Kwanini French speaking African nations ndio zina vita tu?

Is

Islam hata wakiwa 10% Tu Ni Shida...kama ufaransa wako chini ya 1% lakini kasheshe wanayowaletea sio ya kitoto
Hivi Tanzania Islam ni % ngapi
Vipi kwa kenya na Ug nazo ni % ngapi?
 
suda
n, somalia,gambia,sierra leone???
 
Ufaransa alitoa uhuru kwa hizo nchi kutokana na sababu mbalimbali zilizokuwa za ulazima, lakini Ufaransa amekua akitumia ukoloni mamboleo kwa nchi hizo na kutetea maslahi yake katika nchi hizo hasa kufuja mali za mataifa hayo kwa kuweka viongozi vibaraka watakaolinda maslahi yao mfano Blaise compaore pale Burkina Faso , Jean Bedel Bokasa kutoka Central Africa hao ni wachache tu lkn itoshe kusema vita vipo na vitaendelea kwa Kuwa Ufaransa bado anazinyonya kinguvu nchi hizo Ambazo ana ushawishi nazo
 
Ufaransa wanataka rasilimali toka Afrika hasa mafuta, hivyo wanafanya kila wawezalo kuhakikisha wanaweka viongozi watiifu kwa Ufaransa kwenye makoloni yao ya zamani
Kama alivyowahi sema rais wa zamani wa Ufaransa bwana Francois Mitterand
"Bila ya Afrika Ufaransa ingekuwa na historia yoyote Karne ya 21"

Kwa nyongeza Ufaransa wana maslahi mapana sana ya kiuchumi ktk makoloni yao ya zamani, maana makampuni yao ya Mafuta kama Total yanachimba mafuta kwenye nchi hizo huku nao wakichapisha fedha kwa nchi kadhaa za Afrika kumaanisha kuwa fedha hizo zinadhibitiwa na Benki kuu ya Ufaransa.

Ktk hali hiyo ni muhimu kuhakikisha nchi hizo zinakua salama (hasa wa watu walowaweka), ndio maana kitisho chochote cha usalama Ufaransa huwa mstari wa mbele kuingilia kati, chokochoko za kiusalama huwa ni fursa muhimu kqa Ufaransa kuzidi kuzishikilia nchi za Afrika ndio maana unaona haziishi...mara ugaidi mara mapinduzi (Coup dé tat).
 
Nini kifanyike mkuu
 
Nini kifanyike mkuu
Dunia imebadilika sana na kuna mbinu kadha wa kadha za kuhakikisha malengo yanatimia.

Ktk kujibu nini kifanyike hapa inategemea na mgogoro huo ni wa nchi gani, sidhani kama kuna jibu au suluhu ya ujumla kutatua matatizo tofauti ya hizi nchi zinazozungumza kifaransa.
 
mbona hujiulizi raia wakawaida kumpiga vibao rais wa ufaransa na hakuna lamana kufanyika na rais kuonekana anamakosa ,hakuvaa barakoa
 
wafaransa ni washenzi hawakukubali kuwa ukoloni umefikia mwisho waliendelea kutawala kwa kutumia mamruki na wale waliowapinga waliuawa, ndiomaana jeshi la rpf huko rwanda chini ya kagame aliamua kuvunja mahusiano yote na ufaransa ukizingatia ufaransa ilikua na mchango mkubwa kwenye genocide ya nchi hiyo hadi hivi majuzi macron alipokuja kukili kosa na kuomba msamahaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…