewa kwa nguvu, ni mjinga gani atakayeamini kua huu uchaguzi siyo batili? Mnataka hawa wapinzani waseme kipi zaidi ya kupaza sauti na kutoka kudai haki zao?

CCM inachezea sana amani ya nchi hii, wanatolisha watu, wanajifanya kua wao wameshinda kwa uhalali wakati ukweli wanaujua. Kwakua wao ndio chama tawala hawawezi kuliona hilo na wala hawawezi kufurahia wakiona wenzao wakidai haki zao. Wakae kimya maana vitisho vyao haviwezi kua na maana kwa watu walioamua na ipo wazi kuna wapo watakaoumia kwa sababu ya hawa hawa CCM lakini mwafaka utakua umeshafikiwa.

Kikubwa tuviombe vyombo vyetu vya dola vikumbuke mkataba wao na wananchi kua Risasi na mabomu viliunda kwa ajili ya maadui wa nchi. Wananchi siyo maadui wa nchi hii. Wasisikilize maagizo ya walafi na wachumia tumbo wachache wasiokua na huruma na taifa letu.
 
Haya maandamano yaahirishwe hadi siku ya kuapishwa kwa waliopindua maamuzi ya Watanzania. Wakati wanakusanyika kuvishana vilemba vya ukoka ,WaTanzania wapenda amani wanakusanyika kuanzia ngazi zote Mkoa wilaya shina tawi mizizi wakubwa kwa wadogo wake kwa waume lengo ni moja tu lililotangazwa na ACT na CHADEMA.

Hii rai vipi achaneni na kesho.
 
Kama mlikamata kura za wizi kwa nini mlizichoma? Kwa nini msifungue kesi kupinga matokeo mahakamani na huo ndio ukawa ushahidi? Maandamano hayaleti mabadiliko ya uchaguzi ambao Chadema wameshindwa kihalali.
Kihalali au siyo kihalali maandamano ambayo Jeshi hawayataki si ya amani.

Upinzani kama unataka watangaze vita watakaosapoti maandamano nao watoke na silaha, kinyume na hapo sishauri mtu kupeleka kiuno barabarani.

Jeshi limejipanga kwa vita, ww unawadanganya watu waje tu ni maandamano ya amani.
 
Muandamane na wake zenu vyumbani mtuache huku mitaani tufanye kazi.
Tanahitaji kuhudumia maisha yetu na sio kuvurugwa na maandamano.
Kama mnataka kuandamana nendeni sehemu ambapo hakuna watu huko mapolini muandamane,
 
Kihalali au siyo kihalali maandamano ambayo Jeshi hawayataki si ya amani..

Upinzani kama unataka watangaze vita watakaosapoti maandamano nao watoke na silaha, kinyume na hapo sishauri mtu kupeleka kiuno barabarani.

Jeshi limejipanga kwa vita, ww unawadanganya watu waje tu ni maandamano ya amani.
Mh...
 
Bado tuna safari ndefu sana, tunayaone kwa wenzetu tu sisi katiba imekaa kama kiini macho hakuna kinachofwatwa humo hata kidogo.

nikuburutana tu, kwani wakituruhusu tuandamane na wao wakawatuma Polisi kulisimamia hilo shida iko wapi? wao siwameshinda kihalali?

Basi watuache tuandamane wao waapishane kwisha.
 
Maandamano ni kikwazo kwa wengine wanaondelea na shughuli za kujipatia kipato maandamano hayafanyiki ndani hufanyika barabarani mi naamka asubuhi nawasha ndinga barabara unakuta imefungwa kisa wahuni wako barabarani upuuzi huu haukubaliki.
 
Kihalali au siyo kihalali maandamano ambayo Jeshi hawayataki si ya amani..

Upinzani kama unataka watangaze vita watakaosapoti maandamano nao watoke na silaha, kinyume na hapo sishauri mtu kupeleka kiuno barabarani.

Jeshi limejipanga kwa vita, ww unawadanganya watu waje tu ni maandamano ya amani.
Kama ni vita wataianzisha wao wenyewe mapolisi, sisi tuta andamana kwa amani. Mpuuzi yeyote yule akituvuruga basi tutaruka naye juu kwa juu, sasa basi.
 
Kuna uwezekano mkubwa kuwa Watanzania wengi hawajui kama yanaruhusiwa kwa mujibu wa sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tatizo la Elimu ya Uraia ni kubwa sana!

Mambo mengi ambayo ni haki kwa raia raia wengi hawajui hata wanapopatiwa hushukuru kana kwamba wamepewa kwa hisani fulani.

Cha msingi na sekondari ni kufuata taratibu za kuomba kibali na iwapo mtakataliwa ndipo sasa mnaweza ku raise concern kwamba mmefuata taratibu zote kwa mujibu lakini mmekataliwa bila sababu ya msingi.
 
Kama ni vita wataianzisha wao wenyewe mapolisi, sisi tuta andamana kwa amani. Mpuuzi yeyote yule akituvuruga basi tutaruka naye juu kwa juu, sasa basi.
Mapolisi wameshakuambia wamejiandaa kugawa vipigo, hakuna amani hapo acha ulaghai. Toka kabisa na silaha kama unataka vita.
 
Kenya wametupita kwa mambo mengi sana nashangaa wengine ambavyo huwabeza!

Kwa huduma za afya na matibabu Kenya wametuacha mbali sana, kidemokrasia, uchapakazi n.k

Matharani fungua Shule halafu Shule moja ajiri wabongo peke yao halafu ile Shule nyingine ajiri walimu wa kikenya hold other things to remain the same nakwambia utaona perfomance ya ile Shule ya Walimu Kenyans Jinsi itakavyokuja na performance yenye ufanisi mkubwa in all aspects!

Hii inamaana hata sisi wananchi kuna mahala hatujaweza kuwajibika ipasavyo.
 
NIMENUKUU

UKIWAONA HAWA KATIKA MAANDAMANO, ANDAMANA!!
---------------------------------

1. Ukimuona Dudley, mtoto wa kwanza na Freeman Mbowe na wadogo zake wakiongoza maandamano nawe andamana. Freeman Mbowe pekee hatoshi, yeye hawezi kupigwa risasi hata moja. Nafasi yake ya Uenyekiti wa Chama kikuu cha Upinzani nchini inamlinda, ni jicho la Dunia anatazamwa, hakuna risasi inayoweza kuelekezwa kwake hata moja. Pale Mkwajuni Kinondoni risasi ilimkwepa Mbowe ikamuua Akwiline Akwelina. Wazazi wake wanalia hadi sasa, hakuna kitu. Usipowaona watoto wa Freeman Mbowe usiandamane!!

2. Ukimuona Alicia Magabe na watoto wake wa damu andamana. Alicia ni mke wa Tundu Lissu ambae Urais wa Lissu unamhusu zaidi kuliko mimi na wewe. Ukimuona Tundu Lissu peke yake usidanganyike kuandamana. Lissu ndie aliegombea Urais kwa Chama kikuu cha upinzani akiungwa mkono na ACT Wazalendo, huyu ni icon ya uchaguzi, ndie mwanamkakati ktk maandano hayo. Dunia yote ipo kwake, akifa hakuna cha kujificha, mission INATIKI.

Hakuna Askari mpumbavu anaweza kulenga shabaha ktk mwili wa Lissu, risasi zitaelekezwa kwako. Utakufa na si ajabu usifahamike, taarifa zako hazitofika popote, utakufa kama Mbwa, utazikwa siku inayofuata ktk kabuli la futi mbili au usizikwe kabisa. Usipomuona Alicia na wanawe, usiandamane!!

3. Ukimuona Bi Fourtuna Salehe na Bi Aweina Sinani na watoto wao katika maandamano andamana. Hii ni familia ya Maalim Seif ambayo inasemwa kuwa imepelekwa Oman mafichoni tayari. Wanasema watu wameuawa Zanzibar lkn hakuna jina la mtoto wa Maalim Seif wala wa mtoto wa Jussa hata moja. Usiwe mjinga, hukuzaliwa kuwa chambo, hukuzaliwa kwa ajili ya Urais wa Maalim au Lissu. Wakiwa Marais wewe haitokusaidia chochote. Usipomuona mtoto wa Maalim Seif, wake zake na familia yake jilalie zako nyumbani hauna cha kupoteza.

4. Ukimuona Anna Bwana, Wiza na Josina ktk maandamano yaliyoitishwa na wewe ungana nao, andamana kwa moyo mkunjufu kabisa. Hii ni familia ya Zitto Kabwe, akiwa peke yake muache aendelee na kazi yake. Zitto Kabwe ni Kiongozi wa Chama cha upinzani (KC), ni jicho la Dunia hawezi kupigwa risasi taratibu za kuzuia maandamano zinamtambua na kumlinda. Usipomuona mke wake, watoto na ndugu zake wengine achana na kazi hiyo haina faida itakupeleka kuzimu bure.

5. Ukimuona Askofu Bagonza na mkewe, na watoto wake wote ktk maandamano andamana. Akiwa peke yake muombee kwa Mungu, usijiunge nae. Ukimuona Lema na watoto wake, Sugu na mke wake na watoto zake, Msigwa na wadogo zake kutoka Iringa, Heche na mkewe na watoto wake andamana.

Ukiwaona wao peke yao usiandamane, Ubunge na Urais wao hauna maana yoyote kwako. Maisha yako ni ya kwako peke yako, pambana!!
#USIANDAMANE!!
 
Kenya hapo maandamano ni jambo la kawaida kabisa na wanapewa vibali na hata wasipopewa hata wakiandamana wanajielewa hawafanyi Fujo wala uharibifu kwa watu wengine.

Polisi wanaelewa kuwa kuandamana ni haki ya raia kikatiba na kwamba polisi kazi yao ni kutoa ulinzi wa raia na mali zao.

Yani upande wa dola wanajua mipaka yao , haki na wajibu wao vivyo hivyo na upande wa wananchi wanajua mipaka yao haki na wajibu wao.

Napenda kuchukua mfano wa karibu wa Kenya hapo ambapo hata kwa mguu au Baiskeli panafikika maana tukichukua mfano wa nchi kama Africa kusini inaweza kuwa mbali kidogo.
 
Back
Top Bottom