Kwanini Dialysis Zanzibar ni bure na Tanzania bara 180,000 kwa siku

Kwanini Dialysis Zanzibar ni bure na Tanzania bara 180,000 kwa siku

Hazikungoja hisani, mtu kajitolea sadaka yake.

Mbona hata sisi pale Jakaya Kikwete Heart Institte yote ile imejengwa kwa saka ya mtu na mpaka leo analeta madaktari kutoka nje na analipia gharama nyingi tu pale. Kuliko hizo za dialysis tu Zanzibar.

Na mama mwingine wa Kimarekani alitujengea wadi yote ya magonjwa ya meno na Kinywa pale Muhimbili na analipia gharama zote.


Wewe lini ulienda kujitolea japo panadol za wagonjwa Hospitali?
Kumbe Makafiri nao wana Utu pamoja na mambo yao ya Kishoga.

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Mnaharibu figo zenu makusudi kwa kunywa mapombe makali mkidai mnakula bata.

Sasa unalialia kulipa Tsh 180,000 kwa ajili ya malipo ya kusafisha figo, nyambaaaf
Kuna watu hawanywi pombe lakini wanapata ugonjwa wa figo.
Mfano, kama mtu akiumwa ugonjwa unaosababisha anywe dawa mara kwa mara, ni rahisi figo zake kuathirika
 
Mnaharibu figo zenu makusudi kwa kunywa mapombe makali mkidai mnakula bata.

Sasa unalialia kulipa Tsh 180,000 kwa ajili ya malipo ya kusafisha figo, nyambaaaf
Hao wanaosafishwa bure walikunywa nini ?
 
Zanzibar afya Bure kabisa... Hata uumwe nn kumuona dokta mpka dawa ni Bure kabisa. Na kipindi hiko unapewa Hadi uji
Sio uji tu mpaka chakula Cha mchana na usiku wagonjwa wanapewa Bure ni ww tu wakuletee ndizi pukusa upige wali, Kuna jamaa mmoja msukuma asiyekuwa na makazi Kuna siku alikuwa anavuta bangi akiwa ghorofa ya 3 sasa sijui nini kilimtokea uko juu tukashangaa kitu kama kifurushi kizito kimeanguka chini kwenda kuangalia tunamkuta mwamba kazimia kumpeleka hospital ya taifa mnazi mmoja ikaonekakana amevunjika mguu akalazwa mnazi mmoja siku nyingi mno akapona lakini akaomba awe anapumzikia humo humo wodini basi mchana ama jioni unakutana naye nje ya hospital usiku wodini wakaja kumtimua kwa nguvu baadae.
 
Tanzania na Zanzibar ni nchi mbili tofauti?

=======

Mdau anahoji kwanini wagonjwa wa figo wanafanyiwa kwa gharama ya Tshs 180,000 kwa siku Tanzania bara ilhali Zanzibar ni bure. Amesema wapo wanaotakiwa kufanyiwa dialysis mara mbili au tatu kwa siku. Mdao ameomba majibu kwa waziri wa afya.

Sababu wanajali raia wao. Wazee wote nasikia wanalipwa pesa za kujikimu Zanzibar, umeme ni bure kule. Deni likiwa kubwa linasamehewa.

Upande wa pili Watanganyika wanapambana na hali zao. Hawana mtetezi. Watu wanatetea matumbo yao.
 
Huu nao ni utapeli mwingine. Hapo kuna harufu ya ufisadi nyuma ya mkataba.
Mtu anapandikizwa onekane anajitolea kumbe Kuna mtu anatuibia tanganyika afu anamwekea mtu huko Barclays londoni kwa makubaliano kua ajifanye anajitolea zanzibar
 
Tanzania na Zanzibar ni nchi mbili tofauti?

=======

Mdau anahoji kwanini wagonjwa wa figo wanafanyiwa kwa gharama ya Tshs 180,000 kwa siku Tanzania bara ilhali Zanzibar ni bure. Amesema wapo wanaotakiwa kufanyiwa dialysis mara mbili au tatu kwa siku. Mdao ameomba majibu kwa waziri wa afya.

Uchumi wao unaweza kubeba hizo gharama , Sisi tunaweza kubeba ufisudi na kuwa Saidia majirani
 
Kazi kweli kweli
Ndugu yangu , mbona hayo ni madogo!
Wakusanya kodi wa SMZ wanalipwa mishahara kutoka Hazina Dar kwa jina la TRA, ingawa makusanyo hayavuki bahari

Wazanzibar hao hao wakija bara wanatibiwa bure, tena ikibidi kwenda India wanalipiwa na JMT a.k.a Tanganyika.

Proved nakupa challenge moja, tafuta jumla ya Bajeti ya JMT, halafu uje uniulize kulikoni!
 
Ndugu yangu , mbona hayo ni madogo!
Wakusanya kodi wa SMZ wanalipwa mishahara kutoka Hazina Dar kwa jina la TRA, ingawa makusanyo hayavuki bahari

Wazanzibar hao hao wakija bara wanatibiwa bure, tena ikibidi kwenda India wanalipiwa na JMT a.k.a Tanganyika.

Proved nakupa challenge moja, tafuta jumla ya Bajeti ya JMT, halafu uje uniulize kulikoni!
Kama Bara tukipunguza ufisadi na tukapunguza matumizi makubwa ya serikali hatutapata unafuu na sie?
 
Mdau anahoji kwanini wagonjwa wa figo wanafanyiwa kwa gharama ya Tshs 180,000 kwa siku Tanzania bara ilhali Zanzibar ni bure. Amesema wapo wanaotakiwa kufanyiwa dialysis mara mbili au tatu kwa siku. Mdao ameomba majibu kwa waziri wa afya.
Hoja sio "Kwanini wao bure na sisi tunalipa wakati sote ni Watanzania". Ina maana hafahamu kwamba afya sio suala la muungano? Angehoji kwanini Tanzania bara hiyo huduma na yenyewe isiwe bure hasa kwa kuzingatia hicho kiwango ni kikubwa sana kwa Watanzania.
 
Wazanzibar hao hao wakija bara wanatibiwa bure, tena ikibidi kwenda India wanalipiwa na JMT a.k.a Tanganyika.
Kwahiyo mimi mtu wa Tabora nikienda Muhimbili nitalipia matibabu lakini Mzanzibari akifika Muhimbili anatibiwa bure?
 
Back
Top Bottom