Kwanini gharama za kutuma pesa kutoka Akaunti ya benki kwenda mtandao ya simu ni kubwa sana?

Kwanini gharama za kutuma pesa kutoka Akaunti ya benki kwenda mtandao ya simu ni kubwa sana?

Wakusoma 12

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2017
Posts
4,035
Reaction score
11,462
Hili suala limekaaje kitaalamu, mfano benki kama NMB ukitaka kutuma pesa kwa mtu kutoka kwenye Akaunti ya benki kwenda kwa namba yake ya simu Cha mtema Kuni utakiona. Je hii ni sawa wakuu? Kwanza gharama za makato hazionekani kabla ya kutuma pesa, ila utakutana nazo tu ukishatuma tayari. Hii si sawa benki kama taasisi muhimu za kiuchumi zijaribu kuwa wawazi katika mchakato mzima wa utumiaji wa huduma zao kwa njia ya simu.
 
Kwa hiyo mie ndiyo nitafute Hela ya kuwanufaisha wao pekee?, huwezi elewa kama mumeo ndiyo anakutafutia Kila kitu.
Ungekuja na takwimu, ukaonesha NMB makato Yao yako vipi, Kisha ukaonesha na uko unapofikiri kupo sahihi makato Yao yako vipi.
 
Nilishaigundua hii changamoto kutambo baada ya kumtumia mtu elfu50 kutoka CRDB kwenda ktk sim yake nikajikuta nimekatwa almost elfu 5 kwenye huduma hiyo.

Hata ukitoa ela kwa wakala wa kibenki na atm card yako makato ni makubwa sana ukilinganisha na kutoa kwenye atm machine. Nilishawahi toa laki kwa wakala nikakatwa elfu7, wakati pesa hiyo ningeitoa kwenye atm machine ningesave elfu 5 na miatano nzima.

Njia nzuri ya kuepuka hayo ni kwenda moja kwa moja atm machine, toa pesa, nenda kwa wakala aitume kwenye simu ya mpokeaji. Utakua umeokoa kiasi kikubwa cha makato ambayo hayana maana.
 
Huduma nilizoacha kutumia
1. Kutoa fedha zilizoko kwenye account ya bank kwa wakala
2. Kutumia apps mbali mbali za fedha kwenye simu
3. Kutuma ama kutoa fedha kwenye account ya bank kwa njia ya simu

Waweza ona imerahisha huduma bali ni garama sanaa
Kwahio mkuu wewe ni mwendo wa tawini na ATM tu? Kuna bank lutoa tawini wanachaji hela hata 5,000 na ATM bank tofauti pia wanachaji hadi 5,000. Kutafuta ATM ya bank yako sometimes pia shida. Na gharama za usafiri nazo kwenda tawini na muda utakaopoteza. Yaani unaona gharama kubwa ila utafanyaje wamebana kila angle.
 
Sasa kuna kuhamisha kutoka kwenye simu kwenda bank. Kuanzia 500,000 hadi 1m wanakata 7000-8000. Kwa upande mwingine hela hio ukitoa kwenye simu kwa kutumia wakala watakata almost hio hio halafu uipeleke tena bank ni upotevu mwingine wa muda na fedha. Hapo ndio unajikuta huna namna.
 
  • Thanks
Reactions: apk
Ungekuja na takwimu, ukaonesha NMB makato Yao yako vipi, Kisha ukaonesha na uko unapofikiri kupo sahihi makato Yao yako vipi.
Takwimu Gani unataka? Kwa hiyo huamini ama haya mambo ya Kila kitu takwimu wakati hata haya maelezo niliyotoa ni takwimu tosha au mpaka ungeona manamba ndipo ungesadiki?
 
  • Thanks
Reactions: apk
Juzi nilitoa 45,000/= nilikatwa kama 3,389.83 hapo bado hujaitoa tena kwenye simu.Gharama ni kubwa aisee hii ni kwa NMB.
 
usilogwe. kuhamisha benk to mitandao.
hawaonyesh gharama za kutuma ila ukirusha hata 2000. unakatwa almost 2800 .nadhan ni makusud ya apps developer.
mbona azam pesa ukitaka kufanya jambo unaonyeshwa kila kitu makato
 
Nilishauninstall simbanking app.
Ungeiacha tu ili uifanye kama app ya kucheck salio na makato madogo madogo. Jenga utaratibu wa kuchungulia chungulia salio kwa app hata kila baada ya siku tatu, faida ya kwanza ni haina makato, lkn pia itakupa urahisi wa kugundua makato madogo madogo unayokatwa na sababu zake.
 
Back
Top Bottom