Kwanini Kalemani na Chamuriho? Je, ni kuvunja mtandao?

Kwanini Kalemani na Chamuriho? Je, ni kuvunja mtandao?

Nadhani hata lile bomba la mafuta watu walilojiunganishia lilikuwa la Kalemani na genge la sukuma gang. Ndio maana habari zake zikawa siri maana taarifa ingewekwa wazi ingeleta picha mbaya.
Watu hawayajui hayo,wanabwabwaja tu
 
Sisi kanda ya ziwa tunachukulia hii issue kama discrimination against watu wa lake zone na off course January hawezi kuwa bora kuliko Dr. Medard. Tutakutana 2025. Huo uHangaya kama mnadhani ni wa kiukweli you will get to know that you were conned during the next elkection. Matogoro was the best minister ever. Unampigia hakufahamu na anapokea simu na kuifantia kazi hapo hapo. He was so good na amefanya kazi kwa nguvu zake zote. Tukutane 2025.

Sent from my CPH2219 using JamiiForums mobile app
Mama alishasema mumpigie kura au msimpigie... Rais atatangazwa yeye...

Kwahiyo mangosha tulieni na wenzenu wafaidi keki ya taifa

Kutesa kwa zamu
 
Watu makini wanaweza kutoa angalizo kwa Madam President kuhusu utenguzi wa mawaziri vipenzi wa hayati JPM. Ni vyema angewapangia majukumu mengine kabla kuanza kuibuka wingi wa manung'uniko kutoka kanda ile pendwa kwa nyakati hizo.

Mbali ya Chato, maeneo mengi ya kanda ya ziwa yalikuwa ndiyo kipaumbele cha JPM, jambo hilo lilimfanya aonekane shujaa wao. Alichagua mawaziri hawa kimkakati ili waweze kuwa karibu na watu wa kanda hii ili kuwaletea maendeleo.

Kanda hii ilianza kusikia viongozi wao wakiitwa "Sukuma Gang" na kushutumiwa vikali hata pale walipofanya makosa ya kawaida. Chochote kile walichokifanya kiwe chema ama kibaya, kikaanza kuonekana kama wanamkwamisha Mama kuelekea 2025.

Angalizo sasa ni kisije kutokea kile ambacho wengi hawatarajii. Ni kuhusu "sympathy" ya wananchi wa kanda hii juu ya viongozi wao kuanza kutengwa muda mfupi tu mara baada kifo cha JPM. Kanda hii inaweza kugeuka kuwa ndiyo ngome kuu na imara ya upinzani, na mwanzo wa kuelekea katika hitaji la siku nyingi la wapenda mabadiliko la kutaka kupigilia msumari wa mwisho katika jeneza la marehemu mtarajiwa CCM.
Tanzania haijafikia hatua ya kuogopa kufanya maamuzi yenye maslahi ya Taifa kwa kuhofia ukanda au ukabila. Nyie watu wa kanda hiyo for sure mlikuwa mnaenda kuigawa nchi vipande vipande. Kwanini nyie mjione ni kanda isiyoguswa? No wonder mlianza kuibagua kanda ya kaskazini. Tambueni kwamba Rais wa Tanzania hataogopa kufanya maamuzi yenye maslahi ya Taifa kwa hofu ya kidini, ukanda, ukabila au jinsia.
 
Inajulikana Kalemani ndie mbunge wa Chato kipenzi cha Hayati na mrithi wa jimbo lake. Pia inajulikana Chamriho ametokea ngazi za juu huko Tanroads ambayo ndio iliyofanikisha ndoto ya Hayati kutwaa urais 2015.

Ukisikia na hotuba ya leo ya mama na ukiangalia walioondolewa hawakuwa wabaya kiutendaji ndio walioshika wizara kubwa na zinazofanya vizuri na kusimamia miradi mikubwa na ziko hadi vijijini kwenye wananchi.

Je, kulikuwa na harufu ya mtandao wa kumkwamisha mama katika safari yake kuelekea 2025?

Muda utaongea
Mambo magumu Sana haya,,,huenda ikawa japo 2025 itatoa majibu
 
Mwaka 2025 hatuwezi kuongozwa na wazanzibari. Yaani Mzanzibari atawale Zanzibar halafu tena Mzanzibari atawale Tanganyika, hilo halipo.
 
Mwanachato alijichanganya sana kufa halafu marafiki zake karibu wote nao wamekufa

Yaani kiuhalisia sijui kama kuna mtoto wake atakaepatiwa nafasi hata ya udiwani
Matajiri wale mkuu,udiwani tuwazie sisi
 
Inajulikana Kalemani ndie mbunge wa Chato kipenzi cha Hayati na mrithi wa jimbo lake. Pia inajulikana Chamriho ametokea ngazi za juu huko Tanroads ambayo ndio iliyofanikisha ndoto ya Hayati kutwaa urais 2015.

Ukisikia na hotuba ya leo ya mama na ukiangalia walioondolewa hawakuwa wabaya kiutendaji ndio walioshika wizara kubwa na zinazofanya vizuri na kusimamia miradi mikubwa na ziko hadi vijijini kwenye wananchi.

Je, kulikuwa na harufu ya mtandao wa kumkwamisha mama katika safari yake kuelekea 2025?

Muda utaongea
Ni kuvunja mtandao maana sidhani kama kunashida wote walikuwa na tarizo hiyo hapana
 
Akaunti za kalemani zifungwe
Hazikufungwa za akina Kalamagi,Tibajiuka,Chenge.ufunge account za Kalemani kaiba Nini?
Chuki na fitina zenu hazitawafikisha popote.
Hapana shaka hakuna utawala utadumu milele.
 
Inajulikana Kalemani ndie mbunge wa Chato kipenzi cha Hayati na mrithi wa jimbo lake. Pia inajulikana Chamriho ametokea ngazi za juu huko Tanroads ambayo ndio iliyofanikisha ndoto ya Hayati kutwaa urais 2015.

Ukisikia na hotuba ya leo ya mama na ukiangalia walioondolewa hawakuwa wabaya kiutendaji ndio walioshika wizara kubwa na zinazofanya vizuri na kusimamia miradi mikubwa na ziko hadi vijijini kwenye wananchi.

Je, kulikuwa na harufu ya mtandao wa kumkwamisha mama katika safari yake kuelekea 2025?

Muda utaongea
Dai katiba acheni majungu
 
Tulishawaonya hapa mara nyingi. Acheni dharau kwa Mama.

Bado wengine.
Tuliwaambia Simba akiwa anacheka na wewe habadiliki kuwa sungura. Kuweni makini.... Na washaambiwa hii ni comma sio full stop
 
Hakuna anachokifanya hapo hii ni sawa na miguu kuwa gerezani kichwa kipo mtaani panga pangua fanya awezavyo watu walishatambua haya mapema na wakajiandaa

Dawa pekee ya mama kueleweka ni yeye mwenyewe kuachia ngazi
 
Hazikufungwa za akina Kalamagi,Tibajiuka,Chenge.ufunge account za Kalemani kaiba Nini?
Chuki na fitina zenu hazitawafikisha popote.
Hapana shaka hakuna utawala utadumu milele.
Zilipofungwa za mbowe na wafanyabiashara ulishangilia
 
Kivipi mkuu mbona Bashiru Ally na mpayukaji Cyprian Musiba waliwahi kumtuhumu jasusi mbobezi Membe kuwa anataka kumkwamisha bwana hayati mwanachato
Si hii inatosha kuonesha ilivyo kuwa sio rahisi au?
 
Back
Top Bottom