Kwanini kiongozi wetu mkuu hajawahi kukosa USD za kufanya safari za nje ya Nchi ilhali wafanyabiashara wanakosa USD kwenye MABENKI?

Kwanini kiongozi wetu mkuu hajawahi kukosa USD za kufanya safari za nje ya Nchi ilhali wafanyabiashara wanakosa USD kwenye MABENKI?

Sasa ikiwa wafanyabiashara wanakosa dollar kwenye banks,

Kwanini safari za nje zisifutwe Hadi mambo yatakapotengemaa?

Nini maana ya uongozi?
Safari za rais peke yake haziwez kupunguza dollar nchi nzima. Wafanya biashara kukosa dollar sababu si safari za rais, sababu ni mifumo ya fedha ya ndani, rekebisha hiyo dollar zitaonekana or else
 
Safari za rais peke yake haziwez kupunguza dollar nchi nzima. Wafanya biashara kukosa dollar sababu si safari za rais, sababu ni mifumo ya fedha ya ndani, rekebisha hiyo dollar zitaonekana or else
Safari Moja ya Rais na wapambe wake wanaofikia 100 kwenda marekani na kukaa wiki Moja hugharimu Dollar Bei Gani?
 
Hali si nzuri na soon Importers wengi watakuwa taabani kiuchumi..

Tufungue milango,Turegeze sheria
Wageni toka mataifa mbalimbali waje na dola bila kikomo..Wachangamshe uchumi na uwekezaji..

Waganda,Wakongo,Wachina,..
 
Hali si nzuri na soon Importers wengi watakuwa taabani kiuchumi..

Tufungue milango,Turegeze sheria
Wageni toka mataifa mbalimbali waje na dola bila kikomo..Wachangamshe uchumi na uwekezaji..

Waganda,Wakongo,Wachina,..
Viongozi wazuiwe kusafiri nje ya Nchi maana ndio wanaokausha hazina ya dollar nchini.

Pia tuzalishe na kuuza bidhaa nje Ili kupata akiba ya dollar, kiufupi,biashara za uchuuzi kununua vitu china, tunapoteza dollar, viwanda vya ndani vizalishe kukidhi soko la ndani Kisha tupeleke nje.

Tusiruhusu wageni kuingia na kununua Michele au chakula mashambani, waende serikalini, walipe dollar na kununua kwenye maghala ya Serikali.
 
Salaam, Shalom!!

Kila Kona ya nchi yetu Kwa sasa, dollar imekuwa mtihani, hazipatikani hata Kwa tochi,

Mfanyabiashara mwenye pesa za kitanzania, akienda benki kubadili Tshs Ili apewe USD Kwa ajili ya kuagiza bidhaa nje ya Nchi, anaambiwa dollar hamna. Analazimika kuzitafuta mtaani na kuzipata ni rate kubwa Hadi 3000sh Kwa 1 Usd.

Swali linakuja kuwa,

1. Kiongozi wetu anapofanya safari za nje Huwa anatumia Pesa za kitanzania TSHS akiwa huko Nchi za watu?

2. Na ikiwa Huwa anatumia dollar na walioambatana naye ,wao huwa wanapata wapi hizo USD ambazo wafanyabiashara wakienda benki hawazipati?

3. Tukiwaza Kwa sauti kuwa safari za nje za viongozi wetu ndizo zinakausha hazina ya dollar nchini, tutakuwa tumekosea kuwaza hivyo?

4. Ikiwa hizi Bureau de Change za mtaani wanazo dollar, iweje MABENKI yakose USD, hamnu
si harufu ya kitu kibaya hapo?

USHAURI: Kiongozi wetu mkuu na WA chini yake, wasitishe safari za nje Hadi hapo Nchi itakapokuwa na hazina ya pesa za kigeni za kutosha. Uongozi ni vitendo, ni kuongoza njia, Si maneno matupu.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni🙏
Mkuu Rais Samia usimchukulie kama mtu wa kawaida, mh ni taasisi iliyoshika hatamu ya kuongoza nchi.
Itifaki lazima izingatiwe.
 
Mkuu Rais Samia usimchukulie kama mtu wa kawaida, mh ni taasisi iliyoshika hatamu ya kuongoza nchi.
Itifaki lazima izingatiwe.
Ameenda marekani mara ngapi?

Mbona Biden hajakanyaga huku?

Kwani lazima kusafiri Kila kukicha, video conferencing inatosha, wabaki nchini tupate pesa ya kuagiza bidhaa.
 
Inawezekana hayo masafari na team kubwa hadi ya wasanii wajinga ndo yaliotusababishia uhaba wa dola nchini!.
Unaambiwa safari Moja Huwa inagharimu zaidi ya B2 na kuendelea.

Sasa safari za Kila kukicha ,Si lazima mfuko ukauke!!
 
Ameenda marekani mara ngapi?

Mbona Biden hajakanyaga huku?

Kwani lazima kusafiri Kila kukicha, video conferencing inatosha, wabaki nchini tupate pesa ya kuagiza bidhaa.
Mkuu Joe Biden ni rais na Samia Suluhu ni rais.
"Poverty isn’t a lack of character. It’s a lack of cash.” —Rutger Bregman
 
Mkuu Joe Biden ni rais na Samia Suluhu ni rais.
"Poverty isn’t a lack of character. It’s a lack of cash.” —Rutger Bregman
Kwahiyo huko nje kuwa wajomba wanaotoka pesa Bure sio!!
 
Mkuu naona bado una mindset ya Magufuli kwamba sisi ni DONOR country.
Ni Kweli Si uongo.

Nchi yenye madini ya Kila aina kwenda kutembeza bakuli kuomboleza ni fedheha Kwa nchi yetu.

Hujui kuwa Dhahabu yenyewe ni PESA?

Kwanini Serikali isihakikishe Dhahabu yote unaingia kwenye Stock exchange nchini, ndege zisiruhusiwe kupakia gold bars zikaguliwe zote na sisi tupate hisa ya 50%,

Tukifanikiwa Hilo, migodi ya Dhahabu pekee itatoa trillion 50kwa mwaka.

RUSHWA ndio tatizo letu, sisi Si maskini. Ukisema Umaskini wa Akili, nitakubali.
 
Ni Kweli Si uongo.

Nchi yenye madini ya Kila aina kwenda kutembeza bakuli kuomboleza ni fedheha Kwa nchi yetu.

Hujui kuwa Dhahabu yenyewe ni PESA?

Kwanini Serikali isihakikishe Dhahabu yote unaingia kwenye Stock exchange nchini, ndege zisiruhusiwe kupakia gold bars zikaguliwe zote na sisi tupate hisa ya 50%,

Tukifanikiwa Hilo, migodi ya Dhahabu pekee itatoa trillion 50kwa mwaka.

RUSHWA ndio tatizo letu, sisi Si maskini. Ukisema Umaskini wa Akili, nitakubali.
Mkuu usiishi katika hisia ishi katika uhalisia.
 
Mkuu usiishi katika hisia ishi katika uhalisia.
Botswana ni Nchi Iko Africa na Wana hisa ya 50%+ Kutoka makampuni ya almasi na Dhahabu,

Benk zao kwenye mgao wao, wanachukua gold bars na Dhahabu, inatunzwa benki kuu,

Kitu hicho kimeimariaha u humi na kufinance budget Yao Kwa asilimia zaidi ya 70.

Kama Si mbumbumbu, basi ni MMOJA wa wanufaika wa wizi wanaostahili kunyongwa.
 
Back
Top Bottom