Kwanini Afrika tunashadadia Mapinduzi ya Kijeshi?

Kwanini Afrika tunashadadia Mapinduzi ya Kijeshi?

Kwanza nipende kusema mleta mada umeandika uongo huenda ulikua unajua au hujui chochote, nipende tu kukwambia mgabe hakupinduliwa kama unavyozania wew, ndio maana unapaswa kujiuliza baada ya hayo mapinduzi feki ni kwanini marekani na umoja wa ulaya hawakuondoa vikwazo vya kiuchumi kwa zimbabwe.

Kingine demokrasia ni jini ambalo linatafuna haki ya waafrika katika kufikia maendeleo yaliyo bora sababu inamapungufu mengi hata kwa waliyoileta huko ulaya na marekani mfano ni chaguzi za marekani hilary clintoni alimzidi kura Trump mwisho wa siku Trump akawa raisi, ukija kwa biden nae alimzidi Trump na tukaona Trump followers wa republican walivamia bunge kufanya vurugu kwa kupinga matokeo.

Hapa ndio utajua kuna watu nyuma ya pazia wameishikiria marekani na wanaamua nani awe raisi kwa wakati upi na nani asiwe raisi, jambo hili hata hapa nyumbani Tanzania tumeliona mwaka 2020. Ndio maana nasema ni upumbavu kupanga mstari kwenda kupiga kura wakati kiongozi alishajulikana ni yupi.

Tukija kwenye mada yako, mie naona ni ulimbukeni kwa wanaoshabikia (coup d'etat) mapinduzi ya kijeshi zidi ya viongozi wa kiafrika waliokuwa si waadilifu kwa nchi zao.

Sababu haitaweza kuondoa matatizo mengi yanayozikumba nchi za afrika hasa tatizo la umaskini. Nimalizie tu kwa kusema time will tell.
 
Kwa kweli Afrika sijui niseme nini, sasa hata kule Niger ECOWAS itazidi kupata kigugumizi cha kuwaondoa wale wanajeshi waliopindua serikali halali. Na hakuna ushahidi wanajeshi wataleta neema wananchi wanayodhani wataipata. Ni sawa tu na nchi nyingine kama Kenya, Tanzania nk. ambazo wananchi wanakuwa na mzuka kwa raisi fulani anapogombea kisha akikaaa kidogo madarkani wakibaini hawezi kutimiza zile shauku zao wanaanza kumchukia ghafla.

Mfano HAPO KENYA Ruto alidhaniwa ataleta neema ya kiuchumi lakini ilivyoonekana neema haipo kirahisi walewale waliomchagua wanaanza tena kuandamana. Sudani ni hivyohivyo walimtoa Albashiri nini sasa wamepata?

Ni bora wananchi wenyewe wangeandamana jeshi likawasapoti lakini siyo kujifanya linachukua madaraka huku haijulikani ni lini watayakabidhi kwa raia, wanajeshi ni binadamu kama walivyo hao maraisi kwahiyo tusishadidie sana jeshi kushika madaraka.

Nadhani kuna mkono wa Urusi hata kama siyo moja kwa moja lakini Putin na New Order yake ana agenda fulani ya siri na Afrika tusipoangalia tutageuka vibaraka wa Urusi sawa tu na tulivyokuwa vibaraka wa nchi za Magharibi. Tunapigana Vita vya Ukraine bila kujijua
Upo sahihi.
Libya walimng'oa Ghadafi wapate Rais mzuri zaidi ya Ghadafi.sasa hivi hata yule Ghadafi mbaya wanamtamani arudi lakini awampati.
 
Uko sahihi sana kiongozi,

Mathalani Niger,
ufaransa iliamuru Rais Bazum kumtimua kazi mkuu wa majeshi Gen.Tchiani ambae sasa ndie kiongozi wa Mapinduzi, kwa mtazamo wake tofauti na Rais Bazum kuhusu uwepo wa makambi ya Jeshi la ufaransa na Marekani ktk ardhi ya Niger. Sasa b4 hajafutwa kazi akafanya yake na kazi ikawa imekamilika.

Hizi ni miongoni mwa baadhi ya sababu nyingine zilizopelekea Mapinduzi na zitakazoendelea kuwaondoa mamlakani viongozi wengi barani Africa.

Usaliti miongoni mwa viongozi.
Kuzorota kwa uchumi kupindukia,
Kuzorota kwa hali ya kiusalama,
Umaskini wa kutupwa,
Rushwa kupindukia na iliyokithiri kitaasisi.

Ukosefu wa ajira kwa vijana.
Nguvu ya mataifa ya nje kiuchumi na ushawishi ndani ya serikali za Africa.
Kuzorota kwa hali za maisha ya watu na makazi yao.
Njaa na ukosefu huduma muhimu za afya, maji, umeme, Elimu n.k.

Kutofautiana falsafa ya kuongoza. nchi miongoni mwa viongozi.
Uchu na ulafi wa Madaraka.
Kupuuzwa kwa Katiba, utawala wa Sheria na utawala bora.
Kubinywa na kukandamizwa kwa haki na uhuru wa habari na kujieleza.

Kupuuzwa kwa Demokrasia.
Kung'ang'ana Madarakani kwa nguvu au kwa wizi wa kura.
Kukandamizwa haki za binadamu na usawa.
Mabadiliko ya Katiba na Sheria mbalimbali za kuwabakiza viongozi mamlakani.

Haya ni baadhi tu ya mambo machache yanaweza kuchochea Mapinduzi.

Hizi point hakuna hata moja ambayo hai apply Tz
 
Kwanza nipende kusema mleta mada umeandika uongo huenda ulikua unajua au hujui chochote, nipende tu kukwambia mgabe hakupinduliwa kama unavyozania wew, ndio maana unapaswa kujiuliza baada ya hayo mapinduzi feki ni kwanini marekani na umoja wa ulaya hawakuondoa vikwazo vya kiuchumi kwa zimbabwe.

Kingine demokrasia ni jini ambalo linatafuna haki ya waafrika katika kufikia maendeleo yaliyo bora sababu inamapungufu mengi hata kwa waliyoileta huko ulaya na marekani mfano ni chaguzi za marekani hilary clintoni alimzidi kura Trump mwisho wa siku Trump akawa raisi, ukija kwa biden nae alimzidi Trump na tukaona Trump followers wa republican walivamia bunge kufanya vurugu kwa kupinga matokeo.

Hapa ndio utajua kuna watu nyuma ya pazia wameishikiria marekani na wanaamua nani awe raisi kwa wakati upi na nani asiwe raisi, jambo hili hata hapa nyumbani Tanzania tumeliona mwaka 2020. Ndio maana nasema ni upumbavu kupanga mstari kwenda kupiga kura wakati kiongozi alishajulikana ni yupi.

Tukija kwenye mada yako, mie naona ni ulimbukeni kwa wanaoshabikia (coup d'etat) mapinduzi ya kijeshi zidi ya viongozi wa kiafrika waliokuwa si waadilifu kwa nchi zao.

Sababu haitaweza kuondoa matatizo mengi yanayozikumba nchi za afrika hasa tatizo la umaskini. Nimalizie tu kwa kusema time will tell.

Umeonyesha mapungufu ya democrasi ila hujaonyesha ni mfumo upi bora wa kisiasa,mimi naamini democrasia ndio mfumo bora wa kisiasa shida ni kwamba democracia ni rahisi sana kuingiliwa na wenye nguvu.
 
Kuna chama nchi fulani kinajifanya hakioni yanayoendelea hizo nchi nyingine...kiko madarakani miaka yote...viongozi wanabadirishana tu vitengo..mzunguko ni uleule..familia ni zilezile...matatizo ni yaleyale

Hivi hawa watu wa mabakamabaka hawashtuki na hawaoni..wakaondoa hii kadhia??
 
Kwa kweli Afrika sijui niseme nini, sasa hata kule Niger ECOWAS itazidi kupata kigugumizi cha kuwaondoa wale wanajeshi waliopindua serikali halali. Na hakuna ushahidi wanajeshi wataleta neema wananchi wanayodhani wataipata. Ni sawa tu na nchi nyingine kama Kenya, Tanzania nk. ambazo wananchi wanakuwa na mzuka kwa raisi fulani anapogombea kisha akikaaa kidogo madarkani wakibaini hawezi kutimiza zile shauku zao wanaanza kumchukia ghafla.

Mfano HAPO KENYA Ruto alidhaniwa ataleta neema ya kiuchumi lakini ilivyoonekana neema haipo kirahisi walewale waliomchagua wanaanza tena kuandamana. Sudani ni hivyohivyo walimtoa Albashiri nini sasa wamepata?

Ni bora wananchi wenyewe wangeandamana jeshi likawasapoti lakini siyo kujifanya linachukua madaraka huku haijulikani ni lini watayakabidhi kwa raia, wanajeshi ni binadamu kama walivyo hao maraisi kwahiyo tusishadidie sana jeshi kushika madaraka.

Nadhani kuna mkono wa Urusi hata kama siyo moja kwa moja lakini Putin na New Order yake ana agenda fulani ya siri na Afrika tusipoangalia tutageuka vibaraka wa Urusi sawa tu na tulivyokuwa vibaraka wa nchi za Magharibi. Tunapigana Vita vya Ukraine bila kujijua
Watu wanataka wezi wapya sio kila siku wezi hao hao tu na watoto wao. Mwizi mpya anaweza kuja na mbinu mpya za wizi zinazoweza kuwa na unafuu hata mtoto wa masikini akaambulia makombo.
 
Walianza Burkina Faso, wakaja Niger Sasa ni Gabon.

Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.

Nakumbuka hata Mzee Robert Mugabe aliondolewa madarakani "kistaarabu" na jeshi baada ya kuonekana hataki kutoka madarakani ingawa uwezo wake wa kuongoza Zimbabwe ulikuwa unatia shaka.

Tatizo ni nini kwa Afrika kutegemea majeshi kufanya mabadiliko ambayo kimsingi yanatakiwa yafanywe kupitia mifumo ya kiuchaguzi?
Ni Kwa sababu kura hazijawahi kuwa njia Bora ya kupata uongozi mpya
 
Back
Top Bottom