Kwanini Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake?

Kwanini Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake?

Proved,
Ilikuja kujulikana baadae kuwa Mwalimu alikuwa na hofu na historia ya kuamka kwa Tanganyika na kuundwa kwa African Association mwaka wa 1929.

Historia hii haikuwa ikifahamika na wengi kiasi ikawa kama vile historia ya AA haikuweko na hakukuwa na mtu aliyekuwa anaifahamu.

Historia hii ilikuwako pamoja na nyaraza zake kuthibitisha yale yaliyotendeka hadi kufikia kwanza mageuzi makubwa ya TAA 1950 na kuelekea kuundwa kwa TANU 1954.

Kuanzia mwaka wa 1961 uhuru ulipopatikana kulitokea changamoto nyingi kufikia pale ilipotakikana sasa Mwalimu iandikwe historia yake.

Hili lilimtia Mwalimu hofu.

Nilijua tangu mwanzo ulikuwa unazunguka tu lakini nia yako ipo katika sentensi ya mwisho.

Mwl Nyerere kamwe hawezi kuhofia Mambo madogo madogo,Huyu ni jabali wa siasa za Afrika hawezi kuhofia wenyeji wa Tandamti na Msikiti wa Manyema.
 
Nilijua tangu mwanzo ulikuwa unazunguka tu lakini nia yako ipo katika sentensi ya mwisho.

Mwl Nyerere kamwe hawezi kuhofia Mambo madogo madogo,Huyu ni jabali wa siasa za Afrika hawezi kuhofia wenyeji wa Tandamti na Msikiti wa Manyema.
Ngongo,
Nizunguke nini hii leo wakati nishaandika mengi kuhusu historia ya TANU?

Historia hii yawezekana kuwa wewe ukaona ni ''mambo madogo,'' lakini wakati wanaandika hiistoria ya TANU mwanajopo mmoja, Hassan Upeka alileta ''notes,'' za majadiliano aliyofanya na Abdul Sykes kuhusu historia ya TANU.

Kiongozi wa jopo alikataa kupokea ''notes,'' hizo akasema Abdul Sykes hana uhusiano na historia ya TANU.

Hili kwao lilikuwa jambo kubwa na salama yao ni kukataa kupokea chochote ambacho kinaweza kuvuruga kitabu chao walichouwa wanaandika.

Wenyeji wa Tandamti (Mshume Kiyate), Kleist Sykes (Kipata), Ibrahim Hamisi (Kipata), Said Ali Mpima (Mkunguni) hawa ndiyo katika waasisi wa African Association na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Iddi Faiz Mafungo, Iddi Tosiri na Mzee bin Sudi hawa ndiyo walikuwa viongozi wa msikiti wa Manyema uliojengwa mwaka wa 1912.

Unajua historia ya hawa wazalendo katika kupigania uhuru wa Tanganyika?
Nakuwekea hapo chini picha ya Baraza la Wazee wa TANU na mitaa waliyokuwa wakiishi:

1648014365597.png
 
Ngongo,
Nizunguke nini hii leo wakati nishaandika mengi kuhusu historia ya TANU?

Historia hii yawezekana kuwa wewe ukaona ni ''mambo madogo,'' lakini wakati wanaandika hiistoria ya TANU mwanajopo mmoja, Hassan Upeka alileta ''notes,'' za majadiliano aliyofanya na Abdul Sykes kuhusu historia ya TANU.

Kiongozi wa jopo alikataa kupokea ''notes,'' hizo akasema Abdul Sykes hana uhusiano na historia ya TANU.

Hili kwao lilikuwa jambo kubwa na salama yao ni kukataa kupokea chochote ambacho kinaweza kuvuruga kitabu chao walichouwa wanaandika.

Wenyeji wa Tandamti (Mshume Kiyate), Kleist Sykes (Kipata), Ibrahim Hamisi (Kipata), Said Ali Mpima (Mkunguni) hawa ndiyo katika waasisi wa African Association na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Iddi Faiz Mafungo, Iddi Tosiri na Mzee bin Sudi hawa ndiyo walikuwa viongozi wa msikiti wa Manyema uliojengwa mwaka wa 1912.

Unajua historia ya hawa wazalendo katika kupigania uhuru wa Tanganyika?
Nakuwekea hapo chini picha ya Baraza la Wazee wa TANU na mitaa waliyokuwa wakiishi:

View attachment 2161293

Hii si historia ya TANU,labda ukisema ni hadithi za kunogesha bazra mitaa ya Kariakoo ningekuelewa.
 
Hii si historia ya TANU,labda ukisema ni hadithi za kunogesha bazra mitaa ya Kariakoo ningekuelewa.
Ngongo,
Ichukulie upendavyo hakuna ugomvi lakini kwetu sisi hawa ndiyo wazee wetu na hiyo ni picha yao na huyo unaemuona hapo ni Julius Nyerere.

Hii ndiyo historia ambayo kwa miaka mingi haikuwa inafahamika.
 
Inapendeza sana...
Smart...
Ungejua historia za hawa wazalendo ndiyo ungestarehe zaidi.

Nitakupitisha kwa haraka.

Kleist Sykes ni maarufu yeye alikuwa katibu muasisi wa African Association 1929 na Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika 1933.

Ameacha mswada wa maisha yake ambao umesaidia sana katika kuijua historia ya African Association.

Mswada huu ni sura katika kitabu, "Modern Tanzanians," (1973) kilichohaririwa na John Illife.

Iddi Faiz yeye alikuwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya na TANU kwa wakati mmoja na ndiye aliyekuwa mkusanyaji wa fedha kwa ajili ya safari ya Nyerere UNO 1955.

Iddi Faiz, Iddi Tosiri na Sheikh Mohamed Ramiyya ni ndugu na ndiyo waliompeleka Nyerere Bagamoyo kumtambulisha kwa Sheikh Ramiyya Khalifa wa Tarika Kadiriyya.

Iddi Faiz alihudhuria mkutano wa kwanza wa TANU Ukumbi wa Arnautoglo August, 1955.

Picha hiyo hapo chini kushoto ni Iddi Faiz, Sheikh Mohamed Ramiyya, Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro na Hatuna Iddi Taratibu Dodoma Railway Station wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.View attachment 2161729

Mzee Mshume Kiyate na Julius Nyerere.
View attachment 2161730
 
Nyerere alitoa ushirikiano/idhini iandikwe historia yake, kwenye kitabu hiki ninachokitaja chini kabisa, halafu, kitabu kilivyochapishwa, kwa sababu ambazo sijazielewa, hakukipenda.

Toka hapo, akawa mgumu sana kukubali kuandikiwa kitabu.

Ila, kuna kitabu amekiandika Mama Joan Wicken, yule msaidizi wake mzungu. Ameacha maagizo kisichapishwe mpaka miaka mingi ipite baada ya kifo cha Nyerere. Hicho kitabu kina mengi sana kuhusu maisha ya Nyerete na utawala wake.

Godfrey Mwakikagile kandika maisha ya Nyerere.

Dr. Thomas Molony wa Edinburgh ameandika "Nyerere: The Early Years" na Dr. Paul Bjerk wa Ohio ameandika "Julius Nyerere" na "Building a Peaceful Nation: Julius Nyerere and the Establishment of Sovereignty in Tanzania, 1960-1964"

Kitabu ambacho kilimfanya Nyerere awe mgumu sana kuruhusu maisha yake kuandikwa ni hiki.

We Must Run While They Walk: a portrait of Africa's Julius Nyerere by William Edgett Smith New York, Random House, 1971. Pp. 296.

Also Published as "Nyerere of Tanzania" by Victor Gollancz, London, 1972.
 
Nyerere alitoa ushirikiano/idhini iandikwe historia yake, kwenye kitabu hiki ninachokitaja chini kabisa, halafu, kitabu kilivyochapishwa, kwa sababu ambazo sijazielewa, hakukipenda.

Toka hapo, akawa mgumu sana kukubali kuandikiwa kitabu.

Ila, kuna kitabu amekiandika Mama Joan Wicken, yule msaidizi wake mzungu. Ameacha maagizo kisichapishwe mpaka miaka mingi ipite baada ya kifo cha Nyerere. Hicho kitabu kina mengi sana kuhusu maisha ya Nyerete na utawala wake.

Godfrey Mwakikagile kandika maisha ya Nyerere.

Dr. Thomas Molony wa Edinburgh ameandika "Nyerere: The Early Years" na Dr. Paul Bjerk wa Ohio ameandika "Julius Nyerere" na "Building a Peaceful Nation: Julius Nyerere and the Establishment of Sovereignty in Tanzania, 1960-1964"

Kitabu ambacho kilimfanya Nyerere awe mgumu sana kuruhusu maisha yake kuandikwa ni hiki.

We Must Run While They Walk: a portrait of Africa's Julius Nyerere by William Edgett Smith New York, Random House, 1971. Pp. 296.

Also Published as "Nyerere of Tanzania" by Victor Gollancz, London, 1972.
Kiranga,
Kitabu hiki cha William Edget Smith (1971) kilipata umaarufu mkubwa kwa nukuu ya maneno ya Nyerere kuhusu Zanzibar kuwa angekuwa na uwezo angekiburuza akakitupa baharini mbali ya Tanganyika.

Labda maneno haya ndiyo yalimkera kwa kuwa tafsiri yake haikuwapendeza wengi katika jamii ya Kizanzibari.

Mswada wa Abdul Sykes na Wilbard Klerruu Mwalimu hakuupenda n matokeo yake ikawa Abdul kujitoa katika uandishi lakini Klerruu akakamilisha mswada lakini haukuchapwa.

Mswada ''ukapotea,'' maktaba ya TANU ukaibuka ghafla na ukachapwa kitabu (1971).

Abdul Sykes baada ya kujitoa katika uandishi ule hakubakia Dar es Salaam aliondoka akaenda Cairo ambako aliishi kwa muda.

Nimabahatika kusoma barua zake alizokuwa akiandika alipokuwa Cairo.

Kitabu cha Listowel (1965) Mwalimu vilevile akawa na matatizo na mwandishi.
Lakini Mwalimu akakikubali kitabu cha Historia ya TANU cha Chuo Cha CCM Kivukoni (1981).

Lakini Mwalimu baada ya kusoma kitabu cha Abdul Sykes alikubali historia ya maisha yake kiandikwe.

Mwalimu alikubali baada ya mazungumzo na marehemu Prof. Haroub Othman.

Kwa nini Mwalimu alibadilisha msimamo wake na kukubali kitabu chake kiandikwe tena na jopo la wanazuoni?

Picha hiyo hapo chini ni Abdul Sykes akiwa Cairo 1963:

1648059707722.png
 
Itakuwa labda alikuwa busy mno na majukumu..all in all asante mzee wetu kwa kutupa historia bila kuchoka achana na wanaosema wewe NI mdini...binafsi Mimi NI mkristo ila sijawahi kuona huo udini unaosemwa kuwa unaleta.kudos!
Nafsi ilikuwa inamsuta, sio muda. Kama alikuwa na muda wa kutafsiri ngano za Shakespeare asingeweza kuandika ukweli kuhusu yeye mwenyewe?
 
Nyerere hakutaka sifa ndiyo maana akupoteza muda kuandika wasifu wake, hawa wanaoandika sifa zao ni wapuuzi tu. Hivi nani mwenye akili timamu anataka kusoma na kujuwa uozo wa JK au Mkapa, walifanya nini cha maana hapa nchini?
Sio "hakutaka sifa" alikuwa na roho ya kutokuweza kuwapa wengine sifa wanayostahiki. Angeandika vipi bila kuwataja waliompokea na kumuingiza kwenye siasa ya kiwango cha Kimataifa?
 
Kwa watu wanaomfahamu Nyerere ni nadra na tabu kupata kauli yake akisema '' mimi au Nime''. Nyerere hakupenda kutajwa kama yeye bali alitumia sana wingi '' Sisi, tuli.. n.k'

Akiwaaga Wazee wa Dar es Salaam pale Diamond kwa nadra nilimsikia akisema '' Nilikuwa Mkristo peke yangu''. Katika siku nadra sana hiyo ilikuwa moja akitumia neno ''Nili..''

Tatizo la kuandika kitabu chake ni kwa kutambua alishirikiana na watu wengine na ni ngumu sana kuandika 'Memoir' yake . Nyerere hakujifaragua wala kujikweza

Nyerere alifahamu kuandika 'Mmemoir' angegusa mambo mengi kama ugomvi wake na akina Abdul Sykes, Bibi Titi, Rais Karume, ujamaa, kutaifisha mali, Bakwata, Mali za Kanisa n.k. na pengine angeligawa Taifa zaidi kwa kitu kidogo cha kuepukika.

Nimesoma kitabu cha AH Mwinyi na BW Mkapa. Ukweli wamekwepa vitu vingi vya msingi.
Hiyo yote ililenga kutoleta mjadala wa kuligawa Taifa. Mkapa hakupenda alilazimika tu. Hivyo kuna sababu za kwanini hakutaka na kwanini alikubali baadaye

Nyerere alikubali baadaye kwasababu aliona bila sauti yake upotoshaji ulikithiri.

Hoja kwamba aliingizwa siasa na wazee wa Dar es Salaam haina msingi na ni ya kupuuzwa.

Nyerere kabla ya kufika Dar es Salaam alikuwa katika siasa.
Nyerere alikwenda masomoni Scotland ambako alikutana na wanasiasa wa dunia.

Kwa ujio wake Dar es Salaam mambo mengi yalibadilika.

Nyerere aliandika au '' kunukuu'' katiba iliyoitwa ya TANU. Hakuna aliwahi fanya hivyo kabla

Nyerere akasambaza chama kwa nguvu sana nchi nzima, hakuamini siasa za Mzizima pekee
Mwalimu akaungwa mkono na Watanganyika na kupata 'uhalali' wa kwenda UNO.

Uwezo wa Mwalimu unathibitika ndani ya baraza la wazee wa TANU(rejea picha ya Mohamed Said). Mwl aliwakuta na harakati, akafanya nao kazi asilimia 98 ikiwa ni Waislam.

Nyerere akawaongoza kufikia Uhuru wa nchi. Huyu anafundisha au anafundishwa?

Hii haina maana Mwalimu alikuja na harakati, la hasha, vyama vilikuwepo.

Kilichomsaidia Nyerere ni elimu na kuwa na ufahamu wa dunia na siasa za dunia.
Hiyo ndiyo siri ya kupokelewa kisha kuwaongoza! na si kuingizwa !

Ngongo Kiranga
 
Kwa watu wanaomfahamu Nyerere ni nadra na tabu kupata kauli yake akisema '' mimi au Nime''. Nyerere hakupenda kutajwa kama yeye bali alitumia sana wingi '' Sisi, tuli.. n.k'

Akiwaaga Wazee wa Dar es Salaam pale Diamond kwa nadra nilimsikia akisema '' Nilikuwa Mkristo peke yangu''. Katika siku nadra sana hiyo ilikuwa moja akitumia neno ''Nili..''

Tatizo la kuandika kitabu chake ni kwa kutambua alishirikiana na watu wengine na ni ngumu sana kuandika 'Memoir' yake . Nyerere hakujifaragua wala kujikweza

Nyerere alifahamu kuandika 'Mmemoir' angegusa mambo mengi kama ugomvi wake na akina Abdul Sykes, Bibi Titi, Rais Karume, ujamaa, kutaifisha mali, Bakwata, Mali za Kanisa n.k. na pengine angeligawa Taifa zaidi kwa kitu kidogo cha kuepukika.

Nimesoma kitabu cha AH Mwinyi na BW Mkapa. Ukweli wamekwepa vitu vingi vya msingi.
Hiyo yote ililenga kutoleta mjadala wa kuligawa Taifa. Mkapa hakupenda alilazimika tu. Hivyo kuna sababu za kwanini hakutaka na kwanini alikubali baadaye

Nyerere alikubali baadaye kwasababu aliona bila sauti yake upotoshaji ulikithiri.

Hoja kwamba aliingizwa siasa na wazee wa Dar es Salaam haina msingi na ni ya kupuuzwa.

Nyerere kabla ya kufika Dar es Salaam alikuwa katika siasa.
Nyerere alikwenda masomoni Scotland ambako alikutana na wanasiasa wa dunia.

Kwa ujio wake Dar es Salaam mambo mengi yalibadilika.

Nyerere aliandika au '' kunukuu'' katiba iliyoitwa ya TANU. Hakuna aliwahi fanya hivyo kabla

Nyerere akasambaza chama kwa nguvu sana nchi nzima, hakuamini siasa za Mzizima pekee
Mwalimu akaungwa mkono na Watanganyika na kupata 'uhalali' wa kwenda UNO.

Uwezo wa Mwalimu unathibitika ndani ya baraza la wazee wa TANU(rejea picha ya Mohamed Said). Mwl aliwakuta na harakati, akafanya nao kazi asilimia 98 ikiwa ni Waislam.

Nyerere akawaongoza kufikia Uhuru wa nchi. Huyu anafundisha au anafundishwa?

Hii haina maana Mwalimu alikuja na harakati, la hasha, vyama vilikuwepo.

Kilichomsaidia Nyerere ni elimu na kuwa na ufahamu wa dunia na siasa za dunia.
Hiyo ndiyo siri ya kupokelewa kisha kuwaongoza! na si kuingizwa !

Ngongo Kiranga
Hilo alishajibiwa mwengine...


Dudu kaandika hayo hapo chini na mimi nimeona nifungue uzi mpya niweke maelezo katika hayo maneno yake ili kusahihisha makosa ya historia ya TANU ambayo yamekuwa yakijirudia sasa nusu karne:

MAKOSA YANAYOJIRUDIA KATIKA HISTORIA YA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE NA TANU

Dudus said:

''... watu wa pwani walikuwa na advantage ya Kiswahili kwa wakati huo kiliwabeba sana. Ningeletwa mimi mhadzabe na Kiswahili wapi na wapi! Inasemekana hata Nyerere wakati anafanya urafiki na wazee wa Kariakoo hadi wakamkabidhi TANU, Kiswahili kilikuwa kinampa shida to some extent; ila kimalkia ungedhani anaishi kwenye corridor za Buckingham.''

Jibu langu kwake hili hapo chini:

Dudus,
Mwalimu Nyerere hakupokelewa Dar es Salaam na mzee yeyote alipofika mwaka wa 1952.
Hii ni katika moja ya makosa yaliyomo katika historia ya TANU.

Nyerere mtu aliyekuwa anajuananae kwa karibu sana alipofika Dar es Salaam ni Joseph Kasella Bantu.

Kasella Bantu akiishi Temeke.

Ilikuwa wakati mwingine Mwalimu akija mjini basi atalala kwa Kasella Bantu siku ya pili atarejea Pugu.

Kasella Bantu ndiye aliyempeleka Nyerere kwa Abdul Sykes.
Abdul Sykes alikuwa ndiye Secretary na Act. President wa TAA.

Hicho chama cha TAA kimetokana na African Association chama ambacho baba yake Abdul, Kleist Sykes alikuwa katibu muasisi mwaka wa 1929.

Hakuna mzee yeyote aliyempokea Nyerere alipofika Dar es Salaam kutafuta viongozi wa TAA wala hakuna mzee yeyote aliyemkabidhi Mwalimu chama cha TANU.

Wala Mwalimu hakupata kujulikana hadi pale alipokuja kusuhubiana na Abdul Sykes katika siasa za TAA kuelekea kuundwa kwa TANU.

Hii ilikuwa kati ya mwaka wa 1952 - 1954.

Katika historia ya TANU kutokea TAA wazee waliokuwa ndani ya uongozi wa TAA na wao kushiriki katika kuweka msingi wa kuunda TANU walikuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir na Sheikh Said Chaurembo aliyekuwa Liwali Mahakama ya Kariakoo.

Hawa walikuwa wajumbe katika TAA Political Subcommittee ilyoundwa mwaka wa 1950.

Wajumbe wa TAA Political Subcommttee walikuwa Dr. Vedast Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Sheik Hassan bin Ameir, John Rupia na Sheikh Said Chaurembo.

Wala si sawa kusema kuwa Nyerere aliunda TANU.

Historia ya TANU inaanza mbali sana kwa karibu ni mwaka wa 1945 Abdul Sykes, Ally Sykes na askari wenzao katika 6th Batallion KAR Burma Infantry wakiwa Kalieni Camp Bombay hapo ndipo katika mkesha wa Christmas, 1945 walipoamua kuunda TANU kudai uhuru wa Tanganyika na jina hili lilitolewa huko.

Hapo Kalieni Camp askari Waafrika kutoka Afrika ya Mashariki walikuwa wanasubiri kurudishwa makwao baada ya Vita Vya Pili Vya Dunia (1938 - 1945).

Urafiki wa Nyerere na wazee wa Dar es Salaam ulianza baada ya TANU kuundwa 1954 na mzee aliyekuwa karibu sana na Mwalimu alikuwa Mzee Mshume Kiyate mwaka wa 1955.

Ukipenda unaweza ukawaongeza na wengine kama Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Jumbe Tambaza, Mwinjuma Mwinyikambi na Max Mbwana.

Historia hii nimeiandika kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes (1998).

Kulia ni Mzee Mshume Kiyate, Julius Nyerere, Mzee Max Mbwana na Mzee Mwinjuma Mwinyikambi.

Inasikitisha kuwa baada ya uhuru miaka 60 hadi leo hatuijui historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kamabarage Nyerere wala historia ya TANU.

Kulia ni Mzee Mshume Kiyate, Julius Nyerere, Mzee Max Mbwana na Mzee Mwinjuma Mwinyikambi Uchaguzi wa 1962.
 
Kwa watu wanaomfahamu Nyerere ni nadra na tabu kupata kauli yake akisema '' mimi au Nime''. Nyerere hakupenda kutajwa kama yeye bali alitumia sana wingi '' Sisi, tuli.. n.k'

Akiwaaga Wazee wa Dar es Salaam pale Diamond kwa nadra nilimsikia akisema '' Nilikuwa Mkristo peke yangu''. Katika siku nadra sana hiyo ilikuwa moja akitumia neno ''Nili..''

Tatizo la kuandika kitabu chake ni kwa kutambua alishirikiana na watu wengine na ni ngumu sana kuandika 'Memoir' yake . Nyerere hakujifaragua wala kujikweza

Nyerere alifahamu kuandika 'Mmemoir' angegusa mambo mengi kama ugomvi wake na akina Abdul Sykes, Bibi Titi, Rais Karume, ujamaa, kutaifisha mali, Bakwata, Mali za Kanisa n.k. na pengine angeligawa Taifa zaidi kwa kitu kidogo cha kuepukika.

Nimesoma kitabu cha AH Mwinyi na BW Mkapa. Ukweli wamekwepa vitu vingi vya msingi.
Hiyo yote ililenga kutoleta mjadala wa kuligawa Taifa. Mkapa hakupenda alilazimika tu. Hivyo kuna sababu za kwanini hakutaka na kwanini alikubali baadaye

Nyerere alikubali baadaye kwasababu aliona bila sauti yake upotoshaji ulikithiri.

Hoja kwamba aliingizwa siasa na wazee wa Dar es Salaam haina msingi na ni ya kupuuzwa.

Nyerere kabla ya kufika Dar es Salaam alikuwa katika siasa.
Nyerere alikwenda masomoni Scotland ambako alikutana na wanasiasa wa dunia.

Kwa ujio wake Dar es Salaam mambo mengi yalibadilika.

Nyerere aliandika au '' kunukuu'' katiba iliyoitwa ya TANU. Hakuna aliwahi fanya hivyo kabla

Nyerere akasambaza chama kwa nguvu sana nchi nzima, hakuamini siasa za Mzizima pekee
Mwalimu akaungwa mkono na Watanganyika na kupata 'uhalali' wa kwenda UNO.

Uwezo wa Mwalimu unathibitika ndani ya baraza la wazee wa TANU(rejea picha ya Mohamed Said). Mwl aliwakuta na harakati, akafanya nao kazi asilimia 98 ikiwa ni Waislam.

Nyerere akawaongoza kufikia Uhuru wa nchi. Huyu anafundisha au anafundishwa?

Hii haina maana Mwalimu alikuja na harakati, la hasha, vyama vilikuwepo.

Kilichomsaidia Nyerere ni elimu na kuwa na ufahamu wa dunia na siasa za dunia.
Hiyo ndiyo siri ya kupokelewa kisha kuwaongoza! na si kuingizwa !

Ngongo Kiranga
Nguruvi3,
Mwalimu Nyerere hakupata kugombana na akina Sykes kwa maana ya ugomvi kama ule aliogombana na Sheikh Suleiman Takadir na Bi. Titi Mohamed ugomvi wa kutoleana maneno kwa hamaki.

Kilichotokea baina ya Nyerere na akina Sykes ni paliingia ''ubaridi'' baina yao na yale mapenzi na udugu uliokuwa baina yao taratibu ukaondoka na kupotea.

Pamoja na kupotea kwa mapenzi haya na historia ya akina Sykes katika kupigania uhuru wa Tanganyika ikafutika.

Inawezekana pia hali hii ya ''ubaridi'' ilizidishwa na Ally Sykes kumkatalia Mwalimu kumpa Nyaraka za TAA na TANU ambazo aliziomba kwake baada ya kifo cha Abdul Sykes.

Ally Sykes alidai kuwa hizo ingawa ni nyaraka za TANU lakini ni nyaraka zao na wasingeweza kuzitoa na kuzikabidhi kwa mtu yeyote yule.

Ingawa unasema kuwa Mwalimu alichelea kuandika kumbukumbu zake kwa kuogopa ''kuligawa'' taifa, tayari alikuwa keshaligawa kwa kuzuia Waislam wasiendelee na juhudi za kujikwamua katika elimu kupitia EAMWS.

Nyerere akaivunja EAMWS ili Chuo Kikuu Cha Waislam kisijengwe na kumfukuza Sheikh Hassan bin Ameir Tanganyika.

Haya yote ambayo Nyerere hakutaka yafahamike kwa kuhofia mgawanyiko leo hii yanafahamika.

Yote yamo ktika kitabu cha Abdul Sykes.

Hili la katiba wewe unalieleza unavyojua na mimi nimelieleza kwa ushahidi wa Nyaraka za Sykes kuwa Earle Seaton kama mshaurii wa TAA Political Subcommitee alishauri kuwa itumike katiba ya CPP.

Hii ni 1950 na Nyerere alikuwa bado hajafika Dar es Salaam.

Huyu Seaton ndiye aliyemwambia Abdul kuwa njia bora ya kupambana na Waingereza ni kwa wao kufungua mazungumzo na UNO.

Yapo mengi katika kipindi hiki ambayo kwa kuwa Nyerere hakuwako huenda hakuyajua au aliyajua akaamua asiyaseme.

Mfano wa jina lake kuwa kiongozi wa TAA alilolipendekeza alikuwa Hamza Mwapachu.

Abdul Sykes yeye alikuwa keshaanza mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia aingie TAA wamchague rais kisha waunde TANU na Chief Kidaha aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Hili la ''wazee'' hata mimi nakuunga mkono ingawa yeye mwenyewe Nyerere anasema alipokewa na wazee.

Nyerere hakupokewa na mzee yeyote alipokewa na Abdul Sykes.

Bahati mbaya sana yeye mwenyewe hakupata kulisema hili na lililokuwa jepesi ulimini kwake kulitamka ni hili la wazee ambao hata majina yao hakuyataja.

Kuwa Nyerere alisambaza chama inataka maelezo kwani TANU iliundwa kutokana na TAA katika majimbo na waasisi hao wa TANU huko majimboni walikuwa hata sura ya Nyerere hawaijui ikoje.

Mifano iko mingi tu katika historia ya wazalendo kama Salum Mpunga, Yusuf Chembera, Msham Awadh, Abdallah Rashid Sembe wengi wengi waliounda TANU mikoani na Nyerere akafika huko kakikuta chama na wanachama wengi.

Hiyo picha hapo chini ilipigwa Iringa 1956 na ndiyo kwa mara ya kwanza Nyerere anafika huko na hao waliokuja kumpokea ni wanachama wa TANU wakiongozwa na Abbas Max na wengi wao walikuwa hawajapata kumuona.

Abbas Max alimshawishi Abdul Sykes akiwa mgeni wake hapo Iringa kuwa akirejea Dar es Salaam amshawishi Nyerere kuja Iringa.

1648271783567.png
 
Nilijua tangu mwanzo ulikuwa unazunguka tu lakini nia yako ipo katika sentensi ya mwisho.

Mwl Nyerere kamwe hawezi kuhofia Mambo madogo madogo,Huyu ni jabali wa siasa za Afrika hawezi kuhofia wenyeji wa Tandamti na Msikiti wa Manyema.
ULIWAHI kukaa nae meza moja...? au umehadithiwa...?
 
Mzee wetu Mohamed Said anapambania kombe la wazee wake akina Sykes wakae level moja na Mwalimu kwa historia ya Tanganyika, as if hajui katika kila hadithi kuna wahusika wanaishiaga mwanzoni tu mwa hadithi na wengine katikati na wengine hutokea tu mwishoni mwa hadithi mpaka dhumuni la wahusika wote hawa ni kumsapot muhusika mkuu.
Najua kabisa huyu mzee Mohamed ni gwiji mbobezi katika historia na masuala ya uandishi ila anakomaa kwelikweli supportive characters wammeze main character kisa tu waliwahi kumpa chakula akiwa karibu na kifo kwa njaa sababu wao ndio walimuokoa bas wao ni wakuu kuliko yeye
Mwalimu ni mkubwa zaid ya historia ya Tanganyika ukuu wake umeenda mbali zaid Afrika mpaka huko kwenye mabaraza ya umoja wa mataifa
Najua hua mnalishana sana sumu kwamba yule babu alikua mdini ila hamsami kua mwalimu alikataa kuutambua utawala wa Israel pale mashariki ya kati alisimama na Palestine mpaka anarejea kwa mola wake hili hamliongelei
 
Mzee wetu Mohamed Said anapambania kombe la wazee wake akina Sykes wakae level moja na Mwalimu kwa historia ya Tanganyika, as if hajui katika kila hadithi kuna wahusika wanaishiaga mwanzoni tu mwa hadithi na wengine katikati na wengine hutokea tu mwishoni mwa hadithi mpaka dhumuni la wahusika wote hawa ni kumsapot muhusika mkuu.
Najua kabisa huyu mzee Mohamed ni gwiji mbobezi katika historia na masuala ya uandishi ila anakomaa kwelikweli supportive characters wammeze main character kisa tu waliwahi kumpa chakula akiwa karibu na kifo kwa njaa sababu wao ndio walimuokoa bas wao ni wakuu kuliko yeye
Mwalimu ni mkubwa zaid ya historia ya Tanganyika ukuu wake umeenda mbali zaid Afrika mpaka huko kwenye mabaraza ya umoja wa mataifa
Najua hua mnalishana sana sumu kwamba yule babu alikua mdini ila hamsami kua mwalimu alikataa kuutambua utawala wa Israel pale mashariki ya kati alisimama na Palestine mpaka anarejea kwa mola wake hili hamliongelei
Ujoka,
Umeandika na kutoa fikra zako vipi unionavyo lakini sikupendezewa na namna unavyojieleza.

Umetia ujuvi.
Bahati mbaya pia kuna uliyosema si sawa umepotosha.

Na hili ni tatizo kubwa ninaloliona hapa kwa wengi wanapoingia katika mjadala na mimi.
Mathalan kusema kuwa najaribu kumleta Abdul Sykes katika ''level moja na Mwalimu.''

Ingekuwa nimekiandika kitabu cha Abdul Sykes kwa nia hiyo kitabu hiki kingekuwa kimekufa miaka mingi kwani kingekuwa kitabu cha kipuuzi na wasomaji wangekipuuza.

Unazungumza kuhusu ''chakula,'' nasikitika iweje utufikirie hivyo kuwa kwetu kumpa mtu chakula liwe jambo kubwa.

Ni kweli kuna hisani kubwa baina ya Mwalimu na wazee wetu.

Haya yanatosha kujibu hayo mengine uliyosema ambayo nimeona niyakalie kimya kwani hakuna tija kuyarejea hapa.

Mimi nimeandika kitabu: ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,'' (1998) nia yangu ikiwa kueleza historia ya kuundwa kwa TANU kupitia maisha ya Abdul Sykes.

Hii mosi.

Pili ni kueleza historia ambayo ilikuwa haifahamiki kuhusu mchango wa Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kitabu kilibadili historia nzima ya uhuru wa Tanganyika na historia ya Nyerere kama ilivyoandikwa na waandishi wengine waliokuwa wamenitangulia.

Kitabu kimependwa sana na sasa tunakimbilia kwenda toleo la tano.
Hakika kama ulivyosema Mwalimu ni mkubwa sana hakuna anaeweza kukataa ukweli huu.

Lakini Mwalimu kwenye kuasisi chama cha TANU na kupigania uhuru historia yake haikuelezwa kwa ukweli.

Hili ndilo lililonifanya mimi kuandika kitabu.
Sikuandika kitabu ili nimdogoshe Baba wa Taifa.

Umeleta suala la udini wa Nyerere.
Sijui unadhani nini kitapatikana ikiwa tutajadali suala hili hapa?

1648304656732.png
 
Kwako mzee Mohamed Said naomba kujua:Kwanini uhusiano wa Nyerere na kina Sykes uliingia ubaridi?

Abdul Sykes alikuwa mwanachama maarufu wa TANU na mtu mwenye elimu kiasi kwanini hakupewa nafasi ya uongozi katika serikali mpya ya Tanganyika?
 
Back
Top Bottom