Kwanini kujenga nyumba imekuwa ni fashion kwa Watanzania?

Kwanini kujenga nyumba imekuwa ni fashion kwa Watanzania?

Imekuwa ni jambo la kushangaza kwa watanzania wengi kuamua kujenga na kuendelea kuishi maisha yale yale

Unakutana fundi fenicha aliyefanya kazi miaka 15 anakuambia anamalizia ujenzi ukiangalia ufanyaji kazi bado wa kusubiri hela advance kwa mteja hafikirii kabisa kuwa na store kubwa utakayotoa faida kubwa zaidi kwa haraka zaidi kutokana na uzoefu wake.

Unakutana na dereva yeye miaka na miaka anaendesha gari za watu anakuja na habari njema amejenga ni vyema lakini kwanini asikilie kumiliki gari yake.

Unakutana na kijana kinyozi ana uzoefu wa miaka saba anakuambia nimejenga vyumba vitatu nataka nihamie kwangu ni jambo jema lakini hafikirii kama pesa hizo kama angetumia kufungua barbershop kubwa ambayo ingempa faida maradufu
Kama ambavyo wewe unaamini una akili timamu ya kung’amua na kuwashangaa wanaojenga na wao wanakushangaa unachowaza! Kikubwa kila mtu afanye kinachompa furaha.

Yaani we uaamini kodi ya nyumba miaka 15 ni ndogo kuliko kujenga na kukaa kwako freely?!
 
Imekuwa ni jambo la kushangaza kwa watanzania wengi kuamua kujenga na kuendelea kuishi maisha yale yale

Unakutana fundi fenicha aliyefanya kazi miaka 15 anakuambia anamalizia ujenzi ukiangalia ufanyaji kazi bado wa kusubiri hela advance kwa mteja hafikirii kabisa kuwa na store kubwa utakayotoa faida kubwa zaidi kwa haraka zaidi kutokana na uzoefu wake.

Unakutana na dereva yeye miaka na miaka anaendesha gari za watu anakuja na habari njema amejenga ni vyema lakini kwanini asikilie kumiliki gari yake.

Unakutana na kijana kinyozi ana uzoefu wa miaka saba anakuambia nimejenga vyumba vitatu nataka nihamie kwangu ni jambo jema lakini hafikirii kama pesa hizo kama angetumia kufungua barbershop kubwa ambayo ingempa faida maradufu
maisha ni kuchagua. uchaguzi wa mwingine hauwezi ukafanana na wako. kila mtu anajua tafsiri ya maisha kivyake.
 
Hujamuelewa mleta uzi hatakataa kujenga ila jenga ukiwa ushazungusha hela yako mara kadhaa yaani kama una biashara tayari ushazungusha faida hata mara kumi ndo uanze kujenga ili kukuza mtaji.
Acha ajenge kwanza ndo akakusanye za kuzungusha. Hela ina kasumba. Unaenda kuizungushia kwenye biashara, biashara zinasuasua TRA WANAKUJA KUKUNG’OA, mara ulikopa uendeleze
Basi na Yono nao wamefika. Unajikuta hela yote imepotelea kwenye ‘kukuza biashara’.

Acheni watu wajenge kwanza ndo wakakuze hizo biashara hata wakikwama wana uwezo wa kupangisha alipojenga, akaenda kupanga chumba anachomudu huku anakula kodi na anaendelea kupambana.

It’s just an act of
Thinking outside of the box!
 
Nakuunga mkono. Wengi hawatakuelewa.
Nyumba nyingi zinazojengwa ki ukweli ni za viwango duni na zisizo na mpangilio imara kwenye miji yetu. Pia nyumba ina incur liabilities nyingi. Kinachopanda thamani si nyumba bali ni ardhi kwa sababu nyumba iliyowahi jengwa miaka 20 nyuma haiwezi fanana na nyumba za kisasa. Bali thamani ya ardhi hubaki vilevile ama kuongezeka zaidi, ni nadra thamani ya ardhi kupungua.
Kiasi ambacho mtu amekifukia labda tuseme zaidi ya milioni 20 mtu huyo angeweza kujiendeleza vizuri kibiashara na kuwa mshindani mzuri kwenye masoko.

Wengi hujenga nyumba wakitaka security, kwani huogopa kiasi ambacho wangeweza kuwekeza labda pengine kingefilisika na hapa ndipo watu wengi hubakia static katika kujiendeleza kibiashara.
Tatizo hizo m 20 huwezi kuzikamata kwa mara moja ila kujenga unakuwa unapata kidogo unaweka kwenye ujenzi
 
Kimikiki ardhi ni jambo lingine tofauti na kuamsha ujenzi ambo hauumudu, mtu unakuta anajenga nyumba kwa miaka 20 ikiisha tayari ilishatoka kwenye form na imezeeka.

Miliki viwanja kadiri uwezavyo kisha imarisha uchumi wako ili unapoanza kujenga unakuwa ni ujenzi wenye kueleweka.
Nakuunga mkono. Kuna watu hadi wanaacha kula vizuri kisa wanajenga.
 
Ukiwekeza sehemu salama na ukajikita katika kuukuza uchumi wako huku ukijipunguzia stress za matumizi ya pesa (kama kujenga kwa kudunduliza), basi mambo hayawezi kuwa mabaya.

Hiyi nyumba ya ndoto unayodai utaijenga ndani ya miezi miwili tu ukiwa na uchumi mzuri, badala ya kuishi ukijenga nyumba ambayo utakuja kuikamilisha uzeeni, tena ikiwa imeshapitwa na fashion.
Mkuu uko sahihi 100%.
 
Nyumba ni asset pia na wengi wana ndoto za kuishi kwenye nyumba zao kuepuka usumbufu wa kodi masharti ya wenye nyumba zao
Masharti ya kufagia na usafi mwengine wakati mnakaa na watu wachafu sana
 
[emoji23] Kijana inaonekana huna future na maisha yako, inaonekana umekata tamaa kabisa... Yaani mtu kujenga makazi yake ya kudumu wewe unaona si muhimu bali ni fashion..? Hata kama ni fashion basi ni nzuri maana inakuhakikishia maisha bora marefu yenye utulivu...
Hapana. Ana future na ana mawazo mazuri. Na ana taarifa fulani za dunia ya pili na ya kwanza, lakini yupo dunia ya tatu.
Tip yangu kwake akiweza kukwepa viunzi vya dunia ya tatu basi atafika mbali.
Fundi seremala mfano anatakiwa afikirie kuwa na workshop na maduka ya furniture na awe kampuni, akope bank KWA TIJA ya kupanua biashara hata ktk majiji matatu Dar,Arusha na Mwanza. Ajenge au apange nyumba kwa jina la kampuni ili awe anapunguza kodi kama matumizi.
Ajilipe mshahara na watu wake nao ukawekwe katika sehemu ya matumizi ya kampuni.
Humo akizeeka anaifanya kuwa family business, watoto kama wana akili wanazeeka na hela, ajira wanapata humo humo na kuacha kutoa jasho kwa hawa less than 30% (Asians,Arabs na Indians), mnaukwepa "ukoloni-fala" wa Baba alifanya kwa Mo/Bakhressa mtoto nae humo n.k WATUMWA KIUKOO[emoji38].
Bibi NSSF,mpaka mjukuu nae afanye NSSF!!!
Unaajiriwa mpaka unafikisha miaka 60-65 ni upumbavu[emoji1549][emoji1549]Basi tu.
 
Watanzania wasipotumia hii neema tuliyo nayo ya kumiliki ardhi watakuja kujuta. Kujenga ni kuipa thamani ardhi. Kwa mfanyabiashara makini lazima ajue umuhimu wa kuwa na nyumba. Tena sio nyumba tu bali yenye furnitures na vitu vyote muhimu vya ndani.

Inapunguza sana gharama za maisha. Mleta uzi ni miongoni mwa watu wajinga kabisa kuwahi kutokea kwenye historia ya binadamu. APUUZWE.
Point yake hamjaielewa wakuu, ni point ya kuandaa income streams mkuu, japo hajapata miongozo mizuri.Nchi yetu ilivyo kujenga ni muhimu sana kwa sababu biashara zetu zina mambo mengi na unaweza didimizwa any time.
Ila kwa mawazo yake ya mfanano wa dunia ya kwanza na ya pili kiuchumi yuko sawa.
 
[emoji38][emoji38]Kuna raia wamekuja na jazba kwa jamaa, ni opinion badala ya kumtukana mlitakiwa kumuonyesha ugumu uliopo katika mifumo yetu ya kiuchumi, mfano katika suala la nyumba hatuna mfumo mzuri wa kupata nyumba nafuu za kununua na kulipa taratibu kutokana na kipato chako. Inabidi ujenge taratibu kwa hatua.
Sasa labda ana alternative ya hilo, angeulizwa. Anyway ni jamii forums, ni online watu wanakuwa na tabia tofauti na wakiwa live, mtu huyu huyu hamtukani rafiki yake wakiwa sehemu akatoa kauli kama hizi, ila wanajadiliana fresh tu.
 
Mleta mada anadhani Mtanzania huwa anajenga akiwa na mpunga wote kuanzia msingi hadi finishing ili huo mpunga badala ya kujengea auingize kwenye biashara wapo wenye uwezo huo ila ni wachache

Iko hivi wengi tunajenga kwa kuungaunga vipato. Hivyo kusema mtu angewekeza kwenye biashara ni ngumu sana maana hela ilikuwa ya danadana

Kwa mfano mtu anaweza akawa na nyumba ya thamani tufanye tu 30 mln wewe mpita njia unaweza kusema huyu jamaa aliiipataje hii milioni 30 akajenga mbona inaonekana ana maisha ya kawaida sana. Kumbe yeye mwenyewe alijenga kwa kuungaunga mpaka imefika hapo.

Na ndio maana Watanzania wengi huwa hatujui exactly thamani za nyumba zetu
 
Mmekuja na mihemko lakini point yangu ya msingi ilikuwa ni kwamba kwanini watu wanawaza kuanza kujenga kabla hawajamiliki uchumi mkubwa
Hauwwzi ukaeleweka. Wangekuelewa kama ulivyokusudia ningeshangaa sana
 
Wabongo wanapenda sana kujenga, kwao kujenga ndo mafanikio...kuna ndugu yangu majuzi ananishauri nijenge hata chumba na sebule, nikajisemea huyu mzima kweli ..sina kitega uchumi chochote cha maana naanzaje kujenga?
Majuzi zaidi ya 20m nimewekeza kwenye biashara ila ndo hivyo hata kiwanja sina [emoji3].

Sent from my CPH2219 using JamiiForums mobile app
Unazidiwa akili na Hawa ndege 👇👇👇
 

Attachments

  • images.jpeg
    images.jpeg
    30.3 KB · Views: 8
  • images (1).jpeg
    images (1).jpeg
    8.3 KB · Views: 9
  • images (2).jpeg
    images (2).jpeg
    11.5 KB · Views: 9
Imekuwa ni jambo la kushangaza kwa watanzania wengi kuamua kujenga na kuendelea kuishi maisha yale yale

Unakutana fundi fenicha aliyefanya kazi miaka 15 anakuambia anamalizia ujenzi ukiangalia ufanyaji kazi bado wa kusubiri hela advance kwa mteja hafikirii kabisa kuwa na store kubwa utakayotoa faida kubwa zaidi kwa haraka zaidi kutokana na uzoefu wake.

Unakutana na dereva yeye miaka na miaka anaendesha gari za watu anakuja na habari njema amejenga ni vyema lakini kwanini asikilie kumiliki gari yake.

Unakutana na kijana kinyozi ana uzoefu wa miaka saba anakuambia nimejenga vyumba vitatu nataka nihamie kwangu ni jambo jema lakini hafikirii kama pesa hizo kama angetumia kufungua barbershop kubwa ambayo ingempa faida maradufu
Kama unaweza kujenga nyumba jenga, tena sio moja tu. Hutajuta.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna muda kujenga ni hasara sana, bora ukafanya mambo ya msingi kwanza ila kama kujenga ni swala la msingi kwa mtu basi na alifanye tu.
 
Back
Top Bottom