Kwanini Blockchain Si ya Wenye Pesa Tu, Ni ya Kila Mtu!

Kwanini Blockchain Si ya Wenye Pesa Tu, Ni ya Kila Mtu!

Aisee, umetoa pointi kali! 😅 Ni kweli kuna hisia tofauti kuhusu blockchain, hasa kutokana na utapeli na miradi isiyoeleweka ambayo imeibuka na kutumia teknolojia hiyo vibaya. Ila, kiukweli blockchain ni teknolojia yenye uwezo mkubwa na sio kwa ajili ya watu wachache tu au matajiri.

Matajiri wengi duniani wamewekeza sana kwenye teknolojia hii kwa sababu ya uwezo wake wa kuboresha uwazi, usalama, na ufanisi wa miamala mbalimbali. Kwa mfano, blockchain inatumika kwenye sekta ya fedha, afya, usafirishaji, na hata serikali. Ni zana inayowezesha kuondoa wapatanishi na kuongeza uwazi kwenye miamala, kitu ambacho kinaweza kusaidia watu wa kawaida pia, si matajiri tu.

Lakini kama ilivyo kwa teknolojia yoyote, ni muhimu kuwa makini na kujua unachofanya ili kuepuka utapeli na skendo za aina hiyo. Ni sahihi kuwa na tahadhari, lakini pia ni vyema kuelewa thamani halisi ya teknolojia kabla ya kuipuuza kabisa. 🚀
Nzuri
 
Swali zuri umeuliza ndugu, yawezekana wengi uliokutana nao hawakuwa wa kweli, hivyo imekufanya kuona hata anaefundisha hili ni mwizi/tapeli. Ila ukweli ni kwamba wengine tunfanya hivi ili wengi tuwe na uelewa wa hili jambo ni kama zilivyo fursa zingine zinavyofundishwa. Lakini ukiona hauko interested na hayo unaweza ukayapita kama unaaga maiti mkuu.
Nikupongeze umetumia hekima kubwa sana katika kumhibu huyu ndugu.
Bado tunasafari ndefu sana katika kukomboa vizazi vyetu na umasikini, Vizazi vyenyewe vinaamini kuwa Umasikini ni uridhi wa dhaabu ambao hautakiwi kuuacha.

Kwa bahati mbaya sana watanzania wengi hatupendi kujifunza tunajipa nafasi ya kujua vitu tusivyovijua mwisho kiza.

Tuwaze zaidi katika safari ya Teknolojia hii adimu ambayo inaweza kuwaajiri watanzania wote na wakapata matokeo makubwa ya mafanikio.

Kufunga vioo haitakusaidia ila ukitoa sikio na kusikiliza itakupa njia ya kuona dunia kwa taswira ya tatu.
 
Back
Top Bottom