Kwanini CDF aitwe Mkuu wa Majeshi wakati Polisi, Magereza na Uhamiaji wana wakuu wao?

Kwanini CDF aitwe Mkuu wa Majeshi wakati Polisi, Magereza na Uhamiaji wana wakuu wao?

Hivi kuna tofauti gani kati ya askari na mwanajeshi? Huwa nasikia wengine wanaita askari wa jeshi la... kwa nini hawasemi mwanajeshi au polisi tu?!
Najibu ila kama nitakuwa nimekwenda op mtanikosoa.

Askari ni mtu yeyote aliyepitia Mafunzo rasmi ya Kijeshi kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hivyo kama mtu alijifundisha vichochoroni hatambuliki hata akiwa na Mafunzo ya special force, atapewa majina mengine Kama itaonekana inafaa.

Mwanajeshi ni member wa jeshi fulani linalotambulika kisheria. Hapa tuweke mazoea na desturi pembeni.

Hivyo kwa Tanzania Police wote ni wanajeshi, Magereza wote ni Wanajeshi, Wahifadhi ni Wanajeshi [emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]

Turudi kwenye mazoea yetu Watanganyika
Enzi za ukoloni wananchi waliona shida kuwaita wote wanajeshi wakatafuta namna ya kuwatofautisha hivyo kuwaita walio askari kwenye jeshi la mkoloni kuwa wanajeshi na walio polisi askari.

Ila uhalisia wote hawa ni askari na pia ni Wanajeshi.

Sasa jamii imezoea kuwaita askari wa jeshi la uhifadhi kuwa Wahifadhi kutokana na nature ya shughuli zao.

Ila hawa ni askari Magereza na polisi ila jamii hiyo hiyo inapendelea kuwaita walio Immigration maafisa uhamiaji.
 
Hapa nilichogundua ni msamiati wa kiswahili kutokujtosheleza, Hivyo msamiati unaotumika ndio Unawachanganya watu wachache wanaojua kizungu na Wengi wasiokijua kabisa.
CDF- Mkuu wa majesh[emoji1787][emoji1787]
 
Polisi, Magareza, TISS , uhamiaji, zimamoto sio majeshi
Huyu eti hajui kuwa Polisi, Magereza? TISS UAMIAJI , JkT ni tu vitengo tu twa jeshi bali JWTZ ndio kubwa lao. Aangalie hata wakati wa kukabidhi nchi kwa mwingine Rais anayetawazwa anakuwa na nani au anayeachia anakuwa na nani? Na rais kwa ujumla yule mvaa kombati anatokea wapi? Huyu naye sijui veep
 
Tanzania tuna Military au Army?

Unajua sifa na taratibu za kuitwa hivyo?

Kwa hiyo Force ni nini?
Inategemea unataka hili swala ulitatue kwa lugha gani,..

Jeshi kwa kiswaili ni hiyo hiyo unayoiita Military,..

Army ni kikosi kilichomo ndani ya Military
 
Tanzania tuna defence force tu, sio army Wala military.

Kuna kiwango maalumu Cha kikundi Cha askari kuitwa Army au Military sifa ambayo Tz hatuna shubaamiti.
Umewahi kusikia JKU, KMKM? Maana ulinzi ni suala la muungano.
 
Inategemea unataka hili swala ulitatue kwa lugha gani,..

Jeshi kwa kiswaili ni hiyo hiyo unayoiita wewe Amy au Military
Basi Tanzania tuna force tu mkuu

Tanzania Police force
Fire and Rescue force
Tanzania people's defence force

Kwa mujibu wa sheria, na sio kilayman
 
Tatizo lilianza walipoanza kuita polisi JESHI.

Polisi ni polisi na jeshi ni jeshi.

Hakuna kitu kama GESHI RA PORISI.

NI UHUNI TU WA WA KISIASA WA KU-MILITARIZE POLISI ILI KUWATISHA WATU.

ETI JESHI LA POLISI .... WE ULISKIA WAPI?
Tanzania ni ya kwanza

Unafahamu Kuna kipindi jeshi la polisi lilikamata nchi baada ya kuvunjwa jeshi la Tanzania chini ya akina kaptain Maganga.

Unafahamu kabla ya hii Katiba ya mwaka 77, tayari polisi walikuwa ni jeshi.

Hivyo hakuna tofauti kubwa kati yenu isipokuwa Kuna kitu kinaitwa intergovernmental service agency rival

Jw wanawadharau polisi

Polisi atamdharau Magereza

Magereza atamdharau fire

Fire atamdharau Mgambo

Immigration na usalama.

Haya hadi Marekani yapo
Yaani coastal guard na Navy
Army na Navy
Border custom na border forces
CIA na FBI
NSA na CIA
 
Bongo tunaishi kwa mazoea tu, hakuna lingine ana jina ambalo halipo back up na sheria.

Ila hata Mimi nikiwa mdogo nilijuwa mkuu wa majeshi
Ni mkuu wa majeshi (ukipenda malizia kabisa MKUU WA MAJESHI YA ULINZI) yaani CHIEF OF DEFENCE FORCES na wala siyo tafsiri yako hiyo unayolazimisha hapo

Utake ndiyo hivyo usitake itaendelea kubaki kuwa hivyohivyo. Halafu kuna mdau amemaliza mjadala hapo juujuu>>> ameuliza "Ukiambiwa kuwa Kimbute Mkendembanga ni mwanajeshi utakuwa umeelewa mojakwamoja au utauliza tena ni askari magereza au polisi?
 
Mkuu wa majeshi ya ulinzi. Jeshi la anga, maji na ardhini. Polisi, magereza nk siyo majeshi ya ulinzi.
 
Basi Tanzania tuna force tu mkuu

Tanzania Police force
Fire and Rescue force
Tanzania people's defence force..
Kwa mujibu wa sheria, na sio kilayman
Hata Israel ina defence Force,unajua nini maana ya force..

Moja katika Jeshi bora Duniani ni Jeshi la Israel,Jeshi la Israel linaitwa Israel defence force(IDF)

Mkuu,hayo ni majina tu,nchi zimeamua kuita jeshi lake....

kwa ufupi ukitumia neno force kwenye Jeshi,inamaanisha ni moja katika kikosi kwenye Jeshi kubwa(Military)

mfano Air force,Army Force,commando force,Police force nk

Military ni Jeshi,Force ni kikosi,...

Ningelikuomba urudi shule upata knowledge kidogo :-
 
Back
Top Bottom