Kwanini Afrika tunashadadia Mapinduzi ya Kijeshi?

Kwanini Afrika tunashadadia Mapinduzi ya Kijeshi?

Asili ya mwanadamu anapenda kusikia jambo baya kuliko zuri.
Mwanadamu akisikia jambo baya atalifuatilia kwa kalibu kuliko akisikia jambozuri. Hasa kwa sisi watu weusi , maana naona bado mtu mweusi anachembechembe za usokwe.

Mtu mweusi akishika wadhifa anaona ote wajinga.anakosa hofu, huruma, ustaalabu, anajiona yeye ndio anaakili kuzidi wengine ote.
Kwa ufupi bado tupo primitive.
Hii ni ukweli mtupu, tunajiona tuko sawa kiakili ila hapana kwa kweli kuna tatizo mahali
 
Walianza Burkinafaso, wakaja Niger Sasa ni Gabon.

Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.

Nakumbuka hata Mzee Robert Mugabe aliondolewa madarakani "kistaarabu" na jeshi baada ya kuonekana hataki kutoka madarakani ingawa uwezo wake wa kuongoza Zimbabwe ulikuwa unatia shaka.

Tatizo ni nini Kwa Afrika kutegemea majeshi kufanya mabadiliko ambayo kimsingi yanatakiwa yafanywe kupitia mifumo ya kiuchaguzi??
Actually huo ni uchaguzi na pia na ni aina ya Demokrasia maeneo husika yameamua kuichagua na kuitekeleza.

Mathalani Niger, Rais Mohamed Bazum ni kweli alichaguliwa na wananchi kwa kura lakini pia Jeshi lilipompindua wananchi kwa maelfu walijitokeza tena ktk uwanja wa mpira na maeneo mengine nchini humo, kuunga mkono Jeshi kwa Mapinduzi ya Amani, lakini zaidi sana kumuunga mkono Gen. Abdoulrahame Tchiani kwamba ndio kiongozi wao.

Hali hii imetokea pia maeneo mengine kama vile Burkina Faso, Mali na Guinea.

Wananchi kuunga mkono Jeshi na viongozi wa Mapinduzi ni Demokrasia pia Lazima wananchi waheshimiwe Mawazo na matakwa yao.
 
Actually huo ni uchaguzi na pia na ni aina ya Demokrasia maeneo husika yameamua kuichagua na kuitekeleza.

Mathalani Niger, Rais Mohamed Bazum ni kweli alichaguliwa na wananchi kwa kura lakini pia Jeshi lilipompindua wananchi kwa maelfu walijitokeza tena ktk uwanja wa mpira na maeneo mengine nchini humo, kuunga mkono Jeshi kwa Mapinduzi ya Amani, lakini zaidi sana kumuunga mkono Gen. Abdoulrahame Tchiani kwamba ndio kiongozi wao.

Hali hii imetokea pia maeneo mengine kama vile Burkina Faso, Mali na Guinea.

Wananchi kuunga mkono Jeshi na viongozi wa Mapinduzi ni Demokrasia pia Lazima wananchi waheshimiwe Mawazo na matakwa yao.
Lakini hao wanajeshi wakichukua hayo madaraka hawatudishi kwa wananchi mkuu,,
 
Sababu za mapinduzi zipo tofauti,kushindwa kwa serikali kuongoza nchi vyema,maslahi ya jeshi yakipuuzwa,Rais kutofautiana na jeshi,kung'ang'ania madarakani kwa muda mrefu n,k.

Gabon kama nchi kiuchumi iko vizuri,akuna nchi ya africa ilifanya uchaguzi pande zote wakakubali matokeo.ilikua ni kosa jeshi kukubali Ally Bongo kung'ang'ania akuongoza wakati sio mzima ki afya.
 
Lakini hao wanajeshi wakichukua hayo madaraka hawatudishi kwa wananchi mkuu,,
Ni kweli kabisa.
sasa hiyo ni changamoto na ni kasoro kama kasoro nyingine ambazo hata ktk utekelezaji wa Demokrasia ya kawaida, mathalani uchaguzi kasoro hutokea. Huenda tuendako kukawa na hali tofauti let's wait and see..
 
Unapo andika hii comment yako upo Uganda au ni Kwa hisia zako??


Samahani lakini
Nimekaa Uganda najua nachokiandika.Afrika maendeleo yake yanarudishwa sana nyuma(indirectly) na hawa watu wanaitwa wazungu na policies zao za hovyo(sio kama na support kiongozi kubaki madarakani muda mrefu) lakini nachopinga ni hii aina ya naming wanayopewa viongozi wa kiafrika wakikaa madarakani mda mrefu.

Case study Libya: the man was doing good but guess what?wazungu na hii kitu yao inayoitwa democracy waliwamezesha sumu watu kilichotokea kila mtu aliona.

Another case study:Uganda ilifanya misimamo yake juu ya ndoa na misingi ya watu waishi vipi lakini umeona response ya hawa watu kutoka west(capitalist).Sanctions!! I think you heard.(interpretation unayopata hapa ni kwamba we aren't sovereign states) ndio maana naweza sema acha tu na Museveni aendelee kwa maana hakuna namna
 
Walianza Burkinafaso, wakaja Niger Sasa ni Gabon.

Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.

Nakumbuka hata Mzee Robert Mugabe aliondolewa madarakani "kistaarabu" na jeshi baada ya kuonekana hataki kutoka madarakani ingawa uwezo wake wa kuongoza Zimbabwe ulikuwa unatia shaka.

Tatizo ni nini Kwa Afrika kutegemea majeshi kufanya mabadiliko ambayo kimsingi yanatakiwa yafanywe kupitia mifumo ya kiuchaguzi??
Itakuwa tumechoka vyama vilivyojaa madarakani muda mrefu,uminywaji wa demokrasia.
 
Habari ya kuondoana kwa masunduku ya kura ni uhuni wa juzi tu. Umewekwa na aliye madarakani ili aendelee kukaa. Sehemu kubwa ya dunia uhuni huo hauna hata miaka mia. Kwa maelfu ya miaka binadamu wameondoana kwenye utawala kwa nguvu. Kama walivyo wanyama wengine wa jamii yetu.
 
Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.
Sasa ukiangalia ni tawala zimejaa ufisadi mkubwa kuwatoa kweny box la kura ni ngumu maan wanafanya kila namna wajitangaze washind. So hapo kuna nn zaid ya kuwaondoa kwa nguv wakolon weusi
 
Ndio ivyo itakavyokua,watawala wa Dunia wanaamini kwenye demokrasia awawezi kukubali nchi itawaliwe kijeshi kwa muda mrefu.
Je hizo haki ambazo wananchi tunazililia, ambazo tunazikosa kupitia uongozi wa kiraia tunazikosa.tutazipata kupitia uongozi wa kijeshi? Ambao hawarudishi uongozi kwa wananchi zaidi ya wao pia kutanguliza tamaa. Huwa sioni maana ya huu ushabiki.
 
Back
Top Bottom