Kwanini Afrika tunashadadia Mapinduzi ya Kijeshi?

Kwanini Afrika tunashadadia Mapinduzi ya Kijeshi?

Watu wanataka wezi wapya sio kila siku wezi hao hao tu na watoto wao. Mwizi mpya anaweza kuja na mbinu mpya za wizi zinazoweza kuwa na unafuu hata mtoto wa masikini akaambulia makombo.
Aaahaaaa,naunga mkono h
Wewe huoni ni jinsi gani utawala wa kiraia kupitia vyama vya siasa vinavyojimilikisha madaraka na kuiba chaguzi. Kwa chaguzi kama za 2020 hapa Bongo unategemea nini!? Hivi kweli kwa sanduku la kura unategemea nchi kama Tanzania, Uganda, Rwanda au Burundi kufanikiwa.

Sasa hivi tayari wameshakuja na Mikakati kuwa kwanza wanatoa elimu ya katiba kwa miaka 3. Baada ya hiyo elimu ndiyo waanze mchakato. Wanatuona wananchi ni mazuzu.

Next coup ni Equatorial Guinea au Cameron kabla ya kutelemka to East Africa.
Sawa mkuu
 
Walianza Burkina Faso, wakaja Niger Sasa ni Gabon.

Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.

Nakumbuka hata Mzee Robert Mugabe aliondolewa madarakani "kistaarabu" na jeshi baada ya kuonekana hataki kutoka madarakani ingawa uwezo wake wa kuongoza Zimbabwe ulikuwa unatia shaka.

Tatizo ni nini kwa Afrika kutegemea majeshi kufanya mabadiliko ambayo kimsingi yanatakiwa yafanywe kupitia mifumo ya kiuchaguzi?
Shida zimezidi na mifumo ya serikali nyingi za kiafrica zinawapa ulaji jamii ya watu wachache walio kwenye mfumo hivo kupelekea wananchi kutowapenda viongozi wao na pale inapotokea mabaidiliko ya kiuongozi wananchi hufurai wakiwa na matumaini ya huenda hali itabadilika.
 
Walianza Burkina Faso, wakaja Niger Sasa ni Gabon.

Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.

Nakumbuka hata Mzee Robert Mugabe aliondolewa madarakani "kistaarabu" na jeshi baada ya kuonekana hataki kutoka madarakani ingawa uwezo wake wa kuongoza Zimbabwe ulikuwa unatia shaka.

Tatizo ni nini kwa Afrika kutegemea majeshi kufanya mabadiliko ambayo kimsingi yanatakiwa yafanywe kupitia mifumo ya kiuchaguzi?
Pia viongozi wengi wa kiafrica sio machaguo ya wananchi.
 
Kwanza nipende kusema mleta mada umeandika uongo huenda ulikua unajua au hujui chochote, nipende tu kukwambia mgabe hakupinduliwa kama unavyozania wew, ndio maana unapaswa kujiuliza baada ya hayo mapinduzi feki ni kwanini marekani na umoja wa ulaya hawakuondoa vikwazo vya kiuchumi kwa zimbabwe.

Kingine demokrasia ni jini ambalo linatafuna haki ya waafrika katika kufikia maendeleo yaliyo bora sababu inamapungufu mengi hata kwa waliyoileta huko ulaya na marekani mfano ni chaguzi za marekani hilary clintoni alimzidi kura Trump mwisho wa siku Trump akawa raisi, ukija kwa biden nae alimzidi Trump na tukaona Trump followers wa republican walivamia bunge kufanya vurugu kwa kupinga matokeo.

Hapa ndio utajua kuna watu nyuma ya pazia wameishikiria marekani na wanaamua nani awe raisi kwa wakati upi na nani asiwe raisi, jambo hili hata hapa nyumbani Tanzania tumeliona mwaka 2020. Ndio maana nasema ni upumbavu kupanga mstari kwenda kupiga kura wakati kiongozi alishajulikana ni yupi.

Tukija kwenye mada yako, mie naona ni ulimbukeni kwa wanaoshabikia (coup d'etat) mapinduzi ya kijeshi zidi ya viongozi wa kiafrika waliokuwa si waadilifu kwa nchi zao.

Sababu haitaweza kuondoa matatizo mengi yanayozikumba nchi za afrika hasa tatizo la umaskini. Nimalizie tu kwa kusema time will tell.

Tafta taarifa sahihi za Siasa za US.
Hiki ulichokiandika hapa ni kanjanja.
 
Walianza Burkina Faso, wakaja Niger Sasa ni Gabon.

Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.

Nakumbuka hata Mzee Robert Mugabe aliondolewa madarakani "kistaarabu" na jeshi baada ya kuonekana hataki kutoka madarakani ingawa uwezo wake wa kuongoza Zimbabwe ulikuwa unatia shaka.

Tatizo ni nini kwa Afrika kutegemea majeshi kufanya mabadiliko ambayo kimsingi yanatakiwa yafanywe kupitia mifumo ya kiuchaguzi?
Hamna uchaguzi huru na wa haki.
 
Walianza Burkina Faso, wakaja Niger Sasa ni Gabon.

Sielewi ni Kwa nini Afrika inakuwa ni ngumu sana kuwaondoa viongozi "wabovu" wasiotakiwa Kwa njia ya kura, badala yake kazi hiyo hufanywa na wanajeshi.

Nakumbuka hata Mzee Robert Mugabe aliondolewa madarakani "kistaarabu" na jeshi baada ya kuonekana hataki kutoka madarakani ingawa uwezo wake wa kuongoza Zimbabwe ulikuwa unatia shaka.

Tatizo ni nini kwa Afrika kutegemea majeshi kufanya mabadiliko ambayo kimsingi yanatakiwa yafanywe kupitia mifumo ya kiuchaguzi?
MKUU NI KWAMBA HUJUI AMA?

Hivi ni kweli wewe huwa ufuatilii mambo yanayotokea humu AFRICA wakati WA uchaguzi,ufuatilii hatua zinazo chukuliwa na viongozi wa Africa wanapokosolewa kistaarabu kabisa kuwa hapa Mheshiwa Raisi umepuyanga.

NB: kukaa madarakani muda mrefu sio shida,shida unafanya Nini?
 
Yapinduliwe tu TUMECHOKA. Mleta uzi upo hapa hapa Africa. Na chaguzi zake unazijua. Rejea uchaguzi wa Tanzania 2020. Ukiona jeshi linapindua na wananchi wanashangilia, tambua kwamba walishachoka, na kwenye sanduku la kura wamefanyiwa u-JECHA mara kadhaa.
 
Kuna mwingine uganda....yeye Alisha sema wazi wazi......yeye ni kotapini Ile ya kwenye baiskeli...kotapini Huwa inaingia Kwa kugongelewa na nyundo...pia utokaji wake ni Kwa kuigonga....Huwa kotapini haitokagi kirahisi rahisi....
Mzee Museveni juzi amesema ya kwamba yeye HANA uchu wa madaraka SEMA tu Waganda ndio wanataka aendelee kuwa Rais wao na ndio maana wanamchagua Kila uchaguzi! Ahahahahaha!!!
 
Mzee Museveni juzi amesema ya kwamba yeye HANA uchu wa madaraka SEMA tu Waganda ndio wanataka aendelee kuwa Rais wao na ndio maana wanamchagua Kila uchaguzi! Ahahahahaha!!!
Alaf akasema ni marufuku Kwa Uganda kuuzwa nguo za mitumba..........

Akaziita Nguo za MAREHEMU WA ULAYA 😊😊....Nimarufuku kuuzwa miguo ya mitumba Uganda
 
Watu wanataka mabadiliko makubwa. Hapa Africa usulutani hauwezi kuwepo kwa namna moja au nyingine.

Kwamba wewe mtoto wako na wajukuu wako mfaidi rasilimali za taifa kisa tu mlipewa dhamana za kuwa viongozi? Mbaya zaidi mnafaidi kwa ufisadi na uhuni wa kuwaona mnaowatawala wajinga na wapumbavu.

Mapinduzi ya kifikra na ya kuondoa viongozi mafisadi wasiofaa yameenea Africa nzima.
 
Kinachoendela Afrika ni sawa na kile kilichotokea Ulaya mwaka 1848. Mapinduzi yalitokea Ufaransa, Ujerumani, Austria, Ukraine, Poland nk na kulikumba bara zima. Watu walikuwa wakijisikia tu, wanaenda kupindua mfalme.
Kama ilivyotokea ile Arab spring iliyoanzia Tunisia na kuendelea nchi zingine za kiarabu baada ya yule kijana wa Tunisia kujichoma moto.
 
Back
Top Bottom