Kwanini Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake?

Yoda,
Kuna mambo yakimhangaisha sana Mwalimu.
Moja ambalo likimpa shida ilikuwa uasisi wa TANU.

Taji la kuanzisha vuguvugu hadi kupelekea kuundwa kwa TANU nani avishwe?

Hii ndiyo sababu kubwa hata ilipoandikwa historia ya TANU na Chuo Cha CCM Kivukoni Abdul Sykes jina lake halipo.

Tukaishi miaka yote na historia ya TANU bila ya Abdul Sykes mwenye kadi ya TANU No. 3 na mdogo wake kadi No. 2.

Kadi No. 1 ya Territorial President Julius Kambarage Nyerere na aliandikiwa na Ally Sykes.
Ikawa historia hii haipo.
 
Tunakubaliana walikuwepo wengi saaana ...ila Nyerere aliwazidi akili,hekima,busara ,Elimu ...wao (baba zako)walimzidi mali pekee!
Kama ambavyo Waarabu na Fedha zao wanaburuzwa na wazungu!
 
Tunakubaliana walikuwepo wengi saaana ...ila Nyerere aliwazidi akili,hekima,busara ,Elimu ...wao (baba zako)walimzidi mali pekee!
Kama ambavyo Waarabu na Fedha zao wanaburuzwa na wazungu!
Makulanga,
Mimi siko hapa kufanya ubishani na wewe kwani ubishi hauna tija yoyote.
Kawaida yangu mimi hueleza kile ambacho nakijua.

Una khiyari ya kuamini au vinginevyo.

Uwezo wa Nyerere hakuna ambae anaweza kuukataa mara nyingi nimesema kuwa kama kuandika kitabu changu nia ingelikuwa ni kumdogosha Mwalimu kitabu kingekufa miaka mingi sana iliyopita kama kilivyokufa kitabu cha 'Historia ya TANU'' (1981) kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni.

Azma na nia yangu mimi kuandika kitabu cha historia ya TANU ilikuwa kueleza historia ya kweli ya harakati za kudai uhuru.

Hili nimefanikiwa kufanya.
Kitabu kipo sokoni huu mwaka wa 24 na matoleo yaliyochapwa ni manne ''...and counting...''
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…