Uchaguzi 2020 Kwani Maandamano yana tatizo gani watu kudai haki na ni halali askari kuyazuia?

Uchaguzi 2020 Kwani Maandamano yana tatizo gani watu kudai haki na ni halali askari kuyazuia?

Kenya wametupita kwa mambo mengi sana nashangaa wengine ambavyo huwabeza!

Kwa huduma za afya na matibabu Kenya wametuacha mbali sana, kidemokrasia, uchapakazi n.k

Matharani fungua Shule halafu Shule moja ajiri wabongo peke yao halafu ile Shule nyingine ajiri walimu wa kikenya hold other things to remain the same nakwambia utaona perfomance ya ile Shule ya Walimu Kenyans Jinsi itakavyokuja na performance yenye ufanisi mkubwa in all aspects!

Hii inamaana hata sisi wananchi kuna mahala hatujaweza kuwajibika ipasavyo .
Huku kudharau-dharau nchi yako ndiko kumefanya hatuendelei kwa miaka mingi na ndiyo 7bbu mojawapo kuu wananchi wakawapigeni chini kwenye uchaguzi huu. Hata hivyo, ndiyo maana tunamhitaji kiongozi makini & mchapakazi kama JPM atuvushe kwenda juu zaidi ya hao unaowaghilibu.
 
Nitaandamana!

Lumumba bhana mara mama mkanye mwanao mara hakuna mtu ataingia barabarani.

Sasa vitisho vya nini kama mnaona watanzania hatupo tayari?
 
Kama mlikamata kura za wizi kwa nini mlizichoma? Kwa nini msifungue kesi kupinga matokeo mahakamani na huo ndio ukawa ushahidi? Maandamano hayaleti mabadiliko ya uchaguzi ambao CHADEMA wameshindwa kihalali.
Wewe punguza Ukuda!

Matokeo ya urais yanapingwa mahakama gani?
 
Wapinzani wajipange kipindi kuanzia sasa kutoa elimu ya uraia wafike hadi vijijini huko waweze kujenga capacity building na awareness kubwa!

Because of ignorance and lack of exposure huko mikoani, wilayani na vijijini raia hawana awareness kabisa!

Wakiona polisi na magwanda wanaogopa Yani kama enzi za ukoloni , fikiria?!

Raia anapaswa kujua polisi ni watumishi wetu wanalipwa kodi zetu tumewapa dhamana ya kutulinda raia na mali zetu.

Kule vijijini hao mawakala wakiambiwa hebu tupisheni kidogo tokeni nje watatoka bila hiyana wala kuhoji!

Wapinzani kubalini matokeo tudumishe amani!
 
NIMENUKUU

UKIWAONA HAWA KATIKA MAANDAMANO, ANDAMANA!!
---------------------------------

1. Ukimuona Dudley, mtoto wa kwanza na Freeman Mbowe na wadogo zake wakiongoza maandamano nawe andamana. Freeman Mbowe pekee hatoshi, yeye hawezi kupigwa risasi hata moja. Nafasi yake ya Uenyekiti wa Chama kikuu cha Upinzani nchini inamlinda, ni jicho la Dunia anatazamwa, hakuna risasi inayoweza kuelekezwa kwake hata moja. Pale Mkwajuni Kinondoni risasi ilimkwepa Mbowe ikamuua Akwiline Akwelina. Wazazi wake wanalia hadi sasa, hakuna kitu. Usipowaona watoto wa Freeman Mbowe usiandamane!!

2. Ukimuona Alicia Magabe na watoto wake wa damu andamana. Alicia ni mke wa Tundu Lissu ambae Urais wa Lissu unamhusu zaidi kuliko mimi na wewe. Ukimuona Tundu Lissu peke yake usidanganyike kuandamana. Lissu ndie aliegombea Urais kwa Chama kikuu cha upinzani akiungwa mkono na ACT Wazalendo, huyu ni icon ya uchaguzi, ndie mwanamkakati ktk maandano hayo. Dunia yote ipo kwake, akifa hakuna cha kujificha, mission INATIKI.

Hakuna Askari mpumbavu anaweza kulenga shabaha ktk mwili wa Lissu, risasi zitaelekezwa kwako. Utakufa na si ajabu usifahamike, taarifa zako hazitofika popote, utakufa kama Mbwa, utazikwa siku inayofuata ktk kabuli la futi mbili au usizikwe kabisa. Usipomuona Alicia na wanawe, usiandamane!!

3. Ukimuona Bi Fourtuna Salehe na Bi Aweina Sinani na watoto wao katika maandamano andamana. Hii ni familia ya Maalim Seif ambayo inasemwa kuwa imepelekwa Oman mafichoni tayari. Wanasema watu wameuawa Zanzibar lkn hakuna jina la mtoto wa Maalim Seif wala wa mtoto wa Jussa hata moja. Usiwe mjinga, hukuzaliwa kuwa chambo, hukuzaliwa kwa ajili ya Urais wa Maalim au Lissu. Wakiwa Marais wewe haitokusaidia chochote. Usipomuona mtoto wa Maalim Seif, wake zake na familia yake jilalie zako nyumbani hauna cha kupoteza.

4. Ukimuona Anna Bwana, Wiza na Josina ktk maandamano yaliyoitishwa na wewe ungana nao, andamana kwa moyo mkunjufu kabisa. Hii ni familia ya Zitto Kabwe, akiwa peke yake muache aendelee na kazi yake. Zitto Kabwe ni Kiongozi wa Chama cha upinzani (KC), ni jicho la Dunia hawezi kupigwa risasi taratibu za kuzuia maandamano zinamtambua na kumlinda. Usipomuona mke wake, watoto na ndugu zake wengine achana na kazi hiyo haina faida itakupeleka kuzimu bure.

5. Ukimuona Askofu Bagonza na mkewe, na watoto wake wote ktk maandamano andamana. Akiwa peke yake muombee kwa Mungu, usijiunge nae. Ukimuona Lema na watoto wake, Sugu na mke wake na watoto zake, Msigwa na wadogo zake kutoka Iringa, Heche na mkewe na watoto wake andamana.
Ukiwaona wao peke yao usiandamane, Ubunge na Urais wao hauna maana yoyote kwako. Maisha yako ni ya kwako peke yako, pambana!!
#USIANDAMANE!!
Simnasemaga watangulie mbele hao, sasa wamesema wanatangulia mbele kuongoza maandamano mmeanza kuhamisha magoli.
 
Sidhani!

Mbona nchi nyingine maandamano ni jambo la kawaida kufanyika mara kwa mara? Mfano Kenya , Je wenyewe hawaogopi mapinduzi?

Labda ufafanue vizuri ueleweke!
Maandamano ya kutokumtambua raisi mteule aliyepo yanakoma wakati gani?
 
Wapinzani wajipange kipindi kuanzia sasa kutoa elimu ya uraia wafike hadi vijijini huko waweze kujenga capacity building na awareness kubwa!

Because of ignorance and lack of exposure huko mikoani, wilayani na vijijini raia hawana awareness kabisa!

Wakiona polisi na magwanda wanaogopa Yani kama enzi za ukoloni , fikiria?!

Raia anapaswa kujua polisi ni watumishi wetu wanalipwa kodi zetu tumewapa dhamana ya kutulinda raia na mali zetu.

Kule vijijini hao mawakala wakiambiwa hebu tupisheni kidogo tokeni nje watatoka bila hiyana wala kuhoji!

Wapinzani kubalini matokeo tudumishe amani!
Hii yote uliyoandika ni UPUUZI.

Hata uwafundishe wawe na PhD kama kura zinaibiwa na NECcm kushirikiana na Policcm hazitavunjwa ni kazi bure
 
NIMENUKUU

UKIWAONA HAWA KATIKA MAANDAMANO, ANDAMANA!!
---------------------------------

1. Ukimuona Dudley, mtoto wa kwanza na Freeman Mbowe na wadogo zake wakiongoza maandamano nawe andamana. Freeman Mbowe pekee hatoshi, yeye hawezi kupigwa risasi hata moja. Nafasi yake ya Uenyekiti wa Chama kikuu cha Upinzani nchini inamlinda, ni jicho la Dunia anatazamwa, hakuna risasi inayoweza kuelekezwa kwake hata moja. Pale Mkwajuni Kinondoni risasi ilimkwepa Mbowe ikamuua Akwiline Akwelina. Wazazi wake wanalia hadi sasa, hakuna kitu. Usipowaona watoto wa Freeman Mbowe usiandamane!!

2. Ukimuona Alicia Magabe na watoto wake wa damu andamana. Alicia ni mke wa Tundu Lissu ambae Urais wa Lissu unamhusu zaidi kuliko mimi na wewe. Ukimuona Tundu Lissu peke yake usidanganyike kuandamana. Lissu ndie aliegombea Urais kwa Chama kikuu cha upinzani akiungwa mkono na ACT Wazalendo, huyu ni icon ya uchaguzi, ndie mwanamkakati ktk maandano hayo. Dunia yote ipo kwake, akifa hakuna cha kujificha, mission INATIKI.

Hakuna Askari mpumbavu anaweza kulenga shabaha ktk mwili wa Lissu, risasi zitaelekezwa kwako. Utakufa na si ajabu usifahamike, taarifa zako hazitofika popote, utakufa kama Mbwa, utazikwa siku inayofuata ktk kabuli la futi mbili au usizikwe kabisa. Usipomuona Alicia na wanawe, usiandamane!!

3. Ukimuona Bi Fourtuna Salehe na Bi Aweina Sinani na watoto wao katika maandamano andamana. Hii ni familia ya Maalim Seif ambayo inasemwa kuwa imepelekwa Oman mafichoni tayari. Wanasema watu wameuawa Zanzibar lkn hakuna jina la mtoto wa Maalim Seif wala wa mtoto wa Jussa hata moja. Usiwe mjinga, hukuzaliwa kuwa chambo, hukuzaliwa kwa ajili ya Urais wa Maalim au Lissu. Wakiwa Marais wewe haitokusaidia chochote. Usipomuona mtoto wa Maalim Seif, wake zake na familia yake jilalie zako nyumbani hauna cha kupoteza.

4. Ukimuona Anna Bwana, Wiza na Josina ktk maandamano yaliyoitishwa na wewe ungana nao, andamana kwa moyo mkunjufu kabisa. Hii ni familia ya Zitto Kabwe, akiwa peke yake muache aendelee na kazi yake. Zitto Kabwe ni Kiongozi wa Chama cha upinzani (KC), ni jicho la Dunia hawezi kupigwa risasi taratibu za kuzuia maandamano zinamtambua na kumlinda. Usipomuona mke wake, watoto na ndugu zake wengine achana na kazi hiyo haina faida itakupeleka kuzimu bure.

5. Ukimuona Askofu Bagonza na mkewe, na watoto wake wote ktk maandamano andamana. Akiwa peke yake muombee kwa Mungu, usijiunge nae. Ukimuona Lema na watoto wake, Sugu na mke wake na watoto zake, Msigwa na wadogo zake kutoka Iringa, Heche na mkewe na watoto wake andamana.

Ukiwaona wao peke yao usiandamane, Ubunge na Urais wao hauna maana yoyote kwako. Maisha yako ni ya kwako peke yako, pambana!!
#USIANDAMANE!!
Hata uandike gazeti HAISADIII!

Tunaandamana kama kawa

Lissu , mbowe, zitto, maalim tupo nao wanatosha kabisa
 
Wasalaam wajumbe!

Mimi ninashangaa sana wanaodai kuwa ooh sijui maandamano yatavuruga amani ya nchi, kwani maandamano si yapo kikatiba na yameruhusiwa kabisa pale mtu anapohisi kua haki yake imepokwa?

Kama waandamanaji wanadai kua maandamano ni ya amani na wao hawatashika silaha au kitu chochote chenye kuumiza watembea mikono mitupu pengine na watakua na majani ya miti tu kuashiria amani, utaitaje kua maandamano ni ya haramu?

Ni askari yupi au chombo kipi cha dola chenye mamlaka ya kufyatua Risasi kupiga raia ambao hawana hatia yeyote anatembea kwa amani? Anaweza kufyatua risasi hiyo kwa mamlaka ya nani na anaruhusiwa kufanya hivyo kwa kifungu kipi kisheria au kwenye katiba ya nchi?

Kama watu wamekamata kura zilizopigwa tayari na ushahidi upo wazi, matokeo yanabadilishwa vituoni watu wanaona, mawakala wanatekwa na wengine wanatolewa kwa nguvu, ni mjinga gani atakayeamini kua huu uchaguzi siyo batili? Mnataka hawa wapinzani waseme kipi zaidi ya kupaza sauti na kutoka kudai haki zao?

CCM inachezea sana amani ya nchi hii, wanatolisha watu, wanajifanya kua wao wameshinda kwa uhalali wakati ukweli wanaujua. Kwakua wao ndio chama tawala hawawezi kuliona hilo na wala hawawezi kufurahia wakiona wenzao wakidai haki zao. Wakae kimya maana vitisho vyao haviwezi kua na maana kwa watu walioamua na ipo wazi kuna wapo watakaoumia kwa sababu ya hawa hawa CCM lakini mwafaka utakua umeshafikiwa.

Kikubwa tuviombe vyombo vyetu vya dola vikumbuke mkataba wao na wananchi kua Risasi na mabomu viliunda kwa ajili ya maadui wa nchi. Wananchi siyo maadui wa nchi hii. Wasisikilize maagizo ya walafi na wachumia tumbo wachache wasiokua na huruma na taifa letu.
Wanajua dikteta hakushinda
 
Fuata taratibu na kwa nini yawe yasio na kikomo
 
Mbona unaruka kama umechomwa kitu kina ncha kali? Nazungumzia kura za kawe mlizodai mnazichoma. Mngezitumia kumrudisha bi kidude.
We KIAZI KITAMU

Halima kurudi peke yake inasaidia nini?

Kwani kawe hazikuibiwa kura za urais?

Kwa kifupi ni nchi nzima kura zimeibiwa na sio utani nimeshuhudia kwa msimamizi kuondoka na bahasha ya khaki nyumbani, kumi na mbili yupo kituoni
 
Wapinzani wakaechini wafanye tathmini ya kina!

Wakubali watokeo tudumishe Amani !

Watafute wafadhili ndani na nje ya nchi, wapange teams za kupita kijiji na mtaa, wawe na roaster na phases!

Watoe elimu ya uraia !

Nia iwe njema na siyo kuleta hasama miongoni mwa wanajamii au serikali na wananchi!

Mpeleke wasomi ambao mtakuwa mmewapa mafunzo kwa muda maalum.

Itabidi muwalipe maana itakuwa ni kama ajira ya mkataba .

Mtaaambia wafanye vizuri ili baada ya evaluation mtawaongezea mkataba kwaajili ya kazi nyingine na kwamba itakuwa renewable kama watajitoa katika kuhakikisha wananchi wanaelewa.

Wananchi wapewe Uhuru wa kuuliza maswali na kujibiwa kirafiki.

Timing itapswa kuwa Nzuri na kuvutia mahudhurio ya wananchi husika.

Ni ushauri tu
 
We KIAZI KITAMU

Halima kurudi peke yake inasaidia nini?

Kwani kawe hazikuibiwa kura za urais?

Kwa kifupi ni nchi nzima kura zimeibiwa na sio utani nimeshuhudia kwa msimamizi kuondoka na bahasha ya khaki nyumbani, kumi na mbili yupo kituoni
Kama ni kweli kwa nini mzichome moto? Kwa nini mliharibu ushahidi?
Wadanganyeni mafala wenzenu
 
Kenya hapo maandamano ni jambo la kawaida kabisa na wanapewa vibali na hata wasipopewa hata wakiandamana wanajielewa hawafanyi Fujo wala uharibifu kwa watu wengine.

Polisi wanaelewa kuwa kuandamana ni haki ya raia kikatiba na kwamba polisi kazi yao ni kutoa ulinzi wa raia na mali zao.

Yani upande wa dola wanajua mipaka yao , haki na wajibu wao vivyo hivyo na upande wa wananchi wanajua mipaka yao haki na wajibu wao.

Napenda kuchukua mfano wa karibu wa Kenya hapo ambapo hata kwa mguu au Baiskeli panafikika maana tukichukua mfano wa nchi kama Africa kusini inaweza kuwa mbali kidogo.
Chadema ushoga unawapeleka kasi Sana...Kenya Mara ngapi wameuana kwa mambo ya kipumbavu kipindi Cha uchaguzi..fanya HV kesho chukua jiwe ingia mtaani kampopoe FFU Amsterdam atakutetea....jiulize marekani kwanini waafrika wanauliwa na hatujawahi sikia Trump anapelekwa Hague...fanyeni kazi madogo
 
NIMENUKUU

UKIWAONA HAWA KATIKA MAANDAMANO, ANDAMANA!!
---------------------------------

1. Ukimuona Dudley, mtoto wa kwanza na Freeman Mbowe na wadogo zake wakiongoza maandamano nawe andamana. Freeman Mbowe pekee hatoshi, yeye hawezi kupigwa risasi hata moja. Nafasi yake ya Uenyekiti wa Chama kikuu cha Upinzani nchini inamlinda, ni jicho la Dunia anatazamwa, hakuna risasi inayoweza kuelekezwa kwake hata moja. Pale Mkwajuni Kinondoni risasi ilimkwepa Mbowe ikamuua Akwiline Akwelina. Wazazi wake wanalia hadi sasa, hakuna kitu. Usipowaona watoto wa Freeman Mbowe usiandamane!!

2. Ukimuona Alicia Magabe na watoto wake wa damu andamana. Alicia ni mke wa Tundu Lissu ambae Urais wa Lissu unamhusu zaidi kuliko mimi na wewe. Ukimuona Tundu Lissu peke yake usidanganyike kuandamana. Lissu ndie aliegombea Urais kwa Chama kikuu cha upinzani akiungwa mkono na ACT Wazalendo, huyu ni icon ya uchaguzi, ndie mwanamkakati ktk maandano hayo. Dunia yote ipo kwake, akifa hakuna cha kujificha, mission INATIKI.

Hakuna Askari mpumbavu anaweza kulenga shabaha ktk mwili wa Lissu, risasi zitaelekezwa kwako. Utakufa na si ajabu usifahamike, taarifa zako hazitofika popote, utakufa kama Mbwa, utazikwa siku inayofuata ktk kabuli la futi mbili au usizikwe kabisa. Usipomuona Alicia na wanawe, usiandamane!!

3. Ukimuona Bi Fourtuna Salehe na Bi Aweina Sinani na watoto wao katika maandamano andamana. Hii ni familia ya Maalim Seif ambayo inasemwa kuwa imepelekwa Oman mafichoni tayari. Wanasema watu wameuawa Zanzibar lkn hakuna jina la mtoto wa Maalim Seif wala wa mtoto wa Jussa hata moja. Usiwe mjinga, hukuzaliwa kuwa chambo, hukuzaliwa kwa ajili ya Urais wa Maalim au Lissu. Wakiwa Marais wewe haitokusaidia chochote. Usipomuona mtoto wa Maalim Seif, wake zake na familia yake jilalie zako nyumbani hauna cha kupoteza.

4. Ukimuona Anna Bwana, Wiza na Josina ktk maandamano yaliyoitishwa na wewe ungana nao, andamana kwa moyo mkunjufu kabisa. Hii ni familia ya Zitto Kabwe, akiwa peke yake muache aendelee na kazi yake. Zitto Kabwe ni Kiongozi wa Chama cha upinzani (KC), ni jicho la Dunia hawezi kupigwa risasi taratibu za kuzuia maandamano zinamtambua na kumlinda. Usipomuona mke wake, watoto na ndugu zake wengine achana na kazi hiyo haina faida itakupeleka kuzimu bure.

5. Ukimuona Askofu Bagonza na mkewe, na watoto wake wote ktk maandamano andamana. Akiwa peke yake muombee kwa Mungu, usijiunge nae. Ukimuona Lema na watoto wake, Sugu na mke wake na watoto zake, Msigwa na wadogo zake kutoka Iringa, Heche na mkewe na watoto wake andamana.

Ukiwaona wao peke yao usiandamane, Ubunge na Urais wao hauna maana yoyote kwako. Maisha yako ni ya kwako peke yako, pambana!!
#USIANDAMANE!!
hata Mwl Nyerere angekuwa na akili kama zako nadhan bado tungekuwa utumwani
 
Kama watu wamekamata kura zilizopigwa tayari na ushahidi upo wazi, matokeo yanabadilishwa vituoni watu wanaona, mawakala wanatekwa na wengine wanatolewa kwa nguvu, ni mjinga gani atakayeamini kua huu uchaguzi siyo batili? Mnataka hawa wapinzani waseme kipi zaidi ya kupaza sauti na kutoka kudai haki zao?
Hao wanaohimiza maandamano wanajinasibu kuwa ni wabobezi wa kila nyanja za kisheria na katiba. Sasa kama kweli hawana nia ovu dhidi ya Watanzania na Tanzania kwa ujumla kwa nini wasitumie ubobezi wao wa kisheria kutafuta "dhania haki" yao kwa ushahidi huo huo wa " kubumba" unaowafafanulia mleta mada!?

Wanashindwaje kutumia ubobezi wao kwenye jambo ambalo wanaona ni zito kwao!?
 
Back
Top Bottom