Kwanini Blockchain Si ya Wenye Pesa Tu, Ni ya Kila Mtu!

Ndugu yangu tunaweza kuongea lugha moja naomba tuwasiliane kuna kitu kikubwa kinaenda kuzaliwa tukikutana mezani Blockchain Technology ni future kwa kizazi cha sasa na cha baadae...
 
Bado hujapata maarifa sahihi kwenye huu ulimwengu naomba tuwasiliane kama upo Dar tukutane nitakufundisha bure kabisa mpaka uelewe...
 
Hakika mimi nimekuwa miongoni mwa watu wanaofundisha watanzania Teknolojia kulingana na Project tuliyonayo nimekuwa nikisafiri kwenda mikoa mbalimbali hata jana nimetoka Arusha kwaajili ya swala hilo.

Bado kwa Tanzania tuko na safari ndefu sana kwenye swala la watu kujifunza na kupata uelewa.
Yaani mtu unamwambia kuwa unatakiwa uelewe mfumo unavyofanya kazi yeye anakuambia nikiweka mln 40 ninapata kiasi gani kila siku au kila wiki namwambia cha umuhimu ni kuelewa mfumo unakuhitaji ufanye nini ndipo uweze kujua pesa yako ukiwekeza ni kitu gani kinafanyika ili iweze kukuzalishia faida.

Watu wanaona ni kitu kigumu nilibahatika kufika mpaka Mererani wanapochimba Tanzanite aisee watu wako na pesa nyingi sana lakini wanaishia kurudi kwenye umasikini kwasababu bado wanaamini wakizirudisha huko aridhini watapata zaidi lakini wamebaki kuwa na historia ya alikuwa tajiri na vizazi vyake vimebaki kwenye dhiki kubwa.

Blockchain ni mkombozi wa Dunia kwa wale watakaoamua kuchukua hatua kujifunza kwa dhati na kuwekeza maarifa ndani yake hususani vijana wa Tanzania wakati wa kutegemea ajira tu limepitwa na wakati inafaa utafute namna ya kusimama kwa miguu yako kuziishi ndoto zako.
 
Nilishawahi jaribu kuyafuatilia nikaona haya mambo yapo , ila yanahitaji mitaji mikubwa ni uwekezaji tu ila kwa mtu wakawaida ni kama kubashiri tu .
Inafaa usome na kuelewa kuna vyanzo vingi vya taarifa ambavyo vinaweza kukupa uelewa kama sisi tunafundisha bure kabisa...
 
Fanya tuwasiliane mkuu tusaidiane kupata maarifa haya...
 
Ndugu Last_Joker kwani nyie watu wa hayo mambo huwa hamuwezi kupiga hela kimyakimya hadi mtake na watu wengine wapate hela? Ina maana nyie ni watu wema sana kiasi kwamba mnalazimisha kila mtu afanye hizo kazi zenu ili wawe matajiri?
 
Ndugu Last_Joker kwani nyie watu wa hayo mambo huwa hamuwezi kupiga hela kimyakimya hadi mtake na watu wengine wapate hela? Ina maana nyie ni watu wema sana kiasi kwamba mnalazimisha kila mtu afanye hizo kazi zenu ili wawe matajiri?
Swali zuri umeuliza ndugu, yawezekana wengi uliokutana nao hawakuwa wa kweli, hivyo imekufanya kuona hata anaefundisha hili ni mwizi/tapeli. Ila ukweli ni kwamba wengine tunfanya hivi ili wengi tuwe na uelewa wa hili jambo ni kama zilivyo fursa zingine zinavyofundishwa. Lakini ukiona hauko interested na hayo unaweza ukayapita kama unaaga maiti mkuu.
 
Hakuna mfanyabiashara makini atafundisha siri zake zote za biashara ili ajitengenezee washindani.... hiyo ni kuua biashara yake mwenyewe. Ulishaona Bakhresa akiwaita watu kuwafundisha kutengeneza juice? You are just a clique of thieves. Acheni upumbavu
 
Na hata kwenye blockchain hakuna anaefundisha siri zake. Ila atakufungulia njia mengine unapasuka nayo mwenyewe. Maana ingekuwa siri za huku kila mtu aoneshe basi lingekuwa ni jambo rahisi sana kuwahi kutokea
 
Na hata kwenye blockchain hakuna anaefundisha siri zake. Ila atakufungulia njia mengine unapasuka nayo mwenyewe. Maana ingekuwa siri za huku kila mtu aoneshe basi lingekuwa ni jambo rahisi sana kuwahi kutokea
Acha kulazimisha upuuzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…