Kwanini Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake?

Kwanini Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KWA NINI BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE HAKUNYANYUA KALAMU KUANDIKA MAISHA YAKE?

Naikumbuka siku hii kama jana vile.

Niko nje ya mipaka ya Tanzania ni nyakati za usiku niko kwa rafiki yangu mmoja ambae ajabu sana yeye ananiambia kuwa aliona kitu katika maandishi yangu toka enzi nikiandika na Africa Events.

Kila tulipokutana alinisisitiza kuwa nipunguze kuandika katika magazeti na majarida na niwe mwandishi wa vitabu.

Wakati ule nilikuwa hili naliona jambo nisiloliweza kabisa.
Huyu rafiki yangu ni ‘’publisher,’’ yaani mchapaji vitabu tena mchapaji wa sifa.

Sasa siku hii tumekaa nyumbani kwake baada ya chakula cha jioni na tunazungumza kuhusu mswada wa kitabu changu cha maisha ya Abdul Sykes.

Rafiki yangu huyu alikuwa kausoma mswada wote akaniambia, ‘’Mohamed umemwandika sana Nyerere tena kwa undani na umakini mkubwa sijapatapo kusoma popote pale mwandishi ambae amemuandika Nyerere kwa kiasi hiki ulichofanya wewe.’’

Huyu rafiki yangu akaendelea, ’’Mimi niliomba miadi na Nyerere na akakubali kukutana na mimi Butiama.

Tulipoonana nikamwambia kuwa kuna mchapaji angependa kufanya mradi wa kuandika maisha yako.’’

Rafiki yangu akaniambia kuwa jibu la Nyerere lilikuwa, ‘’Mimi sizungumzi na mtu wa kati waambie hawa jamaa zako waje wanione mimi mwenyewe binafsi.’’

Rafiki yangu akanambia kuwa huo ndiyo ukawa mwisho wa mazungumzo yao akanyanyuka na kuondoka kuwahi ndege arudi Dar es Salaam.

Huyu rafiki yangu ndiye alikuwa mwakilishi wa hawa wachapaji katika kanda ya Afrika ya Mashariki na Kati na Mwalimu akiwafahamu vyema hawa wachapaji.

Rafiki akanambia hakuona kama kulikuwa na haja ya yeye kulisema hili kwani anasema Mwalimu hili akilijua fika.

Sahib yangu huyu alinifahamisha kuwa jibu lile alilitegemea kwa kuwa yeye kabla ya kuja kumuona Mwalimu alikuwa amefanya utafiti wake na taarifa alizopata zilikuwa Nyerere hataki maisha yake yaandikwe ingawa aliwaruhusu waandishi wawili kutoka Maryknoll, W. R. Duggan na J. R. kuandika maisha yake, ‘’Tanzania and Nyerere,’’ (1976).

Tukawa tunashughulisha fikra zetu kwa nini Mwalimu Nyerere hataki kuadikwa na kwa nini yeye mwenyewe hanyanyui kalamu yake kuandika maisha yake.

Huyu rafiki yangu akaniambia kuwa yeye angependa sana kuchapa kitabu changu lakini hataweza kwa sababu ya ‘’conflict of interest,’’ kwani yeye anafanya biashara na Serikali ya Tanzania na ana wasiwasi na yale maudhui ya kitabu changu.

Akaniambia kuwa kwa uzoefu wake hakuna mchapaji Tanzania atakaechapa kitabu changu.
Kauli hii ilinitia huzuni sana.

Nikamuuliza kwa nini wachapaji hawataki kukigusa kitabu changu?

Rafiki yangu akanijibu kwa ufupi sana, ‘’Wewe unaandika historia ya Julius Nyerere bila ya idhini yake.’’

Rafiki yangu akaniambia, ''Mohamed you have to learn the trade.''
Kwa hakika nilihangaika sana na kitabu changu kwa miaka mingi.

Miaka ile nilikuwa kijana mdogo nisiyejua siasa za Afrika zinavyochezwa na biashara ya vitabu inazunguka katika mzunguko na muhimili upi.

Lakini baadae kama mtu aliyegutushwa kutoka katika njozi likanijia wazo nijaribu kuwasilianana na wachapaji wa Uingereza.

Hakika kila kitu kinakwenda kama Allah alivyokipanga.
Kitabu kikachapwa London.

Baada ya kuchapwa kitabu hiki changu ndipo ikaonekana lazima kitabu cha Maisha ya Mwalimu Nyerere kiandikwe.

Hiki ni kisa kingine hapa si mahali pake kukieleza.

Lakini laiti Mwalimu mwenyewe angenyanyua kalamu kuandika maisha yake kwa hakika tungestarehe sana na kalamu yake.

Mimi hukaa peke yangu kimya nikajifanya mimi ndiye Julius Kambarage Nyerere na sasa naandika maisha yangu.

In Shaa Allah iko siku nitakuonyesheni nilichoandika.
Nimepata kumuonyesha maandishi haya yangu publisher mmoja.

Ajabu sana akaniambia hiki ni kitabu lakini ni riwaya ya aina yake akanihimiza nikamilishe kazi hii.

Akatanitania akaniambia, ''Mohamed umekuwa Irving Wallace?''

Huyu Irving Wallace ni mwandishi wa riwaya akiandika vitabu vyake kutokana na matukio ya kweli katika jamii.

Ukweli ni kuwa mimi sikumgeza Irving Wallace.
Mimi nimemuiga Shafi Adam Shafi jinsi alivyoandika kitabu chake maarufu, ''Haini.''

Lakini uweli utabakia kuwa laiti Mwalimu angeandika kumbukumbu zake tungepata kitabu ambacho si cha kawaida.

Historia ya Mwalimu Nyerere na TANU na uhuru wa Tanganyika ina ladha ya pekee sana waandishi wa kitabu chake hawakuweza kuionyesha ladha hii katika mseto waliopika.

Mseto wao chooko na mchele haukuwa sawia.
Sikuambii mchuzi wa papa wa kulia mseto.

Viungo havikukamilika.

Screenshot_20220317-073156_Facebook.jpg
 
Itakuwa labda alikuwa busy mno na majukumu..all in all asante mzee wetu kwa kutupa historia bila kuchoka achana na wanaosema wewe NI mdini...binafsi Mimi NI mkristo ila sijawahi kuona huo udini unaosemwa kuwa unaleta.kudos!
 
Itakuwa labda alikuwa busy mno na majukumu..all in all asante mzee wetu kwa kutupa historia bila kuchoka achana na wanaosema wewe NI mdini...binafsi Mimi NI mkristo ila sijawahi kuona huo udini unaosemwa kuwa unaleta.kudos!
Ndege,
Ahsante sana.
 
Kwa watu ambao ni viongozi wa kisiasa, kwa upande wangu mimi nadhani mwanasiasa akishafanya makubwa sana, halazimiki sana kuandika tena kitabu kuhusu maisha yake, hiyo ni kazi ambayo wataifanya wengine, tena wengi tu. Ni yule tu ambaye ana hisia kuwa mahali fulani hakufanya vizuri sana ndiyo anaweza akaamua kufanya hivyo, lengo ikiwa ni kujibu maswali ya watu wengi ambayo wameshakuwa wanayo wakijiuliza kichwani ambayo majibu yake wanakuwa hawana.

Hata hivyo, kwa watu ambao ni wajasiriamali na wafanyabiashara wakubwa kama akina Mengi (RIP) na akina MO; hawa ndiyo wanatakiwa waandike sana ili tujue walipitia changamoto zipi hadi kufika hapo walipo sasa. Hii ni kwa sababu hata sisi pia nasi tunatamani sana kufika pale walipofikia wao. Hawa ndiyo tunatakiwa kuwahamasisha waandike sana, tena sana
 
Nisome kitabu cha mwanasiasa tena CCM kweli?
Viongozi wezi
Viongozi wanaojali familia zao
Viongozi hawahawa wanaotupatia wakati mgumu..

Nitasoma cha Mengi..Mo. bakhiresa..
 
Nisome kitabu cha mwanasiasa tena CCM kweli?
Viongozi wezi
Viongozi wanaojali familia zao
Viongozi hawahawa wanaotupatia wakati mgumu..

Nitasoma cha Mengi..Mo. bakhiresa..
Von...
Kusoma ni kutafuta elimu.
Watu hawasomi kitabu kwa kuangalia mwandishi.

Watu wanamsoma Hitler mpaka leo juu ya uovu wake.
Watu wanamsoma Count Victor Lustig hadi leo juu ya kuwa mwizi bingwa.
 
Nahisi aliona taifa lina majukumu mengi ambayo yanahitaji kufanyiwa kazi,hivyo akaona kukaa chini na kuanza andika andika ni kama kukosea heshima muda anaopata kutumikia hili taifa.

yawezekana angekuwepo sasa,angeruhusu kitabu kiandikwe kwakua ameshaona muda wake umeenda na aliyotamani yamekua basi si mbaya kuyaweka ktk maandishi.

kwa wakati ule na kwa uzalendo wake ambao haukua wakuunga unga si rahisi akubali,n sawa na mtoto aliepewa homework afike nyumbani muda wakwenda kucheza aende kucheza wakati kuna homework inamsubiri.

JK alikua na homework na Nchi yake na ndio sababu ya yeye kutoamua kupoteza hata sekunde 1 kufanya kitu kwa ajili yake, ingekua uandishi kuhusu TAIFA lake sidhani kama angekataaa lakini si uandishi kuhusu YEYE.
 
Nyerere hakutaka sifa ndiyo maana akupoteza muda kuandika wasifu wake, hawa wanaoandika sifa zao ni wapuuzi tu. Hivi nani mwenye akili timamu anataka kusoma na kujuwa uozo wa JK au Mkapa, walifanya nini cha maana hapa nchini?
Una uchungu mkubwa moyoni, chuki ,hasira na wivu.
 
Nyerere hakutaka sifa ndiyo maana akupoteza muda kuandika wasifu wake, hawa wanaoandika sifa zao ni wapuuzi tu. Hivi nani mwenye akili timamu anataka kusoma na kujuwa uozo wa JK au Mkapa, walifanya nini cha maana hapa nchini?
Una uchungu mkubwa moyoni, chuki ,hasira na wivu. Fanya kazi ili watoto wako nao wasije kuwa kama wewe
 
Tulipoonana nikamwambia kuwa kuna mchapaji angependa kufanya mradi wa kuandika maisha yako.’’

Rafiki yangu akaniambia kuwa jibu la Nyerere lilikuwa, ‘’Mimi sizungumzi na mtu wa kati waambie hawa jamaa zako waje wanione mimi mwenyewe binafsi.’’
Mwalimu alikuwa sahihi kabisa kutoa hili jibu.
 
Mwalimu alikuwa sahihi kabisa kutoa hili jibu.
Proved,
Ilikuja kujulikana baadae kuwa Mwalimu alikuwa na hofu na historia ya kuamka kwa Tanganyika na kuundwa kwa African Association mwaka wa 1929.

Historia hii haikuwa ikifahamika na wengi kiasi ikawa kama vile historia ya AA haikuweko na hakukuwa na mtu aliyekuwa anaifahamu.

Historia hii ilikuwako pamoja na nyaraza zake kuthibitisha yale yaliyotendeka hadi kufikia kwanza mageuzi makubwa ya TAA 1950 na kuelekea kuundwa kwa TANU 1954.

Kuanzia mwaka wa 1961 uhuru ulipopatikana kulitokea changamoto nyingi kufikia pale ilipotakikana sasa Mwalimu iandikwe historia yake.

Hili lilimtia Mwalimu hofu.
 
Proved,
Ilikuja kujulikana baadae kuwa Mwalimu alikuwa na hofu na historia ya kuamka kwa Tanganyika na kuundwa kwa African Association mwaka wa 1929.

Historia hii haikuwa ikifahamika na wengi kiasi ikawa kama vile historia ya AA haikuweko na hakukuwa na mtu aliyekuwa anaifahamu.

Historia hii ilikuwako pamoja na nyaraza zake kuthibitisha yale yaliyotendeka hadi kufikia kwanza mageuzi makubwa ya TAA 1950 na kuelekea kuundwa kwa TANU 1954.

Kuanzia mwaka wa 1961 uhuru ulipopatikana kulitokea changamoto nyingi kufikia pale ilipotakikana sasa Mwalimu iandikwe historia yake.

Hili lilimtia Mwalimu hofu.
Mzee Mohamed Mwalimu alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanu, Waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika na baadae Rais wa Kwanza wa Tanganyika huru na baadae Tanzania.

Hadi hapo tayari ana jina kubwa kwenye historia ya hili taifa na hata Africa kwa ujumla, sidhani kama historia ya miaka ya nyuma kabla ya mwaka 1953 (TANU kuasisiwa) ingemjengea hofu mwalimu kiasi aogopwe iandikwe.

Unadhani inawezekana kuuongelea Uhuru wa Tanganyika bila kumtaja Mwl Nyerere ?
 
Proved,
Ilikuja kujulikana baadae kuwa Mwalimu alikuwa na hofu na historia ya kuamka kwa Tanganyika na kuundwa kwa African Association mwaka wa 1929.

Historia hii haikuwa ikifahamika na wengi kiasi ikawa kama vile historia ya AA haikuweko na hakukuwa na mtu aliyekuwa anaifahamu.

Historia hii ilikuwako pamoja na nyaraza zake kuthibitisha yale yaliyotendeka hadi kufikia kwanza mageuzi makubwa ya TAA 1950 na kuelekea kuundwa kwa TANU 1954.

Kuanzia mwaka wa 1961 uhuru ulipopatikana kulitokea changamoto nyingi kufikia pale ilipotakikana sasa Mwalimu iandikwe historia yake.

Hili lilimtia Mwalimu hofu.
Ningeshangaa sana kama nisingeona hii comment yako, kiufupi imebeba kile ulichokusudia kuandika.
 
Mzee Mohamed Mwalimu alikuwa Rais wa Kwanza wa Tanu, Waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika na baadae Rais wa Kwanza wa Tanganyika huru na baadae Tanzania.

Hadi hapo tayari ana jina kubwa kwenye historia ya hili taifa na hata Africa kwa ujumla, sidhani kama historia ya miaka ya nyuma kabla ya mwaka 1953 (TANU kuasisiwa) ingemjengea hofu mwalimu kiasi aogopwe iandikwe.

Unadhani inawezekana kuuongelea Uhuru wa Tanganyika bila kumtaja Mwl Nyerere ?
Proved,
Mwalimu inaelekea au watu walilazimisha historia ya kuamka kwa Watanganyika ianze kwake.

Bahati mbaya Mwalimu alikaa kimya wakati historia isiyo sawa inatamalaki.

Haya nayasema kutokana na yale ambayo mimi nimekutananayo wakati natafiti kitabu cha Abdul Sykes.

Kuna barua ya Mwalimu amemwandikia Judith Listowel kuhusu alivyomwandika katika kitabu chake, ''The Making of Tanganyika,'' (1965) akilalamika kuwa hataki maisha yake yaelezwe na alimfahamisha.

Kitabu hiki kipo karibu sana na historia ya kweli ya TANU kuliko vitabu vyote vilivyopata kuandikwa mpaka pale nilipoandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes (1998).

Kitabu hiki hakihitaji maelezo mengi kwani maudhui yake yanajulikana na kimebadili historia nzima ya TANU.

Listowel katika kitabu hiki kawataja wanasiasa wengi aliowapa jina la ''Makerere Intellectuals, '' yaani Wasomi wa Makerere.

Hawa ni Hamza Mwapachu na madaktari watano: Dr. Joseph Mutahangarwa, Dr. Wilbard Mwanjisi, Dr. Michael Lugazia, Dr. Vedasto Kyaruzi na Dr. Luciano Tsere.

Lakini kitabu hiki kimewataja wanasiasa wenyeji kama wa Dar es Salaam kama Schneider Abdillah Plantan, Kleist Sykes na wanae ambao hawa wana uhusiano mkubwa na historia ya mwamko wa Watanganyika katika African Association iliyoanzishwa mwaka wa 1929.

Haiwezekani kuandikwa kwa historia ya uhuru wa Tanganyika bila kumtaja Julius Nyerere.
Hili haliwezekani.

Lakini haiwezekani pia kuandika historia ya Nyerere mwenyewe na historia ya uhuru bila ya kumtaja Abdul Sykes.

Historia ya uhuru wa Tanganyika haiwezekani kukamilika bila ya kuwataja mathalan hawa Makerere Intellectuals wote.

Historia ya TANU imeandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni (1981) na hawa wote niliowataja hapa hawamo kwenye historia hiyo yuko Nyerere peke yake.

Kwa miaka mingi hii ikawa ndiyo historia rasmi ya uhuru wa Tanganyika na inaanza na Nyerere na inaishia na Nyerere.

Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ikawa imepunjika sana.

Mwaka wa 1962 kulikuwa na mradi wa kuandika historia ya TANU na Nyerere mwenyewe alihusika na kazi hii aliikabidhi kwa Abdul Sykes na Dr. Wilbard Kleruu.

Abdul Sykes alijitoa katika mradi huu kwa kuwa kuna mambo hakuweza kukubaliana na Nyerere katika yale ambayo Abdul aliyaeleza na inaelekea tatizo lilikuwa katika uasisi wa African Association chama ambacho baba yake alikuwa katibu muasisi.

Sasa hapa kuna historia kubwa sana kuanzia 1929 hadi kufikia kuundwa kwa TANU mwaka wa 1954.

Nimebahatika kusoma Nyaraka za Sykes kuhusu kipindi hiki kuna mengi muhimu na yangependeza sana watu kuyajua mathalan kuundwa kwa Al Jamiatul fi Tanganyika Tanganyika kutokana na African Association mwaka wa 1933.

Kuna historia ya Nyerere mwenyewe vipi alikutana na Abdul Sykes na upi mchango wake na nduguze pamoja na wazalendo wengine kama Hamza Mwapachu na wajumbe waliokuwa katika TAA Political Subcommitte katika kuunda TANU.

Upi ulikuwa mchango wa Earle Seaton katika TAA kukiwezesha chama kuanza uhusiano wa karibu na UNO nk. nk.

Naona haya yanatosha nikiamini umeelewa kuwa Mwalimu alikuwa na hofu ya historia hii ambayo hadi leo bado inawatisha baadhi ya watu.

Huwezi kuisoma historia hii popote pale ila kwenye kitabu cha Abdul Sykes.
Historia rasmi ya Chuo Cha Kivukoni imefuta historia hii ya kweli.
 
Ningeshangaa sana kama nisingeona hii comment yako, kiufupi imebeba kile ulichokusudia kuandika.
Masta...
Hakika historia hii ni historia ya wazee wangu naijua vyema.
Ni kawaida yangu siku zote kuwashangaza watu.

Jana nimemuandikia mtu mmoja historia hiyo hapo chini:

''Narudia kukufahamisha.
Hakuna "kila mtu anajiandikia," hao kila mtu nani?

Kwani wangapi wamemuandika Nyerere?
William Edget Smith, Thomas Molony, akina Shivji...nani mwingine?

Hawa ndiyo kwako, "watu wa kujiandikia?"

Kuna watu waliokaa na Nyerere kwa karibu toka siku ya kwanza anabisha hodi nyumbani kwa Abdul Sykes kushinda hawa ambao mimi nimewanukuu mara nyingi tu - Mama Daisy na mwanae Aisha Daisy, Abdul, Ally na Abbas Sykes?

Hawa ndiyo leo wa kuambiwa wanajisemea tu?

Hivi unajua kuwa Abdul alikataa Nyerere asipigwe sindano ya chanjo "vaccination," safari ya kwanza UNO 1955 kwa kuogopa hujuma dhidi ya Nyerere?

Abdul hakumuamini yeyote ila mdogo wake Abbas kuhakikisha kuwa Nyerere hapigwi sindano na cheti cha chanjo kinapatikana.

Hivi unajua hata dhifa ya kumuaga haikufanyika Arnautoglo bali kwenye jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika?

Nadhani ushaelewa kwa nini.
Joan Wicken alikuwapo?''

Ati itaandikwa miaka 50 inayokuja.''

Picha hiyo hapo chini ni lango kuu la kuingia jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ambalo ilikuwa shule na hivi sasa jengo hili limetaifishwa:

1648013486543.png
 
Back
Top Bottom