Kwanini familia ya Kikwete inapendekeza mishahara kwa wake wa viongozi wakati tayari wengi wao wako serikalini?

Kwanini familia ya Kikwete inapendekeza mishahara kwa wake wa viongozi wakati tayari wengi wao wako serikalini?

Ok mi fisadi na wewe Masikini unayeumia watu wakipata
Sawa mr fisadi
Ok, hebu tufanye leo hii Mungu anaiondosha familia nzima ya JK, je ndo mishahara itaongezeka?
Je ndo pension zitalipwa vizuri?
Je ndo nchi yetu itakuwa tajiri?
Kwa mawazo yako unaamini shida zote za watz ni kutokana na uwepo wa familia ya JK.
Una ROHO YA KIMASIKINI!!
Issue ni wakiondoshwa au issue ni waliyoyafanya kulididimiza taifa hili na bado wanaendelea kuyafanya, i can agree kua wakiondoka ndio hayo yote uliyoyataja yanaweza kufanyika. Ufisadi wote unaofanyika nchini source ni CCM na hiyo familia ndio ina mafisadi yaliyokubuhu ukiwemo na wewe, sasa sijui wewe ndio mama salma au vp.
 
Kwakweli kwa hili ni wazi ni udhaifu mkubwa sana!
Familia ambayo ilisha pata fursa ya kuongoza nchi, na bado Kikwete ana uwekezaji mzuri tu wa kibiashara za kitaifa na kimataifa ,lakini mke wake anaamka asubuhi moja kwenda kushawishi wabunge wenzake waongeze marupurupu na mishahara wake za marais na mawaziri kupitia kodi za wananchi wanyonge wanao hangaikana maisha kwa vipatovyao vidogo.

Ni jambo la kusikitisha sana lisilo paswa paswa kuuchwa
 
Imeandikwa:--

"Kwa maana aliye na kitu ataongezewa, na asiye na kitu atanyang’anywa hata kile kidogo alicho nacho.”
 
Ngoja nipambane niwe namba Moja .....mama kija wangu aje kua first lady na kija ale mema ya nchi.
 
Au walizinguana mzee akamwambia hapa huambulii senti 5, tafuta za kwako
Inawezekanaje mke wa mh Kikwete atengwe na ukwasi wa familia?? Nitamaa tu ya mama huyo! Na pengine pamoja na madhaifu ya Kikwete hapa mkewe kamuongezea ubaya kwa wananchi kwa kujua au pasipo kujua mama huyo.
 
Kukaa unamuwazia mabaya JK ni kujitesa nafsi tu



Ukiyajibu maswali hayo hutokaa kuhangaika na JK.
Shika hamsini zako
Fala wewe hunijui huyo JK wako tulikua tunampambania sisi hapa wakati wewe ukila urojo huko mchambawima kenge wewe.
 
Wanajua mtapiga kelele baadae mtasahau lkn wao watakula daima!!
Mke wa kiku kuacha kumtunza mumewe na kukimbilia ubunge ni uroho,ulafi na kutoridhika!! Sasa anataka alipwe dabodabo wakati kuna watoto wanateseka Kwa uyatima na magonjwa!!
Wapo watu wasio na utu wala aibu hutafuta vyanzo viiingi vya pesa kupitia kodi za wananchi...
Mwisho nawasihi kizazi hiki cha marioo kamwe msikubali kutawaliwa na mwanamke!!!
 
Moja kati ya makosa makubwa yaliyowahi kufanyika nchi hii ni kumpa Jakaya Kikwete madaraka ya uraisi. Pamoja na mapungufu makubwa aliyoonyesha kiungozi bado aliingiza familia nzima katika urais huku wakipigana vikumbo kutafuta fursa na kujipenyeza.

Mengi yanajulikana, lakini kinachoniuma zaidi ni familia yake kupeleka hoja ya kuwalipa pensheni wake wa viongozi. Kwa wasiofahamu hoja hii ilipelekwa bungeni na Mama Salma Kikwete ambaye ni mke wa Rais Kikwete. Hiki ni kiwango kikubwa zaidi cha tamaa zaidi hata tamaa ya fisi. Bila shaka hiki ndio legacy anayoacha Kikwete kwa familia yake, kutotosheka.

Pamoja na kufuja rasilimali za nchi katika kipindi chake, pamoja na mauwekezaji rasmi na yasiyo rasmi katika familia yake bado watu hawa hawatosheki?

Familia inakosa utu kabisa. Nchi ina ukata kutwa kuchwa kupokea misaada. Lakini kuna watu baba raisi, mama mbunge, kaka waziri bado hawatosheki wakaja na pensheni kwa wake wa viongozi.

Familia hii haikuona kabisa pesheni ndogo wanazolipwa watumishi wa umma, pengine ipeleke hoja bungeni na kutia ushawishi kwa Rais. Haikuona mishahara midogo yenyewe ikaona walichonacho waongezewe maradufu.

Kuna wakati Rais Magufuli alionyesha chuki ya wazi kwa Kikwete, pengine alichukia sana tamaa za Kikwete na familia yake.

Huyo na Museveni baba mmoja mama mmoja!
 
Inawezekanaje mke wa mh Kikwete atengwe na ukwasi wa familia?? Nitamaa tu ya mama huyo! Na pengine pamoja na madhaifu ya Kikwete hapa mkewe kamuongezea ubaya kwa wananchi kwa kujua au pasipo kujua mama huyo.
Ukweli wanajua wao sisi wengine ni watafsiri tu ila kikubwa bunge kupitisha ule upuuzi ni huzuni sana
 
Hakuna lolote! Rais baada ya Samia atatokea kati ya hawa mastaa 4 toka Msoga Camp:- Ridhiwan, Nape, January na Mwigulu. Wengine endeleeni kuimba iyena iyena tu.
Msoga ishakufa sahv inanuka uozo tu,,,,,..........dadeki mlitaka kumlia timing Konda boy huko kusini halafu maturubai mwishoni mkatandika nyie....hadi ifike 2030 wazuri hawafi watakua wanapumulia njia ya haja kubwa badala ya puani........,kazi ya sasa ni kuhamisha tu rimoti
 
Tunachoangalia hasa ni mzigo mzito ambao serikali zijazo zitashindwa kubeba kutumia kodi za maskini kuhudumia kifahari familia za viongozi wastaafu na wake zao ambao ni walafi, hawashibi na huwaza kuishi milele sasa tabu kubwa itakuja pale marais wastaafu wakifika mia na wake zao mia nne, makamu wa rais mia mbili na wake zao mia sita, mawaziri mkuu wastaafu mia nne na wake zao mia sita!

Hakika nchi maskini kodi za raia maskini zinaliwa bure na viongozi wao waliojaa ulafi , ubinafsi na tamaa za fisi!
 
Back
Top Bottom