Kwanini Biblia ilituficha kuhusu uzao wa majitu/Wanefili?

Kwanini Biblia ilituficha kuhusu uzao wa majitu/Wanefili?

Goliathi hakuwa mmoja wa wanefili ila ni kweli alikuwa mtu mwenye kimo kirefu na nguvu kuzidi wanadamu wengi. Vivyo hivyo kwa wana Anaki walikuwa ni binadamu wenye nguvu ambao baadaye Yoshua alikuja kuteketeza kizazi Chao.

Wanefili ilikuwa ngumu kushindwa kwa nguvu za kawaida za kibidamu. Uhalifu ulizidi ndio maana Mungu akaingilia kati. Watu warefu na majitu yenye nguvu hata leo wapo ila sio wanefili
Pia soma torati 3 10;11 miji yote ya nchi tambarare, na Gileadi yote, na Bashani yote, mpaka Saleka na Edrei, nayo ni miji ya ufalme wa Ogu katika Bashani. 11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho kingali kiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni dhiraa tisa, na upana wake dhiraa nane, kwa mfano wa mkono wa mtu).

Nahitimisha kukwambia hawa jamaa walikuwepo hata Goliath vitabu vingin vimemuandika ni mabaki ya hao wanefili
 
Pia soma torati 3 10;11 miji yote ya nchi tambarare, na Gileadi yote, na Bashani yote, mpaka Saleka na Edrei, nayo ni miji ya ufalme wa Ogu katika Bashani. 11 (Kwani aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho kingali kiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni dhiraa tisa, na upana wake dhiraa nane, kwa mfano wa mkono wa mtu).

Nahitimisha kukwambia hawa jamaa walikuwepo hata Goliath vitabu vingin vimemuandika ni mabaki ya hao wanefili
Sawa hitimisha
 
MARKO naye angeandika INJILI yake historia ya maisha ya Yesu kuanzia alipofikisha umri wa miaka 12 mpaka 29 kwamba (Yesu) alikuwa anaishi wapi,
Kwenye agano jpya huwa nahisi kuna uchakachuaji mkubwa sana wa maandiko .Kuna muda unasoma kisa fln mara ghafla bin vuu hicho kisa kinaisha chap bila hitimisho na kuibuka kwa habari nyingine tofauti kabisa.
Mitume na Manabii wote walioandikwa ktk kitabu cha AGANO LA KALE wametajwa kwa uwazi majina ya wazazi wao wote mpaka ndugu zao... Lakini ukisoma kitabu cha AGANO JIPYA ni vigumu sana kukuta majina ya wazazi wa mama yake Yesu na vigumu sana kukuta majina halisi ya ndugu zake Yesu.
Agano la kale ni kweli lina eleweka na ndio maana walokole huwa hawapendi kulitumia na kujifichia kwenye injiri maana injili haijafafanua wazi mambo kama ulivyosema, .......

Neno BIBLIA lina maana ya mkusanyiko wa vitabu na ndani ya mkusanyiko huo kuna maandiko ya AGANO LA KALE na maandiko ya AGANO JIPYA.... Maandiko ya AGANO LA KALE ni mengi sana yamepangiliwa vyema na ni rahisi sana kueleweka kuliko maandiko machache ya AGANO JIPYA... Ndio maana Wasabato na Waislamu wengi wanayakubali sana maandiko ya AGANO LA KALE kuliko maandiko ya AGANO JIPYA.🙏

Ukisoma kitabu cha AGANO LA KALE kuanzia MWANZO hadi MALAKI unaweza kuwafahamu vyema wahusika wote na hata koo zao.👉 Lakini ukisoma kitabu cha AGANO JIPYA utaona waandishi wamelipua au wameunga unga vipande vya maandishi wala huwezi kukuta kurasa walau 4 zinaelezea kitu kimoja. Stori hazijitoshelezi

Kuanzia MATHAYO mpaka UFUNUO... Utakutana na stori au hadithi zilezile chache zinazofanana harafu utakuta mwandishi ktk AGANO JiPYA, anasema eti "Kuna mambo mengi aliyofanya Yesu, ambayo yakiandikwa mojamoja nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa" YOHANA 21:25.

Je, hii ilikuwa ni kweli? Waandishi walijisahau au waandishi waliamua tu kufanya makusudi Kwa lengo Yesu asiweze kusomeka kwa mambo mengi ambayo mengineyo (huenda) yangedhoofisha 'Utakatifu' 'Unabii' 'Uana wa Mungu' au 'Uungu wake?' Maana haiwezekani waandishi kama MATHAYO, MARKO, LUKA na YOHANA... Wakajikuta wote kwa pamoja wanaandika jambo lilelile kumhusu Yesu, bila ya kusimulia story tofauti wakati kila mmoja aliandika INJILI kwa wakati wake.

Kwamfano... MATHAYO angeandika INJILI yake kwa ufasaha kabisa kuhusu uzao wote wa Yesu uzao wa wazazi wake pamoja na ndugu zake wote. Kisha MARKO naye angeandika INJILI yake historia ya maisha ya Yesu kuanzia alipofikisha umri wa miaka 12 mpaka 29 kwamba (Yesu) alikuwa anaishi wapi, alikuwa anapendelea kufanya nini na nini na alipofikisha umri wa kufanya kazi alifanya kazi gani?

LUKA na YOHANA pamoja nyaraka kadhaa za akina Mtume PAULO... Wenyewe wangeandika kama hivi walivyoandika kazi za Yesu alipoanza kuhubiri INJILI akiwa na umri wa miaka 30... Naamini vitabu vingetosha kabisa na sisi wasomaji tusingechoka kuvisoma na wala tusingefikia hatua ya kutofautiana hata kuzalisha madhehebu mbalimbali ya kidini.

Angalia jinsi waandishi wote wa AGANO JiPYA walivyoacha kuandika Siku, Tarehe, Mwezi na hata Mwaka aliozaliwa Yesu... Watu wengine baadae walipokuja kusema kuwa "Yesu amezaliwa Desemba 25" Ndipo Wasabato na Waislamu walipoamua kupingana ktk hilo... Na sio ktk hilo tu...Hata kwenye masuala ya ulaji wa nyama ya Nguruwe, siku maalum ya kuabudu Mungu, Kufunga mwezi mtukufu, Sikukuu ya Pasaka na hata kuoa, kuolewa na Talaka... AGANO JIPYA halifafanui kwa uwazi kama ilivyo AGANO LA KALE.

Mitume na Manabii wote walioandikwa ktk kitabu cha AGANO LA KALE wametajwa kwa uwazi majina ya wazazi wao wote mpaka ndugu zao... Lakini ukisoma kitabu cha AGANO JIPYA ni vigumu sana kukuta majina ya wazazi wa mama yake Yesu na vigumu sana kukuta majina halisi ya ndugu zake Yesu. Ingawa inasemekana Yesu alikuwa na mama zake wadogo, Shangazj zake, Wajomba zake, Kaka na Dada zake...

Pia alikuwa na Babu pamoja na Bibi zake ambao wanatajwa kuwa ni (Anna na Yoakimu), lakini ndani ya AGANO JiPYA hawakuwekwa wazi.

Vilevile si rahisi kukuta ktk AGANO JIPYA imeandikwa kazi alizofanya Yesu (kabla hajaanza kuhubiri), si rahisi kukuta imeandikwa kama Yesu alikuwa na mke au mpenzi au alikuwa hana kabisa AGANO JIPYA limekwepa kabisa kuandika yote hayo, ingawa inatambua wazi Yesu alikuwa ni mwanadamu mkamilifu kama walivyo wanadamu wengine... Alikuwa Analala, Anakula na Kunywa, Alikuwa anavaa Nguo. Alikuwa anajisaidia haja ndogo na kubwa... Alikuwa anachukia na kufurahi... Alikuwa anachoka, Alibatizwa, Alitahiriwa, Alikuwa anasali na kuomba Dua na pia alikuwa na matamanio kama walivyo wanadamu wengine (maana alitamani hata kula matunda ktk mti fulani) na alipokuta matunda hakuna Yesu alichukia.

Kama ukisoma kwa kuunga unga maandiko ndani ya AGANO JIPYA, utagundua kuwa akina YUDA walikuwa wawili na mmoja ni ndugu yake Yesu. Akina Mariamu walikuwa watatu ambapo mmoja ni mama yake mzazi, wa pili mama yake mdogo na wa tatu ni Mariamu Magdalena (ambaye amezua gumzo sana ulimwenguni). Pia utagundua Simeoni Petro, Andrea, Yakobo, Yohana, Yuda, Yosefu au Yusufu, Salome na Yohana walikuwa ni ndugu wa mama mmoja (Mariamu mama yake mdogo Yesu) lakini baba tofauti. Lakini Yohana Zakaria alikuwa ni kaka wa Yesu (mtoto wa mama yake mkubwa Elizabeth).

Unga unga maandiko haya ili kuwajua ndugu wa Yesu: MATAYO 13:55 👉 MARKO 6:3 👉 LUKA 6:13:16 👉 MARKO 15:40 👉 LUKA 24:10 👉 MARKO 1:29 👉 YOHANA 19:25 👉 MATENDO 12:12:17 👉 MATENDO 12:2 na YUDA 1:1. Petro na Andrea baba yao ni Yohana. Yakobo na Yohana baba yao ni Zebedayo.

Bado kuna hili la mafumbo! Katika AGANO JIPYA kuna maandiko mengi yenye muundo wa Mifano, Methali na Mafumbo... Ambayo ni vigumu kwa watu wengi kuelewa wakati kitabu chenyewe kimatafsiriwa katika llugha zote za ulimwengu... Mfano ni INJILI ya YOHANA INJILI hii ndio imehusika zaidi kumficha mwanafunzi aliyependwa na Yesu bila ya kumtaja jina mpaka mwisho. Je, lengo hapa lilikuwa nini?

AGANO JIPYA haikuandika wazi kusema kama Yusufu na Mariamu (baada ya posa) walioana? Waliendelea kuishi pamoja hadi kifo kilipowatengenisha? Walizaa watoto wengine tofauti na Yesu? Je, walikufa wakiwa na umri wa miaka mingapi? Walizikwa wapi?

AGANO LA KALE wamezingatia kuandika yote haya... Lakini AGANO JIPYA limepuuzia Ndio maana watu wengi wanajikuta wakisema: "INJILI ni ngumu sana kuielewa mpaka uvuviwe na Roho Mtakatifu" MATENDO 19:13: 20 na MATENDO 8:9:25 🙏

Je, waandishi wa AGANO JiPYA walijisahau au waliamua tu kufanya makusudi kutoandika kweli yote?
Hatuwezi badilisha kitu mkuu mambo mengi tumeyakuta hivyo ni wewe na mimi kung'amua kipi cha kuondoka nacho. Mimi sio mjinga unambie kuwa kuna mambo mengi yesu alifanya ambayo yasiandikwa yote yakaisha huu ni UONGO WA KIJINGA SANA.K wanini Musa kaandika kisa chote cha wana wa israeli kwa mpangilio mzuri kabisa na hata alipokufa joshua akaendeleza alipoishia Musa kwa uzuri kabisa.

Ukumbe story ya wana wa israeli imechukua miaka 400 na zaidi na ya yesu hata miaka35 haifiki na haieleweki janja janja nyingi.Kulikuwa na ulazima gani wakuliacha gape la miaka kuanzia akiwa na miaka13-29 ? Siamini kama waandishi wote hawa hawakuandika bali wahuni walitoa na kufanya yao!!!
 
Naweka wazi kuhusu hili Kwa mtumishi mmoja anaitwa Musa meizon wa mbezi alifafanua vizuri ndy hapo utajua Kuna giant na watu warefu.

Egypt pia wanahistory kuhusu watu hao Wana nguvu sana yani kama wange unda jeshi lao kizazi Cha binadamu wa kawaida kingekuwa na wakati mgumu kidg.
View attachment 3224795
Nikifa MkeWangu Asiolewe
Apuuzwe anajichanganya sana. Huyo akiulizwa maswali magumu anakimbia kipindi
 
Achaneni na Biblia za kiswahili, someni za Kiingereza… lugha ya kiswahili ngumu haswa kwa nyie vijana wa dotcom

Plus waliotafsiri sijui walikua wanatumia misamiati ya kwenye kamusi gani maana sehemu pakuandikwa ndege utaona wameandika shoro.. sasa unabaki unajiuliza lengo lao haswa lilikua ni kutufundisha misamiati au neno la Mungu, yaan ni masumbuko!!
 
Kwa ufahamu wangu kuna history ya miaka maefu na maefu haijulikana kutokana na kutokuwepo na technology ya uandishi na utunzaji habari habari nyingi za kale zilikuwa zinatunzwa kwa masimulizi ya kizazi adi kizazi
Na kuna vizazi vilivyotoweka na kumbukumbu nyingi
Kitabu cha mwazo kinataja ni kitabu cha musa ,musa alikulia msri na kusoma chini ya taratibu za kimsri habari za musa mi miaka mia nne na thelasini baada ya israeli baba wa taifa kuhamia misri
Mtiliko wa biblia ulitumia uzao wa Israeli yani yakobo
Kwa hiyo habari zote nyingi zinatokama na jamiii ya yakobo na hii ni ya juzi kulinganisha na kule dunia ilipotoka
Huko nyuma kuna mambo mengi mno yasiyoelezeka ya binadamu wa kwanza na hali ya technology iliyokuwepo
Ikiwa mika ya 1961 hapa tanzania tunaona wanamama matiti i yalikuwa wazi yani hakukuwa na kuvaq nguo je miaka 5000 iliyopita dunia ilikuwa katika hali gani watu wali walikuwa wa namna gani walikuwa majitu hasa
Katika hali ya kisayasi inaonyeaha mazingira uchangia umbo la mwanadamu na sio tu binadamu walikuwa wakubwa hata wanyama pia
Je walitoka wapi? Jibu ni waliubwa katika mazigirq yao
Je walitokana na malaika kujamiana ma wanadamu nadhalia hii inatokana na adiko la mwanzo

Mwanzo 6:1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo 6:2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

Mwanzo 6:4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.
Katika mistari hii inaonyesha manefili kama ndio wanadamu na kizazi cha adamu kama wana wa Mungu kwa hiyo hapa sio malaika
kwani malaika hawakuubwa kuzaliana

Naweza kusema ni viumbe wa kale walioubwa ikiwa pamoja na wanyama wakubwa sana na dunia ile iliangamizwa na kufanya dunia mpya na watu wapya pya wa namna ya leo maana dunia ya kwanza iliangamizwa

2 Petro 3:5 Maana hufumba macho yao wasione neno hili ya kuwa zilikuwako mbingu tangu zamani, na nchi pia, imefanyizwa kutoka katika maji, na ndani ya maji, kwa neno la Mungu;
2 Petro 3:6 kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.
Kwa hiyo wanefili wanotajwa kama mabaki ni mabaki ya watu waliokuwa hasa katokq mji wa kaanani ambapo wana wa Israeli kwa size walijiona kama mapazi

Hesabu 13:2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao. Send thou men, that they may search the land of Canaan, which I give unto the children of Israel: of every tribe of their fathers shall ye send a man, every one a ruler among them.
Hesabu 13:33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi
Ingawa kuna vitabu vingine kama cha enock ambacho kina Habari za kale zaidi kimefichwa na vingine vingi sana
Mambo ni mengi mda ni mchache sana kifupi nyuma yetu kulikuwa kulefu mno kuliko adamu adi leo
 
Achaneni na Biblia za kiswahili, someni za Kiingereza… lugha ya kiswahili ngumu haswa kwa nyie vijana wa dotcom

Plus waliotafsiri sijui walikua wanatumia misamiati ya kwenye kamusi gani maana sehemu pakuandikwa ndege utaona wameandika shoro.. sasa unabaki unajiuliza lengo lao haswa lilikua ni kutufundisha misamiati au neno la Mungu, yaan ni masumbuko!!
Sawa mkuu lakini tusaidie sasa hiyo ya kiingereza hao Giant wametokana na uzao wa nani?
 
Kwa ufahamu wangu kuna history ya miaka maefu na maefu haijulikana kutokana na kutokuwepo na technology ya uandishi na utunzaji habari habari nyingi za kale zilikuwa zinatunzwa kwa masimulizi ya kizazi adi kizazi
Na kuna vizazi vilivyotoweka na kumbukumbu nyingi
Kitabu cha mwazo kinataja ni kitabu cha musa ,musa alikulia msri na kusoma chini ya taratibu za kimsri habari za musa mi miaka mia nne na thelasini baada ya israeli baba wa taifa kuhamia misri
Mtiliko wa biblia ulitumia uzao wa Israeli yani yakobo
Kwa hiyo habari zote nyingi zinatokama na jamiii ya yakobo na hii ni ya juzi kulinganisha na kule dunia ilipotoka
Huko nyuma kuna mambo mengi mno yasiyoelezeka ya binadamu wa kwanza na hali ya technology iliyokuwepo
Ikiwa mika ya 1961 hapa tanzania tunaona wanamama matiti i yalikuwa wazi yani hakukuwa na kuvaq nguo je miaka 5000 iliyopita dunia ilikuwa katika hali gani watu wali walikuwa wa namna gani walikuwa majitu hasa
Katika hali ya kisayasi inaonyeaha mazingira uchangia umbo la mwanadamu na sio tu binadamu walikuwa wakubwa hata wanyama pia
Je walitoka wapi? Jibu ni waliubwa katika mazigirq yao
Je walitokana na malaika kujamiana ma wanadamu nadhalia hii inatokana na adiko la mwanzo

Mwanzo 6:1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
Mwanzo 6:2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

Mwanzo 6:4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa.
Katika mistari hii inaonyesha manefili kama ndio wanadamu na kizazi cha adamu kama wana wa Mungu kwa hiyo hapa sio malaika
kwani malaika hawakuubwa kuzaliana

Naweza kusema ni viumbe wa kale walioubwa ikiwa pamoja na wanyama wakubwa sana na dunia ile iliangamizwa na kufanya dunia mpya na watu wapya pya wa namna ya leo maana dunia ya kwanza iliangamizwa

2 Petro 3:5 Maana hufumba macho yao wasione neno hili ya kuwa zilikuwako mbingu tangu zamani, na nchi pia, imefanyizwa kutoka katika maji, na ndani ya maji, kwa neno la Mungu;
2 Petro 3:6 kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.
Kwa hiyo wanefili wanotajwa kama mabaki ni mabaki ya watu waliokuwa hasa katokq mji wa kaanani ambapo wana wa Israeli kwa size walijiona kama mapazi

Hesabu 13:2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao. Send thou men, that they may search the land of Canaan, which I give unto the children of Israel: of every tribe of their fathers shall ye send a man, every one a ruler among them.
Hesabu 13:33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi
Ingawa kuna vitabu vingine kama cha enock ambacho kina Habari za kale zaidi kimefichwa na vingine vingi sana
Mambo ni mengi mda ni mchache sana kifupi nyuma yetu kulikuwa kulefu mno kuliko adamu adi leo
Umegusia mambo ya msingi sana
 
Hao watu hawana mwili bali ni roho hivyo kuzaa na binadamu unahitaji kuwa na mwili. Hapo wamewezaje kuzaliana na binadamu ikiwa hawana miili?
Mkuu kwa uelewa wangu mdogo nafahamu ya kwamba mapepo/majini yanauwezo wa kujibadirisha na kuvaa umbo la binadamu yoyote.

Rejea kisa cha lutu hadi aliwapikia chakula wale malaika waliokuwa wanaenda kuiteketeza sodoma na gomora
 
1.Vitabu hivi vinavyoitwa vya Mungu vina taratibu za kusoma kwake....kuna baadhi ya maandiko unaweza usome na usielewe chochote bila ya msaada!
2.baadhi ya vitabu hivyo vimepunguzwa sana yale maandiko sababu ingekuwa ni mibuku isobebeka kwa sababu mengi mule ni maneno ya watu
3.kama nilivyosema hapo juu yataka msaada wa wasomi kuelewa matumizi ya LUGHA, NYAKATI NA MAHALI, unadhani iligharikishwa DUNIA nzima kwamaana ya GIMBA lote hili? Mungu anataratibu za kupeleka muonyaji mahala penye shida mkikataa anawaramba, pekua habari za lotu na wengineo...kumbuka zama hizo dunia haikuwa kijiji ilikuwa dunia dunia kweli...ukizaliwa msanga utafia msanga chanika tu kufika ni muhali..!
4.Malaika unamtambuaje kupitia hiko kitabu chako? Kumbuka walipopita kwa Ibrahim na kumpasha habari za uzao na kumwambia kule wanapoenda aliwatayarishia CHAKULA KINONO walikula? Kwa nini hawakula? Je Unadhani wanaweza kutomba na kutombwa?
4.chochote unachokiona ama unaaamini kipo kati ya waandamu basi asili ya yake ni umbo moja la Bwana Adamu na Manzi wake Hawa...na kilichotokea ni kutawanyika tu duniani na maumbo rangi na vimo NI KUTOKANA NA MAZINGIRA.....!
FUNGUKA...halafu we kwanza hayo MAJITU UNATATAKA YA NINI...Si umsome Yesu vile kaishi na wewe uishi japo robo yake vile aliishi mji wako usalimike🤪
ila we jamaa..... lakini bado sijakusoma hapo
 
2 Petro 2:4
Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu;
Huyo Mungu wenu kipindi anawaumba hao malaika waliokosa hakujua kama watakuja kukosa asiwaumbe ikiwa huwa mnatuaminisha ya kuwa yeye anayajua yajayo kabla ya kuyafikia?
 
Back
Top Bottom