Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
- #81
Yoda,Maelezo yako ni ngumi ya uzito wa heavyweight haswa ila hapo uliposema Mwalimu hakutaka kuweka na ilikuwa sahihi kutoweka mambo yote kwenye maandishi mezani ndipo umeharibu. Ni bora yote yangeweka katika historia huru na ya wazi tu, yasingetugawa bali yangemulika mwanga mkubwa katika historia yetu.
US historia ya utumwa, ubaguzi na vita vya wenyewe kwa wenyewe imewekwa wazi hadi kwenye shule za msingi na imesaidia kusahihisha na kuliimarisha sana taifa hilo.
Kuna mambo yakimhangaisha sana Mwalimu.
Moja ambalo likimpa shida ilikuwa uasisi wa TANU.
Taji la kuanzisha vuguvugu hadi kupelekea kuundwa kwa TANU nani avishwe?
Hii ndiyo sababu kubwa hata ilipoandikwa historia ya TANU na Chuo Cha CCM Kivukoni Abdul Sykes jina lake halipo.
Tukaishi miaka yote na historia ya TANU bila ya Abdul Sykes mwenye kadi ya TANU No. 3 na mdogo wake kadi No. 2.
Kadi No. 1 ya Territorial President Julius Kambarage Nyerere na aliandikiwa na Ally Sykes.
Ikawa historia hii haipo.